Vipi kama hii itakuwa njama ya Mabeberu kuwajibisha Serikali hii?

Freewine

JF-Expert Member
Jan 7, 2018
257
212
Wazungu kwa miaka mingi sana wamekuwa wakinyonya serikali maskani za Afrika ikiwemo Tanzania bila kuona haya. Chanzo cha mzungu kuibia waafrka hakuji bahati mbaya ni mipango mathubuti iliyopangws na serikali zao kuhakikisha nchi maskani zinaendelea kuwa maskini.

Wazungu hawa hawajileti kwenye nchi yoyote bila kujua kuna kipi kizuri wanaenda kuvuna kwa wingi. Kwa sababu hawawezi kufika kwenye fursa moja kwa moja wanatumia viongozi wazawa kujiharalishia Neema ndani ya nchi hizi maskini.
Viongozi ndani ya nchi maskini wananeemeka kwa kuwapa wazungu hao utajiri wa nchi huku RAIA Wao wakibaki matopeni chakali kwa umaskini uliokithiri. Na hapo ndipo neno WAZUNGU walipoanzia kuitwa jina MABEBERU kwenye nchi hizi za kimaskini. Hii iliotokana na baadhi ya viongozi wazalendo na waaminifu kukataa kujihusisha na ulaghai huo unaofanywa na mataifa yenye nguvu.

Mahusiano bora baina ya nchi moja na nyingine ni jambo muhimu sana kwenye dunia hii Kwa sababu ndani ya nchi hizi kuna watu na lazima watu wote waishi kwa msingi ya utu na kuheshimiana. Ubaguzi wa aina yoyote unakatazwa na jamii zozote duniani kwa sababu dhambi ya ubaguzi na udhalilishaji hauishii kwa nao uliowabagua Bali husogea mpaka ndani kwako.

Wafirika tumekuwa tukilalamika sana juu ya Kuitwa NYANI kwenye nchi za wazungu, jambo huwakera wazungu wenyewe hata kufikia hatua ya kuwaadhibu mashabiki wa timu Fulani endapo itagundulika walifanya ubaguzi huo kwa mchezaji yoyote kutokea Afrika. Na baada ya adhabu huyo waafrika huwa tunafurahi kwamba haki imetendeka. Vipi kiongozi wa nchi anaposimama mbele ya media na kuitwa wazungu ni MABEBERU hivi Wao huwa wanajisikiaje?

(Ebu ona kwanza sifa za beberu, ni mbuzi dume ambaye anaharufu Kali sana, Silaa yake IPO kichwani na akitaka mapenzi badala ya mwanamke kulia lenyewe ndo linalia) hizi sifa sio nzuri ni matusi.

Wazungu wanafadhili hizi nchi za kimaskini mambo mengi mfano suala LA madawa ya ARVs na matibabu ya UKIMWI sio jambo LA mchezo kama serikali itatakiwa ilisimamie kwa asilimia 100. katika uliza uliza ndipo nikapata taarifa kuwa baadhi ya vituo vya afya havina ARVs za Watoto, Second line ARVs za wakubwa na pia kuna punguzo kubwa LA watumishi linaenda kutokea kuanzia Oct 2019 kutokana na mhisani kupunguza budget ya uendeshaji masuala us CTC. Sasa najiuliza au ndo beberu ameanza kuitingisha serikali hii au ni hisia tu.

Lakini Mimi sidhani kama kuna mzungu mbaya kama utaingia kwenye agreement na yenye huku una maarifa ya kutosha juu ya jambo Fulani. Masuala ya kuitana Mara sijui nyani, beberu au jiwe hayafai kabisa huo ni udhalilishaji wa watu wengine.

Tuwaheshimu wengine wakubwa kwa wadogo ili nasi tuheshimiwe
 
Wazungu Wako Sawa Kutuita Nyani, akili za Mwafrika za hovyo saana! Kunyanyasana wenyewe kwa wenyewe ndiyo Fahari ya Viongozi wetu. Kuwaita Beberu wao ni Sawa Kumwita Mtu mrefu Ngongoti, binafsi naona yote hii inachangiwa na Akili zetu pia Kuwaita hivyo hivyo tunazidi kujitwisha Mizigo.
Kama huyu Mzungu akitoa Mkono wake kwenye ARVs, hakika tutaokotwa kama Kuku wa kideli.
Halafu Jiwe ndiyo ametuharibia Nchi, anaamini kama wote waliomtangulia hawajafanya kitu na walikuwa na Makosa isipokuwa yeye Wakati Kinyume chake ndiyo Ukweli Wemyewe. 2020 Watanzania Msifanye Makosa, hata Kwa Blood muwe Tayari.
 
Mchawi wa mwafrika ni viongozi wa kiafrica. Wakishindwa kuwaletea watu wao maendeleo usingizia mabeberu, mbona nchi zingine zina endelea na zilitawaliwa kama sisi.
 
Nchi zote zilizo shirikiana na mabeberu zimeendelea si masikini tena check hongkong,Korea kusini,China,Malaysia, Taiwan.
 
Mkuu hapo kwenye ARVs umegusa panapo, Endapo wadau kama WRP wakijitoa kwenye Ufadhili wa dawa hizo tumekwisha. Tuombe ulichoandika kisiwe kweli maaana wengi wengi wetu hata ulichoandika hawakijui lkn ni nguzo muhimu sana kwa WAVIU.
 
Wazungu kwa miaka mingi sana wamekuwa wakinyonya serikali maskani za Afrika ikiwemo Tanzania bila kuona haya. Chanzo cha mzungu kuibia waafrka hakuji bahati mbaya ni mipango mathubuti iliyopangws na serikali zao kuhakikisha nchi maskani zinaendelea kuwa maskini.

Wazungu hawa hawajileti kwenye nchi yoyote bila kujua kuna kipi kizuri wanaenda kuvuna kwa wingi. Kwa sababu hawawezi kufika kwenye fursa moja kwa moja wanatumia viongozi wazawa kujiharalishia Neema ndani ya nchi hizi maskini.
Viongozi ndani ya nchi maskini wananeemeka kwa kuwapa wazungu hao utajiri wa nchi huku RAIA Wao wakibaki matopeni chakali kwa umaskini uliokithiri. Na hapo ndipo neno WAZUNGU walipoanzia kuitwa jina MABEBERU kwenye nchi hizi za kimaskini. Hii iliotokana na baadhi ya viongozi wazalendo na waaminifu kukataa kujihusisha na ulaghai huo unaofanywa na mataifa yenye nguvu.

Mahusiano bora baina ya nchi moja na nyingine ni jambo muhimu sana kwenye dunia hii Kwa sababu ndani ya nchi hizi kuna watu na lazima watu wote waishi kwa msingi ya utu na kuheshimiana. Ubaguzi wa aina yoyote unakatazwa na jamii zozote duniani kwa sababu dhambi ya ubaguzi na udhalilishaji hauishii kwa nao uliowabagua Bali husogea mpaka ndani kwako.

Wafirika tumekuwa tukilalamika sana juu ya Kuitwa NYANI kwenye nchi za wazungu, jambo huwakera wazungu wenyewe hata kufikia hatua ya kuwaadhibu mashabiki wa timu Fulani endapo itagundulika walifanya ubaguzi huo kwa mchezaji yoyote kutokea Afrika. Na baada ya adhabu huyo waafrika huwa tunafurahi kwamba haki imetendeka. Vipi kiongozi wa nchi anaposimama mbele ya media na kuitwa wazungu ni MABEBERU hivi Wao huwa wanajisikiaje?

(Ebu ona kwanza sifa za beberu, ni mbuzi dume ambaye anaharufu Kali sana, Silaa yake IPO kichwani na akitaka mapenzi badala ya mwanamke kulia lenyewe ndo linalia) hizi sifa sio nzuri ni matusi.

Wazungu wanafadhili hizi nchi za kimaskini mambo mengi mfano suala LA madawa ya ARVs na matibabu ya UKIMWI sio jambo LA mchezo kama serikali itatakiwa ilisimamie kwa asilimia 100. katika uliza uliza ndipo nikapata taarifa kuwa baadhi ya vituo vya afya havina ARVs za Watoto, Second line ARVs za wakubwa na pia kuna punguzo kubwa LA watumishi linaenda kutokea kuanzia Oct 2019 kutokana na mhisani kupunguza budget ya uendeshaji masuala us CTC. Sasa najiuliza au ndo beberu ameanza kuitingisha serikali hii au ni hisia tu.

Lakini Mimi sidhani kama kuna mzungu mbaya kama utaingia kwenye agreement na yenye huku una maarifa ya kutosha juu ya jambo Fulani. Masuala ya kuitana Mara sijui nyani, beberu au jiwe hayafai kabisa huo ni udhalilishaji wa watu wengine.

Tuwaheshimu wengine wakubwa kwa wadogo ili nasi tuheshimiwe
beberu ni beberu tu, mzungu ataendelea kuitwa beberu mpaka aache tabia ya kumnyonya mwafrika, hiyo laana ya utumwa na ukoloni itawafuata mpaka mambo ya balance, inatakiwa uamini ukoloni bado upo na bado unaendelea, na kwa sasa umepewa jina "ukoloni mamboleo". unamuhurumia asiitwe beberu lakini yeye hajawahi kufikiria kukuhurumia wala kuacha kukunyonya, ukitaka kuthiubitisha hilo jiulize kwamba kila siku vikao vya G8 vina agenda gani na third world country. unasema wanatusaidia madawa, swala la dawa wenyewe ndo wamekuja kuharibu kabisa natural medication ambazo zilikua zinamsaada mkubwa kuliko hizi dawa zinazo tangenezwa viwandani na kuwekewa preservatives.
pia ukumbuke mkuu kwamba ukoloni unaoendelea sa hivi ni nukoloni ambao hauko direct, white system inapambana na nchi masikini kisaikolojia sio tena straight battle. (mtazamo tu)
 
Freewine, hivi ulikuwa unaandika makala au kijarida? Na haya uliyoyaandika yanalisaidiaje taifa? Sidhani kama upon makini katika kupropagate kwani hoja zako ni dhaifu na hazishawishi!
Huko ccm MNA shida kubwa mno kwani kuna watu Wa upande mmoja in wapotoshaji mno tena wanafanya makusudi wakidhani wanakisaidia chama kumbe LA! Mfano mzuri in wewe unayewananga wafadhili wanaokusaidia hadi maji ya kunywa kijijini kwa kodi zao wewe na wenzako mnawabatiza kuwa mabeberu! Mbona michango na misaada yao hamuikatai? Acheni na punguzeni unafiki!
 
Freewine, hivi ulikuwa unaandika makala au kijarida? Na haya uliyoyaandika yanalisaidiaje taifa? Sidhani kama upon makini katika kupropagate kwani hoja zako ni dhaifu na hazishawishi!
Huko ccm MNA shida kubwa mno kwani kuna watu Wa upande mmoja in wapotoshaji mno tena wanafanya makusudi wakidhani wanakisaidia chama kumbe LA! Mfano mzuri in wewe unayewananga wafadhili wanaokusaidia hadi maji ya kunywa kijijini kwa kodi zao wewe na wenzako mnawabatiza kuwa mabeberu! Mbona michango na misaada yao hamuikatai? Acheni na punguzeni unafiki!
Bado cjaamua kuwa mwanachama wa chama chochote
 
Pesa mnazo kwanini hizo ARV msinunue badala yake mtegemee kuombaomba kusaidiwa?!
 
Wakuu naomba hapo chini tuweke
1. orodha ya nchi wahisani
2. Orodha ya nchi mabeberu.

Maana viongozi wa sirikali kupitia ccm wanatuchangaya sana.

Wakipewa misaada wanaziita nchi hizo marafiki/wahisani.

Wakiambiwa wazingatie utawala bora wa sheria wanaziita nchi hizo mabeberu.

NB : Ndugu wananchi wa Tanganyika tuache kuchagua vilaza wawe viongozi.
 
Back
Top Bottom