Vifungu vya sheria vinavyoruhusu mtoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18 vyapingwa mahakamani

Hussein Massanza

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
1,016
2,194
Kesi ya Kikatiba ya Sheria ya Ndoa Imeanza kusikilizwa Tarehe 9 Machi

Kesi ya kikatiba namba 5. ya mwaka 2016, inayopinga vipengele vya sheria ya ndoa imeanza kusikilizwa leo March 9 kwa upande wa mleta maombi kuwasilisha kwa maandishi maelezoya upande wake mahakamani. Kesi hiyo inasikilizwa na jopo la majaji likiongozwa na Jaji Kiongozi Shaban Lila, jaji Sakiet Kihiyo na Jaji Munisi. Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Tar 15 mwezi wa 3 kwa upande wa serikali kuleta maelezo yao.

Kesi hiyo ya Kikatiba ilifunguliwa na Rebeca Gyumi, mwanaharakati wa haki za binadamu hasa haki za mtoto wakike, na mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la MsichanaInitiative linalofanya kazi ya kutetea haki ya mtoto wa kike kupata elimu,kupitia kwa wakili Jebra Kambole wa Law Guards Advocates.

Vipengele vinavyopingwa ni kifungu cha 13 na 17 vya sheria yandoa (CAP 29 R.E 2002) kwa kutoa mwaya kwa mtoto wa kike kuolewa akiwa na miaka 14 kwa kibali cha mahakama, na miaka15 kwa ridhaa ya wazazi. Ambayo ni kinyume na Ibara ya 13,12na 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 zinazotoa haki ya usawa mbele ya sheria, kutokubaguliwa, kuheshimu utu wa mtu na uhuru wa kujieleza.

Vifungu vya sheria ya ndoa vinavyoruhusu mtoto wa kike kuolewa chini ya miaka 18 vyapingwa mahakamani


Kesi hiyo ya Kikatiba iliyosajiliwa na kupewa namba 5 ya mwaka 2016 imefunguliwa na Rebeca Gyumi, mwanaharakati wa haki za binadamu hasa haki za mtoto wa kike, na mkurugenzi wa shirika lisilo la kiserikali la Msichana Initiative linalofanya kazi ya kutetea haki ya mtoto wa kike kupata elimu,kupitia kwa wakili Jebra Kambole wa Law Guards Advocates.

Vipengele vinavyopingwa ni kifungu cha 13 na 17 vya sheria ya ndoa (CAP 29 R.E 2002) kwa kutoa mwaya kwa mtoto wa kike kuolewa akiwa na miaka 14 kwa kibali cha mahakama, na miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi. Ambayo ni kinyume na Ibara ya 13,12 na 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 zinazotoa haki ya usawa mbele ya sheria, kutokubaguliwa, kuheshimu utu wa mtu na uhuru wa kujieleza.

Vifungu hivi vya sheria vimeweka umri tofauti kati ya mtoto wa kike na wa kiume na hivyo kupingana na Ibara ya 13 (1) (2) ya Katiba inayotoa haki ya usawa mbele ya sheria, na kwamba ni kosa kuwa na sheria zinazobagua. Wakati mtoto wa kike anaweza kuolewa akiwa na miaka 14 kwa kibali cha mahakama na miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi, umri wa mtoto wa kiume kuoa ni miaka 18.

Kifungu cha 17 kinachotoa ruhusa kwa mtoto wa kike kuolewa akiwa na miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi, kinaminya utu na haki ya mtu kujieleza kama zilivyoainishwa kwenye Ibara ya 12 na 18 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Masuala ya ndoa si kama mikataba ya biashara, pande zinazoingia kwenye ndoa lazima zikubaliane na si kulazimishwa. Na tumeona hata matukio ambapo wazazi walikatiza mtoto wa kike masomo ili aolewe.

Shauri hili linaiomba mahakama kuu kuvifuta vifungu hivi na kupandisha umri wa chini wa kuoa/kuolewa kwa mwanaume na mwanamke kuwa miaka 18.

Ndoa za utotoni kwa mtoto wa kike zaidi ya kuwa suala la ukiukwaji wa haki za binadamu, pia ni suala la kiafya, elimu na kisaikolojia. Msichana kujifungua katika umri mdogo ni chanzo cha matatizo kama Fistula na vifo vingi vya wajawazito. Ingawa huwezi peleka shauri mahakamani kudai haki ya kupata elimu Kikatiba, lakini haki hii ni muhimu sana kuzingatiwa na kuhakikisha hakuna mianya inayoweza kutumiwa kuzima ndoto za watoto kubaki shuleni na kusoma.

Takwimu za ndoa za utotoni duniani zinaonesha Tanzania kuwa moja ya nchi zenye viwango vikubwa vya ndoa katika umri mdogo. Kwa wastani watoto wakike wawili kati ya watano huolewa kabla ya kufikisha umri wa miaka 18. Kwa mwezi wa 1 tu 2016 tumeshasikia kesi za watoto wa kike kuolewa au kutaka kuozwa wakiwa chini ya miaka 15.

Pamoja na kuwa utoaji wa elimu kwa jamii, vikundi vya dini na kupinga mila na desturi ni muhimu kutokomeza ndoa za utotoni, uwepo wa sheria inayomlinda mtoto wa kike na wa kiume ikiendana na utekelezaji wa sheria hizi ni muhimu zaidi ili kutokomeza kabisa tatizo hili la ndoa za utotoni.
 
Kwa waislamu mtu anaweza kumuoa msichana wa miaka14. Je, mahakama ina uwezo wa kurekebisha sheria na taratibu za dini hiyo?
 
"Vifungu hivi vya sheria vimeweka umri tofauti kati ya mtoto wa kike na wa kiume na hivyo kupingana na Ibara ya 13 (1) (2) ya Katiba inayotoa haki ya usawa mbele ya sheria, na kwamba ni kosa kuwa na sheria zinazobagua. Wakati mtoto wa kike anaweza kuolewa akiwa na miaka 14 kwa kibali cha mahakama na miaka 15 kwa ridhaa ya wazazi, umri wa mtoto wa kiume kuoa ni miaka 18".

Hapo ulipasoma mkuu?!
Nimepasoma mkuu,lakini swali langu Ni jee mahakama inauwezo WA kubadili sheria taratibu na kanuni za dini ya kiIslamuu?
 
Sheria ya ndoa ya namba 5 ya mwaka 1971 inatambua ufungaji wa ndoa kwa mila na desturi, kidini na ki serikali lakini sheria inatoa muongoza ambao kila mtu afuate bila kujali Imani yake kwa hiyo mahakama haifuti sheria ya kiislamu inafuta huo muongozo wa sheria ya ndoa na kuweka umri Sawa
 
Tafiti zinaonyesha kuwa LIFESPAN ya Mtanzania imeshuka sana tofauti na zanmani. Sasa wakati wanasimamia shauri hilo ni vyema wakazingatio kwa muda mfupi ambao mtanzania ataishi hapa duniani inatakiwa awe amekamilisha majukumu likiwemo la kuzaliana.
 
Mahakama ina uwezo wa kufuta sheria iliyotungwa na bunge?
mahakama inatoa declaratory reliefs tu kwa maombi kama hayo, na in most cases itaiagiza serikali na bunge kuhakikisha vifungu hiviyo vinafanyiwa marekebisho na itawapa muda wa kufanya hivyo, a good move.
 
Ikitumika hekima, inawezekana. Why not?
Jamii huwa zina adjust ili kufiti matakwa ya nyakati zilizopo..
Isitoshe siku hizi masuala ya ndoa za watoto kwa misingi ya kidini yamepungua kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na zama hizo. Athari zimeonekana..
Swali lako ni la msingi sana anyway..
Hapana,haiwezekani kwa serikali kubadili sheria ya kiislamu (achilia mbali shariah za uislamu) kwa kigezo cha kuendana na mabadiliko ya jamii uislamu tayari una shariah zake zinazojitosheleza kwenye kila nyanja,hivyo kilicho cha hekima kwa serikali ya kisekula ya Tanzania ni kufanya marekebisho panapo mapungufu kwenye sheria zake na si kubadilisha shariah za kiislamu ambazo jua kamwe hakuna atakayezibadilisha.
 
Miaka 14 ? Huo utakuwa ni ubakaji mkubwa tena wa wazi. Sidhan kama ni kweli dini inaweza ruhusu mtoto huyu aolewe. Hapo ni kuruhusu ubakaj wa wazi kabisa na ukatili kwa wanawake. Tusiisingize dini mambo haya machafu hivi kwa kizaz hiki.






Kwa waislamu mtu anaweza kumuoa msichana wa miaka14. Je, mahakama ina uwezo wa kurekebisha sheria na taratibu za dini hiyo?
 
Hbr za life span weka pembeni. Tamaa ya kuharib watoto weka pembeni. Waacheni watoto wasome achen tamaa ya kuharibu watoto.


Tafiti zinaonyesha kuwa LIFESPAN ya Mtanzania imeshuka sana tofauti na zanmani. Sasa wakati wanasimamia shauri hilo ni vyema wakazingatio kwa muda mfupi ambao mtanzania ataishi hapa duniani inatakiwa awe amekamilisha majukumu likiwemo la kuzaliana.
 
-Wadau ikumbukwe kuwa sheria iliyopelekwa mahakamani ambayo baadhi ya vifungu vyake vinaonekana kupingana na katiba ni sheria ya ndoa,sura ya 29,2002. Pia ikumbukwe pia sheria tajwa ni sheria ya nchi(state law/secular law)na sio sheria ya dini yoyote ile. Kwa kusema hivyo,inamaana kwamba islamic sharia haijaathiriwa,na bado itaendelea kutumika pale vigezo vya kutumia sheria hiyo vitakapotimizwa na wahusika,lakini sharia itaathiriwa tu endapo kutazuka mgongano wa kisheria kati ya islamiv na state law,ambapo automatically secular law cap. 29 will prevail.
-Kwa upande mwengine,Mahakama ina uwezo kikatiba kuitangaza sheria yoyote ile iliyotungwa na Bunge kuwa ipo kinyume na katiba(unconstitutional),endapo sheria iyo itaonekana kupingana na masharti yaliyomo katka Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Na baada ya hilo tamko la Mahakama kutoka basi hiyo Sheria haitokuwa na nguvu kisheria kutumika kama ilivokusudiwa na bunge mpaka pale itakopopotiwa tena na kurekebishwa na Bunge.
Ahsante.
 
Nimepasoma mkuu,lakini swali langu Ni jee mahakama inauwezo WA kubadili sheria taratibu na kanuni za dini ya kiIslamuu?
Niliwahi kumsikia mwalimu wangu akisema sheria zote lazima zisikiuke sheria za nchi (katiba),sikusoma sheria ilikuwa sehemu tu ya kozi kwenye program yangu sijui kama hili limezungumziwa kwenye katiba?
 
hii sheria ya ndoa pia inapingana na sheria ya mtoto No 21 ya mwaka 2009 hivyo ni wazi kuna kila haja ya kuviondoa hvyo vifungu. wanaharakati wamelalamika muda mrefu xana
 
Kwa waislamu mtu anaweza kumuoa msichana wa miaka14. Je, mahakama ina uwezo wa kurekebisha sheria na taratibu za dini hiyo?

Kumbuka dini sio utakatifu, ni taratibu za kibinadamu kumjua Mungu. Watoto wa miaka 14 ya wakati ule sio Sawa na wa wakati huu.
 
hivi wanaokuja na kigezo cha miaka 18 ndio mtu mzima kwa vigezo gan? kuna mabinti wana miaka 14 lakin wana miili mikubwa na hata ki ngono wamekubuhu halafu haya mambo yataanza chokonoa mambo ya kiiman, aliyeleta hili shauri ni mfuasi wa dini gani?
 
Ikitumika hekima, inawezekana. Why not?
Jamii huwa zina adjust ili kufiti matakwa ya nyakati zilizopo..
Isitoshe siku hizi masuala ya ndoa za watoto kwa misingi ya kidini yamepungua kwa kiasi kikubwa ikilinganishwa na zama hizo. Athari zimeonekana..
Swali lako ni la msingi sana anyway..

Kwa upande wangu ikibadilishwa ni kama kupinga dini yangu... full stop ,...... bora nipotoke mimi kama individual lakini nisipinge na kuweka sheria inayo kinzana na imani yangu hata huo umri wa miaka 18 kwa kijana wa kiume hauko poa maana ukubwa wa mtu ni balehe yake... vinginevyo ndio mlundikano wa watoto wa nje.. maana hawa watoto tunawakataza kuolewa au kuoa huku wakidandiana kama kawaida watoto wengi wanao zaa chini ya umri wengi wao hawako kwenye ndoa ...chukua hii mwandishi .... au mnakariri tu?
 
Back
Top Bottom