Viongozi wa UKAWA leteni ufafanuzi kwa hili linaloendelea jimbo la MTAMA

Livejr

JF-Expert Member
Feb 6, 2014
2,068
2,792
Habarini za jion wanajukwaa...!

Naombeni viongozi wa UKAWA taifa pamoja na wale wa Kanda kulitatua hali ya sintofahamu kwa watu wa jimbo la Mtama.

Kwa kifupi ni aliyekuwa mgombea wa Ccm kabla ya Kura za maoni ndg Selemani Methew Luwongo baada kukosa Kura za maoni kupitia Ccm hatimaye alitangaza kuwa atahamia Act-Wazalendo siku ya trh 10/08/2015 lakin jambo la kushangaza alikuja Mtama trh 11/08/2015 na kutangaza kuwa maamuzi ya Kuhamia Act-Wazalendo atayafanya trh 14/08/2015 baada majina kutoka ya wagombea Ubunge kupitia CCM.

Trh 15/08/2015 aliamua Kuhamia CHADEMA na kuikacha Act-Wazalendo Hilo halikuwa tu jambo la kushangaza lakini pia liliwashtua baadhi ya wafuasi wake.

Baada ya Kuhamia CHADEMA huyu jamaa anamlazimisha mgombea Ubunge kupitia CUF ndg Mchinjita amuachie nafasi huku akisema kuwa katumwa na mamlaka ya juu, jamaa alipoona ndg Mchinjita anaweka ngumu akaanza kueneza Habari za uongo kwa wanamtama kuwa Mchinjita ni kambi ya Membe na kusema kuwaambia wanamtama kuwa trh 16/08/2015 angekuja ndg Godbless Lema na Freddy Lowassa kuzungumza na Mchinjita ili ikiwezekana Mchinjita apewe pesa aache jimbo. Huu ni uzushi na uongo aliousema ndg Selemani Methew Luwongo kwa wananchi wa Mtama.

Kilichonisukuma kuandika haya ni kitendo alichokifanya ndg Selemani Methew Luwongo leo trh 18/08/2015 kuamua kuja kufanya mkutano wa hadhara na kutangaza kuwa anachukua fomu ya Ubunge na jumapili anaanza kampeni pia mwenyekiti wa wilaya ndg Chikawe kutangaza hadharani kuwa kusini hapa jimbo la Mtama hakuna Ukawa hivyo kumuambia ndg Selemani Methew Luwongo achukue fomu.

Wanaukawa tunaenda wapi huku mbona tumeshamla ng'ombe mzima bado mkia tu...? Ndg Maalim Seif nasikia leo ulikuwa Mchinga nakuomba ututembelee Mtama uje utoe ufafanuzi na kama hapa mtama hakuna Ukawa naomba utuambie.
 
Huyo aliyeshindwa na Nape kwa goli la mkono inatakiwa awe mpole kama hao wana CCM wanampenda sana wangempigia kura kwa wingi na kulinda akashinda sio kuja UKAWA na kuwavuruga wapiga kura
 
Jimbo la Mtama kwamjibu wa maamuzi ya UKAWA limekabidhiwa kwa CUF, Hivyo ni busara na hekima kwa uongozi wa Chadema Mtama kuheshimu maamuzi ya Ukawa,

Mimi namshauri kamanda Selemani Methew kama anawafuasi wengi ajiunge Cuf, na Hingozi wa CUF bila kushurutishwa "kama wataona anafaa", watampa nafasi hiyo kwakufuata taratibu za chama hicho!

Tunahitaji hekima na busara sana ili kuvuka kiunzi hiki, hizo ndio changamoto na gharama za kuing'oa ccm, tukubali kupata na kukosa ili ccm itoke kwanza!

Ikishindikaka kwa kamanda Selemani Methew kujiunga Cuf, ni bora amuunge mkono mgombea wa Cuf na apigane kwelikweli mpaka ahakikishe mwanaukawa huyo anashinda!

UKAWA ipo nchi nzima hilo lieleweke wazi kila ulipokanyaga pana UKAWA.
 
Mchinjita kuachia jimbo kwa ajili ya mwanaCCM aliyekatwa itakuwa ujinga wa hali ya juu.

Mchinjita amepoteza wakati mwing sana kulishinda jimbo la Mtama.
Ametumia pesa nying sana tena pesa nyngne ni za shule halafu aje mtu kutoka kusikojulikana aliache jimbo? Noo. Mchinjita amekuwa akituachia mzigo mkubwa wa kuendesha shule wakati yeye akiwa hukn kwenye harakati za CCM then umuambie aachie jimbo? Haliwezekani na hawezi kukubali.
 
Habarini za jion wanajukwaa...!

Naombeni viongozi wa UKAWA taifa pamoja na wale wa Kanda kulitatua hali ya sintofahamu kwa watu wa jimbo la Mtama.

Kwa kifupi ni aliyekuwa mgombea wa Ccm kabla ya Kura za maoni ndg Selemani Methew Luwongo baada kukosa Kura za maoni kupitia Ccm hatimaye alitangaza kuwa atahamia Act-Wazalendo siku ya trh 10/08/2015 lakin jambo la kushangaza alikuja Mtama trh 11/08/2015 na kutangaza kuwa maamuzi ya Kuhamia Act-Wazalendo atayafanya trh 14/08/2015 baada majina kutoka ya wagombea Ubunge kupitia CCM.

Trh 15/08/2015 aliamua Kuhamia CHADEMA na kuikacha Act-Wazalendo Hilo halikuwa tu jambo la kushangaza lakini pia liliwashtua baadhi ya wafuasi wake.

Baada ya Kuhamia CHADEMA huyu jamaa anamlazimisha mgombea Ubunge kupitia CUF ndg Mchinjita amuachie nafasi huku akisema kuwa katumwa na mamlaka ya juu, jamaa alipoona ndg Mchinjita anaweka ngumu akaanza kueneza Habari za uongo kwa wanamtama kuwa Mchinjita ni kambi ya Membe na kusema kuwaambia wanamtama kuwa trh 16/08/2015 angekuja ndg Godbless Lema na Freddy Lowassa kuzungumza na Mchinjita ili ikiwezekana Mchinjita apewe pesa aache jimbo. Huu ni uzushi na uongo aliousema ndg Selemani Methew Luwongo kwa wananchi wa Mtama.

Kilichonisukuma kuandika haya ni kitendo alichokifanya ndg Selemani Methew Luwongo leo trh 18/08/2015 kuamua kuja kufanya mkutano wa hadhara na kutangaza kuwa anachukua fomu ya Ubunge na jumapili anaanza kampeni pia mwenyekiti wa wilaya ndg Chikawe kutangaza hadharani kuwa kusini hapa jimbo la Mtama hakuna Ukawa hivyo kumuambia ndg Selemani Methew Luwongo achukue fomu.

Wanaukawa tunaenda wapi huku mbona tumeshamla ng'ombe mzima bado mkia tu...? Ndg Maalim Seif nasikia leo ulikuwa Mchinga nakuomba ututembelee Mtama uje utoe ufafanuzi na kama hapa mtama hakuna Ukawa naomba utuambie.


Mambo aliyaanza Lowasa, kutoka CCM na moja kwa moja kupewa nafasi ya kugombea urais. Kwanini hilo lisiwe halali kwa wabunge? Kuwa ukitoka CCM wewe ndio bora na wale wa Ukawa inabidi wakae pembeni.

Big up Suleyman. Mpaka uchukue jimbo isitoshe una wakubwa wote wenye pesa, maana Chadema a.ka. UKAWA ukiwa na pesa tu yabidi wengine wakupishe.
 
Kama Mathew amejiunga Chadema basi anatakiwa amuunge mkono mgombea wa CUF ambaye ndiye anabeba bendera ya Ukawa kwenye jimbo hilo la Mtama.
 
Inatakiwa Ndg Mathew awe mpole naamini tangu akiwa huko CCM alijua kwamba upande huu kuna kuachiana majimbo....So alipaswa kuwa mfuatiliaji mambo hata km alikuwa CCM isingemsumbua kujua ahamie chama gani vinginevyo Atapuuzwa chakufanya awekeze Nguvu kumsaidia huyo Jamaa wa CUF kushinda hiyo nafasi.....Ukawa sio yakugawa vyeo ila kugawana majukumu
 
Mambo aliyaanza Lowasa, kutoka CCM na moja kwa moja kupewa nafasi ya kugombea urais. Kwanini hilo lisiwe halali kwa wabunge? Kuwa ukitoka CCM wewe ndio bora na wale wa Ukawa inabidi wakae pembeni.

Big up Suleyman. Mpaka uchukue jimbo isitoshe una wakubwa wote wenye pesa, maana Chadema a.ka. UKAWA ukiwa na pesa tu yabidi wengine wakupishe.

Kama ana pesa aende Act-Wazalendo akagombee sio kuleta vurugu kwa wanamtama
 
Lililo la msingi wakubaliane yule anayekubalika amuachie mwenzake kwa maslahi mapana ya Ukawa.
 
Habarini za jion wanajukwaa...!

Naombeni viongozi wa UKAWA taifa pamoja na wale wa Kanda kulitatua hali ya sintofahamu kwa watu wa jimbo la Mtama.

Kwa kifupi ni aliyekuwa mgombea wa Ccm kabla ya Kura za maoni ndg Selemani Methew Luwongo baada kukosa Kura za maoni kupitia Ccm hatimaye alitangaza kuwa atahamia Act-Wazalendo siku ya trh 10/08/2015 lakin jambo la kushangaza alikuja Mtama trh 11/08/2015 na kutangaza kuwa maamuzi ya Kuhamia Act-Wazalendo atayafanya trh 14/08/2015 baada majina kutoka ya wagombea Ubunge kupitia CCM.

Trh 15/08/2015 aliamua Kuhamia CHADEMA na kuikacha Act-Wazalendo Hilo halikuwa tu jambo la kushangaza lakini pia liliwashtua baadhi ya wafuasi wake.

Baada ya Kuhamia CHADEMA huyu jamaa anamlazimisha mgombea Ubunge kupitia CUF ndg Mchinjita amuachie nafasi huku akisema kuwa katumwa na mamlaka ya juu, jamaa alipoona ndg Mchinjita anaweka ngumu akaanza kueneza Habari za uongo kwa wanamtama kuwa Mchinjita ni kambi ya Membe na kusema kuwaambia wanamtama kuwa trh 16/08/2015 angekuja ndg Godbless Lema na Freddy Lowassa kuzungumza na Mchinjita ili ikiwezekana Mchinjita apewe pesa aache jimbo. Huu ni uzushi na uongo aliousema ndg Selemani Methew Luwongo kwa wananchi wa Mtama.

Kilichonisukuma kuandika haya ni kitendo alichokifanya ndg Selemani Methew Luwongo leo trh 18/08/2015 kuamua kuja kufanya mkutano wa hadhara na kutangaza kuwa anachukua fomu ya Ubunge na jumapili anaanza kampeni pia mwenyekiti wa wilaya ndg Chikawe kutangaza hadharani kuwa kusini hapa jimbo la Mtama hakuna Ukawa hivyo kumuambia ndg Selemani Methew Luwongo achukue fomu.

Wanaukawa tunaenda wapi huku mbona tumeshamla ng'ombe mzima bado mkia tu...? Ndg Maalim Seif nasikia leo ulikuwa Mchinga nakuomba ututembelee Mtama uje utoe ufafanuzi na kama hapa mtama hakuna Ukawa naomba utuambie.

Hili jambo ni serious uongozi wa juu wa CHADEMA haraka uzime uasi huu kabla ya kesho, Methew kadandania gari sahihi ila kakosea route awe mpole tu
cc. Mnyika, Sakaya
 
Jimbo la Mtama kwamjibu wa maamuzi ya UKAWA limekabidhiwa kwa CUF, Hivyo ni busara na hekima kwa uongozi wa Chadema Mtama kuheshimu maamuzi ya Ukawa,

Mimi namshauri kamanda Selemani Methew kama anawafuasi wengi ajiunge Cuf, na Hingozi wa CUF bila kushurutishwa "kama wataona anafaa", watampa nafasi hiyo kwakufuata taratibu za chama hicho!

Tunahitaji hekima na busara sana ili kuvuka kiunzi hiki, hizo ndio changamoto na gharama za kuing'oa ccm, tukubali kupata na kukosa ili ccm itoke kwanza!

Ikishindikaka kwa kamanda Selemani Methew kujiunga Cuf, ni bora amuunge mkono mgombea wa Cuf na apigane kwelikweli mpaka ahakikishe mwanaukawa huyo anashinda!

UKAWA ipo nchi nzima hilo lieleweke wazi kila ulipokanyaga pana UKAWA.

Maelezo yako ni mazuri, ila huyu jamaa anachotaka yeye siyo kumuunga mtu mwengine mkono, bali anataka yeye mwenyewe binafsi ndio awe mgombea. Yaani viongozi wa namna hii wanaonekana ni wabinafsi sana na kwa kweli hawafai.
 
Lililo la msingi wakubaliane yule anayekubalika amuachie mwenzake kwa maslahi mapana ya Ukawa.

Tatizo ubinafsi ndugu, na hata ukiangalia wengi waliokimbilia UKAWA ni wale wabinafsi kupitiliza kwa hiyo UKAWA inatakiwa iwe makini na hawa watu wanaowapokea.
 
Yap ukiwachunguza wengi wanaenda kwa maslahi ya madaraka na hili Ukawa wanatakiwa wawe nalo makini sana.
 
Huyo ni pandikizi la Nape, ameletwa makusudi kuvuruga UKAWA ili lile bao la mkono lisiishie bafuni. Tafakari, chukua hatua::rolleyes:
 
Makamanda msipanic viongoz wetu watalishugulikia changamoto ndogo sana, nahis kuna upotoshwaji wa taarifa. Haiingii akilini eti mtu ahamie chama leo alafu alete ubabe labda kama ni kichaa na wenyeji ni vichaa zaidi.
 
Back
Top Bottom