Vijana 'wapiga dili' ndani ya vyama vya kisiasa... Solution.

Vijana 'wapiga dili' ndani ya vyama vya kisiasa... Solution.

Tuko

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2010
Posts
11,180
Reaction score
7,354
Ndugu wanaJF nimerudi kutoka ban,
Nilikula ban kutokana na kushindwa kudhibiti hisia zangu, kwenye ile thread ya Ben Saanane, ikiwa ya kwanza kati ya hizi threads za masalia. Nilikasirika sana. Hata hivyo nikiwa pembeni kama guest, nimepata muda wa kutafakari kwa kina 'tatizo' la msingi la hawa vijana

Mwaka 2002 nikiwa mwanafunzi SUA, nilipata nafasi ya kuwasoma viongozi wa serikali ya wanafunzi (SUASO). Mara nyingi nilipokuwa sekondari, viongozi walikuwa wanachaguliwa miongoni mwa wanafunzi waliokuwa wanaonekana kuwa makini kimaadili, kimasomo na waliokuwa na uwezo wa kuongoza. Nilitarajia chuo kikuu hali itakuwa kama hiyo, tena ikifanywa kwa umakini zaidi.

Nilichojifunza baadae ni kuwa viongozi wa serikali ya wanafunzi pale SUA walikuwa watu wa hovyo kabisa, wenye uwezo mdogo kiuongozi, wala na watoa rushwa wakubwa na kwamba watu walikuwa wanatafuta uongozi pale kwa sababu ya kufuata hela pale ofisini. Nilifadhaika sana na sikutamani kabisa kuingia kwenye mchakato wa uongozi. Mwaka 2004 'nilijikuta nimechaguliwa kuwa 'waziri' katika SUASO baada ya best yangu mmoja kuwa raisi wa SUASO na kwa kuwa mimi ndiye nilikuwa namsaidia kuandika speech na ushauri mwingine, akanipa uwaziri kama fadhila. Hapo nilipata nafasi ya kukutana na viongozi wa vyuo vingine wakiwemo wa UD. Nilishangaa sana baada ya kugundua kuwa viongozi wa vyuo vingine nao walikuwa watu bogus, 'wapiga dili' za ela tu. Nakumbuka sekondari nilisoma na vijana waliokuwa na uwezo mkubwa sana wa uongozi ambao walikuwa UD by then, lakini aina ya viongozi wa UD niliokuwa nakutana nao kwenye vikao, nilishangaa sana...

Nilikuja kusikitika sana baadae nilipokuja kugundua kuwa vijana hawa bogus, waliokuwa wapiga dili na kupata uongozi vyuoni, ndio baadae walikuwa viongozi wa vyama vya siasa wakienda mtaani. Kwa mfano, nakumbuka kulikuwa na raisi wa SUASO aliyekuwa anaitwa Kenneth Nollo, ambaye baadae nilikuja kushangaa eti alikuja kuwa kiongozi wa UVCCM huko Dodoma!!! Nilishangaa maana nilikuwa namfahamu huyu jamaa kuwa na uwezo mdogo saaaana kiungozi na kiakili!!! Hakuwa hata na akili za kuwa monita wa darasa... Lakini ghafla akaingia UVCCM na akawa kiongozi.

Ndugu wanaJF, baada ya historia fupi hapo juu, nirudi kwenye topic kuwa kwa sasa vyama vya siasa vimejaa vijana wapiga dili. Hawana uchungu wa nchi, hawana uchungu na chama cha siasa, na wako radhi kununuliwa hata kwa sh 10,000 akafanya kitu ambacho hukutarajia. Nilisikitika sana kwamba wakati fulani tulimkabidhi kijana mmoja aliyekuwa anaitwa Darabe uongozi wa CDM pale SUA, lakini ndani ya miezi michache nikamwona Darabe amekuwa mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Manyara.

Vijana wapiga dili wamejaaliwa kipaji cha kuongea na kushawishi na wanatumia vipaji hivyo kujipenyeza kwa haraka sana kwenye uongozi wa vyama vya siasa.
Kwa bahati mbaya kutokana na michezo michafu inayochezwa na vijana na viongozi wengine wapiga dili, ni vijana wachache sana makini walio tayari kutafuta nafasi za uongozi kwenye vyama vya siasa. Wapo maelfu ya vijana makini, wenye uwezo mkubwa wa kuongoza, waaminifu na wenye uchungu na nchi hii, lakini hawapo kwenye vyama vya siasa.

Nini kifanyke?
Hili sio suala la chama kimoja. Wapiga dili wapo kwenye kila chama hususani vile vyenye fursa za 'dili' (ela). Kwa bahati mbaya, kwa chama kama CCM ambacho fursa za dili ni kubwa zaidi na zimekuwepo kwa muda mrefu zaidi, tatizo hili limeshaota mizizi mirefu sana, japo ipo nafasi fulani wanaweza kulidhibiti. "Wazee" wengi waliopo CCM ni wapiga dili ambao wamepata fursa hizi hasa baada ya chama kuwapoteza watu makini kama Nyerere. Tembelea nafasi za walaya, mikoa, na hata taifa utakuwa CCM inaongozwa na watu wenye historia ya kuwa wapiga dili, na ambao wanafanya kila linalowezekana kuhakikisha nafasi za vijana katika chama chao zinachukuliwa na watoto wao ambao wengi ni wapiga dili... Mifano iko mingi na wazi.

CDM nayo kwa bahati mbaya imeshakuwa 'infested' kwa kiasi kikubwa na wapiga dili. Simtaji mtu, lakini sote tunashuhudia vijana waliopewa nafasi mahsusi kabisa ndani ya chama, wakionyesha dalili zote za kununuliwa kwa bei nafuu na 'wazee wapiga dili', kwa maslahi ya kisiasa.

Solution...
Haina maana mtu kulima kwa kukwatua majani, na kuyaacha yamesimama nyuma yako, ukienda hatua kadhaa mbele eneo lote ulilolima limestawi majani. Haina maana kwa chama kama CDM, kutumia mabilioni ya shilingi, masaa mengi na nguvukazi nyingi za viongozi kufanya kazi ambayo haitakuwa na progressors. Wakati sasa umefika, kwa kutumia viongozi wajuu wachache wenye maadili, vyama vi-groom viongozi wenye maslahi na chama na nchi, na kuepuka hawa wapiga dili. Vyama viwe na timu za usajili, kama zilivyo club kubwa za soccer, ambazo kazi zao ni kuwa identify, pursuade, recruit and test 'wachezaji' mahiri miongoni mwa vijana ambao watawasuccess kwa maendeleo ya chama. Naamini kabisa waanzilishi na wajenzi wa chama kama CDM walikuwa na objectives zao za muda mfupi na muda mrefu. Naamini mzee Mtei, mathalani, amefanya kazi kubwa kuhakikisha wanaopata nafasi za kuingoza CDM hata sasa, wana uwezo wa kubeba ile dhamira aliyokuwa nayo alipoakianzisha. Viongozi mliopo sasa, Mbowe, Arfi, Slaa na Zitto na wengine, mna deni la kuhakikisha kuwa kesho kama sio nyie mnaoongoza CDM, then wanaoongoza wana uwezo, nia na dhamira kama mlizo nazo nyie. Wekeni timu za usajili zinazojumuisha watu makini kwenye vyuo na maeneo mengine walipo vijana, ambazo kazi yake ni kuidentify vijana potential na kuwapa taarifa, then kwa heshima kubwa viongozi wa chama wawe wanawaaproach vijana hao wajiunge na chama, na waingie katika michakato ya uchaguzi katika chama.
Demokrasia iwepo ndio, lakini wanachama wapewe fursa ya kuchagua miongoni mwa watu ambao ni tested, ili makosa yasijirudie.

Viongozi wa CDM kama ni wakati ndio huu... lakini mkichelewa hadi nafasi zenu zikashikwa na wapiga dili, mjue kuwa nguvu zenu mlizotumia, ni sawa na kusia mbegu juu ya jiwe.

Asanteni...
 
ni kweli usemayo Tuko...nami nimeshuhudia vijana wa aina hiyo wasiokuwa na uwezo wa uongozi wala vision bali ni wazungumzaji na wenye maneno ya ushawishi na uroho wa fedha za wanafunzi chuoni, wakishika nafasi za uongozi vyuoni na baadaye kwenye vyama vya siasa, wawili nimesoma nao,mmoja mwaka jana alikwenda halmashauri flani akawaingiza mkenge kwenye mradi wa mamilion ya shilingi....bahati nzuri walikuja wakamkamata na kutaifisha mali zake alizopata kutokana na wizi ule...ana nafasi kwenye cdm mkoa flani hapa nchini na ana ndoto za kuwa mbunge, mwingine aliiba mamilioni ya fedha za wanafunzi chuoni akazuiwa kugraduate na akapewa condition ya kurudisha fedha zile alizoiba, hawa wawili ni marafiki na walikuwa viongozi kwenye serikali ya chuo enzi hizo....ni hatari kwakweli kwa ustawi wa taifa hili
 
Pamoja sana na umenikumbusha taswira ya vijana niliokutana nao pale udsm enzi hizo. Baadhi yao wapo CHADEMA na wengine CCM
 
vizuri sana.
Kwa kweli wengi katika hawa vijana wasomi wenye historia ya serikali za wanafunzi vyuoni ni wa ajabuajabu

nina hakika kwamba kama ni kuchuma,basi chadema wamachuma janga.

Nilikuwepo udsm kuanzia 2005. Nawajua baadhi ya walioshikilia daruso wakati huo ambao wapo kwenye siasa za upinzani leo.

Na amini,ni waroho wa vyeo,fedha,na washerati wachafu wakubwa.

SOLUTION:
-Hiyo change nayoiona ikiongelewa kwenye m4c,inatakiwa kujikita kubadilisha mitizamo ya watz na pia iwe katika kuandaa viongozi waadilifu na wanaozingatia maslahi ya jamii kubwa.
-ukifuatilia maneno ya huyo mwanamke anaitwa juliana shonza,unaona kabisa kwamba ni mtu ambaye hajaweza kbs kujitambua,pamoja na cheo kikubwa cha makamu wa Bavicha Taifa.

Kutojitambua ni shida ya wahitimu wetu wengi vyuoni,na si yeye tu.

Uwepo utaratibu wa kuwapiga msasa vijana hao wanaotoka vyuoni. Katika vitu ambavyo nimekuwa nikivifikiria ni kwmb iwepo internership kwa wanaotarajia kuingia kwenye soko la ajira,na hao wanaoingia kwenye siasa.

Vinginevyo kwa kuokoteza hawa graduate wa madesa,kuna aibu kubwa zaidi ya hii inakuja.

Nawasilisha.
 
Ni kweli kabisa ndugu , kama haya mambo yangeanza mapema , nadhani hivi leo tusingeona hata hizi Thread zao za kijinga .
 
ni kweli usemayo Tuko...nami nimeshuhudia vijana wa aina hiyo wasiokuwa na uwezo wa uongozi wala vision bali ni wazungumzaji na wenye maneno ya ushawishi na uroho wa fedha za wanafunzi chuoni, wakishika nafasi za uongozi vyuoni na baadaye kwenye vyama vya siasa, wawili nimesoma nao,mmoja mwaka jana alikwenda halmashauri flani akawaingiza mkenge kwenye mradi wa mamilion ya shilingi....bahati nzuri walikuja wakamkamata na kutaifisha mali zake alizopata kutokana na wizi ule...ana nafasi kwenye cdm mkoa flani hapa nchini na ana ndoto za kuwa mbunge, mwingine aliiba mamilioni ya fedha za wanafunzi chuoni akazuiwa kugraduate na akapewa condition ya kurudisha fedha zile alizoiba, hawa wawili ni marafiki na walikuwa viongozi kwenye serikali ya chuo enzi hizo....ni hatari kwakweli kwa ustawi wa taifa hili

Vijana hawa wanatumia udhaifu na hofu ya viongozi wao wa juu wa vyama kupiga dili kwa sababu hata ukiwauliza kazi zao za msingi zenye kuwapa kipato hawana majibu, wanakula kwenye migongo ya wanasiasa, hawana nidhamu na wako tayari kumtukana mtu yeyote ili mradi wawe na uhakika wa kupata mlo wao, siasa za namna hii ndio zinaiponza Tanzania ya leo.
 
Hoja muafaka na inayohitaji kupewa uzito stahiki. Huu ndio umekuwa utamaduni wa siasa za Bongo na matokeo yake ni machungu tunayoyaonja kila kuchapo. nasikia hata mukulu wa nchi wa sasa naye alikuwa katika serikali ya DARUSO enzi hizo. Ukisikiliza madudu aliyokuwa akiyafanya kutoka kwa waliokuwa wanafunzi wenzake unabakia mdomo wazi - ilikuwaje akafikia kuwa mukulu!!!!!!!!!!!!!!
 
-Mara nyingi sana nimekua nikiandika kuhusu umuhimu wa vyama vya siasa kufanya grooming na kuandaa darasa la itikadi kwa vijana ili kujenga loyalty.Kijana ambaye ni Loyal kwa chama atakilinda kwa gharama zote.Unapoteleza ukiwa umembeba mwanao mpendwa hata kama umefanya uzembe utahakikisha unamlinda mtoto hata kama utajuruhiwa wewe.

Huwezi kuwa loyal ukatukana au kufanya chochote cha kuafanya sabotage na ukajisikia huru.

Tuliingia kwenye mfumo wa vyama vingi huku elimu ya uraia na mfumo wa kisiasa ukiwa shaghalabaghala.Leo hii huwezi kujadili itikadi na ukaeleweka vyema.Utaambiwa Itikadi ya nini wakati tuna njaa?Na hili ni widely in Africa

-Cross carpeting kwa vyama vya siasa pia inatokana na matatizo haya haya ya kutokua na msimamo wa kiitikadi na si kwa vijana tu hata kwa wazee.I hate this behaviour

-Leo hii mtu atatafuta watu wa kumuunga mkono kwa kuwa anajua kuna ombwe la fikra kwa vijana na hawatahoji au hawawezi kufikiria unamuunga mtu mkono based on which policy/ideology.

-Tuache kuifanya siasa kuwa kama mashindano ya washiriki wa big brother Africa tu

Mada nzuri sana hii
 
Njaa kali hao jamaa kichwani hamna kitu matokeo yake wananunulika kama mpira wa kiume
 
Unajua kufanya siasa bila kufuata maadili na nidhamu ni vurugu!.. Mfano mdogo ni vijana wa MASALIA kununulika na kuimba wimbo mmoja na magamba kwa maslahi ya wachache!.. Unapokuwa na mtu mwenye matamanio ya kuwa rais wa nchi akinunua na kurubuni vijana waliojeruhiwa katika siasa ni hatari kwa usalama na amani ya nchi!.. Wengi hawana subira. WAMEJAA wivu na tamaa ya utajiri kwa njia za mkato!
 
Njaa kali hao jamaa kichwani hamna kitu matokeo yake wananunulika kama mpira wa kiume

mkuu,njaa ni kitu kimoja na kuendekeza njaa ni kingine kabisa. Maisha yoyote bila resillience huishia kwenye matendo ya kikahaba,-na hicho ndicho kinawasumbua hawa wajinga.

Na sio katika siasa tu.

Tanzania imejaa wapiga deal kila kona ya kila sekta,wazee kwa vijana.

Hii ni changamoto kwa uongozi wa chadema. Nafahamu uwezo wa viongozi waandamizi wa chama hiki.yafaa hili lishughulikiwe kisayansi zaidi. Vizuri limeibuka mapema.

Kijana wa chadema kuitikia vibwagizo vya Nape Nnauye au Mwigulu Nchemba ni aibu kubwa.
 
Umegusa pale hasa na bahati nzuri umezungumzia swala hili kimtazamo wa taifa tatizo la ufisadi lina mzizi mkubwa huku chini huwa najiuliza kwanini kwenye chaguzi za serikali za wanafunzi kuna matumizi makubwa ya pesa kama kuchapisha fulana,vipeperushi na kuambatana na ofa mbali mbali na mbaya zaidi hao viongozi wakitoka hapo ndio wanajiunga na vyama vya siasa na kupewa nyazifa mbali mbali za uongozi lakini vile vile nimefurahi kwa suluhisho ulilotoa kwamba vyama vianze kutafuta watu makinibadala ya kutupia jicho sehemu moja tu wote tunajua sasa hivi ajira imekuwa ngumu kwahiyo wengine wamegeuza siasa kama ajira ndio maana tunaona watu wenye akili zao wakitangatanga wakati tunajua kabisa mtu anapojiunga na chama ni kwa sababu amekubali itikadi ya chama husika hilo sio janga la chama bali ni janga la kitaifa
 
wengi ni watapeli, wapenda umalaya na mengine ya fastafasta.CDM itakuwa nao wengi kwa vile CDM ilikuwa ni kama "land of opportunities". Kil akijana mwenye kuweza aliwezeshwa.Sasa hawa wana vyuo wengine wa mishmishe walikuwa wakijuana tangu vyuoni na ndio hao hao wakapeana michongo.hao ndio ho wakishapata nafsi wanakuwa matozi na kuwa watu wakujiachia sana.Ktk kujiachia ndipo budget inaanza goma, ndio huko huko wanajikuta kuwa wanapewa story ya utamu wa hel ay amafisadi.Kw atamaa wanaulizia nani wa kuwaweka, ndipo watoto wa mjini Presidaa na minister makers wanapowasogeza karibu na machinjio ya wajinga kwa mafisadi.
 
Naamini kila chama makini kina kila sababu ya kuwa na kitengo cha nursery. Iwe ni kurugenzi inayojitetea, na pamoja na kuruhusu na kupokea vijana na wanachama wengine wapya, kurugenzi ifanye kazi kiinteligensia. Kijana yeyote anayejiunga chamani na akaonyesha nia au potentiallity ya uongozi afunguliwe faili la siri litakatafiti na kurekodi mienendo yake japo kwa miaka mitano, kabla mtu huyu hajaletwa mbele ya kadamnasi kupigiwa kura.
 
Naamini kila chama makini kina kila sababu ya kuwa na kitengo cha nursery. Iwe ni kurugenzi inayojitetea, na pamoja na kuruhusu na kupokea vijana na wanachama wengine wapya, kurugenzi ifanye kazi kiinteligensia. Kijana yeyote anayejiunga chamani na akaonyesha nia au potentiallity ya uongozi afunguliwe faili la siri litakatafiti na kurekodi mienendo yake japo kwa miaka mitano, kabla mtu huyu hajaletwa mbele ya kadamnasi kupigiwa kura.

Nilishawahi sema humu humu JF, anayetaka uongozi CHADEMA lazima awe safi. Haitakuwa na maana kupiga kelele kwa walioko madarakani kuwa ni wachafu, wala rushwa, mafisadi n.k huku ndani ya CHADEMA kuna watu ambao sio waadilifu na wanania ya kuchukua uongozi, vilevile itatoa nafasi ya vijana kujihoji wenyewe kabla ya kuamua kuchukua nafasi kwenye vyama vya siasa. Naomba hili lisiwe upepo tu likapita hivihivi au kuishia JF.
 
Kuna kijana wa CDM amekuwa akijitangaza kama rais mtarajiwa humu ndg zangu na aligombea ubunge huko lushoto uwezo wake ni mdogo sana. HII MADA naunga mkono leo kama wabunge wa magamba bungeni kwa asilimia 100%.
 
Back
Top Bottom