Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,862
Bora kuwa mkulima tuLeo nimepata bahati ya kuitazama mifuko yetu mitatu, NSSF, LAPF na PSPF jinsi wanavyokokotoa mafao yao.
NSSF:
Wanatumia wastani wa mshahara wa mwezi kwa miaka yako 3 ambayo ulikuwa unalipwa vizuri.
LAPF:
Wanatumia wastani wa mishahahara wako kwa mwaka
PSPF:
Hawa wanatumia Mshahara wako wa mwisho
Nimeweka assumption zifiatazo
Haya nimeassume kwamba wastani wa mshahara, au mishahara ya miaka 3 au mshahara wako wa wisho ni 2000,000. Pia nimeassume kwamba mwanachama amechangia miezi 180 tu kama kiwango cha chini cha mtu kuwa na sifa ya kupata Mafao.
Mafao kwa mujibu wa NSSF:
Initial Lumpsum 23,275,862.07/=
Monthly Pension 465,517.24/=
Mafao kwa mujibu wa LAPF:
Aina ya Mafao: Retirement(Old) Benefits
Muda Uliochangia (MIEZI): 180
Wastani wa Mshahara kwa mwaka (TSZ): 24,000,000.00
Pensheni ya Mwezi (TZS): 333,333.33
Pensheni ya Mkupuo (TZS): 62,000,000.00
Mafao kwa mujibu wa PSPF
Kama umeairiwa kabla ya july 2014
Initial lumpsum 62,000,000.00 Tsh
Montly pension 333,333.33 TSH
Kama umeajiriwa baada ya july 2014
Initial lumpsum 23,275,862 Tsh
Montly pension 465,517 Tsh
Maoni yangu:
1) Hawa jamaa kwa kiasi fulani wanatumia formula inayofanana. kimsingi hakuna ushindani kwenye formular ya kupata mafao.
2) PSPF wanatumia mshahara wako wa mwisho ni poa kidogo kwa kuwa mishahara mingi ya mwisho huwa ni mikubwa. Kwa waajiriwa binafsi unaweza kuchangia pesa nyingi ya mwezi unapoelekea kustaaf kujiongezea mafao!!!
3) Kama unataka kula fungu la uhakika ukifikisha umri wa kustaaf, bora ujiunge mapeema na LAPF, ingawa malipo yako ya mwezi yatapungua lakini malipo ya awali yatakuwa karibu mara tatu ya pesa zinazotolewa na mifuko mingine . Changamoto ni jinsi ya kupata wastani wa mishahara kwa mwaka, kama wanatumia miaka yote ni hatari kwa kuwa mishahara ya awali unapoanza kazi huwa midogo sana.
4) Kwa kigezo cha hapo juu ni bora PSPF kwa kuwa wanatumia mshahara wako wa mwisho, hasa kwa kwa wale ambao waliajiriwa kabla ya july 2014.
5) Kimsingi hakuna tofauti ya mafao/formular kwa LAPF na PSPF kwa wale walioajiriwa kabla ya july 2014.
6) Hakuna tofauti ya mafao/formular baina ya NSSF na PSPF kwa wale walioajiriwa baada ya july 2014.
Mwisho: Ikiwa wanatumia formular zinazofanana! kuna haja gani ya kuwa na mifuko lukuuuki?
Wenu
Tume ya katiba
Haturuhusiwi kuhoji kuhusu pato la taifa, kuwa mzalendo.Ukokotozi wa Pato la Taifa hutumia formular gani maana Uchumi unakuwa kila kukicha.
Aisee.Haturuhusiwi kuhoji kuhusu pato la taifa, kuwa mzalendo.
Mkuu hilo jina lako kati ya f na w ukiongeza i na l litasomekaje?Ukokotozi wa Pato la Taifa hutumia formular gani maana Uchumi unakuwa kila kukicha.
Weka hizo herufi nione huenda ndio jibu la swali nililoulizaMkuu hilo jina lako kati ya f na w ukiongeza i na l litasomekaje?
Kwanza inabidi ujue tu sahivi mifuko yote inatumia harmonization rule iliyotolewa na SSRA july 2014, kwahyo member wa mifuko yote watakuwa computed sawa kwenye mafao ya uzeeni (old-age pension) na lumpsum zao, isipokuwa wateja wa PSPF na LAPF ambao walikuwa wanachangia before july 2014,Naomba kujulishwa zaidi kwani formula zimekaaje?
Mimi niliyeanza kazi 2016 July mafao yangu yakoje?
Mimi nipo PSPF!
Unakua Mifukoni mwa watu au kwennye makaratasi??Ukokotozi wa Pato la Taifa hutumia formular gani maana Uchumi unakuwa kila kukicha.
LAPF MASKINI, HAWANA KITU WALA SENTI YA KULIPA MAFAO.
HERI YA PSPF.
Mkuu kwamza nikushukuru kwa mchanganuo wako..Weka hizo herufi nione huenda ndio jibu la swali nililouliza
Serikali ndio imesema hivyo mkuu na mimi nikapata ukakasi wa jambo hilo nikataka kulijua kwa undani. Uzuri mleta uzi kaja na formular za ukokotozi wa mapato nikaamua kumuuliza nilidhani huenda anaijua na formula ya kukokotoa Pato la Taifa kumbe kasema ni marufuku kuhoji hicho kitu.Unakua Mifukoni mwa watu au kwennye makaratasi??
Mkuu,Mkuu kwamza nikushukuru kwa mchanganuo wako..
Hapo mwisho kwenye No 7 sijaelewa, unaweza kufafanua kidogo
PPF wapo wapi hapa...
Tuwekee na Formula ya GEPF pia tuthaminisheLeo nimepata bahati ya kuitazama mifuko yetu mitatu, NSSF, LAPF na PSPF jinsi wanavyokokotoa mafao yao.
NSSF:
Wanatumia wastani wa mshahara wa mwezi kwa miaka yako 3 ambayo ulikuwa unalipwa vizuri.
LAPF:
Wanatumia wastani wa mishahahara wako kwa mwaka
PSPF:
Hawa wanatumia Mshahara wako wa mwisho
Nimeweka assumption zifiatazo
Haya nimeassume kwamba wastani wa mshahara, au mishahara ya miaka 3 au mshahara wako wa wisho ni 2000,000. Pia nimeassume kwamba mwanachama amechangia miezi 180 tu kama kiwango cha chini cha mtu kuwa na sifa ya kupata Mafao.
Mafao kwa mujibu wa NSSF:
Initial Lumpsum 23,275,862.07/=
Monthly Pension 465,517.24/=
Mafao kwa mujibu wa LAPF:
Aina ya Mafao: Retirement(Old) Benefits
Muda Uliochangia (MIEZI): 180
Wastani wa Mshahara kwa mwaka (TSZ): 24,000,000.00
Pensheni ya Mwezi (TZS): 333,333.33
Pensheni ya Mkupuo (TZS): 62,000,000.00
Mafao kwa mujibu wa PSPF
Kama umeairiwa kabla ya july 2014
Initial lumpsum 62,000,000.00 Tsh
Montly pension 333,333.33 TSH
Kama umeajiriwa baada ya july 2014
Initial lumpsum 23,275,862 Tsh
Montly pension 465,517 Tsh
Maoni yangu:
1) Hawa jamaa kwa kiasi fulani wanatumia formula inayofanana. kimsingi hakuna ushindani kwenye formular ya kupata mafao.
2) PSPF wanatumia mshahara wako wa mwisho ni poa kidogo kwa kuwa mishahara mingi ya mwisho huwa ni mikubwa. Kwa waajiriwa binafsi unaweza kuchangia pesa nyingi ya mwezi unapoelekea kustaaf kujiongezea mafao!!!
3) Kama unataka kula fungu la uhakika ukifikisha umri wa kustaaf, bora ujiunge mapeema na LAPF, ingawa malipo yako ya mwezi yatapungua lakini malipo ya awali yatakuwa karibu mara tatu ya pesa zinazotolewa na mifuko mingine . Changamoto ni jinsi ya kupata wastani wa mishahara kwa mwaka, kama wanatumia miaka yote ni hatari kwa kuwa mishahara ya awali unapoanza kazi huwa midogo sana.
4) Kwa kigezo cha hapo juu ni bora PSPF kwa kuwa wanatumia mshahara wako wa mwisho, hasa kwa kwa wale ambao waliajiriwa kabla ya july 2014.
5) Kimsingi hakuna tofauti ya mafao/formular kwa LAPF na PSPF kwa wale walioajiriwa kabla ya july 2014.
6) Hakuna tofauti ya mafao/formular baina ya NSSF na PSPF kwa wale walioajiriwa baada ya july 2014.
7) Kama wewe ni mchangiaji wa NSSF au PSPF( kwa wale walioajiriwa baada ya july 2014), kuna uwezekano mkubwa sana wa kufa na kuacha pesa nyingi sana kwenye mfuko wako. Ni ngumu kwa mtu mwenye umri wa 55-60 kuipata pesa yote iliyobaki.
Mwisho: Ikiwa wanatumia formular zinazofanana! kuna haja gani ya kuwa na mifuko lukuuuki?
Wenu
Tume ya katiba