"Demokrasiabila mipaka ni ukichaa na demokrasia bila nidhamu ni uwendawazimu"Mwl Jk Nyerere
Ndugu zangu Watanzania, naomba mfahamu kuwa miongoni mwa wajumbe wote wabunge la katiba takriban 600, wajumbe waliofanya maamuzi haramu yakugomea ni 79 ambao ni pungufu ya asilimia 15% ya wajumbe wote, nasio kweli kuwa wao pekee ndio wenye tafsiri sahihi ya rasimu. Wajumbe wa makundi mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa vyama vyote vya siasa takriban 18 kati ya 22 bado wamo kwenye bunge, kati ya wajumbe wakundi la 201 walioasi ni 15 ambapo bara ni 9 na zanzibar 6 lakini piakatika wanaojiita UKAWA wapo wabunge ambao wameendelea kurudi bungeni kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa. Takwimu hizizinatuthibitishia kuwa UKAWA ni kikundi kidogo cha watu waliojipangakuvuruga AMANI ya nchi, watu ambao hawataki KATIBA wala hawatakiMUUNGANO.
Nduguzangu Watanzania, naomba leo niwape picha na kilichopo nyuma ya pazia ya kikundi hiki kiitwacho UKAWA ambacho kinaratibiwa na viongoziwachache na maslahi yake kujulikana kwa wachache zaidi tena yaliyojikita katika misingi ya kibinafsi. Mfano, ndoa ya CUF naCHADEMA inayopelekea NCCR mageuzi kuwa bendera fuata upepo imejengwakatika misingi ya kuvunja muungano, kwa makubaliano kuwa CUF kubaki na Zanzibar na CHADEMA kubaki na Tanganyika. CUF inataka inufaike namkakati dhalimu wa kunyonya rasilimali za wazanzibar yakiwemo mafuta bila kushurutishwa na sheria za muungano kwani wakiamini kubaki na muungano imara CUF na viongozi hao wachache katika chama hichowanakosa fursa za kupora rasilimali za wazanzibar.
IkubumbukweMuungano ndio unalinda mipaka na usalama wa raia katika kujiendelezana kujinufaisha bila ubaguzi wa kikundi cha watu wachache ambachokinaenda kinyume na utawala wa sheria.
Ikumbukwekuwa rasimu ya CUF walioipeleka kwa Mhe. Raisi mwaka 2011,mapendekezo yao ni tofauti na madai yao sasa ya serikali 3, hapa inatosha kutupa picha kuwa nia yao ni kuvunja muungano ili watuache katika mfarakano kama nchi nyingine zinazoteseka kwa sababu yawanasiasa uchwara.
Ifahamike ajenda ya CHADEMA ni kuvunja muungano ndio maana CHADEMA hawahangaiki kuimarisha chama Zanzibar, nia yao ni kubaki na Tanganyika ili waigawe Tanganyika katika vipande vipande kwa lugha ya majimbo iliadhima yao ya ukanda na ukabila itimie. Moja ya kanda yao ambayowametangaza katika kanda 8 walizo nazo ni Kilimanjaro, Tanga, Arushana Manyara. CHADEMA ina amini kanda hii inajitosheleza kwani ina bandari, mbuga za wanyama, madini, milima . Na hii imepelekea mbunge mmoja wapo wa CHADEMA kulazimika kusema kaskazini ni nchi huru huku mwenyekiti wao Mbowe akiendelea kudai mapato ya mlima Kilimanjaro yabaki Kilimanjaro.
Katikakipindi hiki ambacho wenzetu wamegomea bunge la katiba ambalo lipo kisheria na madai yao yakibadilika kila kunapokucha tena yakiwa na upotoshaji mkubwa kwa kufanya siasa chafu ili mradi watimize azma yakuisambaratisha Tanzania wakiwa makuwadi wazuri wa soko huria.Ukihoji leo sababu iliyowafanya watoke bungeni ni tofauti kabisa na sababu waliyoitoa siku wanatoka bungeni, eti msingi wao mkuu wao ni watetezi wa wananchi. Lakini tumesikia katika vyombo mbalimbali wananchi hao wakiwaasa na wakiwataka warejee bungeni ili kukamilisha kazi ya kisheria na tumaini la watanzania la kuwapatia katiba mpya. UKAWA hawa bila haya wamekataa. Swali? wanamtumikia nani. Mpaka sasa imepelekea wananchi hao wanaosema wanawawakilisha wameamua wenyewe kuja Dodoma kuendelea kusema kero zao na shida zao ili katiba hii iweze kutoa majawabu, mfano tumeshuhudia makundi ya wakulima, jukwaa la wahariri wa vyombo vya habari, wafugaji na makundi kadha wakadha yameendelea kutiririka Dodoma.
Hii ni picha tosha kuwa UKAWAhawawatumikii Watanzania na wameamua kuwahadaa Watanzania kwa mgongo wa kuwatetea huku ajenda yao ikiwa maslahi binafsi.
Nduguzangu Watanzania tunapowaunga mkono watu wanaoendelea kuligomea bunge la katiba wakati tunajua nchi inaongozwa kwa utawala wa sheria, na wao ndio wamevunja sheria, tujue kabisa kuwa tunaenda kinyume na utawala bora, ambao umejengwa kwenye msingi wa sheria na demokrasia.Msingi wa demokrasia sio kususa baada ya kushindwa hoja, UKAWAhawataki hoja za wengine na wanalazimisha hoja zao pekee ndizozikubalike kinyume na msingi wa demokrasia. Na bila haya watu hao wasiojua demokrasia wameendelea kuwashawishi watanzania waingie barabarani huku wakijua kuwa Katiba haipatikani barabarani kama wanahoja kwanini wanaikimbia Dodoma? Mchakato huu ulianza kisheriana utahitimishwa kisheria, sio matamko ya makuwadi wa soko huria.
Miongonimwa madai yao matatu, (i) Rais avunje bunge (2) kinachojadiliwaDodoma sio rasimu ya warioba (3) Serikali tatu ndio maendeleo
Kwaujumla wake, UKAWA wanajua mamlaka ya Rais kwa mujibu wa sheria yamabadiliko ya katiba ya mwaka 2011, sura namba 83 imempa Rais mamlaka ya kuunda tume, kuchagua wajumbe 201, kutangaza na kuitisha bunge nakuzindua bunge la katiba, kupokea katiba inayopendekezwa na kuitangaza kwenye gazeti la serikali.,kwanini wanataka kumlazimishaRais kuvunja Sheria kwani hayo niliyoyataja ndio ambayo Rais anayo mamlaka ya kisheria kuyafanya katika mchakato huu wa Bunge la Katiba,na ndio maana hata wale wajumbe aliowateua ambao wamegomea Rais hajawatengua.,kinachojadiliwa bungeni ni Rasimu ya jaji warioba na kiko wazi, kwa sababu msingi mkuu wa majadiliano ni Rasimu inayotokana na tume tena kwa mujibu wa Sura namba 83 kifungu cha sheria namba 25/26 na kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu namba 33(8). Wanajua mamlaka ya bunge na waliohusika kutengeneza sheria hizi pamoja na kanuni waache kuwahadaa watanzania.
Jambola mwisho lenye kusikitisha zaidi ni kung'ang'ania Serikali tatu kana kwamba ndio kilio kikubwa cha watanzania, naomba niulize swali kati ya Muungano na migogoro ya ardhi ni jambo lipi limepoteza maishaya watanzania wengi na ambalo tunatakiwa kulifanyia kazi ili Watanzania wasiendelee kumwaga damu. Kati ya tatizo la ajira na muungano, kati ya afya na muungano, kati ya maji salama na safi na muungano, kati ya elimu bora na muungano, kati ya haki za binadamu na muungano eti watu hawa wanaojiita UKAWA kwao muhimu muungano kuliko chochote kile.
Watanzania naomba tupime kama ni kweli kuwa hawa ni watetezi wetu au ni makuwadiwa soko huria.
Kwaniaba ya watanzania wazalendo, napenda kuiomba serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kuwatupia UKAWA jicho la pekee katika kuangalia na kufuatilia kwa ukaribu zaidi nyendo za UKAWA nahata kutuambia ni nani wako nyuma yao kiasi cha kuwa na kiburi cha kupindukia. Wito wa watanzania kwa vyombo vya ulinzi na usalama nikuwa amani, umoja na uhai wa nchi hii uko mikononi mwao, kwani nia yaUKAWA sio nzuri kwa mustakabali wa taifa hili na lazima wakumbuke USIPOZIBA UFA UTAJENGA UKUTA na pia MAJUTO NI MJUKUU NA HUJA BAADAE. UKAWA wanataka kutengeneza Misri, Afrika ya Kati, Libya, Syria,Sudani Kusini nyingine hapa Tanzania.
MunguIbariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
PAUL MAKONDA
Katibu, idara ya Hamasa na chipukizi
Jumuiaya vijana chama cha mapinduzi (UVCCM)
Ndugu zangu Watanzania, naomba mfahamu kuwa miongoni mwa wajumbe wote wabunge la katiba takriban 600, wajumbe waliofanya maamuzi haramu yakugomea ni 79 ambao ni pungufu ya asilimia 15% ya wajumbe wote, nasio kweli kuwa wao pekee ndio wenye tafsiri sahihi ya rasimu. Wajumbe wa makundi mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa vyama vyote vya siasa takriban 18 kati ya 22 bado wamo kwenye bunge, kati ya wajumbe wakundi la 201 walioasi ni 15 ambapo bara ni 9 na zanzibar 6 lakini piakatika wanaojiita UKAWA wapo wabunge ambao wameendelea kurudi bungeni kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa. Takwimu hizizinatuthibitishia kuwa UKAWA ni kikundi kidogo cha watu waliojipangakuvuruga AMANI ya nchi, watu ambao hawataki KATIBA wala hawatakiMUUNGANO.
Nduguzangu Watanzania, naomba leo niwape picha na kilichopo nyuma ya pazia ya kikundi hiki kiitwacho UKAWA ambacho kinaratibiwa na viongoziwachache na maslahi yake kujulikana kwa wachache zaidi tena yaliyojikita katika misingi ya kibinafsi. Mfano, ndoa ya CUF naCHADEMA inayopelekea NCCR mageuzi kuwa bendera fuata upepo imejengwakatika misingi ya kuvunja muungano, kwa makubaliano kuwa CUF kubaki na Zanzibar na CHADEMA kubaki na Tanganyika. CUF inataka inufaike namkakati dhalimu wa kunyonya rasilimali za wazanzibar yakiwemo mafuta bila kushurutishwa na sheria za muungano kwani wakiamini kubaki na muungano imara CUF na viongozi hao wachache katika chama hichowanakosa fursa za kupora rasilimali za wazanzibar.
IkubumbukweMuungano ndio unalinda mipaka na usalama wa raia katika kujiendelezana kujinufaisha bila ubaguzi wa kikundi cha watu wachache ambachokinaenda kinyume na utawala wa sheria.
Ikumbukwekuwa rasimu ya CUF walioipeleka kwa Mhe. Raisi mwaka 2011,mapendekezo yao ni tofauti na madai yao sasa ya serikali 3, hapa inatosha kutupa picha kuwa nia yao ni kuvunja muungano ili watuache katika mfarakano kama nchi nyingine zinazoteseka kwa sababu yawanasiasa uchwara.
Ifahamike ajenda ya CHADEMA ni kuvunja muungano ndio maana CHADEMA hawahangaiki kuimarisha chama Zanzibar, nia yao ni kubaki na Tanganyika ili waigawe Tanganyika katika vipande vipande kwa lugha ya majimbo iliadhima yao ya ukanda na ukabila itimie. Moja ya kanda yao ambayowametangaza katika kanda 8 walizo nazo ni Kilimanjaro, Tanga, Arushana Manyara. CHADEMA ina amini kanda hii inajitosheleza kwani ina bandari, mbuga za wanyama, madini, milima . Na hii imepelekea mbunge mmoja wapo wa CHADEMA kulazimika kusema kaskazini ni nchi huru huku mwenyekiti wao Mbowe akiendelea kudai mapato ya mlima Kilimanjaro yabaki Kilimanjaro.
Katikakipindi hiki ambacho wenzetu wamegomea bunge la katiba ambalo lipo kisheria na madai yao yakibadilika kila kunapokucha tena yakiwa na upotoshaji mkubwa kwa kufanya siasa chafu ili mradi watimize azma yakuisambaratisha Tanzania wakiwa makuwadi wazuri wa soko huria.Ukihoji leo sababu iliyowafanya watoke bungeni ni tofauti kabisa na sababu waliyoitoa siku wanatoka bungeni, eti msingi wao mkuu wao ni watetezi wa wananchi. Lakini tumesikia katika vyombo mbalimbali wananchi hao wakiwaasa na wakiwataka warejee bungeni ili kukamilisha kazi ya kisheria na tumaini la watanzania la kuwapatia katiba mpya. UKAWA hawa bila haya wamekataa. Swali? wanamtumikia nani. Mpaka sasa imepelekea wananchi hao wanaosema wanawawakilisha wameamua wenyewe kuja Dodoma kuendelea kusema kero zao na shida zao ili katiba hii iweze kutoa majawabu, mfano tumeshuhudia makundi ya wakulima, jukwaa la wahariri wa vyombo vya habari, wafugaji na makundi kadha wakadha yameendelea kutiririka Dodoma.
Hii ni picha tosha kuwa UKAWAhawawatumikii Watanzania na wameamua kuwahadaa Watanzania kwa mgongo wa kuwatetea huku ajenda yao ikiwa maslahi binafsi.
Nduguzangu Watanzania tunapowaunga mkono watu wanaoendelea kuligomea bunge la katiba wakati tunajua nchi inaongozwa kwa utawala wa sheria, na wao ndio wamevunja sheria, tujue kabisa kuwa tunaenda kinyume na utawala bora, ambao umejengwa kwenye msingi wa sheria na demokrasia.Msingi wa demokrasia sio kususa baada ya kushindwa hoja, UKAWAhawataki hoja za wengine na wanalazimisha hoja zao pekee ndizozikubalike kinyume na msingi wa demokrasia. Na bila haya watu hao wasiojua demokrasia wameendelea kuwashawishi watanzania waingie barabarani huku wakijua kuwa Katiba haipatikani barabarani kama wanahoja kwanini wanaikimbia Dodoma? Mchakato huu ulianza kisheriana utahitimishwa kisheria, sio matamko ya makuwadi wa soko huria.
Miongonimwa madai yao matatu, (i) Rais avunje bunge (2) kinachojadiliwaDodoma sio rasimu ya warioba (3) Serikali tatu ndio maendeleo
Kwaujumla wake, UKAWA wanajua mamlaka ya Rais kwa mujibu wa sheria yamabadiliko ya katiba ya mwaka 2011, sura namba 83 imempa Rais mamlaka ya kuunda tume, kuchagua wajumbe 201, kutangaza na kuitisha bunge nakuzindua bunge la katiba, kupokea katiba inayopendekezwa na kuitangaza kwenye gazeti la serikali.,kwanini wanataka kumlazimishaRais kuvunja Sheria kwani hayo niliyoyataja ndio ambayo Rais anayo mamlaka ya kisheria kuyafanya katika mchakato huu wa Bunge la Katiba,na ndio maana hata wale wajumbe aliowateua ambao wamegomea Rais hajawatengua.,kinachojadiliwa bungeni ni Rasimu ya jaji warioba na kiko wazi, kwa sababu msingi mkuu wa majadiliano ni Rasimu inayotokana na tume tena kwa mujibu wa Sura namba 83 kifungu cha sheria namba 25/26 na kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu namba 33(8). Wanajua mamlaka ya bunge na waliohusika kutengeneza sheria hizi pamoja na kanuni waache kuwahadaa watanzania.
Jambola mwisho lenye kusikitisha zaidi ni kung'ang'ania Serikali tatu kana kwamba ndio kilio kikubwa cha watanzania, naomba niulize swali kati ya Muungano na migogoro ya ardhi ni jambo lipi limepoteza maishaya watanzania wengi na ambalo tunatakiwa kulifanyia kazi ili Watanzania wasiendelee kumwaga damu. Kati ya tatizo la ajira na muungano, kati ya afya na muungano, kati ya maji salama na safi na muungano, kati ya elimu bora na muungano, kati ya haki za binadamu na muungano eti watu hawa wanaojiita UKAWA kwao muhimu muungano kuliko chochote kile.
Watanzania naomba tupime kama ni kweli kuwa hawa ni watetezi wetu au ni makuwadiwa soko huria.
Kwaniaba ya watanzania wazalendo, napenda kuiomba serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi na usalama kuwatupia UKAWA jicho la pekee katika kuangalia na kufuatilia kwa ukaribu zaidi nyendo za UKAWA nahata kutuambia ni nani wako nyuma yao kiasi cha kuwa na kiburi cha kupindukia. Wito wa watanzania kwa vyombo vya ulinzi na usalama nikuwa amani, umoja na uhai wa nchi hii uko mikononi mwao, kwani nia yaUKAWA sio nzuri kwa mustakabali wa taifa hili na lazima wakumbuke USIPOZIBA UFA UTAJENGA UKUTA na pia MAJUTO NI MJUKUU NA HUJA BAADAE. UKAWA wanataka kutengeneza Misri, Afrika ya Kati, Libya, Syria,Sudani Kusini nyingine hapa Tanzania.
MunguIbariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
PAUL MAKONDA
Katibu, idara ya Hamasa na chipukizi
Jumuiaya vijana chama cha mapinduzi (UVCCM)