lawyer lawyer
Senior Member
- Jul 29, 2012
- 145
- 37
Wazee washauri wa CHADEMA mpo?mmejificha wapi? Jitokezeni muwashauri hawa viongozi, ni wazi wameamua kutumia suala la bandari kama kichaka chao cha kupiga fedha za chama. Kwanini?
1. Kwa makusudi wameamua kutumia nguvu isiyo sahihi kuikosoa serikali iliopo madarakani.
2. Gharama wanazozitumia kuzunguka nchi haziendani na fedha walizo nazo.
Ninachokiona hawa viongozi wameamua kutumia bandari kugawana fedha zenu kwa njia ya posho, haiwezekani hili swala la bandari wakalifanya kubwa hivi. Hapa kuna upigaji unaoendelea.
CHADEMA bado ni chama kidogo sana. Kinapaswa kujikita kwenye kujijenga kwanza, nchi hii hatuwezi kuwapa watu kama wao. Hizo gharama mnazozitumia kuzunguka nchi zitumieni kujenga rasilimali watu ili mtakapo fika kwenye uchaguzi na nyie muwe na watu ambao watakuwa na elimu na sifa sawa na wagombea wanaotoka CCM, na sio kuweka hao ambao hawatoshi kwenye sifa kuchuana na wagombea wa upande wa pili.
Jikiteni kwenye kusomesha watu wenu na sio kula ada zao kwa kuzunguka nchi kuikosoa serilikali ambayo imewapa mpaka nafasi ya kufungua shauri mahakamani. Kama kweli mnauchungu na nchi hii, acheni hayo mnayo yafanya, hizo ni pesa za wanachama wenu mnazipiga kwa mgongo wa bandari.
Mama na Serikali yake wameisha wa sikia kuhusu ubovu wa mkataba. Mpeni nafasi afanyie kazi ushauri wenu. Acheni kumpigia kelele kiasi ashindwe kutawala. Pia inaonesha Rais aliye madarakani amefanya mazuri mengi na ndio maana hamna hoja zingine zaidi ya bandari ambayo kwa makusudi mmeamu kuigeuza kichaka cha kula michango na ruzuku kwa njia ya posho.
Mnao uwezo wa kuikosoa serikali na kuishauri hata kwanjia ya kuiandikia barua tu, sasa kwanini mnatumia njia yenye matumizi makubwa ya pesa hili hali nyie bado ni chama kidogo? Kuna upigaji hapa unaendelea wanachadema.
Kuweni makini na hawa jamaa. Vipi mahakama ikitoa uhamuzi wa kutengu huo mkataba, mtarudisha fedha mnazo zitumia kuzunguka nchi kuitukana serikali na viongozi waliotangulia? Vipi Mama Samia akifanyia kazi ushauri wenu kuhusu huo mkataba mtarudisha hizo fedha mnazolipana posho kuzunguka nchi?.
Serikali imeisha wasikia. Rudini sasa mkajenge chama chenu, hakina rasilimali watu wakuweza kushindana na wenzenu. Acheni kutumia pesa za chama vibaya. Wasomesheni wana bavicha kesho wawe kwenye ushindani. Wale wagombea wa kidato cha sita hawa wezi kupewa madaraka kwenye uchaguzi. Na nyie viongozi mnajua hili, ila mnafanya makusudi ili kujinufaisha nyie binafsi, acheni siasa za upotoshaji.
Viongozi CHADEMA mnapaswa kuchunguzwa matendo yenu kwani yanatia mashaka. Kuna janja janja mnaifanya kwenye swala la bandari kwa maslai yenu binafsi. Ilitosha kwa nyie kuiokosa na kuishauri serikali kwa njia ya barua au vyombo vya habari na kuipa nafasi ifanyie kazi maoni yenu.
1. Kwa makusudi wameamua kutumia nguvu isiyo sahihi kuikosoa serikali iliopo madarakani.
2. Gharama wanazozitumia kuzunguka nchi haziendani na fedha walizo nazo.
Ninachokiona hawa viongozi wameamua kutumia bandari kugawana fedha zenu kwa njia ya posho, haiwezekani hili swala la bandari wakalifanya kubwa hivi. Hapa kuna upigaji unaoendelea.
CHADEMA bado ni chama kidogo sana. Kinapaswa kujikita kwenye kujijenga kwanza, nchi hii hatuwezi kuwapa watu kama wao. Hizo gharama mnazozitumia kuzunguka nchi zitumieni kujenga rasilimali watu ili mtakapo fika kwenye uchaguzi na nyie muwe na watu ambao watakuwa na elimu na sifa sawa na wagombea wanaotoka CCM, na sio kuweka hao ambao hawatoshi kwenye sifa kuchuana na wagombea wa upande wa pili.
Jikiteni kwenye kusomesha watu wenu na sio kula ada zao kwa kuzunguka nchi kuikosoa serilikali ambayo imewapa mpaka nafasi ya kufungua shauri mahakamani. Kama kweli mnauchungu na nchi hii, acheni hayo mnayo yafanya, hizo ni pesa za wanachama wenu mnazipiga kwa mgongo wa bandari.
Mama na Serikali yake wameisha wa sikia kuhusu ubovu wa mkataba. Mpeni nafasi afanyie kazi ushauri wenu. Acheni kumpigia kelele kiasi ashindwe kutawala. Pia inaonesha Rais aliye madarakani amefanya mazuri mengi na ndio maana hamna hoja zingine zaidi ya bandari ambayo kwa makusudi mmeamu kuigeuza kichaka cha kula michango na ruzuku kwa njia ya posho.
Mnao uwezo wa kuikosoa serikali na kuishauri hata kwanjia ya kuiandikia barua tu, sasa kwanini mnatumia njia yenye matumizi makubwa ya pesa hili hali nyie bado ni chama kidogo? Kuna upigaji hapa unaendelea wanachadema.
Kuweni makini na hawa jamaa. Vipi mahakama ikitoa uhamuzi wa kutengu huo mkataba, mtarudisha fedha mnazo zitumia kuzunguka nchi kuitukana serikali na viongozi waliotangulia? Vipi Mama Samia akifanyia kazi ushauri wenu kuhusu huo mkataba mtarudisha hizo fedha mnazolipana posho kuzunguka nchi?.
Serikali imeisha wasikia. Rudini sasa mkajenge chama chenu, hakina rasilimali watu wakuweza kushindana na wenzenu. Acheni kutumia pesa za chama vibaya. Wasomesheni wana bavicha kesho wawe kwenye ushindani. Wale wagombea wa kidato cha sita hawa wezi kupewa madaraka kwenye uchaguzi. Na nyie viongozi mnajua hili, ila mnafanya makusudi ili kujinufaisha nyie binafsi, acheni siasa za upotoshaji.
Viongozi CHADEMA mnapaswa kuchunguzwa matendo yenu kwani yanatia mashaka. Kuna janja janja mnaifanya kwenye swala la bandari kwa maslai yenu binafsi. Ilitosha kwa nyie kuiokosa na kuishauri serikali kwa njia ya barua au vyombo vya habari na kuipa nafasi ifanyie kazi maoni yenu.