Tukio la ugaidi ni ugaidi, liwe limefanywa na mwarabu, mkristu, muislamu, Raisi, Waziri, mbunge ama raia yeyote yule. Leo Serikali ya chama cha mapinduzi chini ya waziri wa mambo ya ndani imeutangazia umma imekamata watu sita ambao wanashukiwa kujihusisha na tendo la kujipatia bomu, kulisafirisha na kulitupa katikati ya waumini wa kikakoliki kuuwa na kujeruhi watu vibaya.
Lengo lilikuwa ni kuuwa waumini, kuuwa Mwakilishi wa Papa Tanzania Askofu Padilla na Askofu mkuu wa kanisa katoliki Jimbo la Arusha.
Kinachoshangaza hata kilichoshangaza kanisa pamoja ni usiri wa watuhumiwa hawa wengine huku serikali ikiamua kutangaza jina moja na kuficha majina mengine. Kanisa wao wanadai swala la ugaidi ni ugaidi, Papa alipigwa risasi kanisani, kanisa limeshudia kuteswa na kuuwawa kwa waumini wake kuchomwa makanisa sehemu nyingi za dunia ila hawajawahi kukutana na serikali laghai kama ya tanzania, waliouwawa ni wananchi, walijeruhiwa ni raia pamoja na watoto kwa nini serikali inaogopa kutaja majina ya wote kama imeamua kuyataja?.
Wasi wasi uliopo ni kwamba Victor kama kweli ndio jina lake ananafasi ndogo sana kwenye njama na hujuma hizi zidi ya kanisa. Wanaamini kunakitu kikubwa kinafichwa na serikali ya Tanzania dhidi ya uhalifu huu wa kuuwa kanisa na watu wake.
Wanaendelea kusema hata kama majina mengine yanaonekana ni watu ambao serikali inayaogopa ama kwa rushwa ama kwa uswahiba mhalifu ni mhalifu kwanini alindwe hata jina lake, kwanini huyu mmoja aonekane kwamba ndiye mhalifu kuliko wote. Je nani alimpa bomu, nani alilitengeza au kununua nani alilifikisha arusha malengo yao yalikuwa nini.
Serikali yetu imeanza kucheza mchezo wa kujificha. Maoni yangu kwamba baada ya kutokuaminiana kidini ambako tayari kumejengeka ndani ya nchi, mara baada ya bomu kila raia alihisi ni swala la udini. Hali ya hamaki ni kubwa sana, serikali kupitia kwa Nchimbi wakaona watengeneze jina la haraka la Kikristu ili kuwafanya raia watulie. Mbinu hizi za kuzima moto haziwezi kumaliza matatizo. Mkristu anaweza kuwa gaidi, Muislamu anaweza kuwa gaidi, mpagani anaweza kuwa gaidi, mtanzania anaweza kuwa gaidi.
Serikali yetu inakumbatia udini ndio maana inafikiri kidini. Kwanini leo tuogope wahalifu kwa majina yao?? Imeanza lini hii??
Serikali iache kucheza na roho za watu, isifikiri kuwa inauwezo wa kuchezea maisha yetu siku zote.
Watu wa Arusha tuanze kufuatilia huyu Victor AMbrose ni nani? Je alikuwa na marafiki gani kwa kipindi cha mwezi mmoja kuanzia tarehe 6 may kurudi nyuma. Wapi analala, wapi anakula, wapi anapaki bodaboda yake , maisha yake kiuchumi ndani ya mwaka mmoja. Je alibadilika kimaisha within a month , week, or day prior to attack?
Je pikipiki anayoendesha ni ya kwake au yakukodi. Ni nini Tabia za waendesha bodaboda kuwajua abiria wao. Je anamarafiki kwenye kitua chake cha kazi? Je siku ya tukio alitokea kituoni ama hakuonekana kutwa??
Je hiyo bodaboda ilifika na abiria kanisani? Na kama alifika mwenyewe kuna mtu alimwona akirusha kitu kilicholipuka?? Je kulikuwa na ulinzi kiasi gani kanisani, Je polisi walikuwepo na kama walikuwepo walikuwa na usafiri gani au miguu?? Lazima alikuwa karibu na watu akirusha kitu hicho au alikuwa bado juu ya bodaboda?? Alilibeba bomu kwenye nini? Nani majirani zake?, wazazi wake? ndugu zake? ana mke au mchumba? Ni mzaliwa wa wapi mkoa gani, kijiji gani? Ni muumini wa dini gani? Je huwa anahudhuria nyumba za ibada?? Tabia yake kwa ujumla ikoje anavuta bangi? anakunywa pombe? anavuta sigara? Alisoma shule gani primary na je aliendelea na masomo wapi?? lets dig down then serikali ituletee na hao wengine tutampata tu mhalifu wetu. Citizen intelligence is better than a government one. Once we believe on ourselves we can solve all our miseries
Je alikamatwa muda gani baada ya tukio la kurushwa bomu?? Je ni taarifa gani kanisa la Olasit wanayo mpaka sasa?? Je serikali inashirikiana vipi na paroko wa kanisa, walei, askofu lebulu na Askofu padilla au na wao wako kwenye sintofahamu??
Je kuchomwa kuchomwa kwa makanisa mengine kuna uhusiano wowote wa ni la Arusha, Je kupigwa Risasi Mapadri Zanzibar kuna uhusiano wowote na hili hasa ikizingatia mpiga risasi na mrusha bomu wote walitumia pikipiki.
Kwanini Hawa wahalifu wote target yao ni kanisa? Ni nini chanzo cha uhalifu huu. Hata Magaidi ambao wanaogopwa sana duniani aghalabu sana kudhuru makanisa. Sehemu yeyote inayokuwa na uchoma au ulipuaji makanisa huwa ni chuki za ndani baina ya imani na imani. Ugaidi wa Kimataifa hauhusishi Kuchomwa nyumba za Ibada ila ugaidi wa Ndani.
Je Magaidi hawa kama ni wa Saudia walikuwa nia yao ni kumuuwa Askofu Padilla???
Serikali ijibu haya maswali, wananchi aanzeni utafiti wenu pekee, mkitegemea hii serikali isiyojiamini kesho tutaangamia wote.
Angalizo hili swala tusilaumiane kwa misingi ya dini, ila tukubali wapo wengi kati yetu wanachuki za kidini na wapo tayari kuuwa wenzao kwa chuki zao na hawa wapo kwenye imani zote.
Upendo na ukweli utatuweka huru.
Tusiogope tusibaguane huu ndio uwe wakati wa kuwa pamoja kuliko siku zote za maisha. Tuwakatae hawa wahalifu, na punguze hisia zetu za kiimani. Wote tuseme hatuwataki.