waziri2020
Senior Member
- May 31, 2019
- 197
- 469
Sakata la vitambulisho Vya wamachinga Mkoa wa Arusha,limechukua sura Mpya Mara baada ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha kuamuru wakuu wa Idara mbalimbali za serikali Jijini hapa wakiwemo TRA kuuza Vitambulisho hivyo kwa lazima.
Jambo hilo liliibuka katika baraza la madiwani wa halmashauri ya Jiji la Arusha waliokuwa wakihoji hatua ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuwagawia watumishi wa serikali wakiwemo wakuu wa Idara ya mamlaka ya Mapato TRA Mkoani hapa kuuza vitambulisho hivyo .
Moja ya watumishi wa TRA jina (limehifadhiwa)amekiri kupatiwa vitambulisho 100 akaviuze jambo ambalo alidai limemfanya asifanyekazi aliyoajiriwa nayo kwa ufanisi badala yake amekuwa akishinda mtaani akisaka wamachinga ili auze vitambulisho hivyo alivyokabidhiwa na mkuu wa Mkoa Gambo baada ya kutishiwa asipoviuza atakatwa mshahara wake kufidia.
"Mimi nimepewa vitambulisho 100 Vya machinga nikauze ila sijui nitamuuzia nani maana kila ninayemfuata ananiambia tiyari anacho ,nimeamua kuvikopesa maana tunatishiwa kukatwa mshahara sijui nifanyaje maana hapa kila mkuu wa Idara amepatiwa vitambulisho 100" Alisema mmoja ya mkuu wa Idara TRA.
Wengine waliokumbwa na kadhia hiyo ni pamoja na mamlaka ya maji AUWSA ambao pia wamepatia kuuza Vitambulisho pamoja na taasisi zingine za serikali Mkoani hapa.
Inadaiwa kuwa Gambo alichukua vitambulisho 125,000 kwa sifa ya kuonekana kwamba anauwezo wa kuuza Vitambulisho vingi na kuipita mikoa mingine jambo ambalo linawaumiza watumishi wengine wa serikali kwa kushinda wakiuza vitambulisho mitaani na kusahau Kazi walioajiriwa nayo.
Katika hatua nyingine ,Gambo anadaiwa kutokuwa na maelewano mazuri na viongozi wenzake wa serikali jambo libalisababisha kudhorota kwa shughuli za maendeleo ya Mkoa
Hivi karibuni Gambo aliamuru Takukuru Mkoani hapa kumkamata na Kumhoji katibu tawala wa Mkoa ,Richard Kwitega, pamoja na afisa salama aliyejulikana kwa jina moja la Kassimu kwa madai ya kupata mgao kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya uwindaji ya OBC ambaye bado anashikiliwa mahabusu kwa kosa la uhujumu uchumi.
Jambo hilo linadai kuwakera wafanyakazi mbalimbali Mkoani hapa kwa kitendo hicho kwani mbali ya kuwadhalilisha kimewapunguzia morari wa utendaji Kazi Mkoani hapo.
Jambo hilo liliibuka katika baraza la madiwani wa halmashauri ya Jiji la Arusha waliokuwa wakihoji hatua ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mrisho Gambo kuwagawia watumishi wa serikali wakiwemo wakuu wa Idara ya mamlaka ya Mapato TRA Mkoani hapa kuuza vitambulisho hivyo .
Moja ya watumishi wa TRA jina (limehifadhiwa)amekiri kupatiwa vitambulisho 100 akaviuze jambo ambalo alidai limemfanya asifanyekazi aliyoajiriwa nayo kwa ufanisi badala yake amekuwa akishinda mtaani akisaka wamachinga ili auze vitambulisho hivyo alivyokabidhiwa na mkuu wa Mkoa Gambo baada ya kutishiwa asipoviuza atakatwa mshahara wake kufidia.
"Mimi nimepewa vitambulisho 100 Vya machinga nikauze ila sijui nitamuuzia nani maana kila ninayemfuata ananiambia tiyari anacho ,nimeamua kuvikopesa maana tunatishiwa kukatwa mshahara sijui nifanyaje maana hapa kila mkuu wa Idara amepatiwa vitambulisho 100" Alisema mmoja ya mkuu wa Idara TRA.
Wengine waliokumbwa na kadhia hiyo ni pamoja na mamlaka ya maji AUWSA ambao pia wamepatia kuuza Vitambulisho pamoja na taasisi zingine za serikali Mkoani hapa.
Inadaiwa kuwa Gambo alichukua vitambulisho 125,000 kwa sifa ya kuonekana kwamba anauwezo wa kuuza Vitambulisho vingi na kuipita mikoa mingine jambo ambalo linawaumiza watumishi wengine wa serikali kwa kushinda wakiuza vitambulisho mitaani na kusahau Kazi walioajiriwa nayo.
Katika hatua nyingine ,Gambo anadaiwa kutokuwa na maelewano mazuri na viongozi wenzake wa serikali jambo libalisababisha kudhorota kwa shughuli za maendeleo ya Mkoa
Hivi karibuni Gambo aliamuru Takukuru Mkoani hapa kumkamata na Kumhoji katibu tawala wa Mkoa ,Richard Kwitega, pamoja na afisa salama aliyejulikana kwa jina moja la Kassimu kwa madai ya kupata mgao kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya uwindaji ya OBC ambaye bado anashikiliwa mahabusu kwa kosa la uhujumu uchumi.
Jambo hilo linadai kuwakera wafanyakazi mbalimbali Mkoani hapa kwa kitendo hicho kwani mbali ya kuwadhalilisha kimewapunguzia morari wa utendaji Kazi Mkoani hapo.
si ndo wakubwa walinyimwa likizo eh!!!