Vijana Andaeni Vyeti,Kuna Ajira Zingine Zaidi ya 8,000 Kumwagwa kabla ya June 30

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,049
49,733
NI mwendo wa ajira, ndivyo unavyoweza kusema baada ya jana serikali kutangaza ajira mpya 8,070 za kada ya afya ambazo mchakato wake unakaribia kuiva muda wowote kuanzia sasa.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Deogratius Ndejembi, ndiye aliyetangaza neema hiyo jana bungeni, huku akitoa angalizo kwa wakurugenzi wa halmashauri kutopitisha barua za uhamisho kwa watumishi ambao hawajatimiza miaka mitatu kwenye vituo vyao vya kazi.

Ndejembi alitoa ufafanuzi huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Minza Mjika, aliyehoji ni lini serikali itaongeza watumishi wa afya Hospitali ya Wilaya ya Meatu.

Akijibu swali hilo, Ndejembi alisema katika mwaka wa fedha wa 2022/23, serikali itaajiri watumishi wa kada ya afya 8,070 na baada ya taratibu za ajira kukamilika watumishi hao watapangwa kwenye halmashauri zote nchini, Meatu ikiwamo.

Alisema serikali imeendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya na katika mwaka wa fedha 2021/22 serikali iliajiri watumishi 7, 736 wa afya na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilipangiwa watumishi 104 na watumishi saba walipangwa Hospitali ya Wilaya ya Meatu.

Awali, akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Liwale (CCM), Zuberi Kuchauka kuhusu kuhama kwa watumishi wanaopangwa katika maeneo mbalimbali, Naibu Waziri Ndejembi alikiri serikali inatambua tatizo hilo na tayari inaweka mikakati kwenye ajira mpya ambazo watumishi wanatarajia kuanza kazi hivi karibuni.

Kuchauka, katika swali lake, alisema kumekuwa na wimbi kubwa la watumishi wa afya kuhama kwenye halmashauri hasa za pembezoni ikiwamo ya Liwale ambayo ilipata watumishi 80 na waliobaki sasa hawafiki 15.
“Watumishi wanahama 36 wanaletwa wawili, Je? serikali ina mpango gani wa kudhibiti huu uhamaji holela?” alihoji.

Ndejembi alisisitiza kuwa; “Tutaweka mikakati ambayo itadhibiti wimbi hili la watu kuhama na nichukue nafasi hii kuwaagiza wakurugenzi wa halmashauri ambao ndiyo waajiri katika maeneo hayo wahakikishe hawapitishi barua kwa mtumishi yeyote ambaye hajathibitishwa kazini.

“Mtumishi anatakiwa akae kituo chake kipya cha ajira angalau miaka mitatu, kwa hiyo wafuate utaratibu wasipitishe barua hizi ili watumishi hawa wafanye kazi, wameajiriwa kwenda kupunguza upungufu ambao upo kwenye maeneo hayo, sasa wakipitisha barua ili hawa wahame wanazidisha upungufu kwenye maeneo hayo.”
Ndejembi alisema watumishi hao walipoomba ajira hizo walikuwa tayari kufanya kazi eneo lolote la Tanzania.

My Take
Msipotoka Kimaisha Miaka hii ya Rais Samia kuanzia mkulima Hadi msomi basi hesabu maumivu maana baada yake wanakujga wale wa roho za korosho,nawakumbusha tu.
 
HIVI VIJANA 8000 NI SAWASAWA NA WAHITIMU WANGAP, MKULIMA NI HUYUHUYU AMBAE PEMBEJEO ANAUZIWA KWA BEI KUBWA, MFANYA BIASHARA NDO HUYUHUYU ALIYEJAZIWA KODI NA MATOZO, WAFANYAKAZI WALIO AJIRIWA NDO HAWAHAWA WENYE MISHAHARA MIDOGO NA GHARAMA ZA MAISHA ZINAZIDI KUPANDA KILA UCHWAO.
.
MACHAWA MDA MWINGINE MUACHE KUROPOKA USENG**
Naendelea kusisitiza usipotoka kimaisha awamu ya 6 sahau kuja kutoka..

Unaijua bei ya pembejeo ya Sokoni au unaropoka usenge tuu? Ruzuku a mbolea imetolewa Kwa kina nani zaidi ya wakulima?
Bei ya mazao Sasa sio ya 25,000 Bali ni kuanzia 70,000 hapa anafaidika nani?

Hizo elfu 8 plus elfu 12 za Walimu na madaktari plus zingine za kada tofauti ndani ya mwaka mmja kwako unaona ni kiasi kidogo? Hapo ni zaidi ya 20,000 Kwa mpigo..
Ikumbukwe Kuna mtu alishindwa kuajiri Kwa miaka 5 Kwa visingizio lukuki..
Tozo zipi unazozisemea wewe zilizokuongezea Ugumu wa Maisha?
Kwa.jinsi ulivyo mjinga maisha yaendelee kukunyoosha maana umebeba mzigo sio kichwa wakati wenzio wakiendelea kukamatia fursa..
TRA imetangaza zaidi ya nafasi 500 za kazi.
Screenshot_20230527-184810.jpg

 
NI mwendo wa ajira, ndivyo unavyoweza kusema baada ya jana serikali kutangaza ajira mpya 8,070 za kada ya afya ambazo mchakato wake unakaribia kuiva muda wowote kuanzia sasa.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Deogratius Ndejembi, ndiye aliyetangaza neema hiyo jana bungeni, huku akitoa angalizo kwa wakurugenzi wa halmashauri kutopitisha barua za uhamisho kwa watumishi ambao hawajatimiza miaka mitatu kwenye vituo vyao vya kazi.

Ndejembi alitoa ufafanuzi huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Minza Mjika, aliyehoji ni lini serikali itaongeza watumishi wa afya Hospitali ya Wilaya ya Meatu.

Akijibu swali hilo, Ndejembi alisema katika mwaka wa fedha wa 2022/23, serikali itaajiri watumishi wa kada ya afya 8,070 na baada ya taratibu za ajira kukamilika watumishi hao watapangwa kwenye halmashauri zote nchini, Meatu ikiwamo.

Alisema serikali imeendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya na katika mwaka wa fedha 2021/22 serikali iliajiri watumishi 7, 736 wa afya na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilipangiwa watumishi 104 na watumishi saba walipangwa Hospitali ya Wilaya ya Meatu.

Awali, akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Liwale (CCM), Zuberi Kuchauka kuhusu kuhama kwa watumishi wanaopangwa katika maeneo mbalimbali, Naibu Waziri Ndejembi alikiri serikali inatambua tatizo hilo na tayari inaweka mikakati kwenye ajira mpya ambazo watumishi wanatarajia kuanza kazi hivi karibuni.

Kuchauka, katika swali lake, alisema kumekuwa na wimbi kubwa la watumishi wa afya kuhama kwenye halmashauri hasa za pembezoni ikiwamo ya Liwale ambayo ilipata watumishi 80 na waliobaki sasa hawafiki 15.
“Watumishi wanahama 36 wanaletwa wawili, Je? serikali ina mpango gani wa kudhibiti huu uhamaji holela?” alihoji.

Ndejembi alisisitiza kuwa; “Tutaweka mikakati ambayo itadhibiti wimbi hili la watu kuhama na nichukue nafasi hii kuwaagiza wakurugenzi wa halmashauri ambao ndiyo waajiri katika maeneo hayo wahakikishe hawapitishi barua kwa mtumishi yeyote ambaye hajathibitishwa kazini.

“Mtumishi anatakiwa akae kituo chake kipya cha ajira angalau miaka mitatu, kwa hiyo wafuate utaratibu wasipitishe barua hizi ili watumishi hawa wafanye kazi, wameajiriwa kwenda kupunguza upungufu ambao upo kwenye maeneo hayo, sasa wakipitisha barua ili hawa wahame wanazidisha upungufu kwenye maeneo hayo.”
Ndejembi alisema watumishi hao walipoomba ajira hizo walikuwa tayari kufanya kazi eneo lolote la Tanzania.

My Take
Msipotoka Kimaisha Miaka hii ya Rais Samia kuanzia mkulima Hadi msomi basi hesabu maumivu maana baada yake wanakujga wale wa roho za kutu,nawakumbisha tu.
Screenshot_20230424-084824.jpg
 
Usahili ufanywe Kikanda hii ya kurundika watu Dodoma Sio afya kwa vijana,wakikosa interview wanarudi makwao wakiwa wamenyongonyea kabisa kwa mawazo ya watarejesha vipi madeni waliyokopa ili kwenda kufanya interview.
Toka sumbawanga, bukobaa,songea bila gharama ya si chini ya laki 3 ujaenda kufanyaa interviews Dodoma.
 
Nilikuwa nakuheshimu sana na kuona mtu unayejielewa.

Kumbe Hujuielewi kabisaaa.
Umefikisha habari vzuri ila kitendo cha kuanza kusifia sijui samia sijui mama yako nimeona wewe ni Hovyooooo kbsa
Wewe ndio hovyo na una chuki kisa Rais kusifiwa 😁😁😁😁

Ulitaka nimsifie baba Yako au yule marehemu wako? Walitoa Ajira zipi Hadi wastahili sifa?
 
NI mwendo wa ajira, ndivyo unavyoweza kusema baada ya jana serikali kutangaza ajira mpya 8,070 za kada ya afya ambazo mchakato wake unakaribia kuiva muda wowote kuanzia sasa.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Deogratius Ndejembi, ndiye aliyetangaza neema hiyo jana bungeni, huku akitoa angalizo kwa wakurugenzi wa halmashauri kutopitisha barua za uhamisho kwa watumishi ambao hawajatimiza miaka mitatu kwenye vituo vyao vya kazi.

Ndejembi alitoa ufafanuzi huo wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Minza Mjika, aliyehoji ni lini serikali itaongeza watumishi wa afya Hospitali ya Wilaya ya Meatu.

Akijibu swali hilo, Ndejembi alisema katika mwaka wa fedha wa 2022/23, serikali itaajiri watumishi wa kada ya afya 8,070 na baada ya taratibu za ajira kukamilika watumishi hao watapangwa kwenye halmashauri zote nchini, Meatu ikiwamo.

Alisema serikali imeendelea kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya na katika mwaka wa fedha 2021/22 serikali iliajiri watumishi 7, 736 wa afya na Halmashauri ya Wilaya ya Meatu ilipangiwa watumishi 104 na watumishi saba walipangwa Hospitali ya Wilaya ya Meatu.

Awali, akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Liwale (CCM), Zuberi Kuchauka kuhusu kuhama kwa watumishi wanaopangwa katika maeneo mbalimbali, Naibu Waziri Ndejembi alikiri serikali inatambua tatizo hilo na tayari inaweka mikakati kwenye ajira mpya ambazo watumishi wanatarajia kuanza kazi hivi karibuni.

Kuchauka, katika swali lake, alisema kumekuwa na wimbi kubwa la watumishi wa afya kuhama kwenye halmashauri hasa za pembezoni ikiwamo ya Liwale ambayo ilipata watumishi 80 na waliobaki sasa hawafiki 15.
“Watumishi wanahama 36 wanaletwa wawili, Je? serikali ina mpango gani wa kudhibiti huu uhamaji holela?” alihoji.

Ndejembi alisisitiza kuwa; “Tutaweka mikakati ambayo itadhibiti wimbi hili la watu kuhama na nichukue nafasi hii kuwaagiza wakurugenzi wa halmashauri ambao ndiyo waajiri katika maeneo hayo wahakikishe hawapitishi barua kwa mtumishi yeyote ambaye hajathibitishwa kazini.

“Mtumishi anatakiwa akae kituo chake kipya cha ajira angalau miaka mitatu, kwa hiyo wafuate utaratibu wasipitishe barua hizi ili watumishi hawa wafanye kazi, wameajiriwa kwenda kupunguza upungufu ambao upo kwenye maeneo hayo, sasa wakipitisha barua ili hawa wahame wanazidisha upungufu kwenye maeneo hayo.”
Ndejembi alisema watumishi hao walipoomba ajira hizo walikuwa tayari kufanya kazi eneo lolote la Tanzania.

My Take
Msipotoka Kimaisha Miaka hii ya Rais Samia kuanzia mkulima Hadi msomi basi hesabu maumivu maana baada yake wanakujga wale wa roho za korosho,nawakumbusha tu.
 
Back
Top Bottom