Stabilaiza
JF-Expert Member
- Jul 11, 2012
- 1,843
- 1,143
Kila chama huanzishishwa kwa makusudi maalumu na kinakuwa na fikra za kuhusu uwezo wao, na kwa nadra hufanya tathmini ya mapungufu yao. Katika dokezo hili ninachambua uwezo na mapungufu ya ACT kwa mtazamo wa nguzo zake yaani Zitto, Kitila na Mwingimba.Katika kujiandaa kuanzisha chama cha siasa, Zitto, Kitila na Mwigamba walibuni mbinu ya kufanya mapinduzi ya siri katika chama cha Chadema. Kwa bahati mbaya kwao na nzuri kwa Chadema waraka wao wa siri ulinaswa na wao wakafukuzwa kwa usaliti huo na wametimkia ACT. Uwezo na mapungufu ya washirika hao watatu, ndio uwezo na mapungufu ya ACT.
Katika waraka wa usaliti, MM alitajwa kuwa na uwezo kama kijana, kuungwa mkono na CCM na kwamba dini yake ilikuwa ni mtaji wa kisiasa kwake. Ndio maana katika harakati hizo, wapambe wa washirika hao watatu waliwashambulia sana viongozi wa Chadema na chama chao isivyo halali wakitumia lugha za kibaguzi za karata ya udini na kabila kama njia ya kujitangaza. Bahati mbaya, uwezo ulioainishwa na nguzo za ACT, ni mapungufu wakati huohuo. Hoja ya ujana haina mashiko kwa sababu uongozi bora hautegemei umri na ndio maana nchi kama marekani huchagua kijana au mtu mzima kulingana na uwezo wa kiongozi husika. Hivyo ujana siyo sifa ya kuwa kiongozi bora. Habari ya kuungwa mkono na CCM nayo ni mapungufu makubwa. Inaonyesha kuwa ACT ni chama cha serikali ya CCM. Moja ya tabia ya vyama vya upinzani vinavyoanzishwa na serikali iliyoko madarakani huibuka karibia na uchaguzi ili kujaribu kupunguza kura za wapinzani halisi wa chama kilichopo madarakani, na kwa sasa ni washirika wa UKAWA, ikiwemo Chadema.
Zitto ailishaonyesha kuwa ni mtu wa CCM. Kwa mfano wakati Chadema ikiwahenyesha CCM kule Arumeru Mashariki wakati wa uchaguzi wa ubunge, Zitto alijaribu kuisaidia CCM ipate jimbo hilo bila mafanikio, pale alipotangaza kuwa atagombea uraisi wakati akijua kuwa hakuwa amekidhi kigezo cha kisheria cha umri kugombea urais. Alifanya vile ili wapiga kura wa Arumeru wahamishie mawazo yao kwa Zitto, badala ya kuzingatia kupiga kura za kumwingiza Nasari Bungeni. Zitto pia amenukuliwa akiwaponda UKAWA, muungano ambao unatetea maslahi ya wananchi katika katiba mpya. Hii inaonyesha kuwa Zitto anawaunga mkono CCM na kuwatosa wananchi. Hakuna mzalendo anayewatosa wananchi na kupuuza maslahi yao. Hoja ya dini yake kama karata ya kisiasa nayo ni mapungufu makubwa ya ACT. Chama ambacho kinataka kujinadi kwa uzalendo, kinatumia dini ya Zitto kupata uungwaji mkono. Karata hii ya udini ndiyo hiyohiyo inatumiwa na CCM. Ni kinyume kabisa na fikra za baba wa taifa mwalimu Nyerere. Mwl. Nyerere alipata kusema kuwa mwanasiasa aliyefilisika hutumia udini na ukabika kuungwa mkono. Haya ndiyo wanayofanya Zitto, Kitila na Mwigamba kama walivyoonyesha katika waraka wao wa usaliti wa kuanzisha chama ndani ya chama. Hii inaonyesha wazi kuwa ACT ni chama cha serikali ya CCM. Chama kinachojinasibu kwa uwezo wa udini siyo chama cha kizalendo bali chama chenye malengo ya kuendeleza ukandamizaji wa CCM kwa njia yeyote ile huku kikimomonyoa misingi ya umoja na amani ya taifa aliyoiacha baba wa taifa letu Mwl. Nyerere.
Katika waraka wa usaliti, MM alitajwa kuwa na uwezo kama kijana, kuungwa mkono na CCM na kwamba dini yake ilikuwa ni mtaji wa kisiasa kwake. Ndio maana katika harakati hizo, wapambe wa washirika hao watatu waliwashambulia sana viongozi wa Chadema na chama chao isivyo halali wakitumia lugha za kibaguzi za karata ya udini na kabila kama njia ya kujitangaza. Bahati mbaya, uwezo ulioainishwa na nguzo za ACT, ni mapungufu wakati huohuo. Hoja ya ujana haina mashiko kwa sababu uongozi bora hautegemei umri na ndio maana nchi kama marekani huchagua kijana au mtu mzima kulingana na uwezo wa kiongozi husika. Hivyo ujana siyo sifa ya kuwa kiongozi bora. Habari ya kuungwa mkono na CCM nayo ni mapungufu makubwa. Inaonyesha kuwa ACT ni chama cha serikali ya CCM. Moja ya tabia ya vyama vya upinzani vinavyoanzishwa na serikali iliyoko madarakani huibuka karibia na uchaguzi ili kujaribu kupunguza kura za wapinzani halisi wa chama kilichopo madarakani, na kwa sasa ni washirika wa UKAWA, ikiwemo Chadema.
Zitto ailishaonyesha kuwa ni mtu wa CCM. Kwa mfano wakati Chadema ikiwahenyesha CCM kule Arumeru Mashariki wakati wa uchaguzi wa ubunge, Zitto alijaribu kuisaidia CCM ipate jimbo hilo bila mafanikio, pale alipotangaza kuwa atagombea uraisi wakati akijua kuwa hakuwa amekidhi kigezo cha kisheria cha umri kugombea urais. Alifanya vile ili wapiga kura wa Arumeru wahamishie mawazo yao kwa Zitto, badala ya kuzingatia kupiga kura za kumwingiza Nasari Bungeni. Zitto pia amenukuliwa akiwaponda UKAWA, muungano ambao unatetea maslahi ya wananchi katika katiba mpya. Hii inaonyesha kuwa Zitto anawaunga mkono CCM na kuwatosa wananchi. Hakuna mzalendo anayewatosa wananchi na kupuuza maslahi yao. Hoja ya dini yake kama karata ya kisiasa nayo ni mapungufu makubwa ya ACT. Chama ambacho kinataka kujinadi kwa uzalendo, kinatumia dini ya Zitto kupata uungwaji mkono. Karata hii ya udini ndiyo hiyohiyo inatumiwa na CCM. Ni kinyume kabisa na fikra za baba wa taifa mwalimu Nyerere. Mwl. Nyerere alipata kusema kuwa mwanasiasa aliyefilisika hutumia udini na ukabika kuungwa mkono. Haya ndiyo wanayofanya Zitto, Kitila na Mwigamba kama walivyoonyesha katika waraka wao wa usaliti wa kuanzisha chama ndani ya chama. Hii inaonyesha wazi kuwa ACT ni chama cha serikali ya CCM. Chama kinachojinasibu kwa uwezo wa udini siyo chama cha kizalendo bali chama chenye malengo ya kuendeleza ukandamizaji wa CCM kwa njia yeyote ile huku kikimomonyoa misingi ya umoja na amani ya taifa aliyoiacha baba wa taifa letu Mwl. Nyerere.