Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,014
- 144,372
Baadhi ya watu wanapoesema wabongo IQ ni tatizo, ukitamza hiki kinachoitwa vita dhidi ya rushwa na ufisadi na jinsi baadhi ya watu wanavyopokea taarifa hizi; unaweza kukiri ni kweli sisi IQ yeyu ni tatizo tena tatizo kubwa sana.
Mtu mwenye akili mpaka sasa angejiuliza maswali haya machache:
1.Hivi kupambana na rushwa na ufisadi ni kuwatangaza tu hadharani /majukwaani baadhi ya watuhumiwa?
2.Ni kutamka tu kuwa tutawakamata alafu baadae kimya?
3.Ni kuwapandisha baadhi ya watuhumwa mahakamani alafu vyombo vya habari vikaripoti fulani kapandishwa kizimbani kisha baadae DPP anawafutia kesi?
4.Mmejiuliza kesi za wapinzani na zile mafisadi zipi ni nyingi?
6.Wakati mpaka sasa teyari wanasiasa wawili au watatu wa upinzani wameshahukumiwa jela,kuna fisadi gani mpaka leo hii kafungwa jela?
7.Spidi ya kesi za wapinzani, inafanana na ile ya watuhumiwa wa rushwa na ufisadi?
8.Mahakama ya mafisadi iko wapi?
9.Licha ya tuhuma za ufisadi kuibuka mara kwa mara, Bunge la sasa la Ndugai; limeshaunda kamati teule ngapi kuchunguza kashifa hizo?
10.Katika awamu hii, vyombo vya habari viko huru kuandia tuhuma za wanasiasa wakubwa kama miaka iliyopita?
11.Tuhuma za ufisadi anazoibua Zitto kila wakati, ni kweli vyonbo vyote vya habari huwa havina hizo taarifa isipokuwa Zitto tu?
12.Je, sheria ya manunuzi ya umma leo hii hakuna wabunge wanaolalamika kuwa haizingatiwi?
13.Leo hii wabunge hawalalamika Bunge kutoheshmiwa katika maswala mazima ya Bajeti?
14.Au vita halisi ya kupambana na rushwa na ufisadi ni kwa kufukuza ma-CEO wa mashirika ya umma na kuteua wengine?
15.Alafu unaweza kupambana na rushwa na ufisadi huku kukiwa na madai kuwa media haziko huru?
16.Na je mifumo yetu ya nchi kama vile sheria zetu baadhi na hata katiba yetu, ina facilitate kweli vita dhidi ya rushwa na ufisadi bila kujali cheo cha mtu?
17.Kwa mfano, kama sheria inatakaa kibali cha DPP kufungua mashika wakati TAKUKURU ndio taasisi inayofanya uchunguzi, je sheria hii ni nzuri na bado inatufaa?
18.Na je, Mkurugenzi huyu wa mashitaka (DPP), sheria na utaratibu wa kupatikana kwake na hata kuondolewa kwake ofisini, zinamfanya awe .mtu huru katika kutimiza majukumu yake?
19.Wenzetu wa chama tawala, wako taayari kubadili mifumo hii?
Maswali ni mengi ila binafsi naamini vita halisi ya kupambana na rushwa kamwe haiwezi kupiganwa iwapo CCM bado iko madarakani hata ikitokea leo hii Lissu ni raisi wa nchi hii kupitia CCM.
Endeleeni kusikia watu wanatuhumiwa /wanatajwa kujihusisha na vitendo ya rushwa na ufisadi majukwaani huku baadhi wakifikishwa mahakamani lakini mkiwa makini mtatazama pia ni nini huwa mwisho wa mambo haya.
Kazi kwenu wadanganyika!
Mtu mwenye akili mpaka sasa angejiuliza maswali haya machache:
1.Hivi kupambana na rushwa na ufisadi ni kuwatangaza tu hadharani /majukwaani baadhi ya watuhumiwa?
2.Ni kutamka tu kuwa tutawakamata alafu baadae kimya?
3.Ni kuwapandisha baadhi ya watuhumwa mahakamani alafu vyombo vya habari vikaripoti fulani kapandishwa kizimbani kisha baadae DPP anawafutia kesi?
4.Mmejiuliza kesi za wapinzani na zile mafisadi zipi ni nyingi?
6.Wakati mpaka sasa teyari wanasiasa wawili au watatu wa upinzani wameshahukumiwa jela,kuna fisadi gani mpaka leo hii kafungwa jela?
7.Spidi ya kesi za wapinzani, inafanana na ile ya watuhumiwa wa rushwa na ufisadi?
8.Mahakama ya mafisadi iko wapi?
9.Licha ya tuhuma za ufisadi kuibuka mara kwa mara, Bunge la sasa la Ndugai; limeshaunda kamati teule ngapi kuchunguza kashifa hizo?
10.Katika awamu hii, vyombo vya habari viko huru kuandia tuhuma za wanasiasa wakubwa kama miaka iliyopita?
11.Tuhuma za ufisadi anazoibua Zitto kila wakati, ni kweli vyonbo vyote vya habari huwa havina hizo taarifa isipokuwa Zitto tu?
12.Je, sheria ya manunuzi ya umma leo hii hakuna wabunge wanaolalamika kuwa haizingatiwi?
13.Leo hii wabunge hawalalamika Bunge kutoheshmiwa katika maswala mazima ya Bajeti?
14.Au vita halisi ya kupambana na rushwa na ufisadi ni kwa kufukuza ma-CEO wa mashirika ya umma na kuteua wengine?
15.Alafu unaweza kupambana na rushwa na ufisadi huku kukiwa na madai kuwa media haziko huru?
16.Na je mifumo yetu ya nchi kama vile sheria zetu baadhi na hata katiba yetu, ina facilitate kweli vita dhidi ya rushwa na ufisadi bila kujali cheo cha mtu?
17.Kwa mfano, kama sheria inatakaa kibali cha DPP kufungua mashika wakati TAKUKURU ndio taasisi inayofanya uchunguzi, je sheria hii ni nzuri na bado inatufaa?
18.Na je, Mkurugenzi huyu wa mashitaka (DPP), sheria na utaratibu wa kupatikana kwake na hata kuondolewa kwake ofisini, zinamfanya awe .mtu huru katika kutimiza majukumu yake?
19.Wenzetu wa chama tawala, wako taayari kubadili mifumo hii?
Maswali ni mengi ila binafsi naamini vita halisi ya kupambana na rushwa kamwe haiwezi kupiganwa iwapo CCM bado iko madarakani hata ikitokea leo hii Lissu ni raisi wa nchi hii kupitia CCM.
Endeleeni kusikia watu wanatuhumiwa /wanatajwa kujihusisha na vitendo ya rushwa na ufisadi majukwaani huku baadhi wakifikishwa mahakamani lakini mkiwa makini mtatazama pia ni nini huwa mwisho wa mambo haya.
Kazi kwenu wadanganyika!