Mpauko
R.I.P
- Jan 19, 2019
- 2,323
- 3,451
Habari za leo!
Leo ach nishare safari yangu from Mtwara to Singida tujifunze na kujuzana mengi.
TAREHE 26/09/2019 SAA 11:37.
mnamo saa 11:37 alfajiri niliwasili kituo cha basi Chipuputa Mtwara mjini tayari kwa safari yangu kutoka Mtwara kwenda Morogoro.
Kituo cha basi Chipuputa ni kipya hakina hata miezi mitano tangu kianze kutumika,ni kama hakijakamilika kwani ni vumbi tupu,kadhalika kituo hiki hakina hata hadhi kwani kina jengo dogo tu la kupumzikia abiria kama kinvyoonekana pichani.
Nilibahatika kupata siti ya mbele kabisa katika basi la Maningnice (kampuni pekee inyofanya safari za Mtwara to Morogoro) naamini tupo wengi tunaopenda hizi siti za mbele kabisa.
Saa 12:00 magari yalianza kuondoka kwa fujo tulitanguliwa na basi za Machinga high class(sunlong),Buti la zungu (yutong F12+) na sisi Maningnice (zhongtong climber new model) safari ikaanza na dakika chache mbele tulikuwa tukiitafuta Mikindani.
Kabla ya kufika mikindani tuliipita basi la Machinga high class ikiwa imesimama katikati ya barabara na tuliipita kupitia upande usioruhusiwa (kushoto).
Baada ya dakika zisizozidi mbili basi hilo lilitupita kwa fujo katika eneo lenye kona kali,hii ilinifanya nimuone dereva wake kuwa mpenda ligi na asiye makini na maisha ya abiria pamoja na chombo cha mbunge mstaafu (Hasnan Murji,CCM)
Safari ilipamba moto hatimaye sasa tulikipita kiwanda cha simenti cha Dangote huku usalama wa watumiaji wa barabara hii ukihatarishwa na malori yaliyoegeshwa hovyo pembezoni mwa barabara.
Mwendo ni wa wastani na dereva akiwa mtu wa makamo ya miaka 34 hadi 38 hivi hivi kijana mdogo lakini makini sana,palipo na kibao cha 30 alitembelea 30 na palipo na 50 alitembelea 50.
Kipande cha Mtwara hadi Mingoyo weight bridge Mnazi mmoja kimejaa viraka na manundu yanayopunguza hata hamu ya safari yenyewe,nyakati zingine dereva alibaki kurukaruka ajabu kutokana na muundo wa kiti cha dereva kuwa na mneso zaidi lakini hakuwa ananesa tena bali alikuwa anarukaruka kabisa.
Saa 1:49 tuliwasili Mingoyo weight bridge ambapo tulikutana na basi za Maningnice(zhongtong climber),Navil exspress(yutong F11),Buti la zungu(yutong F12+),Baraka classic (yutong F11) zote zikitokea Masasi,saa 2:30 tuliwasili Lindi.
Safari ya kutoka Lindi ilikuwa ni nzuri sana kutokana na barabara kuwa nzuri ingawaje bado kipande cha Mtwara to Lindi kilikuwa na mvuto wake kutokana n mandhari za kuvutia sana.
Majengo ya kihistoria Mikindani huonekana vizuri na kwa ukaribu sana,kadhalika barabara hupita pembeni mwa bahari ya Hindi hii inavutia sana.
Pia mashamba ya chumvi yaliyotamalki pembezoni mwa bahari ya hindi yalizidisha mvuto hususani kwa wale wasiofahamu jinsi chumvi inavyotengenezwa kwa kutegemea jua tu hii ni nafasi yao kujionea sasa.
Hatimaye saa 10:13 tuliwasiliNangurukuru,hapa ndipo abiria hujipatia chakula na huduma za maliwato ipo mkoa wa Kilwa.
Huduma za choo ni nzuri lakini bei za vyakula ni maumivu kwa abiria,bei za vyakula,ubora wa vyakula na ujazo ni vitu viwili tofauti,kutokana na uwepo wa sehemu hii moja pekee ndiko kubakowatia jeuri wafanyabiashara wa sehemu hii.
Nilinunua maji y tshs 1000 na ndizi tatu na kutulia zangu nikienjoi kifungua kinywa.
Inaendelea......
Leo ach nishare safari yangu from Mtwara to Singida tujifunze na kujuzana mengi.
TAREHE 26/09/2019 SAA 11:37.
mnamo saa 11:37 alfajiri niliwasili kituo cha basi Chipuputa Mtwara mjini tayari kwa safari yangu kutoka Mtwara kwenda Morogoro.
Kituo cha basi Chipuputa ni kipya hakina hata miezi mitano tangu kianze kutumika,ni kama hakijakamilika kwani ni vumbi tupu,kadhalika kituo hiki hakina hata hadhi kwani kina jengo dogo tu la kupumzikia abiria kama kinvyoonekana pichani.
Nilibahatika kupata siti ya mbele kabisa katika basi la Maningnice (kampuni pekee inyofanya safari za Mtwara to Morogoro) naamini tupo wengi tunaopenda hizi siti za mbele kabisa.
Saa 12:00 magari yalianza kuondoka kwa fujo tulitanguliwa na basi za Machinga high class(sunlong),Buti la zungu (yutong F12+) na sisi Maningnice (zhongtong climber new model) safari ikaanza na dakika chache mbele tulikuwa tukiitafuta Mikindani.
Kabla ya kufika mikindani tuliipita basi la Machinga high class ikiwa imesimama katikati ya barabara na tuliipita kupitia upande usioruhusiwa (kushoto).
Baada ya dakika zisizozidi mbili basi hilo lilitupita kwa fujo katika eneo lenye kona kali,hii ilinifanya nimuone dereva wake kuwa mpenda ligi na asiye makini na maisha ya abiria pamoja na chombo cha mbunge mstaafu (Hasnan Murji,CCM)
Safari ilipamba moto hatimaye sasa tulikipita kiwanda cha simenti cha Dangote huku usalama wa watumiaji wa barabara hii ukihatarishwa na malori yaliyoegeshwa hovyo pembezoni mwa barabara.
Mwendo ni wa wastani na dereva akiwa mtu wa makamo ya miaka 34 hadi 38 hivi hivi kijana mdogo lakini makini sana,palipo na kibao cha 30 alitembelea 30 na palipo na 50 alitembelea 50.
Kipande cha Mtwara hadi Mingoyo weight bridge Mnazi mmoja kimejaa viraka na manundu yanayopunguza hata hamu ya safari yenyewe,nyakati zingine dereva alibaki kurukaruka ajabu kutokana na muundo wa kiti cha dereva kuwa na mneso zaidi lakini hakuwa ananesa tena bali alikuwa anarukaruka kabisa.
Saa 1:49 tuliwasili Mingoyo weight bridge ambapo tulikutana na basi za Maningnice(zhongtong climber),Navil exspress(yutong F11),Buti la zungu(yutong F12+),Baraka classic (yutong F11) zote zikitokea Masasi,saa 2:30 tuliwasili Lindi.
Safari ya kutoka Lindi ilikuwa ni nzuri sana kutokana na barabara kuwa nzuri ingawaje bado kipande cha Mtwara to Lindi kilikuwa na mvuto wake kutokana n mandhari za kuvutia sana.
Majengo ya kihistoria Mikindani huonekana vizuri na kwa ukaribu sana,kadhalika barabara hupita pembeni mwa bahari ya Hindi hii inavutia sana.
Pia mashamba ya chumvi yaliyotamalki pembezoni mwa bahari ya hindi yalizidisha mvuto hususani kwa wale wasiofahamu jinsi chumvi inavyotengenezwa kwa kutegemea jua tu hii ni nafasi yao kujionea sasa.
Hatimaye saa 10:13 tuliwasiliNangurukuru,hapa ndipo abiria hujipatia chakula na huduma za maliwato ipo mkoa wa Kilwa.
Huduma za choo ni nzuri lakini bei za vyakula ni maumivu kwa abiria,bei za vyakula,ubora wa vyakula na ujazo ni vitu viwili tofauti,kutokana na uwepo wa sehemu hii moja pekee ndiko kubakowatia jeuri wafanyabiashara wa sehemu hii.
Nilinunua maji y tshs 1000 na ndizi tatu na kutulia zangu nikienjoi kifungua kinywa.
Inaendelea......
