Vibanda vya Wafanyabiashara wadogo vyabomolewa Stendi ya Kawe (kwa Mwamposa) - Je, kutakuwa na ukarabati au ni ubabe wa mamlaka tu?

Vibanda vya Wafanyabiashara wadogo vyabomolewa Stendi ya Kawe (kwa Mwamposa) - Je, kutakuwa na ukarabati au ni ubabe wa mamlaka tu?

OleWako

Member
Joined
Sep 7, 2021
Posts
24
Reaction score
67
Leo nimekuta vibanda vyote huko stendi ya daladala Kawe kwa Mwamposa vilibomolewa. Baada ya vilio vya muda mrefu vya wakazi na wapanda daladala, serikali inaanza kuchukua hatua za kuboresha mazingira ya stendi au ni kusimamia kwa kanuni za eneo tu?

Natumaini sana hatimaye maboresho yatafanywa.. Stendi hii isiendelee kuwa miongoni mwa stendi bovu jijini Dar es Salaam. Hasa wakifungua maghorofa mapya ya makazi hapo karibu na stendi, load itaongezeka. Hali ambayo haisapotigi na stendi ya mchanga na matope..

IMG_20250728_074621.jpg
IMG_20250728_074521.jpg
 
Ndugu yangu Sildenafil Citrate atakunywa wapi tena supu ya utumbo asubuhi na mbupu za kuchoma jioni?

Anyway ni hatua nzuri kwa ajili ya maendeleo. Sasa stendi kama wanaamua kuwepo eneo hilo, basi iboreshwe iwe na hadhi.
 
kwa watafutaji wenzetu poleni sana maana hapo kuna mpaka garages
 
Back
Top Bottom