Vijana wahitimu vyuo, tumshauri Amidu

Vijana wahitimu vyuo, tumshauri Amidu

Mgeni wa Jiji

JF-Expert Member
Joined
Jul 27, 2017
Posts
10,488
Reaction score
20,041
Habari wana JF wote! [emoji1538]

Msimu mpya wa elimu umeanza na wanafunzi nao wanaianza safari mpya ya kielimu, miongoni mwao yupo Amidu. Amidu ndio anaanza kidato cha kwanza ila mpaka sasa bado hajaripoti shule kutokana na kuwa njia psnda hasa juu ya malengo yake ya kimaisha, kulingana na hayo Amidu anatafuta ushauri kutoka kwa kaka na dada zake mliohitimu vyuo na vyuo vikuu hivi karibuni.

Malengo ya Amidu ni kuja kuwa na maisha bora kwa kuwa miongoni mwa matajiri wakubwa Tanzania, Amidu anasema kuwa anapendelea akiwa mkubwa kama mjomba wake Ally anataka awe na familia yake nyumba, biashara na pia ajikite kwenye siasa kwani anampenda sana mwanasiasa Lowasa ambaye pia Amidu anatamani kuwa tajiri kama yeye. Ally ambaye ni mjomba wa Amidu ni miongoni mwa vijana wahitimu wa vyuo mwenye umri wa miaka 28 anayeishi kwa dada yake ambaye pia ni mama wa Amidu.

Kwa simulizi hii fupi ya Amidu na hali halisi ya kimaisha unaweza kumshauri kitu gani Amidu ili azifikie ndoto zake hizo.
d21c00da8a21fdd961193e5454925b5f.jpg
 
Mwambie maisha sio mashindano anataman mambo ambayo niyakupita ..we mwambie asali sana ili akifa azikwe vzr na uko mbinguni asikutane na moto.
 
Hahaha asihangaike sana ajitahidi afahamu kusoma na kuandika tu vinamtosha. Nchi hii hata muhitimu wa kozi ya ualimu hawezi au hafahamu kufundisha, huku tunatafuta vyeti tupate kazi za kuajiriwa na mishahara mikubwa. Elimu haina tija, bora aanze biashara mapema.
 
kama anapenda mashindano katika maisha mwambie ashindane na kifo pia
 
Back
Top Bottom