Azizi Mussa
JF-Expert Member
- May 9, 2012
- 9,197
- 7,533
Jamani eeh; vision ya mama ni very simple and clear. Ni '4Rs' yaani (Reconciliation, Resiliency, Reforms & Rebuild).
'Reconciliation' – Kujenga uhusiano mwema miongoni mwa makundi yaliyokuwa yanahasimiana bila sababu. Hii ni kati ya vyama vya siasa, taasisi na mashirika, wadau wa maendeleo, Tanzania na nchi nyingine na ushirikiano wa kikanda na kimataifa, NGO's n.k.
'Resiliency' - Kuwaponya walioumizwa, kuwatetea waliodhulumiwa, kujaribu kuwarejeshea haki walipokonywa, kuleta furaha kwa wenye huzuni na kuwarudishia matumaini waliokata tamaa n.k.
'Reforms' – Kufanya marekebisho makubwa ya kimifumo ikiwemo kurekebisha sheria mbovu kila zilipobainika, Kutupatia katiba mpya (kwa wakati muafaka ), kufanya mabadiliko ya kiuchumi kutoka uchumi wa ku force hadi uchumi wa kuvutia kisayansi.
'Rebuild' – Kurekebisha penye makosa na kuendeleza kujenga miundombinu muhimu ambayo iko kwenye pipeline.
Na R zote zinaenda kwa mpigo, usiponufaika na 'R' utanufaika na 'R' na usipofikiwa na 'R&R' lazima Upate japo 'R". Enjoy 'R' inayokuhusu huku ukitimiza wajibu wako kwa kuwa mafanikio ya kweli hupatikana pale kila mmoja wetu anapotimiza wajibu wake kikamilifu huku akitanguliza dhamira njema.