Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Katika kuelekea uchaguzi mdogo Jimboni Arumeru Mashariki vimbwenga vingi vimeshaanza kuonekana na vingi vinasikitisha kutokana na makundi yaliyojitokeaza mengi yakitamani yule wao wanaomtaka ndiye awe ama apitishwe ili kuipeperusha bendera ya Chama hasa CCM, jambo ambalo limepelekea uchaguzi kurudiwa ndani ya CCM.
Msuguano mkubwa na fukuto kubwa limeonekana kutoka ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM Wilayani Arumeru pamoja na Mkoani wakishinikiza yule wao wanaomtaka ndiye anayestahili ila katika hali ya kawaida ndani ya Jimbo, Mkoani na hata Taifa picha halisi inaonesha kuwa mawazo yao hayakubaliki na yule wao wasiomtaka ndiye anayetakiwa kukiwakilisha Chama kukiwa na imani kwamba atakiwakilisha Chama vyema katika kupambana na Vyama vingine vya Upinzani vitakavyosimamisha wagombea.
Hivyo basi; mi nadhani katika hali ya namna hii na kwa wakati huu ni lazma ufikie wakati Vijana wa CCM waoneshe BUSARA na HEKIMA ya hali ya juu katika hili waoneshe ukomavu wao Kisiasa, waweke kando makundi, wakumbuke Chama ni kimoja, waoneshe mapenzi yao ndani ya Chama, waridhie kwa kauli moja kuwa wanataka ushindi Arumeru, waone na kutambua kuwa hakuna haja tena kuendelea kusema kundi letu litashinda na kundi flani litashindwa, wajue kwa dhati kuwa hata yule wao wasiomtaka nae ni kijana hivyo hakuna haja ya kutenga mkono wa kushoto na wa kulia kwa kuwa mikono yote ni ya mtu mmoja, waone na kutambua mahitaji ya CHAMA pamoja na kilio cha WANACHAMA ndani ya Jimbo lao, watazame mbele na kuamini kuwa wanakwenda kuingia ulingoni hivyo kuna kushinda na kushindwa, wajue wazi kuwa fikra za walio wengi ni juu ya mahusiano yaliyopo kati ya PM Mstaafu pamoja na yule wanaomtaka, wakubali kuwa nguvu na uwezo wa PM Mstaafu unatambulika vyema na si lazma yule wanaomtaka ashinde ndio hilo liendelee kudhihirika, wajue vile vile kuwa hayo wayafanyayo ni kuendelea kuwapa wananchi mwanya kuendelea kulitumia jina la PM Mstaafu kwa namna isiyofaa;
Baada ya kutambua hayo sasa waamue haya;
1. Chama kwanza mgombea baadae
2. Wakubaliane kuwa Kijeshi kurudi nyumba si kushindwa bali ni kujipanga upya
3. Uwanjani Mgombea vile vile hujinadi na si kunadiwa (Vigezo na Masharti kuzingatiwa)
4. Kwamba mpambano unaweza kuwa mgumu basi atahitaji mwenye kujua kupambana
Ningekuwa Kiongozi wa Vijana ningewaita Vijana wenzangu tungeyazungumza haya na kupitisha uamuzi mgumu ili kukisaidia Chama kama kweli tunakipenda na kwa kuwa namweshimu na nampenda PM Mstaafu (kwa kuweka kumbukumbu sawa binafsi namweshimu na nampenda kweli hili silifichi hata kidogo) vile vile ningezungumza naye hata kama yuko Nje ya Nchi ningemweleza ukweli ili kuepuka jina lake kuendelea kutumika visivyo na vile vile ningemwomba asaidie Kampeni katika Jimbo hili ili ushindi uwe mwepesi kwa kuunganisha nguvu za wote.
Baada ya hapo kwa kauli moja tunapitisha kuweka kando tofauti zetu za kimakundi na kuamua kumpitisha yule tusiyemtaka sisi bali anayetakiwa na Chama chetu na Wananchi walio wengi.......... Viongozi hasa wale wahusika stand and act hapa ndipo busara za viongozi hupimwa muulizeni Suleiman atawaambie'
I humbly submit!
Msuguano mkubwa na fukuto kubwa limeonekana kutoka ndani ya Umoja wa Vijana wa CCM Wilayani Arumeru pamoja na Mkoani wakishinikiza yule wao wanaomtaka ndiye anayestahili ila katika hali ya kawaida ndani ya Jimbo, Mkoani na hata Taifa picha halisi inaonesha kuwa mawazo yao hayakubaliki na yule wao wasiomtaka ndiye anayetakiwa kukiwakilisha Chama kukiwa na imani kwamba atakiwakilisha Chama vyema katika kupambana na Vyama vingine vya Upinzani vitakavyosimamisha wagombea.
Hivyo basi; mi nadhani katika hali ya namna hii na kwa wakati huu ni lazma ufikie wakati Vijana wa CCM waoneshe BUSARA na HEKIMA ya hali ya juu katika hili waoneshe ukomavu wao Kisiasa, waweke kando makundi, wakumbuke Chama ni kimoja, waoneshe mapenzi yao ndani ya Chama, waridhie kwa kauli moja kuwa wanataka ushindi Arumeru, waone na kutambua kuwa hakuna haja tena kuendelea kusema kundi letu litashinda na kundi flani litashindwa, wajue kwa dhati kuwa hata yule wao wasiomtaka nae ni kijana hivyo hakuna haja ya kutenga mkono wa kushoto na wa kulia kwa kuwa mikono yote ni ya mtu mmoja, waone na kutambua mahitaji ya CHAMA pamoja na kilio cha WANACHAMA ndani ya Jimbo lao, watazame mbele na kuamini kuwa wanakwenda kuingia ulingoni hivyo kuna kushinda na kushindwa, wajue wazi kuwa fikra za walio wengi ni juu ya mahusiano yaliyopo kati ya PM Mstaafu pamoja na yule wanaomtaka, wakubali kuwa nguvu na uwezo wa PM Mstaafu unatambulika vyema na si lazma yule wanaomtaka ashinde ndio hilo liendelee kudhihirika, wajue vile vile kuwa hayo wayafanyayo ni kuendelea kuwapa wananchi mwanya kuendelea kulitumia jina la PM Mstaafu kwa namna isiyofaa;
Baada ya kutambua hayo sasa waamue haya;
1. Chama kwanza mgombea baadae
2. Wakubaliane kuwa Kijeshi kurudi nyumba si kushindwa bali ni kujipanga upya
3. Uwanjani Mgombea vile vile hujinadi na si kunadiwa (Vigezo na Masharti kuzingatiwa)
4. Kwamba mpambano unaweza kuwa mgumu basi atahitaji mwenye kujua kupambana
Ningekuwa Kiongozi wa Vijana ningewaita Vijana wenzangu tungeyazungumza haya na kupitisha uamuzi mgumu ili kukisaidia Chama kama kweli tunakipenda na kwa kuwa namweshimu na nampenda PM Mstaafu (kwa kuweka kumbukumbu sawa binafsi namweshimu na nampenda kweli hili silifichi hata kidogo) vile vile ningezungumza naye hata kama yuko Nje ya Nchi ningemweleza ukweli ili kuepuka jina lake kuendelea kutumika visivyo na vile vile ningemwomba asaidie Kampeni katika Jimbo hili ili ushindi uwe mwepesi kwa kuunganisha nguvu za wote.
Baada ya hapo kwa kauli moja tunapitisha kuweka kando tofauti zetu za kimakundi na kuamua kumpitisha yule tusiyemtaka sisi bali anayetakiwa na Chama chetu na Wananchi walio wengi.......... Viongozi hasa wale wahusika stand and act hapa ndipo busara za viongozi hupimwa muulizeni Suleiman atawaambie'
I humbly submit!