Viongozi kuwe waangalifu na nasaha mnazotoa kwa wale wanaoteuliwa

Bulesi

Platinum Member
May 14, 2008
14,211
13,726
Nilikuwa nasikiliza maelezo ya Viongozi wetu wa Taifa kwa wateuliwa wa Rais baada ya kula kiapo cha kazi zao. Moja ya mambo yaliyonishangaza ni pale Spika wa Bunge Mheshimiwa Job Ndugai aliposimama na kuwaasa majaji kuwa ni muhimu kwao kutenda haki pale wanapotoa maamuzi ya kesi watakazokwenda kuzisikiliza

Huo ulikuwa ni ushauri murua kabisa, tatizo kwangu likaja pale nilipokuwa natafakari juu ya maamuzi ambayo spika huyu wa Bunge letu amekuwa ameyafanya huko bungeni kama yanasahabihiana na ushauri alikuwa anawapa hao majaji?

Hebu tuchunguze moja ya maamuzi ambayo Spika Ndugai ameyatoa hapo bungeni hivi karibuni nalo ni lile linalohusu wabunge waliofukuzwa na chama chao kuruhusiwa kuendelea kuwa Bungeni. Katiba inatamka wazi kabisa kuwa mwananchi yeyote hawezi kuwa mbunge kama sio mwanachama wa chama cha Siasa. Hivyo kwa kuwakubalia wale wakina mama waliofukzwa na Chadema kuendelea kuwa Bungeni Ndugai anavunja katiba na hivyo hatendi haki. Kutenda haki maana yake ni kuheshimu na kulinda sheria za nchi!!

Kwanini Ndugai anavunja sheria ya nchi na hakuna hatua zozote zinazochukuliwa? Yote hii inatokana na TAASISI yetu ya Bunge kuwa DHAIFU. Kama Bunge letu lingekuwa imara , lingekuwa linaongozwa na Katiba na sheria ambazo Bunge hilo hilo limeapa kulinda na kutetea hayo yote yasingetokea na haki ingetendeka! Hivyo basi ili kuwa na Taasisi imara ni wazi kuwa Katiba iliyokubaliwa na wananchi ni lazima iheshimiwe.

OUR LEADERS MUST WALK THE TALK!!
 
Ni sawa ulichosema,lakini kama nitakumbuka hao unaowasema wa chadema,inaonyesha wamefukuzwa bila barua kwenda kwa speaker na pia taratibu zinachanganya,maana wamekata rufaa kwenye chama cha chadema na maamuzi bado hayajatoka!Na mimi nikaelewa vizuri na pili hawa ni wakina mama kwa nini wakomaliwe kufukuzwa?!! Hapo sasa.
 
Ni sawa ulichosema,lakini kama nitakumbuka hao unaowasema wa chadema,inaonyesha wamefukuzwa bila barua kwenda kwa speaker na pia taratibu zinachanganya,maana wamekata rufaa kwenye chama cha chadema na maamuzi bado hayajatoka!Na mimi nikaelewa vizuri na pili hawa ni wakina mama kwa nini wakomaliwe kufukuzwa?!;!Hapo sasa.

Sio kweli Barua ya kufukuzwa kwao ilipelekwa ofisini kwa Spika!! Sasa Ndugai anakuja na sababu nyingine kuwa Barua iliopelekwa haikuwa na attachement za Katiba ya chama na muhutasari wa kakao kilichowafukuza!! Kama angekuwa mkweli bungeni pale lazima kuna Katiba za vyama vote vinavyowakilishwa bungeni ambayo angeweza kuipitia na kuona kama ilikiukwa.

Kuhusu rufaa ya hao wakina mama, ingesikilizwaje wakati walikataa kuhudhulia vikao ambavyo ndio vilikuwa vinaskiiliza shauri lao!! Hata mahakamani uamuzi hutolewa hata kama mmoja wa wahusika hayupo mahakamani EX-PARTE! Ndugai anadhoofisha na kudharilisha Taasisi ya bunge na hivyo kuhujumu maendeleo ya nchi kwa kutokutenda haki!
 
TAFUTA HELA KAKA, TZ YETU ISHAUZWA KWA GENGE LA WACHACHE. MIE NIMECHOKA NA TZ. KUANDAMANA SIWEZI NAZUIWA, NIKIANDIKA HAYATIMIZWI, NIKISHAURI VIJANA TUPAZE SAUTI WANANIONA MPUUZI.
 
Back
Top Bottom