Visa za Tanzania na maofisa uhamiahaji

NYENJENKURU

JF-Expert Member
Feb 11, 2011
1,063
288
Ndugu wana JF naleta kwenu hii maada na muone maafisa Uhamiaji wa Tanzania tulivyo wa ajaabu.Kisa ni kama hivi.Mtu anaenda Ubalozi wa Tanzania kama vile Marekani anataka kuja Tanzania kufanya workshop ya week moja au mbili anepewa visa yake anakuja Tanzania.Akifaka labda anaenda Ifakara Morogoro anakutana na afisa uhamihaji anamwambia wewe unafanya nini hapa Mzungu anamwabia nimekuja kwenye workshop hapa Ifakara.Afisa anamwambia hiyo visas yako waliyokupa siyo ya halali unatakiwa unipe tena dola mia nikupe nyingine.Mzungu anauliza kwa vipi unipe nyingine wakati mimi nimeenda kwenye ubalozi wenu hapo WDC nikawaelza nachotaka kwenda kufanya Ifakara halafu wewe unasema WALIKOSEA kukupa visa ya kufanaya workshop.Twende polisi.Je swali la nani wa kulaumiwa?Mgeni au Afisa uhamiaji wa Ubalozi?Au huyu wa Ifakara?Je wezentu wanyafanya hivyo?

Naomba tutajidili kama labda kuna nini hapo kuhusu mfumo wetu wa Visa.
 
Huko ni kujidhalilisha sana kwa watumishi na serikali kwa ujumla waambie wapunguze njaa hao uhamiaji......wanatia aibu taifa!!!!!
 
Ndugu wana JF naleta kwenu hii maada na muone maafisa Uhamiaji wa Tanzania tulivyo wa ajaabu.Kisa ni kama hivi.Mtu anaenda Ubalozi wa Tanzania kama vile Marekani anataka kuja Tanzania kufanya workshop ya week moja au mbili anepewa visa yake anakuja Tanzania.Akifaka labda anaenda Ifakara Morogoro anakutana na afisa uhamihaji anamwambia wewe unafanya nini hapa Mzungu anamwabia nimekuja kwenye workshop hapa Ifakara.Afisa anamwambia hiyo visas yako waliyokupa siyo ya halali unatakiwa unipe tena dola mia nikupe nyingine.Mzungu anauliza kwa vipi unipe nyingine wakati mimi nimeenda kwenye ubalozi wenu hapo WDC nikawaelza nachotaka kwenda kufanya Ifakara halafu wewe unasema WALIKOSEA kukupa visa ya kufanaya workshop.Twende polisi.Je swali la nani wa kulaumiwa?Mgeni au Afisa uhamiaji wa Ubalozi?Au huyu wa Ifakara?Je wezentu wanyafanya hivyo?

Naomba tutajidili kama labda kuna nini hapo kuhusu mfumo wetu wa Visa.

Mbona habari iko juu juu? Baada ya mgeni kusema waende polisi, nini kilichotokea? Walimruhusu kuingia au walimkatalia hata kwenda huko polisi? Au ni hadithi ya kutunga tu?

Amandla..........
 
Huko ni kujidhalilisha sana kwa watumishi na serikali kwa ujumla waambie wapunguze njaa hao uhamiaji......wanatia aibu taifa!!!!!
tatizo hakuna ugawaji sawa wa keki ya taifa, wabunge wanajilipa mishahara mikubwa na hapohapo wanajilipa posho wakiwa kazini, maslah ya watumishi wengine ni duni, sasa tungeanza na kina lowasa tukomeshe wizi wanaofanya na tuwanyang'anye mali walizotuibia, kisha tuboreshe maslah ya watumishi wa chini.
 
Mbona habari iko juu juu? Baada ya mgeni kusema waende polisi, nini kilichotokea? Walimruhusu kuingia au walimkatalia hata kwenda huko polisi? Au ni hadithi ya kutunga tu?

Amandla..........

Hamna haja ya kujua kilichojiri. Mleta uzi alitaka tu kuonesha 'utendaji ulitukuka' ktk ofisi za umma. Hii ni aibu na inakatisha tamaa hata wageni wenye nia nzuri ya kuja Tz kwa minajili mbalimbali. Aina hii ya utendaji wa kihuni is another low kuonesha tulipo kama taifa.
 
Nadhani wageni wanatakiwa wawe wanapewa maelezo kamili na balozi zetu wanapopewa visa. Yani waelezwe kuwa visa yako haikuruhusu kufanya kazi yoyote TZ, bali unaingia kama mgeni mshiriki kwenye mafunzo au utalii. Ukitaka kufanya kazi kama kuendesha semina taratibu zake ni 1,2,3,...
 
kama mzungu akitoa pesa nyie pigeni hiyo pesa tu. hawa walituonea sana kipindi cha ukoloni

hapana sikubaliani na wewe kabisaaaaaa
hata sisi wengine tupo nje kwa sasa na hawa ambao tupo ktk nchi zao hawajatufanyia kama polisi wetu wanavyofanya sasa,kama ingekuwa ni hivyo tungekuwa tunapata tabu sana ktk nchi za watu

kwa mfano,Australia,ujerumani na Uchina wao ukishaenda ubalozi wao na wakakupa viza hapo umamaliza kila kitu,utakwenda ktk nchi husika na utakaa kwa mda uliotakiwa kukaa na utarejea Tz bila matatizo yeyote yale,

labda uwe umekata viza tofauti na kile ulichokusudia kufanya ndio mambo yanaweza kubadilika

kwa mfano unakwenda kusoma nje utakata viza ya kiuanafunzi,kama ni biashara utakata viza ya biashara na mengineyo na pia kama ni kazi hilo ni swala la work permit halihusiani na viza,ila ktk maswala ya semina huwa inajulikana hata aina ya viza huwa ni tofauti na za biashara ama uwanafunzi na zina siku maalumu za kukaa nchi husika

lakini bongo ni ushenzi mtupu,tumeweka umasikini mbele na ndio unaotufanya tutawaliwe kirahisi

makosa yapo kwa huyo polisi aliyeomba tena 100$ kwani nadhani wale wa ubalozi walituwa viza kulingana na maombi ya mhusika.je anavyo kwenda kuibadilisha huwa inakuwa ileile ama ni tofauti na ile ya awali?

Hii nchi umasikini ndio unasababisha tuendelee kutawaliwa
 
Nadhani wageni wanatakiwa wawe wanapewa maelezo kamili na balozi zetu wanapopewa visa. Yani waelezwe kuwa visa yako haikuruhusu kufanya kazi yoyote TZ, bali unaingia kama mgeni mshiriki kwenye mafunzo au utalii. Ukitaka kufanya kazi kama kuendesha semina taratibu zake ni 1,2,3,...

Thanks mtumia busara. Kwa kawaida balozi zetu haziruhusiwi kutoa vibali vya kufanya kazi ikiwa ni kwa muda mrefu au mfupi. Hata vile vya kufanya workshop muda mfupi (Carrying on temporaly assignment.. CTA). Vibali hivyo hutolewa na wiraza ya mambo ya ndani tu chini ya Uhamiaji.Ikumbukwe balozi zetu zipo Mambo ya nje. Tatizo lipo huko kwenye balozi zetu ndio wana wadanganya wageni kuwa wanaweza kuwapa kibali chochote kuja Tanzania wakati wao inavyofahamika wanaruhusiwa kutoa visitors pass tu. Hapo kuna mkanganyiko wa kimaslahi, balozi tezu hayo malipo ya visa huwa wanazitumia kundesha ofisi zao ukiwa ni pamoja na 'kununua mafuta'. Wakati idara ya uhamiaji wanataka fedha irudi Tanzania kuongeza 'makusanyo yao kwa mwaka'. Tusipende mara nyingi kutoa lawama tuu kwa watumishi wa serikali tunawavunja moyo. Huyo afisa uhamaji alikuwa sasa kumkakata huyo jamaa.Vibali vya seminar huwa vinaombwa na mwenyeji wako au ofisi iliyokualika kufanya seminar wala haviombwi na mgeni mwenyewe
 
hapana sikubaliani na wewe kabisaaaaaa
hata sisi wengine tupo nje kwa sasa na hawa ambao tupo ktk nchi zao hawajatufanyia kama polisi wetu wanavyofanya sasa,kama ingekuwa ni hivyo tungekuwa tunapata tabu sana ktk nchi za watu

kwa mfano,Australia,ujerumani na Uchina wao ukishaenda ubalozi wao na wakakupa viza hapo umamaliza kila kitu,utakwenda ktk nchi husika na utakaa kwa mda uliotakiwa kukaa na utarejea Tz bila matatizo yeyote yale,

labda uwe umekata viza tofauti na kile ulichokusudia kufanya ndio mambo yanaweza kubadilika

kwa mfano unakwenda kusoma nje utakata viza ya kiuanafunzi,kama ni biashara utakata viza ya biashara na mengineyo na pia kama ni kazi hilo ni swala la work permit halihusiani na viza,ila ktk maswala ya semina huwa inajulikana hata aina ya viza huwa ni tofauti na za biashara ama uwanafunzi na zina siku maalumu za kukaa nchi husika

lakini bongo ni ushenzi mtupu,tumeweka umasikini mbele na ndio unaotufanya tutawaliwe kirahisi

makosa yapo kwa huyo polisi aliyeomba tena 100$ kwani nadhani wale wa ubalozi walituwa viza kulingana na maombi ya mhusika.je anavyo kwenda kuibadilisha huwa inakuwa ileile ama ni tofauti na ile ya awali?

Hii nchi umasikini ndio unasababisha tuendelee kutawaliwa

Sikubaliani na wewe kwa mambo mengi uliyondika fanya tafiti kwanza kwenye nchi yako kuna vibali vingapi vya ukazi na mamlaka zipi zinatoa vivyo vibali. Tupo wengi tulioshi nchi zingine. Nchi nyingi za magharibi hasa zile za Schengen ikiwemo Ujerumani uliyoitaja visa inatolewa kwa muda miezi mitatu tu. Kama unakaa zaidi ya hiyo miezi lazima kuna registration ambazo utatakiwa uzifanye ili upate resident permit. Mwanafunzi mbaye programme yake ni zaidi ya hiyo miezi lazima apate residence card. Nchi kama Uholanzi ndio inawawakilishi wa Uhamiaji hapohapo vyuoni, wanaita IND. Balozi za hizo nchi huwa zinaruhusiwa kutoa visa tu, unapofika kule kama utakaa zaidi ya miezi mitatu lazima ufanye registration hata kama ni kwa mtandao. Tofauti ya kwetu sisi na wao ni kwamba huwezi kukamatwa hovyo mtaani lakini yote hiyo naamini ni kwa sababu ya teknolog yao iko juu. Makazi yao yameorodheshwa vizuri kila mtu unatakiwa kuwa na anuani. Sioni ajabu kwa maafsa Uhamiaji kumkama mtu njiani, kwa technoj mbovu yetu, makazi hayajapangika, annual si lazima kuwa nayo etc
 
Thanks mtumia busara. Kwa kawaida balozi zetu haziruhusiwi kutoa vibali vya kufanya kazi ikiwa ni kwa muda mrefu au mfupi. Hata vile vya kufanya workshop muda mfupi (Carrying on temporaly assignment.. CTA). Vibali hivyo hutolewa na wiraza ya mambo ya ndani tu chini ya Uhamiaji.Ikumbukwe balozi zetu zipo Mambo ya nje. Tatizo lipo huko kwenye balozi zetu ndio wana wadanganya wageni kuwa wanaweza kuwapa kibali chochote kuja Tanzania wakati wao inavyofahamika wanaruhusiwa kutoa visitors pass tu. Hapo kuna mkanganyiko wa kimaslahi, balozi tezu hayo malipo ya visa huwa wanazitumia kundesha ofisi zao ukiwa ni pamoja na 'kununua mafuta'. Wakati idara ya uhamiaji wanataka fedha irudi Tanzania kuongeza 'makusanyo yao kwa mwaka'. Tusipende mara nyingi kutoa lawama tuu kwa watumishi wa serikali tunawavunja moyo. Huyo afisa uhamaji alikuwa sasa kumkakata huyo jamaa.Vibali vya seminar huwa vinaombwa na mwenyeji wako au ofisi iliyokualika kufanya seminar wala haviombwi na mgeni mwenyewe

Afisa uhamiaji alikuwa sahihi kumkamata huyo mgeni, na huko ubalozini nako walikuwa sahihi kumpa maelekezo ya uongo huyo mgeni. Inaonekana wewe ndio walewale.
 
Sikubaliani na wewe kwa mambo mengi uliyondika fanya tafiti kwanza kwenye nchi yako kuna vibali vingapi vya ukazi na mamlaka zipi zinatoa vivyo vibali. Tupo wengi tulioshi nchi zingine. Nchi nyingi za magharibi hasa zile za Schengen ikiwemo Ujerumani uliyoitaja visa inatolewa kwa muda miezi mitatu tu. Kama unakaa zaidi ya hiyo miezi lazima kuna registration ambazo utatakiwa uzifanye ili upate resident permit. Mwanafunzi mbaye programme yake ni zaidi ya hiyo miezi lazima apate residence card. Nchi kama Uholanzi ndio inawawakilishi wa Uhamiaji hapohapo vyuoni, wanaita IND. Balozi za hizo nchi huwa zinaruhusiwa kutoa visa tu, unapofika kule kama utakaa zaidi ya miezi mitatu lazima ufanye registration hata kama ni kwa mtandao. Tofauti ya kwetu sisi na wao ni kwamba huwezi kukamatwa hovyo mtaani lakini yote hiyo naamini ni kwa sababu ya teknolog yao iko juu. Makazi yao yameorodheshwa vizuri kila mtu unatakiwa kuwa na anuani. Sioni ajabu kwa maafsa Uhamiaji kumkama mtu njiani, kwa technoj mbovu yetu, makazi hayajapangika, annual si lazima kuwa nayo etc

Ya ni kweli,tunachokiongelea ni visa,lakini ktk maswala ya residence permit ni kweli ni lazima ufanye maombi juu ya hiyo residence permit na kwa sasa baadhi ya nchi zimekuwa zikitowa mda wa mwaka mmoja tu hata kama utatakiwa kukaa hapo kwa miaka minne,

lakini pia hapa nilipo niliwahi kukamatwa mtahani lakini lengo lao lilikuwa ni kuuliza kama nina passport na hawakutaka nitoe pesa tena kama tufanyavyo bongo

kama ni hivyo ni bora tuwe wawazi kama wenzetu wafanyavyo,unaelezwa nini cha kufanya hata kabla ya kuingia ktk nchi husika
 
Afisa uhamiaji alikuwa sahihi kumkamata huyo mgeni, na huko ubalozini nako walikuwa sahihi kumpa maelekezo ya uongo huyo mgeni. Inaonekana wewe ndio walewale.

JF Expert Member read between the lines...... Kama afisa angekuwa nataka chochote asingempeleka huyo mtu polisi. Usiwe na ukawa mmoja watoa lawama ambao hawajui inachokilaumu ni nini, hata mimi nakuona ni walewale tu mnaopenda kucomment kila kitu JF hata kwa issue zinahusu majibu ya kitaalamu. Sio kila kitu kinalevel ya comments za magenge ya kahawa
 
JF Expert Member read between the lines...... Kama afisa angekuwa nataka chochote asingempeleka huyo mtu polisi. Usiwe na ukawa mmoja watoa lawama ambao hawajui inachokilaumu ni nini, hata mimi nakuona ni walewale tu mnaopenda kucomment kila kitu JF hata kwa issue zinahusu majibu ya kitaalamu. Sio kila kitu kinalevel ya comments za magenge ya kahawa
Ni wapi nimesema afisa wa Ifakara alikuwa anataka chochote? Hapa lawama ni lazima tulaumu kwa sababu baina ya afisa wa Ifakara na wale wa ubalozini lazima upande mmoja wao una makosa na kusababisha usumbufu kwa wageni. Na sioni unachotetea hapa, labda utuambie wewe ni mmojawao. Mambo kama haya ni very basic na AIBU KUBWA kwa taifa.
 
Ni wapi nimesema afisa wa Ifakara alikuwa anataka chochote? Hapa lawama ni lazima tulaumu kwa sababu baina ya afisa wa Ifakara na wale wa ubalozini lazima upande mmoja wao una makosa na kusababisha usumbufu kwa wageni. Na sioni unachotetea hapa, labda utuambie wewe ni mmojawao. Mambo kama haya ni very basic na AIBU KUBWA kwa taifa.

Mie sie wao ndugu nakushauri tu tembelea ofisa ya maafsa Uhamiaji iliyo jirani nawe wakupe taratibu zikoje. Ila mimi ninavyojua watu wanaokuja kwenye mikutano na seminar huwa wanapewa kitu kinaitwa CTA na ubalozi huwa hawatoi hicho kitu. Labda kama kuna vibali vya aina nyingi kwa shughuli ya aina moja.
 
Mie sie wao ndugu nakushauri tu tembelea ofisa ya maafsa Uhamiaji iliyo jirani nawe wakupe taratibu zikoje. Ila mimi ninavyojua watu wanaokuja kwenye mikutano na seminar huwa wanapewa kitu kinaitwa CTA na ubalozi huwa hawatoi hicho kitu. Labda kama kuna vibali vya aina nyingi kwa shughuli ya aina moja.
Kwanini niende mie ambaye sihitaji hayo maelezo wakati mtu aliyehitaji hayo maelezo kwa ajili ya safari yake, wameshindwa kumpatia? this is a waste of time and space. Kwani unashindwa ku-admitt kwamba kuna tatizo?
 
Ni wapi nimesema afisa wa Ifakara alikuwa anataka chochote? Hapa lawama ni lazima tulaumu kwa sababu baina ya afisa wa Ifakara na wale wa ubalozini lazima upande mmoja wao una makosa na kusababisha usumbufu kwa wageni. Na sioni unachotetea hapa, labda utuambie wewe ni mmojawao. Mambo kama haya ni very basic na AIBU KUBWA kwa taifa.
Kwanini u-conclude kosa liko liko kwa uhamiaji au afisa wa ifakara tu? Kwani mwombaji hawezi kuwa alitenda kosa la kufanya shughuli isiyoendana na visa yake? Huwezi kuja na conclusion za aina hii bila kusikiliza pande zote.
 
Ndugu wana JF huyo mzungu kutoka Amerika amekuja kwa short vist katika tasisi fulani hapo Ifakara na hafanyi kazi yoyote ile.Anaagalia wenzeke wamefanikiwa vipi katki utafiti wa malaria hapo Ifakara.Ofisa uhamiahaji anakutana naye anaomba passport yake anamwambia wewe umepewe visa ambayo siyo lazima ulipe tena CTA mzungu anasema mimi nimeenda ubalozini nikaaambia nataka kwenda Ifakara kwa hiyo vist akagongewa visa kafiak Ifakara.Afisa uhamiaji anambiwa mimi sikuambiwa kama kuna malipo yoyote hapo Tanzania je kwa nini nilipe tena?Afisa uhamiaji anampleka polisi lakini baadae anachiwa je huyu mgeni anakosa gani?Kwa nini afisa uhamiaji asifike kwa wenji wake na kuwapa maelezo?Na kisa cha kwenda polisi ni baada ya kuombwa kitu kidogo na kukataa na baadae polisi afisi uhamiajia anasema jaamaa kamkataza kufanya kazi yake kwa makudi no nd maellezo aliyoandika polisi huyo jamaa wa Uhamiaji
 
Back
Top Bottom