Uwekezaji wa raia wa China uchunguzwe

mwembemdogo

JF-Expert Member
Feb 28, 2016
2,282
1,252
Uwekezaji wa raia wa china unapaswa kuchunguzwa. Imenilazimu niseme hivyo kwani raia hao hawataki kufuata sheria za nchi. Raia hao kila sehemu waliyowekeza ni lazima migogoro na serikali pia wananchi itokee. Kila ukisikiliza taarifa ya habari ni lazima usikie habari zao.

Kwa mfano jana ilisemekana kampuni ya kichina ya ujenzi wabarabara imewafukuza wafanyakazi 300 waliogoma wakiidai kampuni mishahara yao na malimbikizo licha ya kuwa kulikuwa na makubaliano ya nyongeza lakini kampuni hiyo iligoma kutekeleza.

Leo huko Morogoro kampuni ya kichina inachimba mawe ya kutengeneza marumaru licha ya kuzuiliwa miaka mitatu iliyopita na pia kutokulipa kodi. Mahakamani raia wa kichina wamejaa kwa kesi za ukwepaji kodi. Najiuliza kwanini wachina hawa wamekuwa kero ndani ya nchi yetu?
Wanapata wapi jeuri ya kutokutii sheria za nchi?

Tunaiomba serikali ichunguze uwekezaji wao kwani wamekuwa kama watanzania wanajiendea vijijini na kuanza shughuli kama wazawa.
 
hawa watu bwana sijui hata wanaishi vipi kweli ni shamba la bibi, juzi niliona wale wanao jenga uwanja wa mpira Dar wameacha kazi hiyo wako nje kabisa ya mkataba sasa hii dharau gani hii nani yuko nyuma ya hawa watu wanafanya wanavyo taka na si tunavyo taka!!!!!
 
CCM wanayo majibu,,,
wachina si marafiki zetu tuu?!? halafu nyie achen ufukunyuzi
 
riz moko anayo majibu aisee tumlaum yeye kwa Ile sembe aliyokamatwa nayo China
 
cha kumshukuru Mungu ni kwamba wachina siyo waongaji wazuri la sivyo baada ya miaka kumi tungekuwa na sura za kichina kila kona maana popote unapoenda tanzania mchina yupo au tuitwe tanzachina
 
Sasa ivi serikali inatakiwa kuwa makini na wageni kuja kufanya biashara apa nchini. Kingine miaka ya 2011 pale St. Augustine University kulikuwa na mlimbikano wa wakenya kuja kufundisha apa Tanzania. Walikuwa na tendency wakija wanaoa na Kuolewa Na watanzania kwa lengo la kupata aridhi ya kulima na kufuga. Wawaangalie wageni wote Kenyan, Uganda na Rwanda wanakuja kwa ajiri ya kufundisha lakini wakishafika target yao ni aridhi. Serikali ichunguze watu wa NIDA, RITA na OFFICE ya MIGRATION. Nendeni kwy shule za Accademic angalia vibali vya walimu na mali walizo nazo ndio mtaelewa nn namaanisha.
 
Sasa ivi serikali inatakiwa kuwa makini na wageni kuja kufanya biashara apa nchini. Kingine miaka ya 2011 pale St. Augustine University kulikuwa na mlimbikano wa wakenya kuja kufundisha apa Tanzania. Walikuwa na tendency wakija wanaoa na Kuolewa Na watanzania kwa lengo la kupata aridhi ya kulima na kufuga. Wawaangalie wageni wote Kenyan, Uganda na Rwanda wanakuja kwa ajiri ya kufundisha lakini wakishafika target yao ni aridhi. Serikali ichunguze watu wa NIDA, RITA na OFFICE ya MIGRATION. Nendeni kwy shule za Accademic angalia vibali vya walimu na mali walizo nazo ndio mtaelewa nn namaanisha.
 
Uwekezaji wa raia wa china unapaswa kuchunguzwa. Imenilazimu niseme hivyo kwani raia hao hawataki kufuata sheria za nchi. Raia hao kila sehemu waliyowekeza ni lazima migogoro na serikali pia wananchi itokee. Kila ukisikiliza taarifa ya habari ni lazima usikie habari zao.

Kwa mfano jana ilisemekana kampuni ya kichina ya ujenzi wabarabara imewafukuza wafanyakazi 300 waliogoma wakiidai kampuni mishahara yao na malimbikizo licha ya kuwa kulikuwa na makubaliano ya nyongeza lakini kampuni hiyo iligoma kutekeleza.

Leo huko Morogoro kampuni ya kichina inachimba mawe ya kutengeneza marumaru licha ya kuzuiliwa miaka mitatu iliyopita na pia kutokulipa kodi. Mahakamani raia wa kichina wamejaa kwa kesi za ukwepaji kodi. Najiuliza kwanini wachina hawa wamekuwa kero ndani ya nchi yetu?
Wanapata wapi jeuri ya kutokutii sheria za nchi?

Tunaiomba serikali ichunguze uwekezaji wao kwani wamekuwa kama watanzania wanajiendea vijijini na kuanza shughuli kama wazawa.

Mkuu hawa jamaa ni balaa tupu, kusema kweli wanao kuja sio wawekezaji ni wababaishaji tu hakuna cha viwanda wala nini sijui - wanajenga mabanda banda wanaweka vijimashine mshenzi na kuanza kutengeneza furniture na marumaru vitu ambavyo hata watanzania wanaweza kutengeneza - sasa sijui hawa Wachina upewa vibari vya uwekezaji,udalali, umachinga au ruhusa ya kutuibia mali asili zetu, uwezi kusikia wazungu eajingiza kwenye mabo ya wizi wa meno ya Tembo na nyara nyingine - estu hawa hawafai hata kidogo kwa bahati mbaya Taifa letu ndilo linawapo kiburi na jeuri kwa kutowachukulia hstua stahiki.

Serikali inapashwa kuwapa masharti magumu kwa kuwaekea kiwango cha mtaji unaotakiwa awe nao muwekezaji, sio wabakuja wachina wa muchoma mahindi Kaliakoo.
 
Back
Top Bottom