Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,806
- 15,379
Mnamo Juni mwaka 2009 nilivamiwa na vibaka nyumbani kwangu na kuibiwa vitu fulani fulani pamoja na kujeruhiwa mimi na familia yangu. Tukio lile tuliliripoti Polisi, lakini kutokana na majukumu yangu kikazi, nilizimika kusafiri, hivyo siku ya pili baada ya tukio lile nilisafiri na kumuacha mke wangu akiendelea kushirikiana na askari wa upelelezi ili kufanikisha kupatikana kwa wahalifu hao.Baada ya kuulizwa sana kama kuna watu anadhani au anawahisi kuhusika na uhalifu ule mke wangu, hakuwa na jibu lakini lakini askari yule wa upelelezi alimuuliza kama kuna mtu yeyote mgeni aliwahi kufika hapo kwetu siku za karibuni, ndipo mke wangu akawataja vijana fulani waliotupakia rangi nyumba tuliyokuwa tunaishi juma moja lililopita. Vijana wale walifanya kazi ile kwa siku tatu na walipiga rangi hadi vyumbani ambapo waliona kila kitu tunachomiliki. Kutokana na maswali mengi ya Kipolisi mke wangu alishawishika kuwataja wale vijana watatu na mahali wanapoishi.
Nakumbuka tuliwafahamu wale vijana kupitia kwa rafiki yetu ambaye alitufahamisha kwamba ni mafundi wazuri wa kupaka rangi na wametoka kijiji kimoja. Baada ya vijana wale kutajwa Polisi walikwenda kuwakamata na kuwaweka ndani na kufuatia mkong'oto mkali ili wakiri kwamba ndio waliohusika kufanya mchongo wa kutuletea vibaka watuibie ili wagawane. Bahati nzuri nilirudi siku mbili baadae tangu vijana wale wakamatwe na nilipopata taarifa zile nilikwenda mara moja Polisi na kuwauliza kama walifanya upelelezi na kujiridhisha kama wale vijana walihusika au waliwakamata tu na kuwaweka ndani, Polisi wakadai kwamba wako kwenye upelelezi na wanaendelea kuwahoji watuhumiwa. Nilishirikiana na yule jamaa yangu kuwashikia dhamana wale vijana kisha nikawaomba radhi kwa yote yaliyotokea. Mwezi mmoja baadae nikiwa na rafiki yangu mwingine mahali fulani tukipata vinywaji rafiki yake mmoja alijumuika na sisi, na katika mazungumzo yetu, tukajikuta tukizungumzia wimbi la Taxi bubu zinazotumika kupora watu, yule rafikiye akatusimulia kuwa mwezi uliopita mdogo wake aliona Taxi moja mida ya alfajiri maeneo ambayo siyo mbali sana na ninapoishi wakipakia vitu ambavyo alivituhumu kuwa ni vya wizi, alivitaja vitu hivyo nikahisi kuwa inawezekana vikawa ni vya kwangu kwani mwezi huo ndio na mimi niliibiwa.
Tulimpigia mdogo wake simu akaja na tukamdadisi zaidi. Kwa bahati alikuwa amenakili namba za Taxi ile. Nilikwenda na yule kijana hadi Polisi na kuwapa zile taarifa. Siku tatu baadae nilipigiwa simu kwamba vitu vyangu vimekamatwa na watuhumiwa walioniibia wako ndani. Nilikwenda polisi na mke wangu na kuvitambua vitu vyetu vilivyoibwa.
Tukio hili lilinifanya niwatafute wale vijana kwa mara ya pili na kuwaomba radhi.
Nakumbuka tuliwafahamu wale vijana kupitia kwa rafiki yetu ambaye alitufahamisha kwamba ni mafundi wazuri wa kupaka rangi na wametoka kijiji kimoja. Baada ya vijana wale kutajwa Polisi walikwenda kuwakamata na kuwaweka ndani na kufuatia mkong'oto mkali ili wakiri kwamba ndio waliohusika kufanya mchongo wa kutuletea vibaka watuibie ili wagawane. Bahati nzuri nilirudi siku mbili baadae tangu vijana wale wakamatwe na nilipopata taarifa zile nilikwenda mara moja Polisi na kuwauliza kama walifanya upelelezi na kujiridhisha kama wale vijana walihusika au waliwakamata tu na kuwaweka ndani, Polisi wakadai kwamba wako kwenye upelelezi na wanaendelea kuwahoji watuhumiwa. Nilishirikiana na yule jamaa yangu kuwashikia dhamana wale vijana kisha nikawaomba radhi kwa yote yaliyotokea. Mwezi mmoja baadae nikiwa na rafiki yangu mwingine mahali fulani tukipata vinywaji rafiki yake mmoja alijumuika na sisi, na katika mazungumzo yetu, tukajikuta tukizungumzia wimbi la Taxi bubu zinazotumika kupora watu, yule rafikiye akatusimulia kuwa mwezi uliopita mdogo wake aliona Taxi moja mida ya alfajiri maeneo ambayo siyo mbali sana na ninapoishi wakipakia vitu ambavyo alivituhumu kuwa ni vya wizi, alivitaja vitu hivyo nikahisi kuwa inawezekana vikawa ni vya kwangu kwani mwezi huo ndio na mimi niliibiwa.
Tulimpigia mdogo wake simu akaja na tukamdadisi zaidi. Kwa bahati alikuwa amenakili namba za Taxi ile. Nilikwenda na yule kijana hadi Polisi na kuwapa zile taarifa. Siku tatu baadae nilipigiwa simu kwamba vitu vyangu vimekamatwa na watuhumiwa walioniibia wako ndani. Nilikwenda polisi na mke wangu na kuvitambua vitu vyetu vilivyoibwa.
Tukio hili lilinifanya niwatafute wale vijana kwa mara ya pili na kuwaomba radhi.