Uv-CCM kuongoza sekretariet mpya ya NEC kiaina

Mchekechoni

JF-Expert Member
Apr 24, 2008
279
19
Baada ya anguko kuu la Makamba na sekretariet yake kama ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi hususan wapiga debe mahiri ndani ya UV-CCM wakiongozwa na RZ1, sasa kinachofuatia ni mapinduzi kamili kwa vijana kupata nafasi nyeti ndani ya sekretarieti mpya. Kila la heri UV-CCM, wazee wakishindwa ni jukumu lenu kuokoa jahazi!
 
Jaazi lishazama waokoe nini. Hapo chembe na kidevu lazima wakae!!
 
Kama Jakaya atafanya makosa ya kumsikliza mwanae kuwa awaweke kundi la wakina Malisa kwenye sekretarieti basi ujue ndio mwisho wa CCM!! Ningemshauri asikilize ushauri wa Ngombale ingawa inasemekana amestaafu!
 
Baada ya anguko kuu la Makamba na sekretariet yake kama ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi hususan wapiga debe mahiri ndani ya UV-CCM wakiongozwa na RZ1, sasa kinachofuatia ni mapinduzi kamili kwa vijana kupata nafasi nyeti ndani ya sekretarieti mpya. Kila la heri UV-CCM, wazee wakishindwa ni jukumu lenu kuokoa jahazi!

vijana gani?

kina viky kamata?
 
UV-CCM wenyewe mbona wamechoka sana?

Hebu fikiria hawa Wanandoa wa Chooni ndiyo wawe Viongozi wa juu wa chama....

47629_133058880089280_100001555070854_196666_2323048_n.jpg
Kaimu+Mwenyekiti+wa+Umoja+wa+Vijana+wa+CCM%252C+Beno+Malisa.jpg
 
Baada ya anguko kuu la Makamba na sekretariet yake kama ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi hususan wapiga debe mahiri ndani ya UV-CCM wakiongozwa na RZ1, sasa kinachofuatia ni mapinduzi kamili kwa vijana kupata nafasi nyeti ndani ya sekretarieti mpya. Kila la heri UV-CCM, wazee wakishindwa ni jukumu lenu kuokoa jahazi!

Sijui nini kitaendelea ndani ya CCM maana kuna watu walishajimilikisha kuwa ccm ni yao na ni kifo tu kinaweza kuwatenganisha. Ni bahati mbaya sana kuwa hao UVCCM ni vijana ambao hawakuandaliwa toka mapema, ni vitoto vilivyojikuta viko ndani ya siasa aidha kupitia baba zao au ndugu zao, ndiyo maana nasema hii ligi bado ngumu sana.
 
Hawa jamaa wao wenyewe wanamigongano huko uv.... Wakihamia ukubwani si patakua balaa zaidi. Kweli hii chama yaenda kufwa.
 
Baada ya hapo ninashauri wafanye mabadiliko ya makatibu wa ccm wa wilya zote maana wao ndio chanzo kikuu cha vurugu za uchaguzi mwaka jana. Makatibu wa wilaya na na kama MIUNGU WATU! WALIWAKATAA WALIOTEULIWA KATIKA UDIWANI KWA LENGO LA UFISADI TU WA KUTAKA KUWA LAZIMA DIWANI WA ZAMANI ARUDI!! KWA KUWA MADIWANI WENGI WA ZAMANI WALIKUWA NA FEDHA WALIWAHONGA MAKATIBU NA KUSABABISHA KUKTALIWA KWA MAJINA MAPYA YA WALIOPTITA KTIKA UDIWANI UCHAGUZI WA CCM, MATOKEO YAKE WANCHI WALIWASHIKISHA ADABU, MFANO HALISI NI KATIBU WA WILYA YA MUSOMA VIJIJINI ALIFANYA HIVYO WANACHI WAKAMUELEZA KUWA TUTAKUADHIBU AKDHANI UTANI, AKATUMI VITISHO LAKINI WATU WENYEWE HAWATISHIKI NA MATOKEO YAKE VITI VYA UDIWANI VILIENDA cuf, cHADEMA NA TLP NA HATA KURA ZA JK ZILIPUNGUA HIVYO HIVYO. YEYE KAZI YAKE NI KUVAA PETE NYINGI MIKONONI MWAKE UTADHANI .....

HUYU NI LAZIMA AONDOKE HATAKIWI, ALIKUWA NALINDWA NA MAKAMBA ANATOKE TANGA WALIKUWA WANSEMA NI MPYA WAKE! MARA MTU WA USALAMA NA NK, PIA WENGINE WALIOTUMIKA KULTE VURUGU ZA UCHAGUZI HASA NDANI YA CCM NI PCCB, HAWA JAMAA WA AJABU MNO WALICHOKUWA WANKIFANYA KAMA WABONGO MMESAHAU HAWA WALITUMIKA KUHAKISHA WATU WA AINA FULNI NDIO WALINDWA NA KUENDELA KUHONGA ILI WACHAGULIWE LAKINI KAMA MTU ALIKUWA HATAKIWI YEYE ALIFUATILIWA SAAANA KUHAKIKISHA HAPATI NAFASI ZA KUNUNUA WAPIGA KURA WA CCM, NINAKWAMBIA KILA MWANA CCM MPIGA KURA ALIKUWA ANAOMBA HELA NA NA WALA HAWAKUWA WASIKIA SERA ZA WAGOMBEA AMA KWELI CCM YA JK IMETUFIKISHA PABAYA. MTU MWINGINE ALIYECHANGIA KUIMUIZA CCM NI DR EDWARD HOSEA MAAMUZI YAKE YA KULINDA UFISADI, NA ZAIDI YA YOTE VOIONGOZI WA JUU WA CCM KULINDA UFIOSADI NA KUSAHAU WANANCHI, HAKIKA MAMBO BADO NI MAGUMU CCM IJIREKEBISHE NA IACHE PAWE NA CHAMA CHA UPINZANI STRONG KAMA CHADEMA. KAMA KWELI WAITAKIA MEMA TANZANIA AMBAYO NI YETU WOTE NA SI YA KIKUNDI CHA KIJANI TU!

PIA CCM IACHE KUGOMABISHA WATANZANIA KWA KUOGOPA UPINZANI WA KWELI UNAOTOLEWA NA CHADEMA NA BADALA YAKE VIONGOZI HAWA WA JUU WAKUJA NA SIMPLE MIND S KUNA WANSEMWA AU CCM INACHUKIWA KWA SABABU YA UDINI! UONGO MKUBWA KWANI NANI ALISEMA KIONGOZI AKIWA MWISLAM BASI CCM NI YA WAISLAMU AU AKIWA MKRISTU BASI CCM NI YA WAKRISTU! AIBU KUBWA KWA VIONGOZI WA JUU KUWA SIMPLE MINDED KIASI HICHIO, SASA WAMESEMABABISHA TATIZO LA CHUKI INAYOANZA KUKUA KATI YA WAISLAMU NA WAKRISTU.

KIJANA WA KIKWETE PIA NI TATZIO KUBWA UVCCM JISAFISHENI CHAMA NI CHA WATANZANIA WALA SIO CHA WAPWANI WAKWERE AU WANGONI NK, NA WALA SI CHAMA CHA MAFISADI CHAMA HIKI BADO KINA NAFASI KUBWA YA KUTAWALA, VIONGOZI WALIOPO WAKISHAURIWA NA WAZEE WAO WANSEM,A WACHUKIWA! MARA OHH NYERERE FOUNDATION ILANIWE MARA UV CCM WAKAIJIA JUU NYERERE FOUNDATION ETC,

CCM SI YA KIKUNDI CHA WATU NI YETU WOTE.
 
Baada ya anguko kuu la Makamba na sekretariet yake kama ilivyokuwa ikitarajiwa na wengi hususan wapiga debe mahiri ndani ya UV-CCM wakiongozwa na RZ1, sasa kinachofuatia ni mapinduzi kamili kwa vijana kupata nafasi nyeti ndani ya sekretarieti mpya. Kila la heri UV-CCM, wazee wakishindwa ni jukumu lenu kuokoa jahazi!

Hii ni furaha ya muda tu, hakuna cha gamba wala nini, makundi yaliyo nje sasa yanaweza kuungana vema na kuanza kushambulia moja lililobaki na hapo ndio mziki utakuwa mtamu. Hizi ni salamu zangu tu mjomba kwa mwanao RZ1
 
Sekretarieti mpya ya ccm ikiongozwa na Mkama, Chiligati na kijana machachari Nape, fuatilieni kwa makini maoni ya Mkira hapo juu maana yana ukweli mpana kama mna nia ya dhati ya kujivua magamba. Haya kazi kwenu wazee na vijana msio magamba ndani ya sekretarieti ya ccm, msibweteke!
 
Back
Top Bottom