CHADEMA wana kazi kubwa huku Iramba Magharibi. Miezi miwili iliyopita Mwenyekiti wa Wilaya wa CHADEMA alibambikiziwa uchawi nyumbani kwake huko Kijijini Kisana. Wanakijiji wakakusanyika na kutaka kumpiga akakimbia. Tangu kipindi hicho amekuwa akijificha. Watu walidai kipindi hicho kwamba mpango ulisukwa na Mwigulu ili kumchafua na kuharibu taswira ya CHADEMA kwa kuonyesha kwamba viongozi wa CHADEMA ni wachawi! Watu hawakuamini sana.
Sasa mhe Mwigulu amerudi juzi Bungeni na ameanza mikutano katika Jimbo lake. Juzi Mwenyekiti aliitwa akaambiwa kama anataka atulie nyumbani aache kutangatanga kama kunguru arudishe majeshi na yeye Mwigulu atamsafisha kwa sababu mpango mzima anaujua. Kweli, kijana wa watu amejisamisha leo kwenye mkutano na kutangaza kwamba, kwa maneno yake, 'anarudi kwa baba'. Kwa hivyo Mwenyekiti wa Wilaya wa Iramba Magharibi, Bwana Sembe, leo amesalimu amri kwa vitimbi vya Mwigulu na kukamata kadi ya magamba.
Nawapa angalizo CHADEMA: Katibu wenu wa wilaya pia yupo njiani. Actually huyu alikuwa CCM siku zote na amekuwa akitumiwa kuwachota CHADEMA. Sasa inasemekana CHADEMA wamesimamisha ruzuku kwa muda kwenda wilayani, na leo ameripoti kwa mabosi wa CCM hapa wilayani akidai kwamba kama ruzuku hamna hana haja ya kuendelea kubaki CHADEMA. Anasema bora yeye aondoke arudi rasmi na kuwazika CHADEMA hapa wilayani. Hii nimeipata mwenyewe kwa viongozi wa CCM waliokuwa wanaongea kwa kucheka na kutusema sisi tunaoshabikia CHADEMA hapa Kiomboi.
Kwa kifupi: CHADEMA ina watu wengi sana hapa Iramba Magharibi lakini haina VIONGOZI. Viongozi wengi wilayani wapo mfukoni wa Mwigulu na anawakatia kila akija. Ni vizuri kumuwahi huyu katibu mkampiga chini kabla Mwigulu hajamrudisha rasmi. Ni ushauri tu.
Sasa mhe Mwigulu amerudi juzi Bungeni na ameanza mikutano katika Jimbo lake. Juzi Mwenyekiti aliitwa akaambiwa kama anataka atulie nyumbani aache kutangatanga kama kunguru arudishe majeshi na yeye Mwigulu atamsafisha kwa sababu mpango mzima anaujua. Kweli, kijana wa watu amejisamisha leo kwenye mkutano na kutangaza kwamba, kwa maneno yake, 'anarudi kwa baba'. Kwa hivyo Mwenyekiti wa Wilaya wa Iramba Magharibi, Bwana Sembe, leo amesalimu amri kwa vitimbi vya Mwigulu na kukamata kadi ya magamba.
Nawapa angalizo CHADEMA: Katibu wenu wa wilaya pia yupo njiani. Actually huyu alikuwa CCM siku zote na amekuwa akitumiwa kuwachota CHADEMA. Sasa inasemekana CHADEMA wamesimamisha ruzuku kwa muda kwenda wilayani, na leo ameripoti kwa mabosi wa CCM hapa wilayani akidai kwamba kama ruzuku hamna hana haja ya kuendelea kubaki CHADEMA. Anasema bora yeye aondoke arudi rasmi na kuwazika CHADEMA hapa wilayani. Hii nimeipata mwenyewe kwa viongozi wa CCM waliokuwa wanaongea kwa kucheka na kutusema sisi tunaoshabikia CHADEMA hapa Kiomboi.
Kwa kifupi: CHADEMA ina watu wengi sana hapa Iramba Magharibi lakini haina VIONGOZI. Viongozi wengi wilayani wapo mfukoni wa Mwigulu na anawakatia kila akija. Ni vizuri kumuwahi huyu katibu mkampiga chini kabla Mwigulu hajamrudisha rasmi. Ni ushauri tu.