Vimemo Bandarini; Nani walikuwa wanaandika?

mzeelapa toka lini adhabu ya mlipa kodi ikawa ni kulipa ushuru?
Kisheria mtu aliyekwepa kodi anatakiwa kukamatwa, kushtakiwa na kufilisiwa mali ili kulipa fidia ya kodi aliyoikwepa Nukta.
Shida ya wachangiaji wengi humu hamjui maswala ya uchumi. Hawa wakwepa kodi no watu muhimu wanaoingiza fedha serikalini , wanaajiri watu wengi , ukiwafirisi uchumi unaanguka, shida iko wapi ? Acha walipe kodi walizokwepa na waendelee na bihashara zao, sisi humu tunapiga domo lkn hatuingizii chochote taifa
 
Last edited by a moderator:

Alichofanya hapa JK ni kuongeza maswali kuliko kupata majibu. Sasa nikama anaruhusu kama kuna ushahidi kuwa yeye au mmoja wa wanafamilia wake kahusika basi uwekwe wazi.
Wanafamilia wake ni pamoja na mtoto wake mkubwa Ritz, sijui huyu anawezaje kumsemea wakati ni mtu mzima na mwenye shughuli zake ambaye mambo yake ya daily activities yeye hawezi kujua?
Haya wenye vimemo na wavitoe sasa maana wameombwa wadhibitishe. Hapa TUTAONANA WABAYA!
 
Vimemo havitaendelea, ni nani atathubutu kuomba na kupokea vimemo kwa hali ilivyo sasa? Nina imani hao watoa vimemo watawajibishwa.
 
mzeelapa toka lini adhabu ya mlipa kodi ikawa ni kulipa ushuru?
Kisheria mtu aliyekwepa kodi anatakiwa kukamatwa, kushtakiwa na kufilisiwa mali ili kulipa fidia ya kodi aliyoikwepa Nukta.
naona mawazo yangu yanafanana na wachangiaji wengine. Walipe kodi kwanza ili hizo fedha zifanyie kazi nyingine za kutoa huduma na maendeleo kwa wananchi. Hivi akina Mramba, wamepatikana na hatia ya kusababishia hasara serikali, wamerejesha fedha hizo? si wanakula kodi zetu gerezani. Kodi zilipwe mambo mengine yatafuata.
 
Mama Siti Mwinyi lazima ajilaumu kwamba hakupiga vya kutosha.
 
ccm ni ileileee oooh ni ileileee.....:music::music::music:
 
Wewe ungefanya hivyo.kibarua kiote nyasi
 
Asilaumiwe JPM, serikali iliyopita ilikuwa dhaifu sana kupita maelezo pamoja na mhe. JK kujishaua kuwa hakuwahi kupeleka vimemo au maelekezo lkn hakuna aisiyefaham jinsi wafanya biashara walivyokuwa wanapishana kwenda Ikulu kila uchao. Sasa unategemea Rais wa sasa asemeje zaidi ya kuwaambia walipe kodi walizokwepa maana ukisema uwakamate na kuwafungulia mashtaka maana yake na bosi mtangulizi naye segerea. Inakuwa ngumu kidogo hapo Mkuu
 

Sasa Ngoma ndio inaanzia hapo. Taarifa zinasema zaidi ya wafanya biashara 15 wamegoma kulipa hatujui utetezi wao utakuwa nini. Na pia wale maafisa walioruhusu na wako mahakamani bado hatujui utetezi wao utakuwa nini.
All in all, hili swala la vimemo ambavyo vilikuwa ni MAAGIZO rasmi litaibuka tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…