UVCCM waivaa UKAWA

UVCCM waivaa UKAWA

Ila naamini sasa waandishi wa Tanzania hawana thamani. Kweli mmekalishwa na kuambiwa huu upuuuuuuzi. Mkaondoka kwenda kuusambaza? Au ni kweli mnapewa bahasha? Amkeni thamani yenu iko wapi? Ajabu mmeshindwa hata kumuuliza hivyo vifungu vingine wanajadili kwa mfumo wa serikali ngapi au vya seeikali ipi? Maana mfumo wa serikali haujapitishwa kwa kupigiwa kura. What if mwisho waliotaka serikali tatu wakawa wengi na katiba mmetengeza kwa matakwa ya ccm ya serikali mbili? Waandishi nyie ndio mnawalea hawa vilaza kila kukucha waawaiteni saana maana hamjitambui,
 
Ndani ya BMK, wajumbe wengi walilalamikia kitendo cha baadhi ya vyombo vya habari kuonyesha mijadala ya Rasimu inayoandaliwa na taasisi mbalimbali. Wengine walifikia hatua za kutaka hatua kali zichukuliwe dhidi ya wale wanaojadili Rasimu kwani ni mali ya BMK! Sasa inakuwaje tena hizi taasisi kama UVCCM kujadili suala hili wakati tumeambiwa Rasimu ni mali ya BMK baada ya kukabidhiwa pale Bungeni?
 
“Demokrasia bila mipaka ni ukichaa na demokrasia bila nidhamu ni uwendawazimu”Mwl Jk Nyerere
Ndugu zangu Watanzania, naomba mfahamu kuwa miongoni mwa wajumbe wote wabunge la katiba takriban 600, wajumbe waliofanya maamuzi haramu yakugomea ni 79 ambao ni pungufu ya asilimia 15% ya wajumbe wote, nasio kweli kuwa wao pekee ndio wenye tafsiri sahihi ya rasimu. Wajumbe wa makundi mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa vyama vyote vya siasa takriban 18 kati ya 22 bado wamo kwenye bunge, kati ya wajumbe wakundi la 201 walioasi ni 15 ambapo bara ni 9 na zanzibar 6 lakini piakatika wanaojiita UKAWA wapo wabunge ambao wameendelea kurudi bungeni kwa kuzingatia maslahi mapana ya Taifa. Takwimu hizizinatuthibitishia kuwa UKAWA ni kikundi kidogo cha watu waliojipangakuvuruga AMANI ya nchi, watu ambao hawataki KATIBA wala hawatakiMUUNGANO.
MunguIbariki Tanzania, Mungu Ibariki Afrika
PAUL MAKONDA
Katibu, idara ya Hamasa na chipukizi
Jumuiaya vijana chama cha mapinduzi (UVCCM)

Naona na nyie mnaleta uchama sana, maswala wanayoyaongea hawa UKAWA mbona yako dhahiri kabisa, hata mkisema leo hii mtaiburuza hio rasimu na kuhakikisha kura zinapigwa kukubali serikali mbili, bado kuna mambo yatakuwa yanaenda kinyume na serikali mbili, kama mnaogopa Zanzibar kumezwa basi serikali 3 ndio suluhisho, kama hamtaki na tuendelee na serikali 2 basi tutakuwa tunaishi na kujiendesha kiuongo uongo tu, maana tayari Zanzibar na Pemba ni serikali, hio ya pili ni ya muungano? na kama ni ya muungano mbona hatujaona mawaziri wetu huku wakishughulikia masuala kadhaa ya visiwani?! Sie wananchi wa kawaida bila fujo wala kutaka maandamano tunachoomba ni viongozi kutuelewa na kutusikia, kwamba bado tunataka muungano, ila basi mambo yawekwe wazi kama hayo juu, na pia hata tukiweka wasimamizi wa muungano kuna ubaya gani? at least kila kitu kitakuwa wazi na kueleweka...

Ni suala dogo mno mno ila linakuzwa kwa ushabiki na wengine kuwa wapumbavu badala ya wajinga! Kushupaa kwa kushabikia kitu ambacho mioyoni mwao wanajuwa kabisa, ni kwa siku au miaka michache tu lazima kitafutwa na kutupwa tupwa kule vichakani....
 
Hofu ya nini UVCCM wakati mnajinafasi bungeni kuunda katiba bila kuwepo UKAWA wa kuhoji madudu yenu ya kulinda mafisadi wachache? Mwenyeketi wenu wa chama ameulizwa na Obama kuhusu A/c ya Tegeta Escrow? Tuambie nayo alijibu nini?

Unatoa takwimu kuonesha ujinga wa uandishi wa katiba. Watanzani tuko 45 milioni, wajumbe (wawakilishi wa wananchi) zaidi ya 600 ndani ya BMK.

Kwa mfano, mjumbe anayewakilisha jamii ya wavuvi akiondoka ndani ya bunge hilo, kwa sababu hajasikilizwa maoni yake na walio wengi, wewe Makonda unaona ni idadi ndogo hiyo? Jifunzeni mambo kabla ya kuyasema mbele ya watu wenye akili? Au huo ndio UPUMBAVU alioutofautisha Profesa Kabudi na UJINGA wa wanaosema "ahaaa!"

Katiba haiandikwi kwa mtindo wa bunge la kawaida, kwanza MARIDHIANO, pili KISHERIA.
 
lazima uelewe kuwa ccm ndio wasio taka amani ndani ya nchi yetu kwani mnajadili rasimu ya maoni ya watu gani kama maoni ya watanzania mmeyavuruga?takwimu unazotuletea hazina mashiko punguza kuchonga kwenye media huna mpya mawazo yako ni mgando.
 
Back
Top Bottom