Vioja vya kisiasa Tanzani...2010

Jackbauer

JF-Expert Member
Oct 28, 2010
6,038
2,199
Wanajf, haya matukio sitoweza kuyasahau:
1.wafanyakazi wakataa kumualika Rais kwenye mei mosi.

2.kikwete awaita wafanyakazi mbayuwayu lakini baadae aliufyata na kuwaongeza mshahara

3.familia ya Raisi kujitosa kwenye kampeni

4.Wanafunzi wa UDOM kumchangia kikwete kumbe hata fedha za kwenda field hawana.

5.lau Masha kushangilia ushindi kabla ya uchaguzi,hatimaye kuangushwa vibaya na kumpelekea kuchukua thamani za ofisi ya mbunge kupooza hasira.

6.makamba kukataza wabunge wa CCM kushiriki mchakato majimboni baada ya aibu iliyompata mgombea wake jimboni ubungo.

7.nguvu ya umma ilivyotumika kushinikiza utangazaji matokeo maeneo mbalimbali.

8.NEC kutangaza matokeo ya urais ambayo jumla ya kura walizopata wagombea ilizidi jumla ya kura halali.

9.SITTA kuondolewa kwenye mbio za uspika.

10 CHADEMA WALKOUT!!(hili linastahili kuwa tukio bora la mwaka)

wandugu tukumbushane matukio mengine!

WISH U A HAPPY NEW YEAR!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom