Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 141,548
- 284,049
Ujumbe wa Vigogo wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) umewasili Nchini Ubelgiji kutokea Ujerumani , Chadema chama cha siasa kinachotajwa kuwa Maarufu zaidi Barani Africa kwa sasa , huku kikitajwa kwamba kinaendesha shughuli zake kwa njia ya Kisasa zaidi , kiko kwenye ziara ya kikazi Barani Ulaya .
Ujumbe wa Chadema unaoongozwa na Makamu Mwenyekiti Mh Tundu Lissu , umefika kwenye Kituo cha Usimamizi wa Sera na Maendeleo cha Barani Ulaya (ECDPM) na kuzungumza na maofisa wake , Ujumbe huo pia Umetembelea Mtandao wa vyama vya siasa wa Barani Ulaya (ENoP) na kukutana na maofisa wake , Pia Ujumbe huu wa Chadema umefika kwenye Wizara ya Mambo ya nje ya Ubelgiji na kuzungumza na Waziri na Maofisa wa Wizara hiyo .
Lengo la Ziara hii kabambe ni kuchagiza Msukumo wa Demokrasia ya vyama vingi nchini Tanzania , ambako Jumuiya ya Kimataifa inaombwa kuilazimisha Serikali ya Tanzania kuheshimu Katiba ya Nchi , kwa kuachia Mikutano ya hadhara na Maandamano , ikiwa ni pamoja na kuendeleza Mchakato wa Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya 2025 . Chadema imestukia mchezo mchafu unaoandaliwa na Watawala kuelekea 2025.
Unaweza ukashang'aa na kujiuliza sababu hasa za Chadema kwenda Ulaya kwa ajili ya Mambo haya , Ni hivi , Wazungu ndio Wafadhili wa Nchi za kiafrica , na hasa hizi nchi masikini kama Tanzania , wakikohoa tu hakuna wa kuleta fyokofyoko , na hasa kwa nchi zinazoomba misaada sana kama ilivyo Tanzania , ambapo inafika wakati viongozi wote wa juu wanatawanyika duniani kuomba misaada .
Kwa Mfano , Viongozi wa Tanzania walipanga kwa dhati kabisa , tena bila Haya , kumfunga Maisha Gerezani Freeman Mbowe kwa kesi ya Uongo , lakini baada ya Wazungu kuingilia kati , Mbowe na wenzake waliachiwa bila masharti yoyote.
Ujumbe wa Chadema unaoongozwa na Makamu Mwenyekiti Mh Tundu Lissu , umefika kwenye Kituo cha Usimamizi wa Sera na Maendeleo cha Barani Ulaya (ECDPM) na kuzungumza na maofisa wake , Ujumbe huo pia Umetembelea Mtandao wa vyama vya siasa wa Barani Ulaya (ENoP) na kukutana na maofisa wake , Pia Ujumbe huu wa Chadema umefika kwenye Wizara ya Mambo ya nje ya Ubelgiji na kuzungumza na Waziri na Maofisa wa Wizara hiyo .
Lengo la Ziara hii kabambe ni kuchagiza Msukumo wa Demokrasia ya vyama vingi nchini Tanzania , ambako Jumuiya ya Kimataifa inaombwa kuilazimisha Serikali ya Tanzania kuheshimu Katiba ya Nchi , kwa kuachia Mikutano ya hadhara na Maandamano , ikiwa ni pamoja na kuendeleza Mchakato wa Katiba mpya na Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya 2025 . Chadema imestukia mchezo mchafu unaoandaliwa na Watawala kuelekea 2025.
Unaweza ukashang'aa na kujiuliza sababu hasa za Chadema kwenda Ulaya kwa ajili ya Mambo haya , Ni hivi , Wazungu ndio Wafadhili wa Nchi za kiafrica , na hasa hizi nchi masikini kama Tanzania , wakikohoa tu hakuna wa kuleta fyokofyoko , na hasa kwa nchi zinazoomba misaada sana kama ilivyo Tanzania , ambapo inafika wakati viongozi wote wa juu wanatawanyika duniani kuomba misaada .
Kwa Mfano , Viongozi wa Tanzania walipanga kwa dhati kabisa , tena bila Haya , kumfunga Maisha Gerezani Freeman Mbowe kwa kesi ya Uongo , lakini baada ya Wazungu kuingilia kati , Mbowe na wenzake waliachiwa bila masharti yoyote.