DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Ni sauti za Watanzania walioko katika majonzi na hasira, wakiimba kwa uchungu wimbo maarufu wa “Hakuna Mungu Kama Wewe”, lakini wakiwa wameubadilisha na kuimba, “Hakuna muuaji kama Samia, hakuna na hata kuwepo.” Ukijaribu kuvaa viatu vya akina mama hawa, unaweza kuhisi uzito wa maumivu na hasira wanazobeba ndani yao.
Kwa hali hii, huwezi kusema tatizo litamalizwa kwa maneno matamu au wito wa maridhiano pekee. Watanzania wanahitaji kuona hatua za kweli wauaji wa raia wakifikishwa mbele ya sheria, na viongozi wanaohusika wakijitokeza kuwajibika au hata kujiuzulu. Hapo ndipo hasira na maumivu ya wananchi yanaweza kuanza kutulia, na si kwa maneno ya kisiasa yasiyo na vitendo.
Kwa hali hii, huwezi kusema tatizo litamalizwa kwa maneno matamu au wito wa maridhiano pekee. Watanzania wanahitaji kuona hatua za kweli wauaji wa raia wakifikishwa mbele ya sheria, na viongozi wanaohusika wakijitokeza kuwajibika au hata kujiuzulu. Hapo ndipo hasira na maumivu ya wananchi yanaweza kuanza kutulia, na si kwa maneno ya kisiasa yasiyo na vitendo.