Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,318
- 33,125
Basi la Sebena lililopinduka na kuua jumla ya watu 17 | Thursday, August 09, 2012 10:09 AM WATU 17 wamefariki dunia na wengine 78 kujeruhiwa baada ya basi la abiria walilokuwa wakisafiria kupinduka eneo la Kitunda Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora. |
Basi hilo la Sabena aina ya Scania yenye namba za usajili T 570 AAM ndilo lililosababisha vifo hivyo majra ya jana mchana. Basi hilo lilikuwa likitokea mkoani Tabora kuelekea mkoani Mbeya Miongoni wa watu waliokufa walikuwemo watoto watano, wanawake sita na wanaume sita ambao miili yao imehifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa Kitete kwa ajili ya kutambuliwa na ndugu na jamaa zao. Chanzo cha ajali hiyo imedaiwa kugoma kwa usukani wakati dereva alipokuwa akijaribu kulikwepa Fuso lililokuwa limeegeshwa katika kona eneo hilo, hivyo basi hilo likaacha njia na kupinduka |
<tbody>
</tbody>
VIDEO - 17 Wafariki Papo hapo, 78 Wajeruhiwa Kwenye Ajali Tabora
Last edited by a moderator: