PreGE2025 Viongozi wangu wa Dini, Tanzania

PreGE2025 Viongozi wangu wa Dini, Tanzania

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Mushkov

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2024
Posts
546
Reaction score
1,114
Kumekuwa na msuguano mkali sana kati serikali iliyopo madarakani na Vyama vya Upinzani. Vyama vya Upinzani vimekuwa vikilalamika kuwa vimehujumiwa sana hasa kwenye chaguzi za mwaka 2019, 2020 na 2024. Kutokana na upande wa serikali kutotaka kukaa pamoja na Vyama vya Upinzani na kuzimaliza tofauti zao, baadhi ya vyama hivyo vya Upinzani vimeanzisha vuguvugu la kulazimisha mabadiliko. Pamoja na hayo, serikali bado haijaona umuhimu wa kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao.

OMBI LANGU KWENU viongozi wa Dini ni kwamba, ebu fanyeni utaratibu. Waiteni viongozi wa serikali kwa upande mmoja na upande mwingine viongozi wa vyama vya Upinzani. Ninyi mkiwa kama wapatanishi wakuu, toeni nafasi kwa kila upande kueleza dukuduku zake zote kisha jipeni muda ili kuchambua kwa kina maelezo ya kila upande, na mwishowe toeni majibu bila kupendelea upande wowote na yasimamieni makubaliano ya hizo pande mbili.
Nafikiri kwa kufanya hivyo mtakuwa mmetimiza wajibu wenu vizuri sana na Mungu atawabariki.

Ifahamike kuwa, tukiacha hizi pande kutunishiana misuli bila kusuluhisha, ipo siku hakutakuwa tena na fursa hiyo ya kuzikutanisha pande hizo kwa sababu maji yatakuwa yameshamwagika tayari.
Nawasilisha.
 
Serikali haina ugomvi na vyama vya siasa, chadema ndo wana ugomvi na CCM na Sasa wameamua hawatashiriki uchaguzi kwa kauli mbiu ya No reform, no elections.
Vyama vingine vingi havina ugomvi na CCM na vitashiriki uchaguzi.
Rai yangu ni Bora vyama vichache vishiriki uchaguzi kuliko utitiri wa vyama ambavyo havina hata dalili ya kupata 5%.
 
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliharibiwa kwa makusudi, na Samia amekiri jana.

Kwahiyo basi huo Uchaguzi ni batili urudiwe tena baada ya kupatikana Tume HURU ya Uchaguzi.

NO REFORMS NO ELECTION LINDA DEMOKRASIA
 
Kumekuwa na msuguano mkali sana kati serikali iliyopo madarakani na Vyama vya Upinzani. Vyama vya Upinzani vimekuwa vikilalamika kuwa vimehujumiwa sana hasa kwenye chaguzi za mwaka 2019, 2020 na 2024. Kutokana na upande wa serikali kutotaka kukaa pamoja na Vyama vya Upinzani na kuzimaliza tofauti zao, baadhi ya vyama hivyo vya Upinzani vimeanzisha vuguvugu la kulazimisha mabadiliko. Pamoja na hayo, serikali bado haijaona umuhimu wa kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao.

OMBI LANGU KWENU viongozi wa Dini ni kwamba, ebu fanyeni utaratibu. Waiteni viongozi wa serikali kwa upande mmoja na upande mwingine viongozi wa vyama vya Upinzani. Ninyi mkiwa kama wapatanishi wakuu, toeni nafasi kwa kila upande kueleza dukuduku zake zote kisha jipeni muda ili kuchambua kwa kina maelezo ya kila upande, na mwishowe toeni majibu bila kupendelea upande wowote na yasimamieni makubaliano ya hizo pande mbili.
Nafikiri kwa kufanya hivyo mtakuwa mmetimiza wajibu wenu vizuri sana na Mungu atawabariki.

Ifahamike kuwa, tukiacha hizi pande kutunishiana misuli bila kusuluhisha, ipo siku hakutakuwa tena na fursa hiyo ya kuzikutanisha pande hizo kwa sababu maji yatakuwa yameshamwagika tayari.
Nawasilisha.

Ccm haina Cha kitu cha kupoteza kwa Sasa isipokuwa Wapinzani ndio ambao wanayo ya kupoteza kutokana na kuwepo kwa Katiba mbaya inayakandamiza Haki zao. Hivyo, hata Kama watakutanishwa ili kupatanishwa Kamwe hapatakuwa na matokeo yoyote yale ya maana yatakayopatikana kwa sababu Ccm itagomea kurekebisha kasoro zilizopo kwenye Katiba ambazo ndiyo kiini cha kuwepo kwa misuguano Kati yao.
Ili kuhakikisha kwamba kunakuwepo na Mjadala wa Upatinishi wenye kuleta matunda mazuri kwa pande hizo zote ni kwa kuifanya Ccm nayo iathirike au iwe inapoteza kitu fulani sawasawa na hali jinsi ilivyo kwa Washindani wao wa kisiasa. Kwa kufanya hivyo, ndipo muafaka wenye manufaa kwao pande zote unaweza ukapatikana.
 
Kumekuwa na msuguano mkali sana kati serikali iliyopo madarakani na Vyama vya Upinzani. Vyama vya Upinzani vimekuwa vikilalamika kuwa vimehujumiwa sana hasa kwenye chaguzi za mwaka 2019, 2020 na 2024. Kutokana na upande wa serikali kutotaka kukaa pamoja na Vyama vya Upinzani na kuzimaliza tofauti zao, baadhi ya vyama hivyo vya Upinzani vimeanzisha vuguvugu la kulazimisha mabadiliko. Pamoja na hayo, serikali bado haijaona umuhimu wa kukaa pamoja na kumaliza tofauti zao.

OMBI LANGU KWENU viongozi wa Dini ni kwamba, ebu fanyeni utaratibu. Waiteni viongozi wa serikali kwa upande mmoja na upande mwingine viongozi wa vyama vya Upinzani. Ninyi mkiwa kama wapatanishi wakuu, toeni nafasi kwa kila upande kueleza dukuduku zake zote kisha jipeni muda ili kuchambua kwa kina maelezo ya kila upande, na mwishowe toeni majibu bila kupendelea upande wowote na yasimamieni makubaliano ya hizo pande mbili.
Nafikiri kwa kufanya hivyo mtakuwa mmetimiza wajibu wenu vizuri sana na Mungu atawabariki.

Ifahamike kuwa, tukiacha hizi pande kutunishiana misuli bila kusuluhisha, ipo siku hakutakuwa tena na fursa hiyo ya kuzikutanisha pande hizo kwa sababu maji yatakuwa yameshamwagika tayari.
Nawasilisha.
Hakuna muda huo kwa sasa hivi. Muda uliopo ni wa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu kwa taratibu ambazo vyama vingi vya siasa nchini viliuridhia.
 
Hakuna muda huo kwa sasa hivi. Muda uliopo ni wa maandalizi ya Uchaguzi Mkuu kwa taratibu ambazo vyama vingi vya siasa nchini viliuridhia.

Waridhiaji wa kupitishwa kwa Taratibu, Sheria, Kanuni na Katiba ya nchi katika nchi yoyote ile ni Wananchi wengi zaidi waliopo katika nchi husika. Na Katiba ya nchi ikiwa Kama ni Muongozo Mkuu kabisa katika kuendelesha shughuli zote katika Nchi.
Je, ni Wananchi gani hasa katika nchi hii waliipigia Kura za ndiyo na kuipitisha Katiba hii iliyopo hivi sasa hapa Tanzania???
 
Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliharibiwa kwa makusudi, na Samia amekiri jana.

Kwahiyo basi huo Uchaguzi ni batili urudiwe tena baada ya kupatikana Tume HURU ya Uchaguzi.

NO REFORMS NO ELECTION LINDA DEMOKRASIA

..uchaguzi wa serikali za mitaa kuharibiwa ni dalili mbaya sana.

..Uchaguzi ule uliharibiwa na Wizara ya Tamisemi iliyoko ktk Ofisi ya Raisi.

..Kikatiba RAISI ndiye Waziri wa Tamisemi, hivyo anawajibika moja kwa moja na uharibifu uliotokea.

..sasa mhusika aliyeharibu uchaguzi serikali za mitaa bado anang'ang'ania mamlaka ya kuumiliki mfumo mzima wa uchaguzi mkuu.

..Ni afadhali uchaguzi wa serikali za mitaa ungekuwa mzuri, angalau watu wangejenga imani kwenda ktk uchaguzi mkuu kwa mifumo iliyopo.

..No Reforms No Elections imelazimishwa na matendo ya Samia Suluhu akishirikiana na Mohamed Mchengerwa.
 
Kuna haja ya kuendesha opersheni ya kuwakataa viongozi wote wa dini wanaoshabiki uchawa wa kifara
Wakiongozwa na mufti njaa ,anayejali zaidi tumbo lake
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Ccm haina Cha kitu cha kupoteza kwa Sasa isipokuwa Wapinzani ndio ambao wanayo ya kupoteza kutokana na kuwepo kwa Katiba mbaya inayakandamiza Haki zao. Hivyo, hata Kama watakutanishwa ili kupatanishwa Kamwe hapatakuwa na matokeo yoyote yale ya maana yatakayopatikana kwa sababu Ccm itagomea kurekebisha kasoro zilizopo kwenye Katiba ambazo ndiyo kiini cha kuwepo kwa misuguano Kati yao.
Ili kuhakikisha kwamba kunakuwepo na Mjadala wa Upatinishi wenye kuleta matunda mazuri kwa pande hizo zote ni kwa kuifanya Ccm nayo iathirike au iwe inapoteza kitu fulani sawasawa na hali jinsi ilivyo kwa Washindani wao wa kisiasa. Kwa kufanya hivyo, ndipo muafaka wenye manufaa kwao pande zote unaweza ukapatikana.
Nimekuelewa vyema.
Wakiongozwa na mufti njaa ,anayejali zaidi tumbo lake
Mimi nilipokuwa nikimwona huko nyuma nilidhani ni mtu mmoja wa maana sana, kumbe hamna kitu kabisa
 
Waridhiaji wa kupitishwa kwa Taratibu, Sheria, Kanuni na Katiba ya nchi katika nchi yoyote ile ni Wananchi wengi zaidi waliopo katika nchi husika. Na Katiba ya nchi ikiwa Kama ni Muongozo Mkuu kabisa katika kuendelesha shughuli zote katika Nchi.
Je, ni Wananchi gani hasa katika nchi hii waliipigia Kura za ndiyo na kuipitisha Katiba hii iliyopo hivi sasa hapa Tanzania???
Katiba ya Marekani ilipigiwa kura na Wamarekani wangapi? Katiba ya Uingereza ilipigiwa kura na Waingereza wangapi? Usilete ujuaji usioujua!
 
Back
Top Bottom