Kyaiyembe
JF-Expert Member
- Dec 1, 2011
- 1,706
- 665
Ritz it's all about division of labour!.Wanaukumbi,
Ni vizuri Watanzania wote tuwe na ujasiri wa kuwaambia ukweli hawa ndugu zetu wa Chadema, ukiangalia hali ya kisiasa ndani ya Chadema utaona kabisa baadhi ya viongozi wa Chadema hawana dhamira nzuri baada ya kuteka madaraka ya chama.
Kuna kikundi cha watu wanne tu ndani ya Chadema ndiyo wenye nguvu ya kuiendesha Chadema, katika utendaji wake wa kila siku, Dr Slaa, Freeman Mbowe, Godbless Lema, John Mnyika.
Kuna wabunge wa Chadema pamoja na viongozi wa Chadema hawa wanaonekana tu kwenye ukumbi wa bunge peke yake, hili kundi likipeleka M4C kwenye majimbo kwa ajili ya kuchangisha pesa M4C hawa wabunge huwa hawana nafasi yoyote ya kuhoji achilia mbali michango ya M4C.
Hebu tuwaangalie hawa wabunge kwa uchache majina yao na majimbo yao.
1) Salvatory Machemuli Jimbo la Ukwerewe.
2) Antony Mbasa Jimbo la Biharamulo.
3) John Shibuda Maswa Magharibi.
4) Syvester Kasulimbayi Mhoja Maswa Mashariki.
5) Mustaph Akonaay Mbulu.
6) David Silinde Mbozi Magharibi.
7) Zitto Kabwe Kigoma Kaskazini.
8) Said Arfi Mpanda Mjini.
Ukiangalia hawa viongozi wawili wa Chadema, Makamu Mwenyekiti Taifa Said Arfi, hawajahi kufanya kazi za chama, Mbowe akisafiri anamuachia ofisi John Mnyika, Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe, naye ana miaka mingi hajawahi kufanya kazi za chama kiofisi, Dr Slaa akisafiri anamuachia ofisi John Mnyinka.
Last edited by a moderator: