Uthubutu wa Rais Magufuli...

Uthubutu wa Rais Magufuli...

Maghufuli atabaki kuwa icon kubwa sana, time will tell, ana mapungufu yake ila ni raisi wa aina yake ,hawa hawa wanaomlaumu ndo watakuwa wa kwanza kumkumbuka jamaa,
Ipo siku utashuka tu kutoka kwenye gari la huyu mtu. Subiri awamu ya pili utaona.
 
Hoja yako inanikumbusha jukwaa la siasa kuanzia 2013 kurudi nyuma.

Uchambuzi wa siasa wa aina hii ulikuwa ni suala la kawaida wakati huo lakini sasa hoja kama hizi zimekuwa ni kama mnyama kakakuona!

Nikirudi kwenye hoja yako. Ni kweli taifa letu lina tatizo la uthubutu.

Hata huyu Rais Magufuli nimemsikia akiwaambia watendaji wake ni afadhari unathubutu na kutenda hata kama utakosea lakini unakuwa umetenda.


Kutokuwa na uthubutu nchini imekuwa kama tabia/haiba na utamaduni.

Watanzania wengi ni wapole sana. Upole na uthubutu haviendi pamoja.

Nadhani haiba inayoenda pamoja na uthubutu ni ruthless.

Ndio maana imefikia hatua baadhi ya watu wanadai Rais Magufuli hana Utanzania kwa sababu ni ruthless.

Watanzania wengi wanajua sana kuongea kuliko kutenda. Nahani hii imetokana na historia ya taifa letu.

Rais Magufuli ana mapungufu yake lakini uthubutu siyo moja ya mapungufu kwake.
 
Hoja yako inanikumbusha jukwaa la siasa kuanzia 2013 kurudi nyuma.

Uchambuzi wa siasa wa aina hii ulikuwa ni suala la kawaida wakati huo lakini sasa hoja kama hizi zimekuwa ni kama mnyama kakakuona!

Nikirudi kwenye hoja yako. Ni kweli taifa letu lina tatizo la uthubutu.

Hata huyu Rais Magufuli nimemsikia akiwaambia watendaji wake ni afadhari unathubutu na kutenda hata kama utakosea lakini unakuwa umetenda.


Kutokuwa na uthubutu nchini imekuwa kama tabia/haiba na utamaduni.

Watanzania wengi ni wapole sana. Upole na uthubutu haviendi pamoja.

Nadhani haiba inayoenda pamoja na uthubutu ni ruthless.

Ndio maana imefikia hatua baadhi ya watu wanadai Rais Magufuli hana Utanzania kwa sababu ni ruthless.

Watanzania wengi wanajua sana kuongea kuliko kutenda. Nahani hii imetokana na historia ya taifa letu.

Rais Magufuli ana mapungufu yake lakini uthubutu siyo moja ya mapungufu kwake.

Duh!

Mzee upo?
 
Kama kuna kitu cha wazi ambacho ni funzo kubwa kwetu Watanzania katika miaka minne hii ya Awamu ya Tano na "Utawala" (maksudi kabisa badala ya kutumia uongozi) wa Magufuli ni UTHUBUTU!

Uthubutu, ni uwezo wa kufanya mambo bila kuwa na kigugumizi au kujishuku. Ni kufanya mambo, kusimamia unaloliamini bila kujali au bila woga. Sasa kwa Magufuli ambaye tulijua akiwa waziri alikuwa ni mchapakazi mpaka kuitwa bulldozer, ilimaanisha alifanya mambo jinsi alivyoona ni sawa kwa nafasi yake na sasa kwa kupata Urais n kuwa Rais wa Jamhuri, basi Ari, Kasi na Nguvu zake za kuwa Bulldozer na uthubutu zimeongezeka maradufu.

Uthubutu si lazima tuutazame kwa matokeo chanya pekee, hata matokeo hasi yanaweza kutokea kutokana na mtu kuwa na uthubutu, kudhamiria na kufanya lile alilokusidia.

Rais Magufuli ametusaidia sana kutuonyesha kwa vitendo, na si semi, kauli au porojo kuwa kwenye nia pana njia.

Naam, kuna maamuzi mengi yaliyotokana na Uthubutu huu yameleta maswali mengi na hata matokeo ya "uthubutu" kuonekana kama hatua ambazo zilikosa weledi, busara, uhakika au hata hekima. Lakini cha msingi kwa andiko langu hili si kukosoa au kusifia mafanikio au kushindwa kwa maamuzi aliyoyafanya, la hasha... naangalia silika ya kibinadamu ya kuwa na uthubutu, Daring!

Nakumbuka miaka 10 ya Rais Kikwete, uongozi au utawala wake ulionekana umepwaya kwa kukosa Uthubuu wa ukali na kusimamia mambo yafanyike, bila kujali matokeo. Nakumbuka mgombea wa Urais 2015 Bwana Lowassa alinukuliwa mara kadhaa akisema Tanzania inahitaji mtu mwenye kufanya maamuzi magumu, na Watanzania ule u-soft soft wa awamu ya nne, ulitufanya tutake kupata mtu "Dikteta" kauli na nadharia ambazo kwa umoja wa Kitaifa bila hata chembe ya tofauti za kisiasa ai itikadi, ilikuwa ni "natural" kukubali uhitaji wa kuwa na Rais Mkali, Dikteta!

Magufuli kathibitisha katika uanadamu kuwa Uthubutu si jambo la kusadikika, bali li jambo la kweli, lina uhai na kila mtu akikusudia na kujiamini, anaweza kuwa na Uthubutu!

Nikiiangalia Tanzania ilipo leo hii, miaka 58 tangu tupate Uhuru ambapo bado tuko kwenye hatua za mwanzo za kujaribu kupiga vita Ujinga, Umasikini, Maradhi, Unyonge na Utegemezi (UUMUU)pamoja na kutamka kwa vinywa vyetu mahitaji ya maendeleo ya taifa kuwa ni Watu, Ardhi, Siasa Safi na Uongozi Bora, sifa, hulka na wajihi wa kuwa na Uthubutu bado ni mchanga sana na ndio chimbuko la kukosa kujiamini, kuwa wanyonge na waoga kufanya maamuzi magumu.

Kuna dhana na falsafa inayosema fanya jambo, lisipozaa matunda chanya au uliyotegemea-matokeo hasi yanakupa fursa kurudia mchakato na kujifunza pale ulipokosea na kurudia jambo kwa ubora na umakini zaidi. Cha msingi ni kujiamini na kuwa na uthububu wa kufanya mambo.

Sasa kwa Tanzania yetu ya leo "Ya Magufuli" ya "MATAGA" na "CCM Mpya" utegemezi wa mwenye kujiamini na mwenye kuthubutu kumebakia kuegemea na kumtegemea mtu mmoja, Rais Magufuli. Wengine wote wamekaa kando wakishangilia na kusifia lakini hawana Uthubutu wa kwao wa kujitegemea na kwa nafsi zao bila kutegemea na kuzengea Uthubutu wa magufuli ambao sasa umeambatana na mamlaka na dhama kubwa kama Rais wa nchi.

Tumeshuhudia watendaji wa Serikali na Wanasiasa ambao wana majukumu ya kuongoza nchi, wakigeuka kuwa Wanyapara, wasiojiamini, wakitegemea sana UDola wa Kimamlaka na zaidi turufu yao kubwa ni kusema "maagizo kutoka juu" wakimaanisha ni maelekezo na maagizo ya Magufuli, wakikimbilia kuutegemea Uthubutu wa Magufuli kama ngao na nguzo.

Nasi wananchi ambao hatuna mamlaka au dhamana ya kiuongozi au madaraka, nasi tumekaa kando kwa unyonge au kuachia kila kitu kifanywe na kuamini na kutegemea "ah Magufuli ni kiboko".

Leo haki ya mwananchi inakanyagwa na kupuuzwa, tunakosa Uthubutu wa kudai haki na kusimama imara kukataa kuburuzwa. Ndio kuna hofu na mazingira ya kutishiana ambayo yanatufanya kukosa kujiamini, lakini kwa nini hatumtazami Magufuli yule aliyekuwa Waziri ambaye alisimama na kupata alichotaka na kudhamiria mpaka tukamsifia kwa ujenzi wa miundo mbinu Tanzania?

Nimesema awali, Uthubutu si lazima uzae matoke chanya (ambayo yanaweza kuwa ni mtazamo wa mtu, kikundi au wa aina moja au nyingine) au matendo yanayotikana na Uthubutu yapokelewe kwa mikono miwili na kila mtu. Lakini laiti kama kila mmoja wetu kwa miaka 58 tangu tupate Uhuru wetu tungekuwa na utashi, uimara, ujeuri, kujiamini na uthubutu hata kwa asilimia 50% a uthubutu wa Magufuli, si ajabu Tanzania ingekuwa mbali sana kwenye maendeleo yake ya uchumi, kupanuka na kukomaa kwa haki za watu na yote ambayo tunanung'unikia leo, si ajabu yasingekuwa manung'uniko au kero za kutukosesha raha.

Nikiangalia na kupima Uthubutu wa Magufuli, kuna mengi kafanya (kutenda si lazima kuwe ni sifa ya kufanikiwa jambo) kwa kuamua. Ama ni kutoa maagizo, kuamrisha na kusimamia kikafanyika bila kujali matokeo (consequences or final result) au kuangalia hisia za watu. Mfano, aliazimia kupanuliwa kwa barabara, kukafanyika ubomoaji ili kupisha upanuzi wa barabara hata njia ya reli ya SGR. Hakusubiri majadiliano ingawa yawezekana kukawa na gharama kubwa kwa maamuzi hayo hasa pale penye malalamiko ya fidia.

Akaamua kununua ndege kwa fedha taslimu, zimenunuliwa ndege 5 kwa mkupuo tena kwa fedha taslimu bila kuwa na ukiritimba ambao Serikali na ATCL walifanya kwa miaka 20 kabla ya Magufuli kuboresha au kuwezesha Shirika la ndege kuwa na ndege za kutosha (wengi mtakumbuka ndege za Mattaka). Akasitisha mazoea ya kusafirisafiri ya viongozi na watendaji wa Serikali bila kujali kama kulikuwa na umuhimu wa uwepo na uwakilishi wetu au la, lakini amri yake ilisikilizwa kwa kuwa alisema atatumbua. Leo tumeona Chato inajengwa kwa kasi kubwa; iwe ni maagizo, amri au watu "kujituma" kuhakikisha Chato inakuwa na hadhi kubwa na sasa inageuka kuwa kivutio cha biashara na utalii. Akasema kufanyike uhakiki wa vyeti, wa wafanyakazi wa Serikali, nayo yakatimia. Akasema lazima kila mtu apate stakabadhi akinunua bidhaa ili Serikali ipate mapato... leo kila mtu anahangaika kuwa na stakabadhi! Akasema lazima tuhamie Dodoma, iwe kumekamilika au la, watu wakahamia Dodoma, wengine ofisi ziko kwenye vibanda na wanakaa vyumba vya kupanga.. lakini Serikali imehamia Dodoma.

Sasa najiuliza, sisi kilitushinda nini miaka yote kufanya maamuzi kama haya?ni kigugumizi gani kilitushika kwa muda mrefu kufanya mambo na kuwa na uthubutu, bila kuwa na woga au kujiumauma? kwa nini tuliamini hatuna uwezo wa kufanya mambo kwa hiari lakini tunafanya sasa kwa kuamrishwa na ni sawa na kwamaba tunachapwa mijeledi, tunazinduka na kufanya?

Leo nina uhakika Magufuli akisema tunarasimisha Katiba ya Wananchi iliyotokana na Rasimu ya Warioba, litafanyika bila kupingwa au miguno. Sheria kadhaa na miswaada imepelekwa bungeni na "Chama tawala" ama kwa woga, unafiki au labda ukweli halisi kimepigia kura na kupitisha kila kilichopelekwa na Serikali ya awamu ya tano. Rais Magufuli leo akisema ni marufuku kuzuia mikutano ya kisiasa ya vyama vya siasa, hakuna atakayebisha.

Sasa ni rahisi kusema yeye ana mamlaka makubwa na anatumia cheo chake, lakini ukweli unabakia kuwa anayafanya kutokana na Uthubutu, daring.. hata kama mara nyingine ni kiholela (reckless) au ni kishari (mercilessly), but he gets shit done regardless.

Je sisi wote tungeanza kujiamini na kuanza kuwa na uthubutu bila woga kufanya mambo tunayoamini ni haki yetu kikatiba, ni wajibu wetu kusimama kuyapigania. Iwe ni nyumbani, makazini, kwenye masuala ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, kiuzalishaji na kila jambo, uwe ni mfanyakazi, mwajiri, mfanyabiashara, mwanasiasa.. tukiwa wote na uthubutu, na tukafanya maamuzi kwa umakini lakini tukisimama imara kwa uthubutu, basi Tanzania ya Viwanda na Gurudumu letu la maendelo litapiga hatua kubwa na za haraka sana.

Lakini tukiendelea kwua Wategemezi wa magufuli, siku anaondoka tutarudi kule kule, kukwama matopeni na hata kuwa na mawazo potofu ambayo yanajengwa sasa hivi kusema tunahitaji Magufuli akae zaidi ya muda ulioko kwenye katiba.

Namshukuru sana kwa kutuonyesha Uthubutu, tuungane, tusimame imara tufanye mambo kwa uthubutu kupata haki zetu na maedneleo ya kweli na endelevu.

Ahsante Rais Magufuli kwa kutufundisha Uthubutu!

Wakati ukiandika haya nakukumbusha tu:

1. Lissu alipigwa risasi 16 na nyingine zaidi ya 20 zikimkosa
2. Ben Saanane kapotea
3.Azory Gwanda kapotea
4.Akwilina alikufa kwa risasi
5. Kamanda mawazo alikufa kwa mapanga
6. Roma mkatoliki alitekwa
7.Kada Chadema wa kata ya Hananasif aliokotwa amekufa coco beach
8. Msaidizi wa Membe alitekwa
9. Mo alitekwa

Nikija kwenye mada sasa:
  1. Uthubutu wa kutumia pesa za umma kufanya manunuzi bila kufuata sheria za manunuzi ya umma, lini tender ya bomdia ilitangazwa kama sheria ya manunuzi inavyotaka?
  2. Kwa nini ATCL aiweke chini ya ofisi yake ili isikaguliwe na CAG?
  3. Kwa nini atuondolee bunge live halafu LIve awe yeye Ikulu?
  4. Kwa nini atumie Jeshi kutwaa korosho za wananchi halafu asiwalipe pesa zao?
  5. Kwa nini atumie nguvu nyingi kuminya na kuwabana wapinzani wasitumie haki yao ya kikatiba kufanya siasa?
  6. Kwa nini atengeneze sheria kandamizi za vyama vva siasa, sheria ya takwimu, sheria ya habari n..k

Mleta mada, huo ndo uthubutu unaousema?
 
Uthubutu si lazima tuutazame kwa matokeo chanya pekee, hata matokeo hasi yanaweza kutokea kutokana na mtu kuwa na uthubutu, kudhamiria na kufanya lile alilokusidia.
Rev. ni vizuri kukusoma mara moja moja hivi.

"UTHUBUTU," kwa hakika Magufuli ni mtu wa kufanya mambo kwa 'uthubutu.' Ni mtu mwenye kuitumia dhana ya 'in your face' kisawasawa bila kujali matokeo yake yatakuwa vipi.

Ni kweli kiongozi anayetumia 'uthubutu' hasa katika mambo kadhaa wa kadhaa huweza kuleta mabadiliko makubwa na ya haraka, kwa sababu ule uchelevu unaoletwa na njia za majadiliano 'deliberations' huwa umeondolewa. Lakini hapo hapo kama 'uthubutu' unakuwa ni wa kimakosa, hapo ndipo husababisha majanga makubwa kwa nchi.

Uthubutu anaofanya Rais Magufuli unaogusa uvunjifu wa taratibu, sheria na hata Katiba ya nchi, huo ni 'uthubutu' mbaya kabisa, bila kujali matokeo ya 'uthubutu' huo. Nchi ni lazima iendeshwe katika misingi iliyojiwekea. Haiwezi kutifuliwa tu na 'mtu mmoja eti kwa sababu tu yeye anauthubutu. Hali hiyo huleta vurugu.

Nikiandika haya bila kuweka mifano sitaeleweka..
1. Uthubutu wa kujenga Stieglers' gorge. Ni uthubutu mzuri kwa mtizamo wangu na ninauunga mkono. Lakini anapolazimisha taratibu zisifuatwe wala kusikilizwa katika maswala ya mazingira, panakuwa na dosari. Wasikilize wenye maoni ya utaalam wao, na jitahidi kuelewa wanayosema na uyapime vizuri. Mradi kama huo wenye thamani kubwa kwa taifa hauwezi kuzuiwa na kampeni za kelele tu toka ndani na nje. Mwisho wa siku, mradi unajengwa lakini sio kwa mtindo wa "in your face" anaopenda sana kuutumia.

2. Ujenzi wa International Airport ya Chato. Ni nani anayejua chimbuko la maamzi hayo na jinsi mipango ya utekelezaji wake ulivyofanywa? Bunge walikuwa na taarifa. Walipitisha matumizi ya Tsh 39 billion. Hela hiyo ilipatikana toka wapi?
Kulikuwa na sababu yoyote ya lazima kujenga mradi mkubwa wa kiasi hicho katika eneo hilo? Kulifanyika upembuzi wowte wa kitaalam kuonyesha faidi itakayotokana na mradi huo?
Huu ni 'uthubutu' mbaya moja kwa moja.
Watu hapa wanasema Chato ni Tanzania pia, inahitaji miradi. Nasema sawa kabisa; lakini hapakuwa na miradi bora zaidi ya huo?
Tsh39 bilioni, uwekeze kwa nguvu za wanaChato. Wale wakulima, wavuvi, wachimba madini ...tena basi unahakikisha wananchi hawa miradi watakayosaidiwa kuifanya iwe darasa kwa maeneo mengine nchini. Kama ni kilimo wataalam wanamwagwa pale kutumia utaalam wao wote wa kilimo kuhakikisha kilimo cha hawa wananchi wa Chato kinakuwa ni cha mfano hasa. Miaka miwili mitatu, Chato inakuwa tofauti kabisa na eneo lingine lolote nchini katika maendeleo ya kilimo. Wananchi wakishajua kilimo bora inabaki tu kusimamia mwendelezo kilimo kiwe 'sustainable'. Baada ya hapo hata ujenzi wa International airport unaweza kuonekana ni wa maana.

Hii ni mifano miwili inatosha kuhusu hii dhana ya kufanya maamuzi kwa 'uthubutu'. Ipo mifano mingi sana sasa inayoweza kutolewa kutokana na uongozi wa 'uthubutu' wa rais Magufuli.
 
Wakati ukiandika haya nakukumbusha tu:

1. Lissu alipigwa risasi 16 na nyingine zaidi ya 20 zikimkosa
2. Ben Saanane kapotea
3.Azory Gwanda kapotea
4.Akwilina alikufa kwa risasi
5. Kamanda mawazo alikufa kwa risasi
6. Roma mkatoliki alitekwa
7.Kada Chadema wa kata ya Hananasif aliokotwa amekufa coco beach
8. Msaidizi wa Membe alitekwa

Nikija kwenye mada sasa:

  1. Uthubutu wa kutumia pesa za umma kufanya manunuzi bila kufuata sheria za manunuzi ya umma, lini tender ya bomdia ilitangazwa kama sheria ya manunuzi inavyotaka?
  2. Kwa nini ATCL aiweke chini ya ofisi yake ili isikaguliwe na CAG?
  3. Kwa nini atuondolee bunge live halafu LIve awe yeye Ikulu?
  4. Kwa nini atumie Jeshi kutwaa korosho za wananchi halafu asiwalipe pesa zao?
  5. Kwa nini atumie nguvu nyingi kuminya na kuwabana wapinzani wasitumie haki yao ya kikatiba kufanya siasa?
  6. Kwa nini atengeneze sheria kandamizi za vyama vva siasa, sheria ya takwimu, sheria ya habari n..k

Mleta mada, huo ndo uthubutu unaousema?

Nimekupa like I wish tungekua tunaweza kutoa likes nyingi lol
 
Nimekupa like I wish tungekua tunaweza kutoa likes nyingi lol

Ile kuvunjavunja nyumba za wananchi wa kimara na mbezi halafu hata hela za kujenga hizo barabara kumbe hana mleta mada anaona ni bonge la uthubutu!- ajabu sana!
Kuna uthubutu wa maana na uthubutu usio wa maana, kama huu wa kuvunja nyumba za watu na kuwatia umasikini wakati hata hela zenyewe za mradi huna siyo uthubutu ni kukurupuka!
 
Kizazi cha majanga. Kila kitu ni uvivu mbele. Watu waandika vitabu sembusi hizi sentensi mbili. Na mbaya zaidi unaweza kukuta ni mhitimu wa chuo kikuu ndiyo mwenye haya mawazo! Elimu yetu iko kuzimu
Nina mtizamo tofauti na wako kumhusu huyo jamaa anayetaka mashine inayo-type' maneno anayoongea.
Huyu jamaa amaona tatizo, kinachotakiwa ni kuweka akili katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo hilo, Uvumbuzi huanza hivyo.

Je mkuu, unajua kama kuna "mashine zinazotaipu maneno anayosema mtu'? Kama hazipo, je zikivumbuliwa kutakuwepo na watu watakaopenda kuzitumia?

Binafsi swali lake hilo mimi limenifikirisha sana, na kujaribu kupata jibu. Sijui jibu. Ni ajabu sana na teknolojia yote hii tuliyonayo sasa mashine hizi hazipo! Kuna sababu ya kutozivumbua, kwa sababu najua pesa nzuri ipo hapo kwa mvumbuzi!

Waziri wa Kaskazini, usiachie 'chance' hii.
Jamani sorry naomba kuuliza, hivi kuna machine za mtu kuongea zinyewe zika type unacho ongea?
 
..Mh.Tundu Lissu kupigwa risasi ni uthubutu.

..kwa sababu, where else in this world, chief whip wa opposition camp anacharangwa risasi mchana kweupe, na serekali haimsaidii kwa matibabu, na mwisho wake majeruhi huyo nakuwa anafukuzwa ktk nafasi yake?

Umemsoma vizuri Rev. lakini?

Mimi kama nimemuelewa vizuri, yeye kazungumzia uthubutu tu, bila kujali sana matokeo ya huo uthubutu!

Hebu msome vizuri tena...
 
Umemsoma vizuri Rev. lakini?

Mimi kama nimemuelewa vizuri, yeye kazungumzia uthubutu tu, bila kujali sana matokeo ya huo uthubutu!

Hebu msome vizuri tena...

..nadhani nimemsoma vizuri.

..na ameeleza uko uthubutu ambao matokeo yake ni mabaya.

..na mfano ni huo nilioutaja ktk bandiko langu uliloninukuu.

..uthubutu mwingine ni wa kununua ndege. So far shirika la ndege linajiendesha kwa hasara.
 
Ile kuvunjavunja nyumba za wananchi wa kimara na mbezi halafu hata hela za kujenga hizo barabara kumbe hana mleta mada anaona ni bonge la uthubutu!- ajabu sana!
Kuna uthubutu wa maana na uthubutu usio wa maana, kama huu wa kuvunja nyumba za watu na kuwatia umasikini wakati hata hela zenyewe za mradi huna siyo uthubutu ni kukurupuka!

..labda ni uchanga wa lugha yetu adhimu ya Kiswahili.

..hili neno "UTHUBUTU" halijajitosheleza kueleza alichotaka kueleza mtoa mada.

..Waingereza wangeweza kusema mhusika ni " BOLD."

..au huyu mhusika ni "RECKLESS."

Nyani Ngabu
 
Sasa najiuliza, sisi kilitushinda nini miaka yote kufanya maamuzi kama haya?ni kigugumizi gani kilitushika kwa muda mrefu kufanya mambo na kuwa na uthubutu, bila kuwa na woga au kujiumauma? kwa nini tuliamini hatuna uwezo wa kufanya mambo kwa hiari lakini tunafanya sasa kwa kuamrishwa na ni sawa na kwamaba tunachapwa mijeledi, tunazinduka na kufanya?
Reverend, nilipotoa maoni mwanzo nilikuwa sijasoma bandiko lako lote hadi mwisho. Sasa nimelisoma lote.

Hapana, mengine si kweli kama hilo nililo'quote hapo juu.

Unakumbuka maamzi ya kuhamia vijijini? Unakumbuka elimu ya UPE; unakumbuka, hata ushiriki wa Tanzania katika ukombozi wa nchi zilizokuwa bado zinatawaliwa? Haya yote utayaita nini, kama sio 'uthubutu' ulioongozwa na kusimamiwa na kiongozi mwenye 'uthubutu' wa kushirikisha viongozi wenzake ndani ya chama na serikalini.

Haya yote yalifanyika katika 'taratibu za vikao.' Hayakuwa maamuzi ya 'uthubutu' tu wa mtu mmoja. Ndio maana pakawepo na 'a lasting legacy' ya maamuzi mazito kama hayo. Kiongozi alisimamia 'uthubutu' wa kufanya mambo kama taifa, sio 'uthubutu' wa mtu mmoja kuliburuza taifa zima.
Tena mengi ya haya yaliamuliwa ndani ya chama, na maamuzi hayo kushuka chini hadi kwa wananchi na kuyajadili katika vikao vyao huko huko vijijini.

Magufuli akidondoka leo, ni nini kitakachobaki alichokifanya kwa 'uthubutu' wake binafsi! Ufisadi, rushwa, nidhamu? kazini. Hayo ni mafanikio kweli? Kuna mfumo wowote wa kuyaendeleza haya hata Magufuli akiwa hayupo? Ile international airport itadumu kule Chato?
 
Nianze kwa kutoa Shukrani kwa michango na maoni tofauti ambayo imefanikisha lengo langu kuandika makala hii.

Natambua wazi hisia tofauti na hata mapokeo ambayo ama yameudhi au kufurahisha upande mmoja au mwingine.

Hivyo hamaki (reaction) ni kitu nilikitegemea na kukusudia.

Swali langu kwa wote; hitimisho langu linatoa mbiu kwa kila mmoja wetu kuwa na Uthubutu kudai haki, kusimama imara bila kuruhusu kunyanyaswa au kuwa wanyonge.

Je wote tukipata uimara na uthubutu huu, manyanyaso tuliyoshuhudia miaka 25 tangu tuachane na siasa za chama kimoja zitaendelea?

Ujeuri wa kimamlaka, kiburi na ubabe kutudharau kungeendelea?

Tuendelee kuitafakari dhana ya Uthubutu kwa kina kabla ya kufanya assessment ya kama aliyofanya Magufuli ni manufaa au uthubutu ulikuwa sahihi au la!

Leo tukipata kwa ujumla uthubutu wa kukataa kutawaliwa na CCM... tungekuwa tunaburuzwa?
Rev. karibu tena bana. Ulipotea mno hadi nikadhani labda umerithishwa kiti cha Dick Kovacevich...

Kuhusu Magu, licha ya mapungufu yake, huo ujeuri wake na uthubutu wake mimi unanikosha sana.

Huwa napenda watu vichaa vichaa flani hivi...

Siku hizi hadi watu wa balozi zetu DC na NY ukiwaandikia email wanajibu [promptly].

I’d like to think it’s the Magufuli effect....
Nyani,

People forget I could write in details to criticize Magufuli and list all his failures with such an ease and it will simply be a bitch rant similar to all that has already been said about him for last 20 plus years since he became a politician and now a president.

I chose to use a different prism to construct this piece, making it a thought provoking and it ain’t about Magufuli and his misdeeds nor praising him that he can get things his way...

One has to be Familiar with my writing and thought provoking style... it ain’t about him... it’s about us...!
 
Nianze kwa kutoa Shukrani kwa michango na maoni tofauti ambayo imefanikisha lengo langu kuandika makala hii.

Natambua wazi hisia tofauti na hata mapokeo ambayo ama yameudhi au kufurahisha upande mmoja au mwingine.

Hivyo hamaki (reaction) ni kitu nilikitegemea na kukusudia.

Swali langu kwa wote; hitimisho langu linatoa mbiu kwa kila mmoja wetu kuwa na Uthubutu kudai haki, kusimama imara bila kuruhusu kunyanyaswa au kuwa wanyonge.

Je wote tukipata uimara na uthubutu huu, manyanyaso tuliyoshuhudia miaka 25 tangu tuachane na siasa za chama kimoja zitaendelea?

Ujeuri wa kimamlaka, kiburi na ubabe kutudharau kungeendelea?

Tuendelee kuitafakari dhana ya Uthubutu kwa kina kabla ya kufanya assessment ya kama aliyofanya Magufuli ni manufaa au uthubutu ulikuwa sahihi au la!

Leo tukipata kwa ujumla uthubutu wa kukataa kutawaliwa na CCM... tungekuwa tunaburuzwa?

Nyani,

People forget I could write in details to criticize Magufuli and list all his failures with such an ease and it will simply be a bitch rant similar to all that has already been said about him for last 20 plus years since he became a politician and now a president.

I chose to use a different prism to construct this piece, making it a thought provoking and it ain’t about Magufuli and his misdeeds nor praising him that he can get things his way...

One has to be Familiar with my writing and thought provoking style... it ain’t about him... it’s about us...!

💯%.

Now folks can see why some of us missed your presence!

Don’t be a stranger no more!
 
Uthubutu gani huo wakusubiri mpaka jeshi, polisi, mahakama, tiss, takukuru na bunge viwe upande wake.

Kipindi nchi inaliwa wakati wa mkapa yuko kimya, pia wakati kikwete yuko kimya, na sasa hivi kipindi chake yuko kimya, sana sana anaishia kupiga kelele nchi imetafunwa sana hii na huchukui hatua zozote, lakini wakina lisu na mbowe na wwngineyo kutwa kuwafungulia kesi mahakamani na kutaka kuwaua juu.

Ndugu jitahidi utapata hata ubalozi au ukuu wa wilaya.
 
Back
Top Bottom