Utitiri wa baa Sinza, kero kwa wapita njia

Boran Jakutay

Senior Member
Apr 8, 2023
110
255
IMG_20230729_190749.jpg
Raha ya starehe, ifanye usimkere mwenzio, lakini kwa kinachofanyika Sinza, ni kukiuka mipaka ya starehe.

Kila siku zinavyozidi kwenda, baa zinazidi kuota maeneo ya Sinza na nyingi zipo kando kidogo mwa barabara.

Hivi karibuni kuna kiota kipya kimejengwa hapa Barabara ya Sinza Mori, ni mita chache kutoka Small Planet (zamani La Charlz).

Kiota hicho kipya kinaitwa Icons Lounge, kipo pale zamani kulikuwa na baa ya Uwoya.

Kwa ujumla baa nyingi za aina yake zinatukera sisi watembea kwa miguu tunaoitumia Barabara ya Sinza Mori.

Ukiangalia kutoka hapo Icons Lounge, unaenda mbele kuna Small Planet, kisha B-Max, halafu kule mbele ndio Kitambaa Cheupe.
IMG_20230729_190649.jpg

Ukipita barabara hiyo hasa wikiendi kuanzia saa 12 jioni, utakuta gari zimepaki sehemu ya watembea kwa miguu.
IMG_20230729_190627.jpg

Hapo watembea kwa miguu tunalazimika kupita barabarani kabisa yanapopita magari.

Yani usipokuwa makini, utashangaa shwaaa, umegongwa na gari au bodaboda.
IMG_20230729_165110.jpg
Hali hii ni hatari kwa watembea kwa miguu.

Neno kwa wamiliki wa hizi baa, wekeni parking ya kutosha ili magari yasipaki sehemu ambayo watembea kwa miguu wanaitumia.
 
View attachment 2702371Raha ya starehe, ifanye usimkere mwenzio, lakini kwa kinachofanyika Sinza, ni kukiuka mipaka ya starehe.

Kila siku zinavyozidi kwenda, baa zinazidi kuota maeneo ya Sinza na nyingi zipo kando kidogo mwa barabara.

Hivi karibuni kuna kiota kipya kimejengwa hapa Barabara ya Sinza Mori, ni mita chache kutoka Small Planet (zamani La Charlz).

Kiota hicho kipya kinaitwa Icons Lounge, kipo pale zamani kulikuwa na baa ya Uwoya.

Kwa ujumla baa nyingi za aina yake zinatukera sisi watembea kwa miguu tunaoitumia Barabara ya Sinza Mori.

Ukiangalia kutoka hapo Icons Lounge, unaenda mbele kuna Small Planet, kisha B-Max, halafu kule mbele ndio Kitambaa Cheupe.
View attachment 2702374
Ukipita barabara hiyo hasa wikiendi kuanzia saa 12 jioni, utakuta gari zimepaki sehemu ya watembea kwa miguu.
View attachment 2702375
Hapo watembea kwa miguu tunalazimika kupita barabarani kabisa yanapopita magari.

Yani usipokuwa makini, utashangaa shwaaa, umegongwa na gari au bodaboda. View attachment 2702370Hali hii ni hatari kwa watembea kwa miguu.

Neno kwa wamiliki wa hizi baa, wekeni parking ya kutosha ili magari yasipaki sehemu ambayo watembea kwa miguu wanaitumia.
Tafuta hela acha majungu. Acha Watoto wa town wale maisha
 
Dar ni moja ya majiji holela na ya hovyo duniani ambaye hajazungukazunguka duniani hawezi kuelewa hili.
Hayo ya biashara za pembezoni ya barabara kuziba njia za waenda kwa miguu ni Dar nzima sio Sinza tu na hayo ni matokeo ya rushwa iliyokithiri kwenye jamii yetu.Watendaji wa serikali wanaziba masikio baada ya kupewa rushwa
na wenye hizo Bar za pembeni mwa barabara.Miaka kumi ijayo huu mji sijui utakuwaje kwa upuuzi huu unaofumbiwa macho na watendaji wa serikali.
 
View attachment 2702371Raha ya starehe, ifanye usimkere mwenzio, lakini kwa kinachofanyika Sinza, ni kukiuka mipaka ya starehe.

Kila siku zinavyozidi kwenda, baa zinazidi kuota maeneo ya Sinza na nyingi zipo kando kidogo mwa barabara.

Hivi karibuni kuna kiota kipya kimejengwa hapa Barabara ya Sinza Mori, ni mita chache kutoka Small Planet (zamani La Charlz).

Kiota hicho kipya kinaitwa Icons Lounge, kipo pale zamani kulikuwa na baa ya Uwoya.

Kwa ujumla baa nyingi za aina yake zinatukera sisi watembea kwa miguu tunaoitumia Barabara ya Sinza Mori.

Ukiangalia kutoka hapo Icons Lounge, unaenda mbele kuna Small Planet, kisha B-Max, halafu kule mbele ndio Kitambaa Cheupe.
View attachment 2702374
Ukipita barabara hiyo hasa wikiendi kuanzia saa 12 jioni, utakuta gari zimepaki sehemu ya watembea kwa miguu.
View attachment 2702375
Hapo watembea kwa miguu tunalazimika kupita barabarani kabisa yanapopita magari.

Yani usipokuwa makini, utashangaa shwaaa, umegongwa na gari au bodaboda. View attachment 2702370Hali hii ni hatari kwa watembea kwa miguu.

Neno kwa wamiliki wa hizi baa, wekeni parking ya kutosha ili magari yasipaki sehemu ambayo watembea kwa miguu wanaitumia.
Sinza ya Leo, kila baada ya nyumba bar,
Na zote zinajaa,
Hapo ndipo utakaposhangaa.

Na kwenye night club ni lundo la dada poa,
Huwezi kuamini jinsi walivyojipodoa!!

Get well soon Prof J.
 
Kuna Mtu hapahapa atakuambia:

"" Tafuta hela uache kuteseka na starehe za watu""
 
Kama vipi hilo eneo liwe Bar Area; kama vile kulivyo na sehemu za Industrial Areas..., ila wakiachiwa hii sio waendelee kuwafuata watu..., Ingawa Supply and Demand italeta equilibrium
 
Back
Top Bottom