GE2025 Viongozi wa Kimasai Wamuunga Mkono Rais Samia kuendelea kuongoza miaka mitano ijayo

GE2025 Viongozi wa Kimasai Wamuunga Mkono Rais Samia kuendelea kuongoza miaka mitano ijayo

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,437
Reaction score
5,235
Viongozi wa jamii ya kimasai nchini (Malaigwanani) wametoa msimamo wao wa kumchagua tena rais Dkt.Samia Suluhu Hassan kuendelea kuongoza nchi kwa miaka mitano ijayo kutokana na utendaji kazi wake.

Akizungumza baada ya kikao kilichowakutanisha viongozi hao kutoka Siha na Longido, mwenyekiti wa Malaigwanan Tanzania, Joseph Ole Paserian amesema jamii hiyo imeridhishwa na kazi zilizofanywa na Rais Samia na hivyo watahakikisha wanahamasishana ili wanajamii wa kimasai wajitokeze kupiga kura kumchagua Rais Samia.

Aidha katika kikao hicho pia wameiomba serikali kupitia Kampuni ya ranchi za taifa (NARCO) kurudisha kwa jamii hiyo eneo ambalo walikua wakitumia kwa malisho kabla ya kupewa mwekezaji jambo ambalo linawaweka katika hatari ya kukosa malisho ya mifugo.
 
Tulidhani huu upuuzi umeisha kumbe ndio kwanza unaota mbawa
 
Back
Top Bottom