Jamaa_Mbishi
JF-Expert Member
- Jun 15, 2013
- 9,146
- 6,052
Wadogo zangu Vera na Hamisa (wote wana miaka 20 ni wadogo zangu), hongereni kwa kujaribu kuimba, sio kwa ubaya ila hamjui kuimba dears, mziki mnaupenda ila wenyewe hauwapendi. Sauti zenu nyembambaa haziburudishi labda mkaimbe nyimbo za injili.
Kipaji cha kuimba hamna, mashairi mabovu yanayotokana na hisia tu Vera baada ya kuchoka kiben ten chake kaibuka na wimbo, Hamisa nae kuzaa huku na kule bila uelekeo na bado hawamuelewi kaibuka na wimbo. Vi nyimbo havina mbele wala nyuma
Sio lazma kila mtu aimbe wengine tubaki mashabiki, tuburudishwe na wenye vipaji vyao. Ni hayo tu.
Na si kuwa na sauti nyembamba tu ila hawawezi kuimba hata kidogo....wako out of tune. Bora mwenzao Jokate aliona haya mapema maana naye alikuwa hivyo hivyo. Muziki una kanuni zake si kila mbongo fleva ni mwanamuziki kweli, wanasaidiwa na studio tu ku tune sauti zao.