Viongozi hawawezi leta Maendeleo - Mkapa

MJIMPYA

JF-Expert Member
Mar 27, 2011
506
272
RAIS mstaafu, Benjamin Mkapa, amewataka viongozi wa serikali kuacha kuwadanganya wananchi kuwa wao ndio wenye uwezo wa kuwaletea maendeleo.

Mkapa alisema hakuna kiongozi mwenye uwezo wa kumletea maendeleo mwananchi kama hatashirikiana naye kwenye harakati za kupambana na umaskini.

Kauli hiyo aliitoa alipokuwa akitoa salamu ya misa ya Jubilei ya miaka 25 ya uaskofu, 38 ya upadri, 66 ya Ukristo na 66 ya umri ya Mhashamu Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Songea, Norbert Mtega, iliyofanyika katika kanisa Katoliki la Mtakatifu Matias Mulumba Kalemba.

Mkapa, alisema kuwa jukumu la kujiletea maendeleo ni la wananchi wenyewe si la viongozi wa serikali au wahisani mbalimbali wanaofadhili miradi ya maendeleo inayoibuliwa na wananchi au kuandaliwa na serikali.

Aliongeza kuwa wananchi ndiyo wenye uchungu wa nchi yao hivyo wanapaswa waongeze jitihada katika shughuli za kujiongezea kipato
.
Alisema kuwa hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere, aliwahi kusema kuwa maendeleo ya Watanzania yataletwa na Watanzania wenyewe na serikali jukumu lake ni kutengeneza miundombinu mizuri itakayoweza kurahisisha wananchi kufikia malengo waliyoyakusudia.

"Mimi nafadhaishwa sana ninaposikia viongozi wa kitaifa wanapowadanganya wananchi kuwa watawaletea maendeleo mbalimbali katika maeneo yao, kauli hizo ni potofu," alisema.

Alibainisha kuwa wananchi wanatakiwa wazipuuze kauli hizo kwani zinarudisha nyuma maendeleo husika pamoja na kujenga ukuta kati ya wananchi na viongozi wao.

Alisema viongozi hao wanapaswa kushirikiana na viongozi wa dini ili waweze kuwaonyesha juhudi mbalimbali zinazofanywa na wananchi walioamua kujiendeleza.

Naye Askofu Mtega, alisema viongozi wa serikali wanapaswa kutambua kuwa uhuru na kazi ndio dhana pekee itakayopunguza na kuondoa malalamiko ya wananchi ambayo yanazidi kushamiri siku hadi siku.

Askofu Mtega alisema kuwa nchi haiwezi kuwa na uhuru kamili mpaka itakapojijengea uwezo wa kufanya kazi yenyewe na kujitegemea kiuchumi, kisiasa na kimawazo kulingana na mahitaji ya wananchi wake.

Alisema nchi inapaswa kuwa na dira, mwelekeo ambao utasaidia kuwaongoza viongozi kwa kushirikiana na wananchi kuyafikia malengo, mikakati na mipango waliyojiwekea.

Aliongeza kuwa kama nchi haina mambo hayo na inapenda kunakiri kutoka kwenye mataifa mengine duniani basi haiwezi kuwa na uhuru uliokamilika bali inakuwa na uhuru wa bendera.

Alibainisha kuwa uhuru huo wa bendera unaweza kupotea kwa muda mfupi kwa kuwa hakuna misingi ya kuwafanya wananchi wawe huru na wanaojitegemea.

Alisema msingi wa uchumi wa Tanzania unapaswa kuwa kwenye uzalishaji mali kwa wananchi wenyewe ili waweze kuwa na uchumi imara kwani vyanzo vya uzalishaji mali vipo hapa hivyo ni vema viongozi wakatumia mawazo ya wananchi.

Alisema viongozi wakitumia mawazo yao, ya wananchi pamoja na dira, mwelekeo wa taifa watajenga uchumi imara badala ya kujipendekeza kwenda katika nchi nyingine kuomba misaada.

Alibainisha kuwa katika kipindi hiki cha bajeti ya serikali iliyosomwa juzi mjini Dodoma wabunge wanapaswa kuhakikisha kuwa inakuwa bajeti ya kuwasaidia wananchi katika shughuli za kujiletea maendeleo.

Alisema wananchi wakiwekewa mazingira mazuri ya kufanya kazi, kuwa wajasiriamali wenye kuzalisha bidhaa zenye tija kwa gharama nafuu itakuwa hatua kubwa ya kumkomboa kutoka katika lindi la umaskini.

Alisema kama serikali itakuwa imeandaa bajeti kwa kunukuu kutoka nchi nyingine au bajeti ya matumizi ya serikali tu basi bajeti hiyo haiwezi kuwasaidia Watanzania.

Alisema mwananchi anapokuwa na fursa ya kuuza mazao au bidhaa aliyozalisha katika mazingira mazuri nchi itaendelea kupiga hatua kiuchumi pamoja na amani na utulivu kuimarika zaidi kinyume na hapo ni kutengeneza matabaka yatakayokuja kuibua vurugu.

Sherehe za Jubilei hiyo ya Askofu Mtega ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwamo Mwadhama Kadinari Polycap Pengo, maaskofu zaidi ya 30, Anna Mkapa, na viongozi mbalimbali wa dini, serikali na vyama vya siasa.


Source: TZ Daima
 
Ujumbe huu ulichelewa kutoka kinywani kwa Mkapa kwani wapo watu wanalianza kufikiri na kudhani kuwa wanaweza kutembeza bakuli la maendeleo na kuligawa kama zawadi kwa wananchi wao.

Viongozi wa aina hii hawajui maana ya maendeleo maendeleo si idadi ya shule wala zahanati maendeleo ni huduma iliyotolewa katika miundo mbinu ya shule hospitali, barabara, nk inavyoweza kuharakisha juhudi za mwananchi kubadili maisha yake.

Ukigawa vitenge, ukijenga shule, Zahanati bila kuwashirikisha wananchi kuamua na kuona umuhimu wa huduma hizo unafanya maandalizi ya kuwafuga na kuwapumbaza wasione mbali ndivyo sisiemu na viongozi wake wanavyofanya.
 
Well said Mzee Mkapa. Sasa hivi uko kwenye nafasi ya kujua ukweli ni upi na usanii ni upi. Zaidi you have a legacy of positive achievements Watanzania wanaona na wanakumbuka
 
Well! Ni kama mlokole aliyefanya sana dhambi na sasa anaanza kujirudi. Ni ukweli japo umechelewa
 
Hata mmi naunga mkono kama vile kujikwapulia mgodi wa makaa ya mawe wa taifa na kuufanya wa familia yake na kumilikisha viongozi wa serikali nyumba za serikali na yeye mwenyewe kwa bei poa
 
Mkapa huyu ni mnafiki alishindwa nini kuwasaidia wanainchi na kuwaelikeza alivyokuwa rais zaidi ya kuigeuza Ikulu kama sehemu ya kufanyia biashara.
 
Anamaanisha siyo kutoa ahadi tu ukisikia tatizo lolote. Dar kuna Joto, nitauhamisha mlima Kilimanjaro Dar ili kupunguza joto. Shinyanga kuna ukame, nitawaletea Bahari ya Hindi. Hakuna usafiri nitawaletea denge za kutosha . Maisha hayaendeshwi hiyo. Wananchi wanatakiwa kuwewezeshwa tu, na maisha bora watayaona na kuyaishi.
 
Kijembe hiki Mkapa anampiga nani? Maana imekuwa kawaida ya viongozi wa vyama kutumia ahadi za kuleta maendeleo wanapo tembelea wananchi
 
<FONT size=3><SPAN style="COLOR: #000080"><STRONG><SPAN style="FONT-FAMILY: comic sans ms">Kijembe hiki Mkapa anampiga nani? Maana imekuwa kawaida ya viongozi wa vyama kutumia ahadi za kuleta maendeleo wanapo tembelea wananchi</SPAN></STRONG></SPAN></FONT>
 
Ni kweli. Lakini kazi ya viongozi ni kuweka environment ya kuleta maendeleo. Kikwete ameweza hilo?
 
Hakuna ukweli wowote ktk hili.. Ni sawa na kusema kutumia nguvu nyingi kazini kunaleta mafanikio..

Mkapa alichokizungumza kina walakini tena mkubwa sana kwa sababu marais wote duniani huchaguliwa ktk uchaguzi mkuu kwa lengo la kuongoza wananchi kupata maendeleo hivyo huwezi kusema kwamba viongozi hawaleti maendeleo bali ni wananchi.

Pasipo kiongozi bora akiongozwa na itikadi, sera na ilani safi zinazounda sheria (policy)bora za uwekezaji na hata ujenzi wa hiyo miundombinu bora hakuna maendeleo hata iwe kutazama maendeleo ya jamii au shirika.

Nchi yeyote inayoshuka kiuchumi lawama humfuata kiongozi wa nchi hiyo na sio wananchi na huwezi kunambia China miaka ya Mao TseTung walishindwa kuendelea kutokana na nguvu ndogo ya wananchi lakini leo hii Wachina hao hao wanaendelea kwa sababu ni uwezo mkubwa wa wananchi wale wale..

Hayati Baba wa Taifa, Julius Nyerere, aliwahi kusema kuwa maendeleo ya Watanzania yataletwa na Watanzania wenyewe na serikali jukumu lake ni kutengeneza miundombinu mizuri itakayoweza kurahisisha wananchi kufikia malengo waliyoyakusudia.

Kwa mwenye kuelewa kauli hii atagundua kwamba pasipo kutengenezwa miundombinu mizuri mwananchi hawezi kuleta maendeleo.. na vita kubwa ya nchi yetu ni kwamba hatuna miundombinu bora ya maendeleo achalia mbali policy mbovu za uwekezaji.

The goal of Governance initiatives should be to develop capacities that are needed to realise development that gives priority to the poor, advances citizen, sustains the environment and creates needed opportunities for employment and other livelihoods


Kwa nini tusiwalaumu viongozi?
 
Hii si mara ya kwanza kwa Mzee Mkapa kusema hivi. Ni nani asiyekumbuka enzi zile za "Mtaji wa Masikini ni nguvu zake mwenyewe" ? Sera na sheria za madini zinazolalamikiwa na wengi zilitoka katika awamu yake. Huyu mzee kuna mengi alifanikisha ila pia kuna madudu mengi sana pia aliyoyalea na "kuyapa hifadhi". Mambo ya EPA, IPTL, Meremeta na mengineyo mengi tu ni mafuvu ya Mkapa. Mnafiki mkubwa na yeye
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Aliyosema Mkapa ni ya ukweli. Shida ni kwamba waTz wengi ni watu wasioweza kuelewa hii dhana kwani imekaa kibepari zaidi.

WaTz wengi wanategemea wataletewa maendeleo na serikali. Wanategemea serikali ifanye kila kitu, itengeneze faida halafu iwagawie wananchi hiyo faida. Ndiyo maana utasikia watu wengi wanalalama kwamba GDP inaongezeka lakini hali yao bado ni mbaya. Watu hawa hawajui kuwa ili uneemeke na huko kukuwa kwa GDP, shurti ujiingize kwenye mfumo wa utengezaji wa thamani. Kama siyo kwa kufanya ujasiriamali, basi angalau soma vizuri uajiriwe.

Hauwezi ukakaa pembeni unalalamika tu kuwa unataka serikali ihodhi biashara zote kubwa halafu utegemee kuendelea. Utabaki nyuma huku wenzako wakisonga mbele.

Hiyo kitu ambayo waTz wanategemea ni dunia ya Kufikirika. Hakuna nchi duniani iliyoweza kuendelea kwa kufuata huo mfumo
 
Hizo sita sita zenu zinatustua wenzenu,ni coincidence au makusudi?
rais mstaafu, benjamin mkapa, amewataka viongozi wa serikali kuacha kuwadanganya wananchi kuwa wao ndio wenye uwezo wa kuwaletea maendeleo.
mkapa alisema hakuna kiongozi mwenye uwezo wa kumletea maendeleo mwananchi kama hatashirikiana naye kwenye harakati za kupambana na umaskini.
kauli hiyo aliitoa alipokuwa akitoa salamu ya misa ya jubilei ya miaka 25 ya uaskofu, 38 ya upadri, 66 ya ukristo na 66 ya umri ya mhashamu askofu mkuu wa jimbo kuu la songea, norbert mtega, iliyofanyika katika kanisa katoliki la mtakatifu matias mulumba kalemba.
Mkapa, alisema kuwa jukumu la kujiletea maendeleo ni la wananchi wenyewe si la viongozi wa serikali au wahisani mbalimbali wanaofadhili miradi ya maendeleo inayoibuliwa na wananchi au kuandaliwa na serikali.
aliongeza kuwa wananchi ndiyo wenye uchungu wa nchi yao hivyo wanapaswa waongeze jitihada katika shughuli za kujiongezea kipato.
alisema kuwa hayati baba wa taifa, julius nyerere, aliwahi kusema kuwa maendeleo ya watanzania yataletwa na watanzania wenyewe na serikali jukumu lake ni kutengeneza miundombinu mizuri itakayoweza kurahisisha wananchi kufikia malengo waliyoyakusudia.
“mimi nafadhaishwa sana ninaposikia viongozi wa kitaifa wanapowadanganya wananchi kuwa watawaletea maendeleo mbalimbali katika maeneo yao, kauli hizo ni potofu,” alisema.
Alibainisha kuwa wananchi wanatakiwa wazipuuze kauli hizo kwani zinarudisha nyuma maendeleo husika pamoja na kujenga ukuta kati ya wananchi na viongozi wao.
Alisema viongozi hao wanapaswa kushirikiana na viongozi wa dini ili waweze kuwaonyesha juhudi mbalimbali zinazofanywa na wananchi walioamua kujiendeleza.
Naye askofu mtega, alisema viongozi wa serikali wanapaswa kutambua kuwa uhuru na kazi ndio dhana pekee itakayopunguza na kuondoa malalamiko ya wananchi ambayo yanazidi kushamiri siku hadi siku.
Askofu mtega alisema kuwa nchi haiwezi kuwa na uhuru kamili mpaka itakapojijengea uwezo wa kufanya kazi yenyewe na kujitegemea kiuchumi, kisiasa na kimawazo kulingana na mahitaji ya wananchi wake.
Alisema nchi inapaswa kuwa na dira, mwelekeo ambao utasaidia kuwaongoza viongozi kwa kushirikiana na wananchi kuyafikia malengo, mikakati na mipango waliyojiwekea.
Aliongeza kuwa kama nchi haina mambo hayo na inapenda kunakiri kutoka kwenye mataifa mengine duniani basi haiwezi kuwa na uhuru uliokamilika bali inakuwa na uhuru wa bendera.
Alibainisha kuwa uhuru huo wa bendera unaweza kupotea kwa muda mfupi kwa kuwa hakuna misingi ya kuwafanya wananchi wawe huru na wanaojitegemea.
Alisema msingi wa uchumi wa tanzania unapaswa kuwa kwenye uzalishaji mali kwa wananchi wenyewe ili waweze kuwa na uchumi imara kwani vyanzo vya uzalishaji mali vipo hapa hivyo ni vema viongozi wakatumia mawazo ya wananchi.
Alisema viongozi wakitumia mawazo yao, ya wananchi pamoja na dira, mwelekeo wa taifa watajenga uchumi imara badala ya kujipendekeza kwenda katika nchi nyingine kuomba misaada.
Alibainisha kuwa katika kipindi hiki cha bajeti ya serikali iliyosomwa juzi mjini dodoma wabunge wanapaswa kuhakikisha kuwa inakuwa bajeti ya kuwasaidia wananchi katika shughuli za kujiletea maendeleo.
Alisema wananchi wakiwekewa mazingira mazuri ya kufanya kazi, kuwa wajasiriamali wenye kuzalisha bidhaa zenye tija kwa gharama nafuu itakuwa hatua kubwa ya kumkomboa kutoka katika lindi la umaskini.
Alisema kama serikali itakuwa imeandaa bajeti kwa kunukuu kutoka nchi nyingine au bajeti ya matumizi ya serikali tu basi bajeti hiyo haiwezi kuwasaidia watanzania.
Alisema mwananchi anapokuwa na fursa ya kuuza mazao au bidhaa aliyozalisha katika mazingira mazuri nchi itaendelea kupiga hatua kiuchumi pamoja na amani na utulivu kuimarika zaidi kinyume na hapo ni kutengeneza matabaka yatakayokuja kuibua vurugu.
Sherehe za jubilei hiyo ya askofu mtega ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwamo mwadhama kadinari polycap pengo, maaskofu zaidi ya 30, anna mkapa, na viongozi mbalimbali wa dini, serikali na vyama vya siasa.


Source: Tz daima
 
Aliyosema Mkapa ni ya ukweli. Shida ni kwamba waTz wengi ni watu wasioweza kuelewa hii dhana kwani imekaa kibepari zaidi.

WaTz wengi wanategemea wataletewa maendeleo na serikali. Wanategemea serikali ifanye kila kitu, itengeneze faida halafu iwagawie wananchi hiyo faida. Ndiyo maana utasikia watu wengi wanalalama kwamba GDP inaongezeka lakini hali yao bado ni mbaya. Watu hawa hawajui kuwa ili uneemeke na huko kukuwa kwa GDP, shurti ujiingize kwenye mfumo wa utengezaji wa thamani. Kama siyo kwa kufanya ujasiriamali, basi angalau soma vizuri uajiriwe.

Hauwezi ukakaa pembeni unalalamika tu kuwa unataka serikali ihodhi biashara zote kubwa halafu utegemee kuendelea. Utabaki nyuma huku wenzako wakisonga mbele.

Hiyo kitu ambayo waTz wanategemea ni dunia ya Kufikirika. Hakuna nchi duniani iliyoweza kuendelea kwa kufuata huo mfumo
Mkuu kama maneno haya ni kweli nambie kimetokea nini Rwanda hadi wamefanikiwa na pia kimetokea nini Zimbabwe hadi wakafilsika. Nionyeshe ni wapi uwezo wa wananchi umechangia mabadiliko yote hayo!

Na mwisho wa yote nipe nchi yeyote iliyoendelea na viongozi wake hawakuwa mstari wa mbele ktk uongozi na ujenzi wa maendeleo hayo.
 
Ni bora kuwa na mwanzo mbaya ukawa na mwisho mzuri.Kama sio unafiki, na kweli katambua makosa aliyoyafanya na anayajutia, namtakia kila la heri.
Well! Ni kama mlokole aliyefanya sana dhambi na sasa anaanza kujirudi. Ni ukweli japo umechelewa
 
Back
Top Bottom