Vidhibiti mwendo kwenye mabasi ya abiria kuhujumiwa na wahusika

ambagae

JF-Expert Member
Mar 2, 2009
3,241
1,301
Wiki iliyopita nilisafiri na basi kwa jinsi nilivyoona mwendo nikahisi mwendo umeshapita km 80 kwa saa hivyo nikaingia kwenye application ya speedometer kwenye simu yangu.

Gari lilikuwa linakwenda zaidi ya km 90 kwa saa hata sehemu zenye kona kali. Nikamuuliza konda akasema eti speed haizidi 85.

Nikasikiliza kwa makini nikasikia sauti ya kidhibiti mwendo ikilia mfululizo lakini kwa sauti ya chini sana. Kumbe wanapunguza sauti halafu wanaenda mwendo kasi mwendo wanaotaka.

Wahusika limulikeni hili kama mlikuwa hamjui au mnajua maana maisha ya watu yanachezewa na vichaa.
 
Suluhisho ni mabasi yatembee usiku kule ambako ni salama

Fikiria basi litoke Arusha saa moja/19h00 jioni na linatakiwa lifike dar saa kumi na mbili asubuhi (06h00)

Sana sana litaenda kms70 kwani watu wanahitaku wafike kumekucha

Huku Africa tuna poteza muda mwingi sana halafu tunalalamika kuwa Nchi ni masikini

Fikiria mabasi kama 450 yanatembea mchana mzima, ina maana tuna watu wazalishaji 27,000 kila siku wanakaa kwenye mabasi kutwa nzima; zidisha kwa mwezi na kwa mwaka?

Wanaotamani mabasi yakimbie ni wafanyabiasha na wanaowahi majukumu ambao wangesafiri usiku kwa raha zao. Mchana wangebakia wale wanaokwenda kusalimia
 
Suluhisho ni mabasi yatembee usiku kule ambako ni salama
Fikiria basi litoke Arusha saa moja/19h00 jioni na linatakiwa lifike dar saa kumi na mbili asubuhi (06h00)
Sana sana litaenda kms70 kwani watu wanahitaku wafike kumekucha
Huku Africa tuna poteza muda mwingi sana halafu tunalalamika kuwa Nchi ni masikini
Fikiria mabasi kama 450 yanatembea mchana mzima, ina maana tuna watu wazalishaji 27,000 kila siku wanakaa kwenye mabasi kutwa nzima; zidisha kwa mwezi na kwa mwaka???
Wanaotamani mabasi yakimbie ni wafanyabiasha na wanaowahi majukumu ambao wangesafiri usiku kwa raha zao. Mchana tuwachie wale wanaokwenda kusalimia
Una hoja ya msingi sana ndugu.... watawala wetu ni ngumu kuamua hivi kwa kuwa wao safari zao wanafika kwa wakati na kwa haraka.........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom