Vile mashauzi yalivyoniumbua

Vile mashauzi yalivyoniumbua

Carleen

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
8,407
Reaction score
28,837
Kwa mlioko Dar, Poleni kwa mgao wa kuanzia maji, umeme mpaka mapenzi, ila ndugu zangu tutafika kwa Baba tuko hoi sana maskiini, imagine duniani tunateseka hivii na bado huko naskia kuna moto tena..! Nyieeeeeeh'..!

Nisiwachoshe maana mshajichokea zenu tayari, kuna siku natoka zangu huko 'duniani' ilikuwa mida ya jioni ndiyo narudi zangu nyumbani, ile natoka getini nikakuta kuna watu wengi kweli wamekaa hapo pia wapo dereva toyo wamepaki kwa pembeni kidogo..!

Kama mnavyojua mdada ukipita mbele ya watu wengi ule ujasiri huwa unapotea tu ghafla, unatafuta cha kuzugia.! Luckily, nilikuwa niko na simu mkononi na kuna voice note ya whatsap nilikuwa nimetoka iskiza, ikabidi na mie nianze kurekodi V.N kujibu, shida hasa ilikuwa tu nivuke kwenye wale watu wengi, na venye walikuwa wananikodolea macho ndiyo nikahisi kuzimia kabisa.!

Sikupita hata hatua nyingi barabarani kwenyewe sijafika, nikaanza kuitwa na baadhi ya wale toyo 'swahiibaaa' 'swahibaaa', nikawaskia kiukweli ila nikajikausha mazima, nikaona enhee' washaanza uchokozi hawa bila shaka, maana akili zao huwa wanazijua wenyewe,

Nikaona wee' wasinizoee ndiyo kwanza nikazidi kuzidisha mashauzi na kutembea kwa pozi ili nijifanye niko serious na busy mradi tu waniache, pochi mkononi, maji yangu ya kunywa kisha nikakaza macho kwenye simu yangu nikajitia 'u-business face', dear Lord, laiti ningejua ningesimama niwaskize eti hata.! Lakini ile kiburi ya uzima itakuwa imeenda wapi sahiyo maskiini.!!

Nafika mbele kidogo, nikashangaa mbona kama hatua zangu hazizuiliwi na ile kimini tena nini kimetukia ghafla..!? Haha.! Sitaki kukumbuka ile siku walaqhi'..! Nilitamani ardhi ipasuke nidumbukie huko.! Kumbe watu wote walivyokuwa wananishangaa na toyo wananiita waniambie ni namna zipu ya mini skirt kuna namna nilikuwa imeachia huko nyuma.!

So kadri natembea na yenyewe inazidi kushuka..! Jizoooozi..! Niliishiwa pozi, uso ulinishuka na yale mashauzi yakayeyuka yooote ghafla kama siagi motoni.! Nilijikuta naweka maji chini, pochi na simu bila kujijua wala kujali tena..! Nikakamata skirt yangu nikaibana zipu haraka haraka hapo najikaza nisianguke.! Ningechelewa ningeiokotea magotini.. Haha.! Nyieeeeh'..!

Niliinua vitu vyangu ardhini bila kugeuza hata shingo kwa aibu, nikajikuta napanda daladala niliyokutana nayo ya kwanza ambayo hata haina uelekeo ninaoenda shida yangu tu ni kuondoka lile eneo, catwalk ikapotea ghafla ikawa ni mwendo wa kuruta, nimekaa kwenye daladala nikawa nahisi kama kila mtu anajua kilichotokea.!!

Ila tbh, nilijifunza kitu kikubwa sana siku ile,

anyways, nimejikuta tu nashea.!! Uliwahi aibika mbele za watu.? Ilikuwaje.?
 
Umenikumbusha zamani kuna mdada alikaa vibaya nikamfata kumwambia kama amekaa vibaya.(chupi inaonekana) kumkaribia namwita dada alifoka huyo nenda kanyonye huko unataka nitongoza nini?

Duh nikamwambia chupi nyekundu ulovaa watu wanaiona aliruka huyo. machali walibaki kumwambia papuchi yako inaonesha tamu. Baadhi ya wanawake wakiitwa akili zao wanaona wanataka kupewa mtongozo tu.

Lunatic
 
Kwa mlioko Dar, Poleni kwa mgao wa kuanzia maji, umeme mpaka mapenzi, ila ndugu zangu tutafika kwa Baba tuko hoi sana maskiini, imagine duniani tunateseka hivii na bado huko naskia kuna moto tena..! Nyieeeeeeh'..!
Hiki kisa ni cha siku nyingi, why ukilete usiku hivi? Muda huu, umenyimwa kitu au umenyima kitu? Ndoa ngumu mazee, mwenyewe nimeamshwa kuulizwa masuala fulani hivi;-
 
Umenikumbusha zamani kuna mdada alikaa vibaya nikamfata kumwambia kama amekaa vibaya.(chupi inaonekana) kumkaribia namwita dada alifoka huyo nenda kanyonye huko unataka nitongoza nini? Duh nikamwambia chupi nyekundu ulovaa watu wanaiona aliruka huyo. machali walibaki kumwambia papuchi yako inaonesha tamu. Baadhi ya wanawake wakiitwa akili zao wanaona wanataka kupewa mtongozo tu.


Lunatic
Ulikuwa katoto nini? Hiyo "nenda kanyonye"
 
Ila hizi mambo zetu wadada za kuignore na kuringa tukiitwa barabarani na watu tusiowafahamu sometime sio kabisa😂😂

Imewahi nitokea nakumbuka enzi za chuo hiyo siku weekend tumetoka hostel na shosti yangu lengo tukatafute msusi ila tukaenda mtaa ambao hatuufahamu vizuri.

Sasa tuko busy tunabahatisha njia tukapita sehemu wakaka wamekaa kama wa4 hivi na ilikua kama garage hizi za mtaani tu ambazo sio rasmi wakawa wanatuita aah tukakaza huku tunaambiana hao vipi kutuita ita hamna kuitika! Lahaulaaa kumbe tulipokua tunaelekea mbele hakuna njia inatoka😂😂 hiyo njia ilikua inaenda ishia nyumbani kwa mtu! Kufika mbele hatuoni njia yaan kwanza tulijikuta tunacheka na aibuu maana tutapita vipi pale na tumegoma kupokea salamu zao.

Ikabidi turudi na kukutana nao tena tukawasalimia kwa aibu yaan walitupa maneno kibao tukajikaza na kuwauliza njia wakatuelekeza tukaendelea na safari yetu.
Kiukweli tangia siku hiyo kiburi barabarani niliweka pembeni salamu za watu naitikia vema na kwa adabu.
 
Kwa mlioko Dar, Poleni kwa mgao wa kuanzia maji, umeme mpaka mapenzi, ila ndugu zangu tutafika kwa Baba tuko hoi sana maskiini, imagine duniani tunateseka hivii na bado huko naskia kuna moto tena..! Nyieeeeeeh'..!
Pole halafu safi na Kisha koma!. Ndo muache ubishi mnajionaga Sana nyie wadada tena ningalikuwepo ningelipanda nawewe hiyo gari nikautangazie uma humo garini..🤣
 
Tulienda kwenye harusi,muda wa kufungua champagne Mc akatangaza anataka watu nane watu hakuna nikasema ngoja niende na mimi.

Jamani wote champagne zao zilifunguka faster mimi sasa nilijikuta mwenyewe mbele watu wananiangalia na chupa haijafunguka.Niliitikisa ile chupa kama chibuku.

Mpaka kuja kufunguka watu walishachoka kuniangalia,sherehe niliiona chungu sikunyanyuka tena mpaka muda wa kuondoka.
 
Hii akili ipo

"Mwanaume akimsimamisha mwanamke njiani akili yake ya kwanza inajua unataka kumtongoza.
Mwanaume ukisimamishwa na mwanamke njiani unahisi huyu ana shida"

Katika harakati zangu huwa najizuia saana kuzungumza na mwanamke nisiyemfahamu.
 
Tulienda kwenye harusi,muda wa kufungua champagne Mc akatangaza anataka watu nane watu hakuna nikasema ngoja niende na mimi.
Jamani wote champagne zao zilifunguka faster mimi sasa nilijikuta mwenyewe mbele watu wananiangalia na chupa haijafunguka.Niliitikisa ile chupa kama chibuku.

Mpaka kuja kufunguka watu walishachoka kuniangalia,sherehe niliiona chungu sikunyanyuka tena mpaka muda wa kuondoka.
🤣🤣🤣 i can imagine, pole sana daah.

Umenikumbusha kitambooo nilienda kijijini kwenye harusi ya bro, siku ya harusi muda wa kufungua champagne wakatangaza watu waende me nikamute kwa kiti maana nilikua sijawah hata kuishika kufungua na sijui.

Kuna aunt tulitoka nae huku town akaniita akaniambia mwanangu njoo ufungue hii uwii nilitamani kukataa ila nakataaje na kila mtu kasikia nilivyoitwa!! Bana wee nikajikaza pale mbele nikamwambia kwa sauti ya chini aunt me sijawah kufungua hii akaniambia ni simpo usihofu we itikise af uwe unaniangalia mimi navyofungua.

Kweli nikapambana ila sasa kwenye kutoa kile kizibo badala ya kutolea kidole gumba me nikakivuta na vidole vyote huku nimeiface aisee ilifunguka ikanirukia usoniiii na kwenye nguo kidogo daah nilijiskia aibu sana nikajikaza nikaenda kumiminia wageni hivyo hivyo nikatafuta maji nikanawa nikatulia.
 
Niliwahi taka kuruka kwenye daladala kama makondakta wanavyofanya,aisee siji sahau namna nilivyolamba lami,na ilikua mchana kweupee.

Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
Hahahaa kuna dada nae alijifanya mbabe akashuka gari bado halijasimama ebhana alianguka vibaya mwili wote ulijaa vumbi maana si kwa kugaragara kule
 
Tulienda kwenye harusi,muda wa kufungua champagne Mc akatangaza anataka watu nane watu hakuna nikasema ngoja niende na mimi.
Jamani wote champagne zao zilifunguka faster mimi sasa nilijikuta mwenyewe mbele watu wananiangalia na chupa haijafunguka.Niliitikisa ile chupa kama chibuku.

Mpaka kuja kufunguka watu walishachoka kuniangalia,sherehe niliiona chungu sikunyanyuka tena mpaka muda wa kuondoka.
Pole mkuu, Kuna harusi nilihudhuria miezi 2 iliyopita, sasa MC kaita mdada aliyependeza akafungue champagne,, mara paap kanyanyuka mdada na mashauzi kama yote, alikuwa kashaanza kulewa, sasa kumbe alilowana km Ni hivi obviously alienda toilet akajiswafi na vuzi lake maji yakalowesha au alianza breed, Sina hakika maana rangi ya nguo ilikuwa maroon,, watu wakamuita ili kumzuia, dada akahisi wanamshangilia yaani ndo biize kubinua mgongo anacheza kwa madoido,,, aibu niliyopata siku ile Kama ndo mie Yani

By the way, tangu nilipopataga breed katikati ya hadhara na mie sinaga kuumwa tumbo, Sina hili Wala lile,, nachoshukuru tu nyuma yangu alikuwepo mkaka naefahamiana nae aliniita taratibu akasema umechafua nguo yako, akavua sweta, nikajifunga, nilipata fundisho kubwa mno nilipunguza kabisa mashauzi kwa wakaka, hivyo hutokea unapita sehemu hadhara inakupa umakini wao,, Cha Kwanza huwa najiwazia nguo,, ni zipu Kama ya mtoa mada, nikijikagua akilini nikaona niko poa najua wadau wanashangaa uumbaji wa Mungu tu

Wanaume mna roho nzuri Sana katika hizi ishu mbarikiwe mno huwa mnatusitiri Sana kuliko wanawake wenzetu, anakuona unaaibika ila ndo kwanza anamuonyesha na mwenzie
 
Back
Top Bottom