Vielelezo vingi vina Sema Maombi kwenye taifa yanahitajika

ndege JOHN

JF-Expert Member
Aug 5, 2015
19,544
44,690
Upepo wa mabadiliko mengi ya kisiasa na ki utawala duniani yameonekana. Yameathiri viongozi wetu baadhi. Kila sehemu ya ardhi ni kama kuna nguvu fulani naturally inashindana na nguvu fulani. Tupo kipindi kibaya sana. Mpito mgumu usio na uhakika wa kufika mahali fulani. Serikal inapoingia Mategemeo ya wengi ni kuona agenda mbalimbali kipindi cha kampeni hasa zile muhimu zinajadiliwa positive way. Tupo tunadai katiba mpya hii ndiyo Inagusa maisha ya wengi . mpaka Sasa bado kama taifa hatuelewei Nani atatuvusha katika hili. Maugomvi na kutoelewana kutatupoteza. Tupo Zama ambazo unaweza usiamini. Umaskiji kuongezeka, madawa ya kulevya kuongezeka matumizi Kwa watu wapya, ushoga kuongezeka. Hii ni kutokana na ROHO fulani asiye Penda maendeleo kuwepo MIOYONI.. Ni kama kila mtu anatafakari nini kinafuata kesho. Maisha hayapo live tena Kwa baadhi ya watu. Natangaza kuliombea taifa na Naomba mniunge mkono ntafanya maombi kila siku Kwa siku saba. Nitamwomba MUNGU afungue Fahamu za watu wengi. Wanasiasa nitawaombea muwe na fikra ya agenda za kututengenezea taifa lenye mshikamano sisi vijana wa kesho. MUNGU ameumba Galaxy, ameumba anga LA ajabu lenye nguvu za ajabu hawezi kushindwa kubadilisha akili za watanzania. MUNGU hashindwi kumwaga hekima Kwa Viongozi wake. Pande zote naziombea. Tunapenda kuona mazungumzo yenye tija kila Kona. Nchi Nzima Kusiwe na tofauti. Lengo letu liwe moja na hasa mambo muhimu. Taifa la kuombewa. ROHO za kisasi zitaharibu utulivu. Tujaribu na upande wa maombi. Tuombee Hali ya hewa
 
Inawezekana dunia inaandika historia mpya kama ilivyoandika kwa ukoloni...first world war... Second world war.... Ujamaa... Ubepari.... Ufashisti na Unazi...

Dunia kukumbwa na uongozi wenye muelekeo wa kuwehuka ndo inaandika funzo la kihistoria kwa kizazi kijacho!!

Nchi yetu inazama kwenye tope zito itatugharimu miaka mingi kuamka!!
 
Inawezekana dunia inaandika historia mpya kama ilivyoandika kwa ukoloni...first world war... Second world war.... Ujamaa... Ubepari.... Ufashisti na Unazi...

Dunia kukumbwa na uongozi wenye muelekeo wa kuwehuka ndo inaandika funzo la kihistoria kwa kizazi kijacho!!

Nchi yetu inazama kwenye tope zito itatugharimu miaka mingi kuamka!!
Kabisa mkuu. Nyakati ambazo zinatia Shaka. Magufuli asingekuwa anakimbizana na wahasimu wake wa kisiasa. Basi maisha yangekuwa hivi kwamba watu wasingepata vinyongo. Watu wangekuwa huru hakika tungeingia kwenye systems mpya ya maisha. Tumepandikizwa ROHO ya KUSHINDANA isiyo na ulazima. Kwenye siasa za kwetu tumebaki kama Tupo kwenye DuniA ya kipekee. Kuparangana Kwa raia Tuombe kusitokee
 
Au tatizo halipo Kwa wanasiasa bali ni mabadiliko ya maisha MAPYA. Hatupaswi kusubir Muda uamue sisi tuamue maisha tunayotaka kuishi. Kipindi hiko ni cha kujiongeza kuliko Muda wowote tangu DuniA uikute. Ungana na MUNGU kutuliza nafsi
 
Tupo pamoja inshallah mana siku hizi unalala na stress unaamka na stress mambo hayaeleweki yn
Ni kama tunangoja kiama. Kuna jamaa ananichekesha ananiambia maisha magumu na kifo hakimtaki. Tatizo ni kubwa. Wababe vs jeuri matokeo Yake yanafahamika. Hatupaswi kufikiria huko ishu ndogo Sana MUNGU pekee ataweza kutu Unganisha. Inshaaallah
 
Kabisa mkuu. Nyakati ambazo zinatia Shaka. Magufuli asingekuwa anakimbizana na wahasimu wake wa kisiasa. Basi maisha yangekuwa hivi kwamba watu wasingepata vinyongo. Watu wangekuwa huru hakika tungeingia kwenye systems mpya ya maisha. Tumepandikizwa ROHO ya KUSHINDANA isiyo na ulazima. Kwenye siasa za kwetu tumebaki kama Tupo kwenye DuniA ya kipekee. Kuparangana Kwa raia Tuombe kusitokee
Wakati wenzetu wanahangaika na uchumi sisi tunahangaishwa na visasi.... Magufuli anaacha kukimbizana na muda anakimbizana na mahasimu wake.. Sijui Afrika tumelaaniwa vipi aisee..... Viongozi ni wabinafsi kupitiliza na wapo tayari kupoteza rasilimali kwenye kulipa visasi kuliko maendeleo ya watu wao...

Vijijini huko hali ni mbaya mno.... Maji bado si ya uhakika... Miundombinu hovyo....uchumi hovyo.... Chakula hakishikiki tunakimbizana na wapinzani!!!

Tunatia kinyaa sana!!
 
JOHN NDEGE PAMOJA NA KWAMBA NAMI NI MWANADAMU LAKINI NAKUOMBEA MAISHA MAREFU, UMEANDIKA POINT TUPU, TUMBO LILILOKULETA DUNIANI NA UZAO WAKO WOTE MBARIKIWE ! Na tujinyenyekeze mbele za Bwana !
 
Inawezekana dunia inaandika historia mpya kama ilivyoandika kwa ukoloni...first world war... Second world war.... Ujamaa... Ubepari.... Ufashisti na Unazi...

Dunia kukumbwa na uongozi wenye muelekeo wa kuwehuka ndo inaandika funzo la kihistoria kwa kizazi kijacho!!

Nchi yetu inazama kwenye tope zito itatugharimu miaka mingi kuamka!!
inashangaza mtu kama Mr Pengo anasema tuunge mkono haya maadhira. nadhani ni wakati sasa wa Yesu kurudi tena ashushe dhahma kama ya wakati wa Nuhu au Sodoma na Gomora.
 
Mimi huwa nadhani Mungu hayupo nchi hii maana angekuepo kwa sala na dua zinazopigwa kila leo tayari tungeshaona mabadiliko.Huwez kua na nchi kama hii yenye marasilimal kibao na utulivu wakutosha alafu watu wake bado wakawa maskini wakutupa na wajinga.Njia yakujikwamua hapa nikutafuta tulipojikwaa ili sasa ayo maombi yaweze kufanya kazi.
 
Upepo wa mabadiliko mengi ya kisiasa na ki utawala duniani yameonekana. Yameathiri viongozi wetu baadhi. Kila sehemu ya ardhi ni kama kuna nguvu fulani naturally inashindana na nguvu fulani. Tupo kipindi kibaya sana. Mpito mgumu usio na uhakika wa kufika mahali fulani. Serikal inapoingia Mategemeo ya wengi ni kuona agenda mbalimbali kipindi cha kampeni hasa zile muhimu zinajadiliwa positive way. Tupo tunadai katiba mpya hii ndiyo Inagusa maisha ya wengi . mpaka Sasa bado kama taifa hatuelewei Nani atatuvusha katika hili. Maugomvi na kutoelewana kutatupoteza. Tupo Zama ambazo unaweza usiamini. Umaskiji kuongezeka, madawa ya kulevya kuongezeka matumizi Kwa watu wapya, ushoga kuongezeka. Hii ni kutokana na ROHO fulani asiye Penda maendeleo kuwepo MIOYONI.. Ni kama kila mtu anatafakari nini kinafuata kesho. Maisha hayapo live tena Kwa baadhi ya watu. Natangaza kuliombea taifa na Naomba mniunge mkono ntafanya maombi kila siku Kwa siku saba. Nitamwomba MUNGU afungue Fahamu za watu wengi. Wanasiasa nitawaombea muwe na fikra ya agenda za kututengenezea taifa lenye mshikamano sisi vijana wa kesho. MUNGU ameumba Galaxy, ameumba anga LA ajabu lenye nguvu za ajabu hawezi kushindwa kubadilisha akili za watanzania. MUNGU hashindwi kumwaga hekima Kwa Viongozi wake. Pande zote naziombea. Tunapenda kuona mazungumzo yenye tija kila Kona. Nchi Nzima Kusiwe na tofauti. Lengo letu liwe moja na hasa mambo muhimu. Taifa la kuombewa. ROHO za kisasi zitaharibu utulivu. Tujaribu na upande wa maombi. Tuombee Hali ya hewa
Usisahau kuombea na roho za chuki ziwaondoke watu fulani
 
Back
Top Bottom