Vigogo watano Polisi Arusha mbaroni kwa rushwa ya Milioni 10,mmoja ashikwa na presha aanguka akihojiwa na tume ya IGP

Tena ni uchumi mkubwa sana kwa Kenya huo, sisi tunayo version yetu huko Lushoto ambayo ingetapakaa Afrika mashariki na ya kati nzima ikawanyanyuwa watu kiuchumi, eti tunaifungia.

Kuna haramu zaidi ya pombe na sigara zenye madhara ya wazi kabisa na zinaruhusiwa.

Tanzania ingeruhusu boiashata ya mirungi na bangi kuukuza uchumi, zina faida hizo zaidi ya pombe na sigara.
Kuna wakati unapambanua mambo kikubwa,huo ndo ukubwa,sio ule ushabiki wako na hoja za ajabu ajabu ka mama mjamzito,thumb up
 
Tena ni uchumi mkubwa sana kwa Kenya huo, sisi tunayo version yetu huko Lushoto ambayo ingetapakaa Afrika mashariki na ya kati nzima ikawanyanyuwa watu kiuchumi, eti tunaifungia.

Kuna haramu zaidi ya pombe na sigara zenye madhara ya wazi kabisa na zinaruhusiwa.

Tanzania ingeruhusu boiashata ya mirungi na bangi kuukuza uchumi, zina faida hizo zaidi ya pombe na sigara.
Ujue FaizaFoxy kuna muda huwa zinachaji sema basi tu 😄
 
Mirungi tuseme ukweli haina madhara ya kuitwa madawa ya kulevya hapo kenya tu ambayo ni east african community siyo kosa, na sijaona mtu akipata madhara kama kulewa au afya kudorora kama pombe , serikali itathimini
Wewe una hoja kuliko huyo anayeshadadia kuwa wanaochukua rushwa wasamehewe bila kutambua kuwa ipo siku haki yake itapindwa na mwenye uwezo alafu akabaki na machungu.
 
Huyo jamaa aliyepandwa ghafla na presha baada tu ya kuingia kwenye chumba cha mahojiano, ametisha sana.
 
VIGOGO Wandamizi watano wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha wanatuhumiwa kuchukua rushwa ya shilingi milioni 10 na kuachia madawa ya kulevya aina ya Mirungi kilo zaidi ya 1200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 katika tukio lililotokea desemba 5 mwaka huu eneo la Burka kata ya Elerai ndani ya Jiji la Arusha majira ya saa 5 asubuhi.

Vigogo hao ambao ni wakaguzi wa Polisi wanatuhumiwa kuhusika katika sakata hilo na jalada la uchunguzi kufunguliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha lenye namba ARS/IR/10741/2023 na tayari wameshatoa maelezo Polisi ni pamoja na Mkaguzi Mwandamizi Mwinyimvua Shomari na Riziki Khatibu ambao wote kituo chao cha kazi ni ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha.

Wengine ni pamoja na Mkaguzi Mwandamizi wa Polisi, Yahaya Mokiwa ambaye kituo chake cha kazi ni Polisi Post Tengeru Wilayani Arumeru,Mkaguzi Msaidizi aliyetambuliwa kwa jina moja la Rashid ambaye kituo chake cha kazi ni Polisi uwanja mdogo wa Ndege Kisongo Air Port Arusha na Mkaguzi Msaidizi Frank ambaye kituo chake cha kazi Polisi Arumeru.

Tume ya watu watano ya Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini{IGP}, Camilius Wambura imeshindwa kukamilisha mahojiano kwa watuhumiwa hao watano baada ya mmoja ya watuhumiwa hao kupata ugonjwa wa ghafla wa shinikizo la damu{BP} na kuanguka mara baada ya kungia katika chumba maalumu cha tume hiyo.

Wambura aliunda tume dhidi ya Wakaguzi Waandamizi watano wa jeshi hilo kutuhumiwa kushawishi na kuomba ya rushwa ya shilingi milioni 10 na kuachia gari lililokuwa na madawa ya kulevya aina ya Mirungi yenye uzito wa kilo 1200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 katika tukio lililotokea desemba 5 mwaka huu maeneo ya Burka kata ya Elerai ndani ya Jiji la Arusha majira ya saa 5 asubuhi.

Habari za uhakika kutoa ndani ya jeshi la polisi zilisema kuwa Mkaguzi Mwandamizi ambaye alibaki pekee yake kuhojiwa na tume hiyo aliingia katika chumba hicho kwa kujiamini lakini alivyokutana na Makamishina Wasaidizi wa Polisi Makao Makuu na kuanza kupewa maelezo ya awali kabla ya kuanza kuhojiwa ghafla hali yake ilibadilika na kuishiwa nguvu na kutaka kuanguka katika kiti lakini alidakwa na maofisa hao na kupewa huduma ya kwanza ikiwemo kupewa maji ya kunywa na kupepewa na vitabu vya ofisi hiyo na pamoja na nguo.

Vyanzo vilisema baada ya hali hiyo kujitokeza mtuhumiwa alipelekwa katika zahanati ya polisi iliyopo eneo la karibu na kituo kikuu cha Polisi Arusha ili aweze kupata matibabu zaidi.

Vyanzo vilisema baada ya kuwepo kwa hali hiyo tume hiyo ya Makamishina Wasaidizi wa Polisi waliamua kuhairisha kikao cha mahojiano na kuamua kuondoka Jijini Arusha Dsemba 22 mwaka huu na kurudi Dodoma.

Hata hivyo habari zilisema kuwa Tume hiyo ilifanikiwa kumhoji Ramadhani Omary aliyekamatwa desemba 20 mwaka huu ndani ya Jiji la Arusha ambaye ni mmoja wa watuhumiwa wa mirungi aliyekuwa katika gari aina ya Prado yenye namba za usajili T683DZZ rangi ya silver lakini yeye na mwenzake waliondoka baada ya kukabidhi awali rushwa ya shilingi milioni 6.

Vyanzo vilisema Polisi inamsaka kwa udi na uvumba mtuhumiwa mwingine aliyekuwa katika Prado kwani mtuhumiwa huyo ni muhimu sana katika kesi hiyo inayowakabili vigogo hao wa polisi Arusha.

‘’Tume imebakiza watu wawili kuwahoji akiwemo Mkaguzi aliyepata BP{Presha} na Raia mmoja anayesakwa na polisi na tume imeondoka kurudi Dodoma’’ alisema mtoa taarifa

Wakaguzi wa Polisi wanatuhumiwa kuhusika katika sakata hilo na jalada la uchunguzi kufunguliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha lenye namba ARS/IR/10741/2023 na wameshatoa maelezo yao mbele ya tume hiyo.

Awali Vigogo hao walilikamata gari aina Prado yenye namba za usajili T683DZZ rangi ya silver iliyokuwa na mirungi kilo 1200 na watuhumiwa wawili waliokuwa ndani ya gari hilo likiwa na Mirungi majira vya saa 5 asubuhi maeneo ya Burka kata ya Elerai Jijini Arusha.

Vyanzo vilisema baada ya kukamata Mirungi hiyo muda huo,Vigogo hao waliomba rushwa ya shilingi milioni 10 kwa watuhumiwa hao wa usafirishaji madawa ili waweze kuachiwa lakini watuhumiwa hao walikuwa na fedha taslimu shilingi milioni 6 tu.

Habari zilisema baada ya mabishano ya muda mrefu,vigogo hao wa Polisi walitoa masharti ya kupokea kiasi hicho cha fedha na kutelemsha katika gari Bunda 496 sawa na kilo kiasi hicho za Mirungi na wanapokwenda watume mtu wa kuwapelekea rushwa iliyobaki ya shilingi miloini 4 iliyobaki.

Mirungi kilo 496 iliyobaki ilipakuliwa na kupakiwa katika gari aina ya Toyota Mark 11 yenye namba za usajili T536BQB iliyopelekwa na Alfayo na alikuwa anamsubiri mtu mwingine ambaye alipaswa kwenda rushwa shilingi milioni 4 tu na Alfayo hakujua chochote.

Vyanzo viliendelea kusema kuwa vigogo hao walikaa eneo hilo siku nzima hadi majira ya saa 7.15 usiku wa desemba 6 mwaka huu na taarifa ya kukamatwa kwa mirungi katika eneo hilo zilimfikia Mkuu wa Polisi Arusha{OCD} na yeye kuweka mtego wake kwa kutumia gari mbili za doria zinazotambuliwa kwa jina la chita 5 na chita 7 kwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa magari hayo ya Dolia yalikuwa yakiongozwa na askari kanzu Sajenti Haji hadi eneo la tukio lakini walipofika eneo la tukio walikutana na upinzani mkali kwani walikamata mirungi na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 wana vyeo vya juu kuliko sajenti Haji.

Vyanzo ndani ya Jeshi la Polisi vilisema kuwa baada ya Sajenti Haji kukutana na upinzani huo na kutakiwa kuondoka eneo la tukio,Sajenti huyo alimpigia OCD George Malewa kumweleza hali hiyo na vigogo hao walivyosikia sauti ya Kamanda Malewa waliamua kutimua mbio na Sajenti haji alibeba Mirungi hiyo na mtuhumiwa Alfayo hadi Polisi kati Arusha.

Msemaji Mkuu wa Polisi Nchini, Kamishina David Misime hakuweza kupatikana kueleza tukio hilo la IGP kuunda tume hiyo kwani simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa lakini bado jitihada zinaendea za kumsaka.
Wakenya wakisikia hii story watabaki kushangaa sana
 
VIGOGO Wandamizi watano wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha wanatuhumiwa kuchukua rushwa ya shilingi milioni 10 na kuachia madawa ya kulevya aina ya Mirungi kilo zaidi ya 1200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 katika tukio lililotokea desemba 5 mwaka huu eneo la Burka kata ya Elerai ndani ya Jiji la Arusha majira ya saa 5 asubuhi.

Vigogo hao ambao ni wakaguzi wa Polisi wanatuhumiwa kuhusika katika sakata hilo na jalada la uchunguzi kufunguliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha lenye namba ARS/IR/10741/2023 na tayari wameshatoa maelezo Polisi ni pamoja na Mkaguzi Mwandamizi Mwinyimvua Shomari na Riziki Khatibu ambao wote kituo chao cha kazi ni ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha.

Wengine ni pamoja na Mkaguzi Mwandamizi wa Polisi, Yahaya Mokiwa ambaye kituo chake cha kazi ni Polisi Post Tengeru Wilayani Arumeru,Mkaguzi Msaidizi aliyetambuliwa kwa jina moja la Rashid ambaye kituo chake cha kazi ni Polisi uwanja mdogo wa Ndege Kisongo Air Port Arusha na Mkaguzi Msaidizi Frank ambaye kituo chake cha kazi Polisi Arumeru.

Tume ya watu watano ya Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini{IGP}, Camilius Wambura imeshindwa kukamilisha mahojiano kwa watuhumiwa hao watano baada ya mmoja ya watuhumiwa hao kupata ugonjwa wa ghafla wa shinikizo la damu{BP} na kuanguka mara baada ya kungia katika chumba maalumu cha tume hiyo.

Wambura aliunda tume dhidi ya Wakaguzi Waandamizi watano wa jeshi hilo kutuhumiwa kushawishi na kuomba ya rushwa ya shilingi milioni 10 na kuachia gari lililokuwa na madawa ya kulevya aina ya Mirungi yenye uzito wa kilo 1200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 katika tukio lililotokea desemba 5 mwaka huu maeneo ya Burka kata ya Elerai ndani ya Jiji la Arusha majira ya saa 5 asubuhi.

Habari za uhakika kutoa ndani ya jeshi la polisi zilisema kuwa Mkaguzi Mwandamizi ambaye alibaki pekee yake kuhojiwa na tume hiyo aliingia katika chumba hicho kwa kujiamini lakini alivyokutana na Makamishina Wasaidizi wa Polisi Makao Makuu na kuanza kupewa maelezo ya awali kabla ya kuanza kuhojiwa ghafla hali yake ilibadilika na kuishiwa nguvu na kutaka kuanguka katika kiti lakini alidakwa na maofisa hao na kupewa huduma ya kwanza ikiwemo kupewa maji ya kunywa na kupepewa na vitabu vya ofisi hiyo na pamoja na nguo.

Vyanzo vilisema baada ya hali hiyo kujitokeza mtuhumiwa alipelekwa katika zahanati ya polisi iliyopo eneo la karibu na kituo kikuu cha Polisi Arusha ili aweze kupata matibabu zaidi.

Vyanzo vilisema baada ya kuwepo kwa hali hiyo tume hiyo ya Makamishina Wasaidizi wa Polisi waliamua kuhairisha kikao cha mahojiano na kuamua kuondoka Jijini Arusha Dsemba 22 mwaka huu na kurudi Dodoma.

Hata hivyo habari zilisema kuwa Tume hiyo ilifanikiwa kumhoji Ramadhani Omary aliyekamatwa desemba 20 mwaka huu ndani ya Jiji la Arusha ambaye ni mmoja wa watuhumiwa wa mirungi aliyekuwa katika gari aina ya Prado yenye namba za usajili T683DZZ rangi ya silver lakini yeye na mwenzake waliondoka baada ya kukabidhi awali rushwa ya shilingi milioni 6.

Vyanzo vilisema Polisi inamsaka kwa udi na uvumba mtuhumiwa mwingine aliyekuwa katika Prado kwani mtuhumiwa huyo ni muhimu sana katika kesi hiyo inayowakabili vigogo hao wa polisi Arusha.

‘’Tume imebakiza watu wawili kuwahoji akiwemo Mkaguzi aliyepata BP{Presha} na Raia mmoja anayesakwa na polisi na tume imeondoka kurudi Dodoma’’ alisema mtoa taarifa

Wakaguzi wa Polisi wanatuhumiwa kuhusika katika sakata hilo na jalada la uchunguzi kufunguliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha lenye namba ARS/IR/10741/2023 na wameshatoa maelezo yao mbele ya tume hiyo.

Awali Vigogo hao walilikamata gari aina Prado yenye namba za usajili T683DZZ rangi ya silver iliyokuwa na mirungi kilo 1200 na watuhumiwa wawili waliokuwa ndani ya gari hilo likiwa na Mirungi majira vya saa 5 asubuhi maeneo ya Burka kata ya Elerai Jijini Arusha.

Vyanzo vilisema baada ya kukamata Mirungi hiyo muda huo,Vigogo hao waliomba rushwa ya shilingi milioni 10 kwa watuhumiwa hao wa usafirishaji madawa ili waweze kuachiwa lakini watuhumiwa hao walikuwa na fedha taslimu shilingi milioni 6 tu.

Habari zilisema baada ya mabishano ya muda mrefu,vigogo hao wa Polisi walitoa masharti ya kupokea kiasi hicho cha fedha na kutelemsha katika gari Bunda 496 sawa na kilo kiasi hicho za Mirungi na wanapokwenda watume mtu wa kuwapelekea rushwa iliyobaki ya shilingi miloini 4 iliyobaki.

Mirungi kilo 496 iliyobaki ilipakuliwa na kupakiwa katika gari aina ya Toyota Mark 11 yenye namba za usajili T536BQB iliyopelekwa na Alfayo na alikuwa anamsubiri mtu mwingine ambaye alipaswa kwenda rushwa shilingi milioni 4 tu na Alfayo hakujua chochote.

Vyanzo viliendelea kusema kuwa vigogo hao walikaa eneo hilo siku nzima hadi majira ya saa 7.15 usiku wa desemba 6 mwaka huu na taarifa ya kukamatwa kwa mirungi katika eneo hilo zilimfikia Mkuu wa Polisi Arusha{OCD} na yeye kuweka mtego wake kwa kutumia gari mbili za doria zinazotambuliwa kwa jina la chita 5 na chita 7 kwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa magari hayo ya Dolia yalikuwa yakiongozwa na askari kanzu Sajenti Haji hadi eneo la tukio lakini walipofika eneo la tukio walikutana na upinzani mkali kwani walikamata mirungi na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 wana vyeo vya juu kuliko sajenti Haji.

Vyanzo ndani ya Jeshi la Polisi vilisema kuwa baada ya Sajenti Haji kukutana na upinzani huo na kutakiwa kuondoka eneo la tukio,Sajenti huyo alimpigia OCD George Malewa kumweleza hali hiyo na vigogo hao walivyosikia sauti ya Kamanda Malewa waliamua kutimua mbio na Sajenti haji alibeba Mirungi hiyo na mtuhumiwa Alfayo hadi Polisi kati Arusha.

Msemaji Mkuu wa Polisi Nchini, Kamishina David Misime hakuweza kupatikana kueleza tukio hilo la IGP kuunda tume hiyo kwani simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa lakini bado jitihada zinaendea za kumsaka.
Wawasamehe jamani. Wanajiandaa na machungu ya kikokotoo. Bila ya hivyo watastaafu wakiwa hawajajenga nyumba kwani mishahara yao ni kichekesho na wakistaafu wanakutana na kikokotoo.
 
1200kg yenye thamani ya 60m ingekuwa halali TRA wangekusanya ngapi kwa mirungi tu?

Tatizo sisi tunaiga sana wazungu
Mirungi na gongo ni jadi yetu sasa unakubali Whiskey unakataa gongo na mirungi kisa mzungu kakataa
Tena sio wazungu wote kwani Netherlands wao hawana shida kiasi chai inakuja wewe unasokota bangi kusubiria

Serikali ijitafakari na kuachana na kuburuzwa kila siku
Achieni mirungi mzidishe kipato ili mfikie 3.5b kwa mwezi makusanyo ya kujisifia
 
VIGOGO Wandamizi watano wa Jeshi la Polisi Mkoani Arusha wanatuhumiwa kuchukua rushwa ya shilingi milioni 10 na kuachia madawa ya kulevya aina ya Mirungi kilo zaidi ya 1200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 katika tukio lililotokea desemba 5 mwaka huu eneo la Burka kata ya Elerai ndani ya Jiji la Arusha majira ya saa 5 asubuhi.

Vigogo hao ambao ni wakaguzi wa Polisi wanatuhumiwa kuhusika katika sakata hilo na jalada la uchunguzi kufunguliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha lenye namba ARS/IR/10741/2023 na tayari wameshatoa maelezo Polisi ni pamoja na Mkaguzi Mwandamizi Mwinyimvua Shomari na Riziki Khatibu ambao wote kituo chao cha kazi ni ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoani Arusha.

Wengine ni pamoja na Mkaguzi Mwandamizi wa Polisi, Yahaya Mokiwa ambaye kituo chake cha kazi ni Polisi Post Tengeru Wilayani Arumeru,Mkaguzi Msaidizi aliyetambuliwa kwa jina moja la Rashid ambaye kituo chake cha kazi ni Polisi uwanja mdogo wa Ndege Kisongo Air Port Arusha na Mkaguzi Msaidizi Frank ambaye kituo chake cha kazi Polisi Arumeru.

Tume ya watu watano ya Jeshi la Polisi Makao Makuu Dodoma iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini{IGP}, Camilius Wambura imeshindwa kukamilisha mahojiano kwa watuhumiwa hao watano baada ya mmoja ya watuhumiwa hao kupata ugonjwa wa ghafla wa shinikizo la damu{BP} na kuanguka mara baada ya kungia katika chumba maalumu cha tume hiyo.

Wambura aliunda tume dhidi ya Wakaguzi Waandamizi watano wa jeshi hilo kutuhumiwa kushawishi na kuomba ya rushwa ya shilingi milioni 10 na kuachia gari lililokuwa na madawa ya kulevya aina ya Mirungi yenye uzito wa kilo 1200 yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 60 katika tukio lililotokea desemba 5 mwaka huu maeneo ya Burka kata ya Elerai ndani ya Jiji la Arusha majira ya saa 5 asubuhi.

Habari za uhakika kutoa ndani ya jeshi la polisi zilisema kuwa Mkaguzi Mwandamizi ambaye alibaki pekee yake kuhojiwa na tume hiyo aliingia katika chumba hicho kwa kujiamini lakini alivyokutana na Makamishina Wasaidizi wa Polisi Makao Makuu na kuanza kupewa maelezo ya awali kabla ya kuanza kuhojiwa ghafla hali yake ilibadilika na kuishiwa nguvu na kutaka kuanguka katika kiti lakini alidakwa na maofisa hao na kupewa huduma ya kwanza ikiwemo kupewa maji ya kunywa na kupepewa na vitabu vya ofisi hiyo na pamoja na nguo.

Vyanzo vilisema baada ya hali hiyo kujitokeza mtuhumiwa alipelekwa katika zahanati ya polisi iliyopo eneo la karibu na kituo kikuu cha Polisi Arusha ili aweze kupata matibabu zaidi.

Vyanzo vilisema baada ya kuwepo kwa hali hiyo tume hiyo ya Makamishina Wasaidizi wa Polisi waliamua kuhairisha kikao cha mahojiano na kuamua kuondoka Jijini Arusha Dsemba 22 mwaka huu na kurudi Dodoma.

Hata hivyo habari zilisema kuwa Tume hiyo ilifanikiwa kumhoji Ramadhani Omary aliyekamatwa desemba 20 mwaka huu ndani ya Jiji la Arusha ambaye ni mmoja wa watuhumiwa wa mirungi aliyekuwa katika gari aina ya Prado yenye namba za usajili T683DZZ rangi ya silver lakini yeye na mwenzake waliondoka baada ya kukabidhi awali rushwa ya shilingi milioni 6.

Vyanzo vilisema Polisi inamsaka kwa udi na uvumba mtuhumiwa mwingine aliyekuwa katika Prado kwani mtuhumiwa huyo ni muhimu sana katika kesi hiyo inayowakabili vigogo hao wa polisi Arusha.

‘’Tume imebakiza watu wawili kuwahoji akiwemo Mkaguzi aliyepata BP{Presha} na Raia mmoja anayesakwa na polisi na tume imeondoka kurudi Dodoma’’ alisema mtoa taarifa

Wakaguzi wa Polisi wanatuhumiwa kuhusika katika sakata hilo na jalada la uchunguzi kufunguliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Arusha lenye namba ARS/IR/10741/2023 na wameshatoa maelezo yao mbele ya tume hiyo.

Awali Vigogo hao walilikamata gari aina Prado yenye namba za usajili T683DZZ rangi ya silver iliyokuwa na mirungi kilo 1200 na watuhumiwa wawili waliokuwa ndani ya gari hilo likiwa na Mirungi majira vya saa 5 asubuhi maeneo ya Burka kata ya Elerai Jijini Arusha.

Vyanzo vilisema baada ya kukamata Mirungi hiyo muda huo,Vigogo hao waliomba rushwa ya shilingi milioni 10 kwa watuhumiwa hao wa usafirishaji madawa ili waweze kuachiwa lakini watuhumiwa hao walikuwa na fedha taslimu shilingi milioni 6 tu.

Habari zilisema baada ya mabishano ya muda mrefu,vigogo hao wa Polisi walitoa masharti ya kupokea kiasi hicho cha fedha na kutelemsha katika gari Bunda 496 sawa na kilo kiasi hicho za Mirungi na wanapokwenda watume mtu wa kuwapelekea rushwa iliyobaki ya shilingi miloini 4 iliyobaki.

Mirungi kilo 496 iliyobaki ilipakuliwa na kupakiwa katika gari aina ya Toyota Mark 11 yenye namba za usajili T536BQB iliyopelekwa na Alfayo na alikuwa anamsubiri mtu mwingine ambaye alipaswa kwenda rushwa shilingi milioni 4 tu na Alfayo hakujua chochote.

Vyanzo viliendelea kusema kuwa vigogo hao walikaa eneo hilo siku nzima hadi majira ya saa 7.15 usiku wa desemba 6 mwaka huu na taarifa ya kukamatwa kwa mirungi katika eneo hilo zilimfikia Mkuu wa Polisi Arusha{OCD} na yeye kuweka mtego wake kwa kutumia gari mbili za doria zinazotambuliwa kwa jina la chita 5 na chita 7 kwenda eneo la tukio.

Habari zilisema kuwa magari hayo ya Dolia yalikuwa yakiongozwa na askari kanzu Sajenti Haji hadi eneo la tukio lakini walipofika eneo la tukio walikutana na upinzani mkali kwani walikamata mirungi na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 wana vyeo vya juu kuliko sajenti Haji.

Vyanzo ndani ya Jeshi la Polisi vilisema kuwa baada ya Sajenti Haji kukutana na upinzani huo na kutakiwa kuondoka eneo la tukio,Sajenti huyo alimpigia OCD George Malewa kumweleza hali hiyo na vigogo hao walivyosikia sauti ya Kamanda Malewa waliamua kutimua mbio na Sajenti haji alibeba Mirungi hiyo na mtuhumiwa Alfayo hadi Polisi kati Arusha.

Msemaji Mkuu wa Polisi Nchini, Kamishina David Misime hakuweza kupatikana kueleza tukio hilo la IGP kuunda tume hiyo kwani simu yake ya kiganjani ilikuwa ikiita bila ya kupokelewa lakini bado jitihada zinaendea za kumsaka.
Duh hawa ndugu zetu katika Imani mbona ni hatari? Wote ni wao
 
Back
Top Bottom