Video: Haj Manara awashukia Waislamu

Inside10

Platinum Member
Joined
May 20, 2011
Posts
34,758
Reaction score
42,878
Pengine Sio Tone nzuri ya kubembeleza lakini kwa jambo hili naamini nilikuwa sahihi!

Haiwezekani tusifiane Wafanyabiashara wengi ni Waislaam kisha Maimamu wengi wanaotuswalishia Miskiti yetu na Waalimu wanaotufundishia Watoto wetu elimu ya dini wawe omba omba na malofa!!

Tufikirie sasa kutengeneza mifumo sahihi itakayoondoa kabisa hili tatizo kwa jamii yetu!!

Mtu akiwa Imaam au Ustaadh wa Madrasa licha ya kulipwa malipo mema na Allah lakini tuwalipe vizuri ili kazi wanayoifanya iwe na thamani duniani na akhera Insha'Allah πŸ™πŸ™

Nb: Msisahau tukifa hawa tunaowadharau hv sasa ndio wanaotustiri kwa kutuosha na kutuweka Makaburini

Your browser is not able to display this video.
----------------------------
Video sheikh akilalamika hawathaminiwi na waumini wao.


View: https://www.instagram.com/reel/DIvM3Mntvyq/?igsh=MTNpZnR4bzUyMW1u
 
Walipwe vizuri kivipi na wakati sadaka zenyewe mnatoa jero jero mkiwa na kamchango hata ka laki 1 mna pitisha bakuli hadi mitaani kuomba omba bila hata aibu, badilikeni nyie watoto wa mnyaazi "mungu"
 
Ni kweli Wafanyaniashara wengi ni Waislam ila ni Waarab, Wapemba Wahindi/Wapakistani na Wabangladesh. Hawa hawapendi mashirikiano na Waswahili, hata misikiti yao ya Upanga Maimam ni wao wenyewe

Washahili bado ni wagonga nyundo tu wakimiliki vigenge hapa na pale
 
Hii hata mashekhe wengi sana huwa wanaisema na kuwasihi wafuasi wa mnyazi kutoa ila bado imekuwa ngumu maana wafuasi wengi wameoa wake wa 4 Sasa kipato kurumanyati ndio maana hutoa kwa uchache mno Sasa huenda wakaanza kutoa baada ya kufokewa na aliyekuwa mme wa zaylsia
 
Mnyazi ndo nani tena huko Dar πŸ˜ƒπŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Uislamu unataka kila mtu afanyekazi,uimamu sio kazi ,ni ibada,yeye imamu pia anatakiwa afanyekazi.watafute kazi za kufanya.Mtume Muhammad(SAW),alifanyakazi,mwanzo aliajiriwa na Bi khadija,katika kusimamia misafara ya biashara za Bi Khadija,na pia alikuwa,mchungaji wa wanyama,hakukaa akasubiri sadaka.
 
Kwa hiyo wewe unamzidi manara kujua uislamu?!
Mwenzako alishakusa mkufunzi wa dini
 
Uislamu tofauti na dini nyinginezo,uimamu sio kazi,ni ibada,inatakiwa,Imam atafute kazi au biashara afanye.Mtume Muhammad (SAW),alifanyakazi Kwa Bi Khadija ya kusimamia misafara ya biashara za Bi Khadija,na pia alikuwa mfugaji wa wanyama,alifanyakazi,hakutegemea sadaka.Na ndio pia ukaona katika uislamu,siku ya ijumaa,sio yote ni ya mapunziko,mnakwenda kazini au biashara kama kawaida,ikifika mda wa swala,mnaswali,mkimaliza kuswali mnarudi kazini au kwenye biashara
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…