VITA VIMEFIKIA TAMATI

VITA VIMEFIKIA TAMATI

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,462
Reaction score
32,985
MAREKANI IMETENGENEZA MPANGO WA KUMALIZA VITA VYA IRAN NA ISRAEL

Baada ya saa 24 In Shaa Allah vita baina ya Iran na Israel In Shaa Allah vita kuwa vimemalizika.

Vita vimedumu kwa siku 12.

Hizi siku 12 mimi binafsi nimejifunza mengi na si kwa mwalimu kunisomesha darasani bali kwa kushinda, kulala na kuamka katika mitandao ya Kijamii.

Kumalizika kwa vita hivi hili ni jambo kubwa na la kushukuriwa.

Vilipoanza vita mitandao ya kijamii hapa nyumbani ilijaa chereko chereko furaha na vifijo.

Nini lilikuwa kinafurahiwa?

Furaha hiyo ilitokana na kushambuliwa vibaya Iran na kuuliwa kwa wataalamu wake muhimu katika Nuclear na viongozi wake katika jeshi.

Iran ikaingia vitani.

Haukupita muda vita vikanoga kwani kulikuwa kunaliwa kote kwa mwalimu na kwa kungwi.

Taratibu nderemo zikawa zinapungua haziandikiki tena kwani rundinga zilikuwa zinaonyesha Tel Aviv na Haifa inayofanana na Ghaza.

Nyoyo za washangiliaji ziliumia.

Macho yao hayakuweza kuamini walichokuwa wanashuhudia.

Miji ya Israel ilikuwa ikiangamizwa kwa makombora.

Tehran inapigwa na Tel Aviv inapigwa.

Furaha mitandaoni ya kufurahia kupigwa kwa Iran ghafla ikatoweka na pakawa na utulivu na ukimya mkubwa usio na kifani.

Hata Marekani ilipoingia vitani kuisaidia Israel paliendelea kuwa na ukimya mitandaoni.

Wapiga vigelegele waliinamisha vichwa vyao kwa fadhaa kwani walikuwa washaijua tafsiri isiyo na shaka ya kitendo hicho.

Kitendo hicho kilidhihirisha ukweli kuwa Israel imeelemewa haina uwezo wa kupambana na Iran.

Vyombo vikubwa vya habari duniani vikawa vinauliza endapo Iran itapambana na Marekani kulipiza kisasi.

Jibu limetolewa tena kwa haraka.

Iran katika muda mfupi sana imepiga kituo cha kijeshi Qatar.

Marekani katika muda mfupi mno imetangaza kusitishwa kwa vita baina ya Iran na Israel.

Naamka usiku mkubwa natupia jicho Al Jazeera ndiyo nakuta "Breaking News."

Israel hii ambayo leo Wayahudi wanaamka na kurejea majumbani mwao na kuangalia barabara na mitaa yao ya Tel Aviv si ile waliyoiacha walipoingia katika sehemu za kujificha mabomu.

Tel Aviv imekuwa mfano wa Ghaza kwa magofu na kifusi.

Ukweli wa vita utawadhihirikia.

Wengi Wayahudi wamekimbia vita kupitia baharini kujificha Cyprus na kwengineko.

Wayahudi waliofanikiwa kukimbia na wale waliobakia nyuma wote wana kitu cha kujifunza katika vita hivi.

Vipi kuhusu Iran?

Wamarekani wanawatazama vipi Wairani?

Halikadhalika dunia inawaonaje Wairani?
Leo Israel ina lipi la kusema kuhusu Iran?
 
Iran kasimama kiume. Israel amezoea kupigana na wanamgambo sasa kapigana na jeshi ambalo lilikuwa likimpa kipimo sawia cha adhabu.
Nilikuwa natazama vyombo vya habari Israel walikuwa hawaruhusu waandishi wa habari kurekodi majanga mengine wasionekane wamepata tabu sana.
Ila yale ya kupigwa hospitali hayo waliruhusu ili waonewe huruma na dunia.
Ila Iran awe makini Trump tapeli huenda wamepanga kumlaghai ili akitulia wamuue Ayatollah kama ambavyo aliposema atafanya maamuzi baada ya week mbili russia akawambia wawe tayari huyu atashambulia muda wowote.
Jana nomeona taarifa kuwa yale mashambulizi yalipofanywa hakuna ongezeko la mionzi na nikaona video watu wamepatembelea. Hii ina maana hakukuwa na kitu
 
USA, ilipombutua yule general wao, Qasseim suleiman, Iran walipotaka kulipiza kisasi, kabla, hawajapiga kombora kambi ya jeshi LA USA pale Iraq, waliwapa US taarifa kwanza, through back channel, Ila watu kama wewe, huwezi, jua hili,
Hata hayo ma kombora waliorusha Qatar, kwanza, hayajeleta madhara, pili yalidunguliwa juu kwa, juu na mifumo ya ulinzi, wa anga ya Qatar.
MTU mweusi shida Sana, Israel inaua watoto na wanawake,wa, kipalestina, Ila mkristo wa bongo, anakuambia Israel ni taifa LA Mungu!
Mbongo Muslim, mweusi, weusi, wenzie kule Sudan wakiuliwa na mwarab, hakuna shida, Ila mwarab wa mashariki ya Kati akiuliwa na US, Israel, mishipa inamtoka balaa, hapa bongo, Samia Muslim, akiua Muslim kama mzee kibao, wa Islam kimya,Mkapa alipoua wa Islam wa mwembechai, balaa
 
Ngojera za vita ya siku sita,sijui taifa la mungu imefikia tamati, hamna tena wa kumdangaya kuhusu uwezo wa kijeshi wa Israeli, ni jeshi zaifu mmno lisiloweza kufanya chochote bila ya msaada. Hata 2006 ilikua hivi hivi baada ya Israeli kizidiwa na Hizbolla Marekani akingilia kati na kuomba vita iishe, Israeli sio taifa la Mungu maana wao wenyewe hawamtegei Mungu wanamtegemea Marekani awalinde, bila ya Marekani Israeli hawezi kutoboa hata kwa Hamas.
 
USA, ilipombutua yule general wao, Qasseim suleiman, Iran walipotaka kulipiza kisasi, kabla, hawajapiga kombora kambi ya jeshi LA USA pale Iraq, waliwapa US taarifa kwanza, through back channel, Ila watu kama wewe, huwezi, jua hili,
Hata hayo ma kombora waliorusha Qatar, kwanza, hayajeleta madhara, pili yalidunguliwa juu kwa, juu na mifumo ya ulinzi, wa anga ya Qatar.
MTU mweusi shida Sana, Israel inaua watoto na wanawake,wa, kipalestina, Ila mkristo wa bongo, anakuambia Israel ni taifa LA Mungu!
Mbongo Muslim, mweusi, weusi, wenzie kule Sudan wakiuliwa na mwarab, hakuna shida, Ila mwarab wa mashariki ya Kati akiuliwa na US, Israel, mishipa inamtoka balaa, hapa bongo, Samia Muslim, akiua Muslim kama mzee kibao, wa Islam kimya,Mkapa alipoua wa Islam wa mwembechai, balaa
Tanzania tuna uchizi wa kidini
 
Ngojera za vita ya siku sita,sijui taifa la mungu imefikia tamati, hamna tena wa kumdangaya kuhusu uwezo wa kijeshi wa Israeli, ni jeshi zaifu mmno lisiloweza kufanya chochote bila ya msaada. Hata 2006 ilikua hivi hivi baada ya Israeli kizidiwa na Hizbolla Marekani akingilia kati na kuomba vita iishe, Israeli sio taifa la Mungu maana wao wenyewe hawamtegei Mungu wanamtegemea Marekani awalinde, bila ya Marekani Israeli hawezi kutoboa hata kwa Hamas.
Na kama ni la mungu basi na mungu ana mapungufu kibao nadhani bibilia zichomwe moto
 
Back
Top Bottom