Utumishi waachia kazi zingine

Utumishi waachia kazi zingine

tamsana

Platinum Member
Joined
Jan 13, 2012
Posts
3,836
Reaction score
8,257
Habari zenu wanajamvi, utumishi wameachia kazi nyingine; tembelea website ya utumishi!

1.0 MJIOLOJIA DARAJA LA II (GEOLOGIST GRADE II) – NAFASI 8
1.1 MAJUKUMU YA KAZI
  • Kupokea na kufuatilia upatikanaji wa taarifa za utafiti wa mistari ya uchungi na mitetemo katika utafutaji wa madini au petroli;
  • Kukusanya na kuchambua taarifa za mitetemo, mienendo na mabadiliko ya miamba ardhini;
  • Kutunza kumbukumbu za miamba, madini au petroli;  Kutayarisha rasimu za taarifa za kitaalam na kuziwasilisha kunakohusika;
  • Kusimamia matumizi ya vifaa vya kitaalam na utunzaji wake; na  Anaweza kuongoza timu ya mafundi sanifu wanapokuwa katika shughuli za utafutaji wa madini au petroli.
1.2 SIFA ZA MWOMBAJI
  • Kuajiriwa wenye Shahada ya Sayansi katika fani ya Jiolojia (pamoja na fani za Jiofizikia au Jiokemia) au sifa nyingine zinazolingana na hizo kutoka vyuo vikuu vinavyotambuliwa na Serikali,

1.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.

2.0 MHANDISI MIGODI DARAJA LA II – (MINING ENGINEER)- NAFASI 14

2.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kufanya kazi chini ya uangalizi wa mhandisi aliyesajiliwa na bodi ya Usajili wa Wahandisi kama “Professional Engineer” ili kupata uzoefu unaotakiwa.  Kufanya kazi kwa vitendo katika fanii zinazomhusu ili kumwezesha Mhandisi kupata sifa za kutosha kusajiliwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi.  Kuwaelimisha wachimbaji wadogo kuhusu sheria, kanuni na masuala ya kitaalamu ya uchimbaji, uchenguaji na masoko ya madini.  Kupitia taarifa za kila mwezi za ofisi za madini.  Kukusanya na kuchambua taarifa na takwimu za uchimbaji madini.  Kutunza kumbukumbu za usafirishaji, utangazaji biashara na matumizi ya baruti.

2.2 MSHAHARA
Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS E kwa mwezi.

3.0 MCHAMBUZI MIFUMO YA KOMPYUTA DARAJA LA II – NAFASI 13 Nafasi

3.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kuweka kumbukumbu za taratibu za kisasa na mbinu za kufanyia kazi.
  • Kutekeleza chati za mtiririko wa mifumo ya nyendo za taarifa na uthibiti unaohusu Kompyuta.  Kutoa msaada wa kiufundi kwa Wizara/Idara/Vituo mbalimbali vya kazi.

3.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye Shahada/Stashahada ya Juu katika masomo ya Sayansi ya Kompyuta kutoka kwenye Taasisi/Chuo kinachotambuliwa na Serikali.

3.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D.

4.0 MTAKWIMU DARAJA LA II (STATISTICIAN GRADE II) – NAFASI 11

4.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kubuni na kuendeleza mfumo wa kitaifa wa kukusanya na kuratibu takwimu
  • Kutengeneza utaratibu wa kukusanya takwimu pamoja na ule wa kuchukua takwimu za mfano/vielelezo (Sampling)
  • Kukusanya, Kuchambua na kuwasilisha takwimu ngazi za juu.

4.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza katika fani ya Takwimu au Hisabati au sifa
zinazolingana na hizo kutoka Chuo Kikuu kinachotambuliwa na Serikali na wenye ujuzi wa kutumia Kompyuta.

4.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.

5.0 NAHODHA DARAJA LA II – (SKIPPER GRADE II) – NAFASI 1

5.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kubuni na kuunda zana za kuvulia samaki (Fishing Gears).
  • Kutunza na kutengeneza zana za kuvulia samaki.  Kuongoza na kuendesha meli/boti ndogo za futi 40 zenye uzito wa kuandikishwa wa tani 50-200 (GRT).
  • Kuendesha shughuli za uvuvi katika meli/boti.

5.2 SIFA ZA MWOMBAJI

  • Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha sita (VI) wenye Stashahada (Diploma) ya Unahodha na Uvuvi (Master Fisherman) kutoka Chuo cha Uvuvi Mbegani au vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali.

5.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.C kwa
mwezi.

6.0
FUNDI SANIFU DARAJA LA II - MIGODI (MINING TECHNICIAN GRADE II) – NAFASI 14

6.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kukagua na kupima viwanja kwa ajili ya waombaji wadogo wadogo
  • Kusimamia wapimaji na kuhakikisha wanapima kwa kiwango kinachotakiwa
  • Kuandaa “action plan” na kuhakikisha inafuatwa

6.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wenye mojawapo ya sifa zilizotajwa hapa chini:
  • Waliohitimu kidato cha VI na kufuzu mafunzo ya ufundi ya miaka miwili kutoka Chuo kinachotambuliwa na Serikali katika moja ya fani migodi
  • Waliohitimu kidato cha IV na kufuzu kozi ya ufundi ya miaka mitatu kutoka Vyuo vya Ufundi vinavyotambuliwa na Serikali katika mojawapo ya fani za migodi
  • Wenye Cheti cha Majaribio ya Ufundi hatua ya I kutoka Chuo cha Ufundi kinachotambuliwa na Serikali,
  • Wenye Stashahada ya Kawaida katika fani za ufundi migodi kutika Chuo kinachotambuliwa na Serikali.

6.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS C kwa mwezi.

7.0 DOBI DARAJA LA II – NAFASI 1 7.1

MAJUKUMU YA KAZI

  • Kufanya uchambuzi wa nguo kwa ajili ya kuosha, kukausha, kunyoosha na kuzifungasha.

7.2 SIFA ZA MWOMBAJI

  • Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne waliofuzu mafunzo ya miaka miwili au mitatu katika fani ya Dobi (Laundry Services) kutoka katika vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
7.3 MSHAHARA
  • Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGOS. C kwa mwezi.

8.0 MKUTUBI DARAJA LA II – NAFASI 1

8.1 MAJUKUMU YA KAZI
 Kuratibu shughuli za ukuzaji wa utamaduni kitaifa.
  • Kuratibu na kusimamia shughuli za ukaguzi na udhibiti maonyesho ya filamu na video katika ngazi ya taifa.
  • Kushauri juu ya mitaala ya mafunzo na elimu ya fani za utamaduni.
  • Kusimamia usajili wa vikundi na vyama vya fani za utamaduni.
  • Kushauri juu ya ujenzi wa majukwaa na majumba ya utamaduni yenye hadhi ya kitaifa.
  • Kuratibu shughuli za utafiti wa mila na desturi nchini.
  • Kusimamia na kuratibu ukuzaji wa matumizi fasaha na sanifu ya Kiswahili nchini.
  • Kazi nyingine atakazopangiwa na Mkuu wa kituo.

8.2 SIFA ZA MWOMBAJI

  • Kuajiriwa wenye shahada ya kwanza katika fani ya ukutubi au sifa inayolingana na hiyo kutoka katika vyuo vikuu vinavyotambuliwa na Serikali.

8.3 MSHAHARA

  • Kwa kuzingatia ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS D kwa mwezi.

9.0 MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA II (NYARAKA) – NAFASI 50 9.1

MAJUKUMU YA KAZI

  • Daraja hili ni la mafunzo katika kazi, hivyo atafanya kazi kwa maelekezo ya Wasaidizi wa Kumbukumbu walio juu yake. Kazi atakazojifunza na kufanya ni zile zifanywazo na Msaidizi wa Kumbukumbu Daraja la I
  • Kutafuta kumbukumbu/nyaraka/mafaili yanayohitajiwa na wasomaji.
  • Kudhibiti upokeaji, uandikishaji wa kumbukumbu/nyaraka.
  • Kuchambua, kuorodhesha na kupanga kumbukumbu/nyaraka katika makundi kulingana na somo husika (classification and boxing) kwa ajili ya matumizi ya ofisi.
  • Kuweka/kupanga kumbukumbu/nyaraka katika reki (file racks/cabinets) katika masjala/vyumba vya kuhifadhia kumbukumbu.
  • Kuweka kumbukumbu (barua, nyaraka nk.) katika mafaili.  Kushughulikia maombi ya kumbukumbu/nyaraka kutoka Taasisi za Serikali
9.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha sita wenye cheti cha utunzaji kumbukumbu katika mojawapo ya fani za Afya, Masjala, Mahakama na Ardhi.

9.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia Ngazi za mishahara ya Serikali yaani TGS B kwa mwezi

10.0
MSAIDIZI UFUGAJI NYUKI DARAJA LA II - NAFASI 3 10.1

MAJUKUMU YA KAZI

  • Kusimamia manzuki.
  • Kutunza hifadhi za nyuki.
  • Kukusanya takwimu za ufugaji nyuki.
  • Kutunza kumbukumbu za kazi za utafiti.
  • Kuondoa nyuki wanaodhuru binadamu na mifugo.
  • Kutoa leseni za biashara ya mazao ya nyuki.
  • Kutoa ushauri wa kitaalam kwa wananchi juu ya ufugaji endelevu wa nyuki na matumizi bora ya mazao ya nyuki.
  • Kutunza makundi ya nyuki wanaouma na wasiouma.

10.2 SIFA ZA MWOMBAJI
Kuajiriwa wahitimu wa kidato cha nne au Sita wenye Astashahada (Cheti) au Stashahada (Diploma) ya Ufugaji Nyuki kutoka katika vyyuo vinavyotambuliwa na Serikali.

10.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.B


11.0
MTUNZA BUSTANI DARAJA LA II - (GARDNER II) NAFASI 3

11.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kupanda mboga, matunda, n.k. katika bustani.
  • Kupalilia mazao katika bustani.
  • Kupanda maua katika maeneo yanayohusika.
  • Kupanda na kukata majani na kumwagilia maji.
  • Kufanya kazi zingine zitakazoelekezwa na Viongozi wa Kitengo chao.

11.2 SIFA ZA MWOMBAJI

Kuajiriwa wenye Cheti katika fani ya utunzaji bustani za maua, mboga na upandaji majani kutoka chuo cha Maendeleo ya Wananchi, VETA, au JKT au Vyuo vingine vinavyotambuliwa na Serikali wenye uzoefu wa kazi kwa muda usiopungua miaka mitatu.

11.3 MSHAHARA

Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGOS.A kwa mwezi.


12.0
MWANDAZI DARAJA LA II (WAITER GRADE II) - NAFASI 1

12.1 MAJUKUMU YA KAZI
  • Kuandaa meza ya kulia chakula.
  • Kupamba meza ya kulia chakula  Kupanga vifaa vya kulia chakula mezani.  Kuondoa vyombo baada ya kula chakula

12.2 SIFA ZA MWOMBAJI

  • Kuajiriwa wenye cheti cha Mtihani wa Kidato cha IV na kufuzu mafunzo si chini ya mwaka mmoja katika fani ya ‘Food and Bevarages’ yatolewayo na vyuo vya Forodhani Dar es Salaam. Masoka Moshi, Arusha Hotel na Y.M.C.A ya Moshi na Vyuo vingine vinavyolingana ambavyo vitatambuliwa na Serikali.

12.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.B kwa mwezi.


13.0 MSAIDIZI WA HESABU (ACCOUNTS ASSISTANT) - NAFASI 26 13.1

MAJUKUMU YA KAZI

  • Kuandika na kutunza “register” zinazohusu shughuli za uhasibu.
  • Kuandika hati za malipo na hati za mapokezi ya fedha.
  • Kutunza majalada yenye kumbukumbu za hesabu
  • Kupeleka barua/nyaraka za uhasibu Benki.
  • Kufanya usuluhisho wa masurufu, karadha, Hesabu za Benki na Amana.

13.2 SIFA ZA MWOMBAJI

Kuajiriwa wenye Cheti cha ATEC level II au “Foundation Level” kinachotolewa na NBAA

13.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.B kwa mwezi


14.0
FUNDI SANIFU MSAIDIZI UPIMAJI NA RAMANI (MAPPING/CARTOGRAPHER ASSISTANT) – NAFASI 1

14.1 MAJUKUMU YA KAZI

  • Kutayarisha alama za upimaji (survey pillars, becons etc).
  • Kufanya kazi za upimaji zisizohitaji ujuzi (semi skilled tasks).
  • Kutunza kumbukumbu za ramani zinazotayarishwa.
  • Kuchora michoro ya upimaji (survey plan)
14.2 SIFA ZA MWOMBAJI
  • Kuajiriwa wahitimu wa Kidato cha Nne au Kidato cha Sita wenye mchepuo wa mafunzo ya ufundi ya miaka miwili katika fani ya Upimaji na Ramani, Usimamizi Ardhi, Uthamini na Usajili katika Vyuo vinavyotambuliwa na Serikali.
14.3 MSHAHARA
Kwa kuzingatia viwango vya Serikali yaani ngazi ya Mshahara TGS.B kwa mwezi.


Maombi yatumwe

Katibu,
Sekretariati ya Ajira katika Utumishi wa Umma,
SLP.63100,
Dar es Salaam.


Mwisho wa kupokea barua za maombi ni tarehe19 Agosti, 2014

X.M. DAUDI Katibu
Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma.
 

Attachments

Wabongo sijui nani kawaroga. Mtu kawapa taarifa then awawekee na link wakati mnajua pa kupata taarifa hiyo.
Akiweka link mtamwuliza deadline lini, akiweka deadline mtamwuliza anwani ya kutuma ni ipi. Jamani jamani!!!!!!
Nchi hii bado ina safari ndefu sana, kama ina wasomi wa namna hiyo ya Az 89. Bado sana tena sana.
 
Jamani mbna pale pa utunzaji kumbukumbu wameandika eti cheti cha form six wapendwa inakuaje wakati wengne hawajafika form six wapendwa ila wameenda chuo na wana vyeti vizuri vya career iliyitongazwa
 
Mengi yanayo omba link yamesoma private school,wazee wa kutafuniwa.

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Watu wanataka uwaandikie barua za maombi, noma sana dah
 
À santé kwa news. Jk anatoa Ajira kwa watu wake Kabla hajaondoka. Asante MH. Rais.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom