Virusi vya Corona: Waandamanaji wataka marufuku ya kutokutoka nje iondoshwe Marekani kufungua uchumi

Sandiego

JF-Expert Member
Dec 18, 2018
1,289
2,076
Waandamanaji nchini Marekani wameingia mitaani katika majimbo kadhaa wakishinikiza magavana kufungua uchumi wa majimbo yao kwa kuondosha amri ya kutokutoka nje ama 'lockdown'.
Marufuku hiyo ya kutokutoka nje imewekwa katika majombo yote ya Marekani ili kudhibiti kusambaa kwa janga la virusi vya corona, hali iliyotikisa uchumi wa taifa hilo kubwa zaidi kiuchumi duniani.
Maaandamano yameripotiwa jana Jumapili katika majimbo ya Arizona, Colorado, Montana na Washington, huku mwendelezo wa maandamano hayo ukitarajiwa leo Jumatatu.
Hasira juu ya marufuku hizo imeongezeka nchini humo huku waandamanaji wakitaka masharti yalegezwe licha ya hatari ambayo ingalipo ya maambukizi ya virusi vya corona.
Rais wa Marekani Donald Trump ameoesha dalili za kukubaliana na maandamano hayo.
Kwa sasa, Marekani ndiyo kitovu cha janga la ugonjwa wa virusi vya corona (Covid-19), kukiwa na wagonjwa zaidi ya 735,000 na vifo zaidi ya 40,000.
Hata hivyo kuna dalili kuwa maambukizi yanafikia kileleni nchini humo na kasi ya maambukizi kuanza kushuka katika baadhi ya majimbo.
Magavana katika majimbo mbalimbali wameanza majadiliano ya kufungua uchumi baada ya kushuhudiwa kupungua kwa maambukizi, lakini maeneo mengine bado yangali kwenye marufuku kali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hali ngumu huko,mafuta yamekufa Bei,corona inawamaliza,lockdown inaua uchumi,
Sasa kunaenda kutokea kitu,tujiandae tu,mchina tayari kaanza mazoezi ya kijeshi,Kuna Vita inaweza kutokea,tutizame Sana nchi tatu,China,Iran au venezuela
IMG_20200420_131457.png

Wapo tiari!!!!!!
 
Back
Top Bottom