Vimambo na vijimambo safari yangu Mtwara to Singida

Vimambo na vijimambo safari yangu Mtwara to Singida

Mpauko

R.I.P
Joined
Jan 19, 2019
Posts
2,323
Reaction score
3,451
Habari za leo!

Leo ach nishare safari yangu from Mtwara to Singida tujifunze na kujuzana mengi.

TAREHE 26/09/2019 SAA 11:37.

mnamo saa 11:37 alfajiri niliwasili kituo cha basi Chipuputa Mtwara mjini tayari kwa safari yangu kutoka Mtwara kwenda Morogoro.

Kituo cha basi Chipuputa ni kipya hakina hata miezi mitano tangu kianze kutumika,ni kama hakijakamilika kwani ni vumbi tupu,kadhalika kituo hiki hakina hata hadhi kwani kina jengo dogo tu la kupumzikia abiria kama kinvyoonekana pichani.

Nilibahatika kupata siti ya mbele kabisa katika basi la Maningnice (kampuni pekee inyofanya safari za Mtwara to Morogoro) naamini tupo wengi tunaopenda hizi siti za mbele kabisa.

Saa 12:00 magari yalianza kuondoka kwa fujo tulitanguliwa na basi za Machinga high class(sunlong),Buti la zungu (yutong F12+) na sisi Maningnice (zhongtong climber new model) safari ikaanza na dakika chache mbele tulikuwa tukiitafuta Mikindani.

Kabla ya kufika mikindani tuliipita basi la Machinga high class ikiwa imesimama katikati ya barabara na tuliipita kupitia upande usioruhusiwa (kushoto).


Baada ya dakika zisizozidi mbili basi hilo lilitupita kwa fujo katika eneo lenye kona kali,hii ilinifanya nimuone dereva wake kuwa mpenda ligi na asiye makini na maisha ya abiria pamoja na chombo cha mbunge mstaafu (Hasnan Murji,CCM)


Safari ilipamba moto hatimaye sasa tulikipita kiwanda cha simenti cha Dangote huku usalama wa watumiaji wa barabara hii ukihatarishwa na malori yaliyoegeshwa hovyo pembezoni mwa barabara.


Mwendo ni wa wastani na dereva akiwa mtu wa makamo ya miaka 34 hadi 38 hivi hivi kijana mdogo lakini makini sana,palipo na kibao cha 30 alitembelea 30 na palipo na 50 alitembelea 50.

Kipande cha Mtwara hadi Mingoyo weight bridge Mnazi mmoja kimejaa viraka na manundu yanayopunguza hata hamu ya safari yenyewe,nyakati zingine dereva alibaki kurukaruka ajabu kutokana na muundo wa kiti cha dereva kuwa na mneso zaidi lakini hakuwa ananesa tena bali alikuwa anarukaruka kabisa.


Saa 1:49 tuliwasili Mingoyo weight bridge ambapo tulikutana na basi za Maningnice(zhongtong climber),Navil exspress(yutong F11),Buti la zungu(yutong F12+),Baraka classic (yutong F11) zote zikitokea Masasi,saa 2:30 tuliwasili Lindi.

Safari ya kutoka Lindi ilikuwa ni nzuri sana kutokana na barabara kuwa nzuri ingawaje bado kipande cha Mtwara to Lindi kilikuwa na mvuto wake kutokana n mandhari za kuvutia sana.

Majengo ya kihistoria Mikindani huonekana vizuri na kwa ukaribu sana,kadhalika barabara hupita pembeni mwa bahari ya Hindi hii inavutia sana.

Pia mashamba ya chumvi yaliyotamalki pembezoni mwa bahari ya hindi yalizidisha mvuto hususani kwa wale wasiofahamu jinsi chumvi inavyotengenezwa kwa kutegemea jua tu hii ni nafasi yao kujionea sasa.


Hatimaye saa 10:13 tuliwasiliNangurukuru,hapa ndipo abiria hujipatia chakula na huduma za maliwato ipo mkoa wa Kilwa.

Huduma za choo ni nzuri lakini bei za vyakula ni maumivu kwa abiria,bei za vyakula,ubora wa vyakula na ujazo ni vitu viwili tofauti,kutokana na uwepo wa sehemu hii moja pekee ndiko kubakowatia jeuri wafanyabiashara wa sehemu hii.

Nilinunua maji y tshs 1000 na ndizi tatu na kutulia zangu nikienjoi kifungua kinywa.

Inaendelea......





images%20(2).jpeg
Dangote-to-commission-Cement-Plant-in-Tanzania.jpeg
Bay-6.jpeg
chumvi%201%20copy.jpeg
 
Hatimaye saa saba na nusu tuliwasili mbagala,kwa kweli stendi hii ni mbovu kwelikweli ingawaje kuna matumaini ya uboreshaji wake

Saa nane mchana tuliwasili Ubungo na abiria wanaoishia Dar es salaam walishuka,tulikaa zaidi ya dakika 30 wakijazia abiria wa kuelekea Morogoro.

Ingawaje ilikuwa mchana lakini bado foleni ilikuwa ni kubwa ikichagizwa na ujenzi wa barabara kuu ya Dsm-Morogoro,tulipitia kituo cha mbezi na abiria wakajazwa na kurundikwa hadi kwenye varanda.


Achilia mbali wingi wa Magari yanyofanya safari za Morogoro-DSM bado abiria walikuwa ni wengi mno kiasi kwamba walikua radhi kukaa chini ya varanda.

Kila tuliposimamishwa na trafiki konda alishuka na noti ya elfu tano au elfu kumi naye trafiki hakuwa akiingia garini kusema kwamba huu ni mchezo wao wa kila siku na natumaini wengi wetu huwa tunajionea haya.

Hii inamaan ya kuwa Rushwa haiwezi kuisha leo wala kesho na ni mbaya sana kurundika abiria katika varanda hususani pale inapotokea ajali.


Mnamo saa nne kasoro tuliwasili stendi ya basi Msamvu,kwa stendi hii hongereni Manispaa ya Morogoro ni stendi kubwa na ya kisasa.

Lakini jengo lililopo ghorofani lilionekana kimya kama kwamba halitumiki,ofisi hazijakodishwa na kampuni za mabasi mengi wanakatisha tiketi zao nje kwa mawakala,halmashauri ya Morogoro ijitadthmini kwa kulazimisha makampuni kuwa na ofisi maalumu ili iweze kupata wapangaji wa ofisi zilizo tupu.


Madudu mengine ni maandishi yanayoitambulisha stendi hii KITUO CHA MABASI CHA KISASA MSAMVU,huyu mshauri aliyeyeshauri kiitwe hivyo amekosea sana,je kuna haja gani kuandika neno CHA KISASA?

Eneo la kupumzikia abiria limejaa wafanyabiashara wa vyakula na sikuweza kuona mahali salama kwangu kujipumzisha hadi alfajiri nikaamua tu nitafute Lodge ya bei poa nisije haribu bajeti yangu.


Nikatoa oda kwa bodaboda anipeleke lodge inayotoza chini ya elfu 10 kulingana na bajeti yangu,shughuli ikaja hapa kwani kila mahali chumba ni elfu kumi n tano lakini ukivitazama havina hata hadhi hiyo kabisa.

Lodge zote zimeweka vyoo vya kukaa,hivi nani kawadanganya kuwa kila mtu anapenda aina hii ya vyoo? Mwisho nikakubali lodge mojawapo baada ya kutafuta zisizo na vyoo vya kukaa bila mafanikio,ikabidi niwe naenda kutumia choo cha staff maana sipendi kabisa vyoo hivi labda kiwe changu binafsi.


Inaendelea......
IMG_20191001_215629_2.jpeg
 
Hatimaye saa saba na nusu tuliwasili mbagala,kwa kweli stendi hii ni mbovu kwelikweli ingawaje kuna matumaini ya uboreshaji wake

Saa nane mchana tuliwasili Ubungo na abiria wanaoishia Dar es salaam walishuka,tulikaa zaidi ya dakika 30 wakijazia abiria wa kuelekea Morogoro.

Ingawaje ilikuwa mchana lakini bado foleni ilikuwa ni kubwa ikichagizwa na ujenzi wa barabara kuu ya Dsm-Morogoro,tulipitia kituo cha mbezi na abiria wakajazwa na kurundikwa hadi kwenye varanda.


Achilia mbali wingi wa Magari yanyofanya safari za Morogoro-DSM bado abiria walikuwa ni wengi mno kiasi kwamba walikua radhi kukaa chini ya varanda.

Kila tuliposimamishwa na trafiki konda alishuka na noti ya elfu tano au elfu kumi naye trafiki hakuwa akiingia garini kusema kwamba huu ni mchezo wao wa kila siku na natumaini wengi wetu huwa tunajionea haya.

Hii inamaan ya kuwa Rushwa haiwezi kuisha leo wala kesho na ni mbaya sana kurundika abiria katika varanda hususani pale inapotokea ajali.


Mnamo saa nne kasoro tuliwasili stendi ya basi Msamvu,kwa stendi hii hongereni Manispaa ya Morogoro ni stendi kubwa na ya kisasa.

Lakini jengo lililopo ghorofani lilionekana kimya kama kwamba halitumiki,ofisi hazijakodishwa na kampuni za mabasi mengi wanakatisha tiketi zao nje kwa mawakala,halmashauri ya Morogoro ijitadthmini kwa kulazimisha makampuni kuwa na ofisi maalumu ili iweze kupata wapangaji wa ofisi zilizo tupu.


Madudu mengine ni maandishi yanayoitambulisha stendi hii KITUO CHA MABASI CHA KISASA MSAMVU,huyu mshauri aliyeyeshauri kiitwe hivyo amekosea sana,je kuna haja gani kuandika neno CHA KISASA?

Eneo la kupumzikia abiria limejaa wafanyabiashara wa vyakula na sikuweza kuona mahali salama kwangu kujipumzisha hadi alfajiri nikaamua tu nitafute Lodge ya bei poa nisije haribu bajeti yangu.


Nikatoa oda kwa bodaboda anipeleke lodge inayotoza chini ya elfu 10 kulingana na bajeti yangu,shughuli ikaja hapa kwani kila mahali chumba ni elfu kumi n tano lakini ukivitazama havina hata hadhi hiyo kabisa.

Lodge zote zimeweka vyoo vya kukaa,hivi nani kawadanganya kuwa kila mtu anapenda aina hii ya vyoo? Mwisho nikakubali lodge mojawapo baada ya kutafuta zisizo na vyoo vya kukaa bila mafanikio,ikabidi niwe naenda kutumia choo cha staff maana sipendi kabisa vyoo hivi labda kiwe changu binafsi.


Inaendelea......View attachment 1222278
Pole kwa safari
 
Asubuhi ya terehe 29 nikaamka salama tayari kwa safari ya kwenda,Singida lakini nilihisi hali ngeni tumboni.

Tumbo lilichafuka nikakimbilia kumeza dawa za kuzuia kuendesha(sio flagil) hatimaye likatulia,nikawasili stendi kukata tiketi ya basi la POLEPOLE likitokea Dar es salaam,gari iliwasili saa saba mchana.

Ilikuwa ni gari chakavu kweli kweli lakini ilikuwa imejaza abiria wa kutosha,vyuma vilijitokea katika baadhi ya siti,nyaya na mikanda ilikuwa mibovu.

Hakika yule dereva alikuwa rafu kweli kweli,mwendo ulikuwa ni mkali aliovertake hovyo akipiga breki hovyo kiasi cha kusumbua mno abiria mara kadhaa alilazimisha magari mengine kusogea pembeni wakati akiovateki angalabu tulikaribia kuumana uso kwa uso na lori la mafuta.

Jirani yangu alikaa dada mmoja mrembo wa haja,hazikupita dakika thelathini akauliza kama nina dakika ili aweze kupiga simu,nikakubali na kumpa simu mara baada ya kumaliza alishukuru na safari ikaendelea.

Tabia ya dada huyu ilinishangaza kidogo,alikuwa anakula kila kituo tunchosimama mara chipsi,mahindi,karanga,juisi,mayai,nyama choma na hata karanga.

Kama ilivyo ada abiria walirundikwa wa kutosha katika varanda na bado waliendelea kupakia na kushusha vituo mbali mbali.

Trafiki waliendelea kupewa elfu tano tano kila walipopiga mkono,hakuna trafiki aliyeingia ndani zaidi ya kumalizana na konda kibingwa.

Hali yangu ilianza kubadilika,kwani tumbo lilizidi kuchafuka ajabu,nilijikaza huku kijasho kikinitoka nikajisemea "niliyokuwa nasikia kwa wengine yananikuta leo"..

Hali ilizidi kuwa mbaya kiasi kwamba uvumilivu ulinifika kikomo,jasho lilinitoka na nilitetemeka kwa mbali nikaona huku ndiko kudhalilika kwenyewe sasa..

Nikamwita konda kumweleza hli yangu akapuuzilia mbali akasema ngoja tufike dodoma,baada ya robo saa hivi nikamweleza kuwa sitoweza tena hivyo wafanye utaratibu wa kuniacha zahanati au stendi,pia niliwaomba wanirudishie nauli nusu..

Waligoma katakata nikaona nitadhalilika kwa sasa nikawambia wanishushe tu,nikashukia Kongwa na kuwahi zahanati...

Baada ya kupewa dawa nikaenda kuripoti polisi juu ya suala la wenye gari kutochukua hatua yoyote kwa abiria aliyeugua,walitoa ushirikiano na nikalala Kongwa kusubiri siku inayofuta.....


Inaendelea.....
 
Asubuhi ya terehe 29 nikaamka salama tayari kwa safari ya kwenda,Singida lakini nilihisi hali ngeni tumboni.

Tumbo lilichafuka nikakimbilia kumeza dawa za kuzuia kuendesha(sio flagil) hatimaye likatulia,nikawasili stendi kukata tiketi ya basi la POLEPOLE likitokea Dar es salaam,gari iliwasili saa saba mchana.

Ilikuwa ni gari chakavu kweli kweli lakini ilikuwa imejaza abiria wa kutosha,vyuma vilijitokea katika baadhi ya siti,nyaya na mikanda ilikuwa mibovu.

Hakika yule dereva alikuwa rafu kweli kweli,mwendo ulikuwa ni mkali aliovertake hovyo akipiga breki hovyo kiasi cha kusumbua mno abiria mara kadhaa alilazimisha magari mengine kusogea pembeni wakati akiovateki angalabu tulikaribia kuumana uso kwa uso na lori la mafuta.

Jirani yangu alikaa dada mmoja mrembo wa haja,hazikupita dakika thelathini akauliza kama nina dakika ili aweze kupiga simu,nikakubali na kumpa simu mara baada ya kumaliza alishukuru na safari ikaendelea.

Tabia ya dada huyu ilinishangaza kidogo,alikuwa anakula kila kituo tunchosimama mara chipsi,mahindi,karanga,juisi,mayai,nyama choma na hata karanga.

Kama ilivyo ada abiria walirundikwa wa kutosha katika varanda na bado waliendelea kupakia na kushusha vituo mbali mbali.

Trafiki waliendelea kupewa elfu tano tano kila walipopiga mkono,hakuna trafiki aliyeingia ndani zaidi ya kumalizana na konda kibingwa.

Hali yangu ilianza kubadilika,kwani tumbo lilizidi kuchafuka ajabu,nilijikaza huku kijasho kikinitoka nikajisemea "niliyokuwa nasikia kwa wengine yananikuta leo"..

Hali ilizidi kuwa mbaya kiasi kwamba uvumilivu ulinifika kikomo,jasho lilinitoka na nilitetemeka kwa mbali nikaona huku ndiko kudhalilika kwenyewe sasa..

Nikamwita konda kumweleza hli yangu akapuuzilia mbali akasema ngoja tufike dodoma,baada ya robo saa hivi nikamweleza kuwa sitoweza tena hivyo wafanye utaratibu wa kuniacha zahanati au stendi,pia niliwaomba wanirudishie nauli nusu..

Waligoma katakata nikaona nitadhalilika kwa sasa nikawambia wanishushe tu,nikashukia Kongwa na kuwahi zahanati...

Baada ya kupewa dawa nikaenda kuripoti polisi juu ya suala la wenye gari kutochukua hatua yoyote kwa abiria aliyeugua,walitoa ushirikiano na nikalala Kongwa kusubiri siku inayofuta.....


Inaendelea.....
Hahahahahahah unaona madhara ya kula kula vitu vya bei chee ? Ndo maana mwanzo nikakuambia acha kulia lia kisa bei
 
Back
Top Bottom