OMOYOGWANE
JF-Expert Member
- Dec 30, 2016
- 3,646
- 9,226
Mwana saikolojia ABRAHAM MASLOW anasema kwamba, kupenda au kupendwa ni hitaji la msingi akimaanisha kuwa na mke, watoto na familia kiujumla ni hitaji la msingi la kila binadamu.
Ikitokea mtu akawa anaenda kinyume na hitaji hilo mfano kampeni ya kataa ndoa, huyo mtu anakua anaenda kinyume na jamii na matakwa ya kibinadamu kiujumla.
Kisaikolojia ni mgonjwa na kuna sababu za msingi za yeye kuwa hivyo mfano kutelekezwa utotoni na mzazi au wazazi wote, kufanyiwa vitendo vya kikatili utotoni na mama wa kambo, kuishi kwenye familia yenye migogoro, kubakwa au kulawitiwa utotoni n.k.
Moja kati ya hizo sababu ndizo zinaperekea mtoto hasa hasa wa kiume kupata hasira na chuki ambazo hujichimbia kwenye ufahamu usiokuwa wa hiari yaani huko ukubwani anajikuta tu anachukia mambo ya familia/mahusiano bila yeye kujua wala kuwa na sababu za msingi.
Akiona matukio ya migogoro ya ndoa huitumia kama kielelezo cha kuhalalisha imani yake kuwa ndoa ni kitu haramu na mara nyingi huishi kwa kutembea na wanawake wengi
Ikitokea mtu akawa anaenda kinyume na hitaji hilo mfano kampeni ya kataa ndoa, huyo mtu anakua anaenda kinyume na jamii na matakwa ya kibinadamu kiujumla.
Kisaikolojia ni mgonjwa na kuna sababu za msingi za yeye kuwa hivyo mfano kutelekezwa utotoni na mzazi au wazazi wote, kufanyiwa vitendo vya kikatili utotoni na mama wa kambo, kuishi kwenye familia yenye migogoro, kubakwa au kulawitiwa utotoni n.k.
Moja kati ya hizo sababu ndizo zinaperekea mtoto hasa hasa wa kiume kupata hasira na chuki ambazo hujichimbia kwenye ufahamu usiokuwa wa hiari yaani huko ukubwani anajikuta tu anachukia mambo ya familia/mahusiano bila yeye kujua wala kuwa na sababu za msingi.
Akiona matukio ya migogoro ya ndoa huitumia kama kielelezo cha kuhalalisha imani yake kuwa ndoa ni kitu haramu na mara nyingi huishi kwa kutembea na wanawake wengi