Vile mashauzi yalivyoniumbua

kuna wadada wanauzaga juice nzurii ya tende na maziwa, nikamwomba namba alichonijibu sikutegemea kbs! Nikanyamaza jana nikaenda tena, bahati nzuri nikamkuta bosi wao, (sikuwa namjua) nikamshauri hapa ungeweka namba ya cm kwasbb kukaa usubirie ili utengenezewe juice ni kupoteza muda ni bora mtu apige cm halafu aje akute keshatengenezewa.

Akanipa namba yake, nikihitaji nampigia anawaambia watengeneze nikifika nakunywa naondoka, hawa wadada wanaojionaga wazuri akili zao ni takataka kbs!
 
Wadada wana hofu wakiitwa , zamani kidogo nikiwa chuo,ilikua siku ya jumatatu ni siku ambayo huwa ni busy sana watu mnapishana hawa wanaelekea darasani , wengine wanatoka !! Mimi nilikua naelekea darasani mbele yangu nikamwona dada kadondosha hela elfu kumi alikua anatembea kwa haraka sana ! Nikaiokota sasa kwa kuwa watu ni wengi njiani na nimeonwa nikaona haitakua busara kuichukua !! Basi nikawa namwita akageuka huyo akaenda zake !! Alivyoingia darasani kulikua na mwalimu basi nikamwoneshea ishara ya kumwita nikiwa nje akageuka tu ! Akaendelea na shughuli zake !! Niliogopa kuingia darasani maana nilikua mwaka wa kwanza ndo tumefika fika week za mwanzoni !! Ikabidi niondoke zangu sijui ilikuaje huko [emoji23][emoji23] me ugali nyama choma tu na mtindi hukoo
 
Kuna mshkaji wangu anaishi Kawe. Nishawahi kuishi kwao kwa zaidi ya mieizi miwili kwahiyo nazijua njia za maeneo hayo vizuri tu. Kisha nikaondoka Dar kwa zaidi ya mwaka nilivyorudi tena Dar nikawa naishi kwetu sasa nikapanga kwenda kumtembelea mshkaji.

Siku imefika nikafunga safari nikaelekea Kawe. Kipindi hicho wimbo maarufu ni Prakatatumba wa Cabo Snoop na nilivaa kama mshkaji. Supra, jinzi chupa (enzi hizo haziitwi model), halafu jinzi inaingizwa ndani ya supra na fulana nikachomekea.

Nikafika sehemu ambayo ina kibaraza natakiwa niambae kufuata kibaraza kisha nikutane na kichochoro halafu hiko kichochoro kimekunja kulia halafu hapo ndo kinitoe kwenye njia pana ndiyo nikute uwanja anapokaa mshkaji.

Kwenye kibaraza nikakuta mabinti na wanawake wanasukana, nikawapita mwendo mdundo. Nikaingia kichochoroni nikakunja kulia nakuta kumezibwa kwa michongoma. Nikafikiria mwendo niliowapita pale nikaona kurudi siyo kweli na nilivyovaa itakua aibu.

Nikaparamia ile michongoma.

Kumbe katikati waliweka na miti ili michongoma isimame.

Nikakomaa. No backing down hapa.

Paramia na teke kwa mara ya pili pakalegea. Nikajipenyeza penyeza nikafanikiwa kupita.

Bwana wee nilijichana chana na ile miiba maeneo ya usoni na mgongoni. Fulana imechafuka kwa vumbi.

Did I learn anything? No. Am the same nigga who is shy kusalimia kundi la wamama.
 
Nimecheka sana , kwa hiyo mwanetu ukakaza kibingwa [emoji23][emoji23][emoji23] Hebu fikiria ungekutwa unatengeneza njia !
 
Hukukubali kushindwa 🤣🤣🤣🤣 🤣🤣
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]Kama nakuona vileee, Dona
 
Siku hiyo nipo kitaa..jamaa angu akawa amekuja nimsindikize kwenye harusi ya kilokole wazee wake wameona wasiende kwa kua hakuna pombe hivyo akaniomba kampani.Bila ajizi nikaulamba tukaenda maeneo ya Salvation Army pale JKT tumefika vijana wa kiume rika letu tulikua watatu tu mimi jamaa angu na mshikaji mwingine..sasa MC akaita vijana 6 waende mbele wa 3 wa kiume na wa 3 wakike mimi nikavunga MC akaniambia wewe kwani sio kijana wa kiume? Na ukicheki pale mbele kuna wawili tu jamaa angu na yule mwingine..basi nikaenda pale mbele hamadi wakapiga kwaito tucheze dah niliabika kishenzi mbele za watu kwanza nina aibu kinoma ya kucheza halafu sijui kucheza hata kidogo ukumbi ulibaki kucheka tu[emoji16].

Ila niliwanyoosha muda wa kula[emoji38]
 

Hapo baadae ndo ataanza kujiuliza labda yule aliyeniita aliiokota
 
Sijui huwa mnawaza nini?

Kuna kipindi fulani nilimpa dada mmoja shati langu pale Kairuki ajisitiri. Mpaka anagundua kinachoendelea, tayari alikua ameshanijibu hovyo hovyo.

She was bleeding, nikaona nimsaidie kuficha aibu. Kusema nimuongeleshe, nikajikuta najibiwa kwa nyodo wakati I tried to keep it as casual as possible.
 
Wa Africa tofauti na wanawake wa kizungu wao madem wa kizungu ukiwaita Wana kuja kukusikiliza hawa ogopi na hawana wasiwasi Kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asee binafsi nikiitwa njiani ntasimama niskilize sababu ya kuitwa..

Kuna siku nlikua natembea njiani sina habari.. kuna kaka alikua anakuja mbele yangu, akanisimamisha akanisalimia kama ananijua nkamwitikia vizuri tu (nna haiba ya ku smile everytime 😊).. akaniambia dada chupi yako nzuri nkashtuka kaonaje chupi yangu huyu? Kuja kujiangalia zipu ya suruali ipo wazi🙆‍♀️🙆‍♀️🙆‍♀️ nkacheka nkamshukuru nkaifunga nkaendelea na safari.
Sa nkawaza ningeringa ningechunguliwa na wangap sku iyo🤣🤣🤣
 
Dah alifaidi kweli[emoji16]
 
Nilipita mtaa mmoja hivi Kuna mdada alikuwa amevaa kiahasara alivaa t shirt kubwa sijui ndio gauni limefika magotini ndani hakukuwa na dalili ya kuvaa pichu basi kalibia kila mtu alikuwa anamshangaa na Mimi nikashiriki maandamano nikaungana nao kumuangalia .....hatua kadha nikajikwaa bhana na sendo ikakatika Kuna jamaa akaropoka "....jamaa Hadi sendo yake imekatika" waliosikia wakaningalia wakaanza kucheka ndani ya sekunde kadhaa wote wakawa wananiangalia Mimi . Ile siku nilijisikia aibu Sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…