Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,500
Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama cha Mapinduzi Tanzania (UWT) mkoa wa Lindi, wamempongeza Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa ujenzi wa shule ya sekondari ya wavulana ya Kanda ya Kusini katika eneo la kata ya Kiwalala Halmashauri ya Mtama inayogharimu kiasi cha Tsh 4.1 Bilioni .
Akizungumza wakati wa ziara ya kama ya utekelezaji wa UWT mkoa wa Lindi, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Kuruthumu Runje alisema kuwa kujengwa kwa shule hiyo kutasaidia kukuza sekta ya kwa watoto wa kiume kwa mikoa ya kanda ya Kusini.
Runje alisema kuwa kwa kipindi cha miaka minne ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi ya shilingi Trilioni 1.324 katika mkoa wa Lindi kwa ajili ya miradi ya Maendeleo katika sekta za Afya, Elimu, Maji, kilimo,madini, nishati,miundombinu na miradi mingine.
Aidha mwenyekiti wa UWT Runje aliwataka Wanawake wote wa mkoa wa Lindi kuhakikisha wanapigia kura za kutosha ili Dkt.Samia Suluhu Hassan ashinde kwa kishindo kutokana na kazi kubwa aliyoifanya.
Runje alisema kuwa kwa kipindi cha miaka minne ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa zaidi ya shilingi Trilioni 1.324 katika mkoa wa Lindi kwa ajili ya miradi ya Maendeleo katika sekta za Afya, Elimu, Maji, kilimo,madini, nishati,miundombinu na miradi mingine.