Utendaji sifuri, kiinua mgongo 46 millioni kwa kila Mbunge

Na ni kwanini kipindi hiki au ni namna ya kuupoza mgomo wa watumishi? Au ndio mbwa wa kiswahili akiwa anapigapiga kelele wakati ukila ukimtupia mfupa ananyamaza
 
mimi nihasi hi kuwa mbunge sasa ni kama ka chanel ya kupata fedha.kwanza mimi nigeshauri hizi mshara za wabunge zingekuwa kaka za wafanyakazi wengine zianze na ma TGS scale.mwenye elimu kubwa apate chake kubwa.halafu hizi marupurupu na nini viwe kama za wafanyakazi wengine.sisi hatuwalazimishi kugombea ubunge,sasa yule mwenye chuki na hii nchi atagombea kama kweli ana penda nchi,na wale ambao wanafuata fedha hawatogombea automatically.eboh,yani kwanza hii ni kazi ya wito,halafu bado wanataka hela kubwa,basi wasigomnbee,hamna anayewalazimisha.kama unataka ubunge,na ukubalu kuapata mshahara mdogo.to hell with this politics.we will die poor,unless godyesu afufuke tanzania na kut save.ama sivyo ile maisha bora ni ndoto ya mgonjwa aliyepo kwenye comma.
 
Mh.Slaa, lazima ukubali kwamba jibu la No Comment mlilotoa upinzani linatuma different messages na ukizingatia suala lenyewe lina maslahi kwenu pia....
sidhani kwamba unahaja ya kulitetea hili na kumsemea Mh.Zito kwenye hili, wananchi wanataka viongozi muwe wazalendo zaidi na sio kuangalia maslahi yenu tu, fuatilia michango mingi ya wanaJF inavyoonyesha kutofurahishwa na hili, hata kama serikali inawaburuza lakini sio lazima na nyinyi mburuzike.....

Uzalendo Kwanza......
 
Bw. Miundombinu,

Huu ni uamuzi wa busara sana. Nchi hii haiwezi kuendelea ikiwa watumishi wa umma wana mashaka na hali zao za maisha na uchumi. Ni bahati mbaya tu kuwa kwa desturi, umasikini una kawaida ya kupandikiza hisia za chuki na wivu. Busara ndogo tu inatufundisha kuwa huwezi kuwa na ng'ombe ambaye humpatii malisho mazuri na madawa halafu utegemee atoe maziwa mazuri, ngozi nzuri na nyama laini. Kukosekana kwa uhakika wa hali nzuri ya maisha kwa watumishi wa umma kunaathiri sana maendeleo kwa kuwalazimu kwanza kutumia muda mwingi kujitafutia unafuu wa maisha yao; na pili kufikiria kuibaiba na ubadhirifu. Katika mazingira hayo, mahitaji ya wananchi yanapewa kipaumbele kidogo sana. Mikopo hii yaweza kuwa suluhisho zaidi kuliko posho ambazo zinafanya watumishi wa umma kuwehuka kuzitafuta na kuacha kazi za majalada na uchambuzi mezani kwenda kwenye warsha na safari.

Ni vyema kufahamu kuwa pamoja na mambo mengine, maboresho ya utumishi wa umma katika nchi za kusini mashariki mwa asia (tiger economies) yalichangiwa sana na maboresho ya utumishi wa umma yaliyotoa neema kwa wafanyakazi. Neema ile ilivutia wataalamu na vijana kutoka katika sekta binafsi kujiunga na sekta ya umma. Tija na morali viliongezeka na heshima ya utumishi wa umma ikapanda. Punde mabadiliko katika uchimi yakaanza kuonekana. Na ni kweli kuwa katika mchakato ule, wananchi walilalama na hawakufurahishwa na kitendo cha wafanyakazi wa sekta ya umma kuboreshewa hali zao. Wengi waliona ni unyonyaji na ubadhirifu kuwaongezea watumishi wa umma kipato na fursa za mikopo ilihali wananchi ni maskini. Kilichasaidia ni kuwa serikali zile zilikuwa za kidikteta si kidemokrasia hivyo, sauti za wananchi zilififishwa na matokeo mazuri yalionekana baadae.

Na hapa kwetu tusitarajie ongezeko hili litapokelewa kwa mikono miwili na wananchi. Wakp watakaopinga. Ukweli unabaki kuwa Sekta ya Umma iliyo fukara haiwezi kuondoa umaskini, itazidisha ufukara tu. Ni wakati sasa tuondokane na dhana tuliyobeba vichwani mwetu kuwa mtumishi wa umma, padri, mwalimu lazima awe masikini masikini hivi au fukara fukara hivi.

Leo kijana aliyetoka Chuo Kikuu anaingia kwenye sekta binafsi na ndani ya mwezi mmoja anakopeshwa mara kumi ya mshahara wake ananunua gari yake au anapanga nyumba na kuanza kujitegemea. Aidha, amekatiwa bima ya afya AAR inayomruhusu kutibiwa kwenye hospitali yenye uhakika yeye na dependants 3-4. Kwa upande wa utumishi wa umma, kijana huyo anaanza na mshahara wa TGS D ambao kimantiki unamruhusu kupanga chumba kimoja tu na si nyumba, kutokuwa na simu ya mkononi ambayo ni muhimu kwa mawasiliano na haumruhusu kununua gari wakati standing order inamtaka awe amefika ofisini saa 1 na dk 30 asubuhi. Katika mazingira hayo unategemea nini? Hataacha file mezani akimbizie workshop au safari itakayomlipa mara mbili au tatu ya mshahara wake? Je ukimkopesha akanunua samani na gari ukawa unamkata kidogo kidogo hutamjengea loyalty na hali ya kuthamini kazi yake kwa kuwa akizembea atafukuzwa na ili hali ana deni? je hatufahamu kuwa wako wengi katika sekta binafsi ambao wanafanya kazi kwa bidii na hawahami kwa kuwa wana mikopo au wanahama tu pale ambapo wamemaliza mikopo yao? Leo hii, the best brains zinakimbilia sekta binafsi zaidi kuliko sekta ya umma. Uzalendo hauliwi mkavu mkavu.

Ifike mahala tukubaliane kuwa ni kweli nchi yetu ni maskini wa kipato na kwamba suluhisho si kwa wote kubaki kuwa maskini na wote tuondokane na umasikini kwa wakati mmoja. Tunaweza kulazimika kuwa na awamu, tunaweza kuamua kuwaweka watumishi wa sekta ya umma katika hali nzuri kwanza, kisha tukajikuta tumechochea maendeleo katika sekta nyingine.


Lakini kwanini iwe wakuamuliwa kuwa wa kwanza kwa kunufaika wawe walewale na wale ambao hawahitaji kupewa kipaumbele kwa vile wana uwezo?
 
Hivi huo mchanganuo wa kwamba wabunge ndio wahitaji sana kuliko wabongo woooooooote nani kafanya???
Nilitegemea hizo 48 bn wapewe wanyonge.....
Inatia aibu na kushangaza.........
 
Kwa mantiki ya mfuko huu Mbunge ni mtumishi wa Umma. Je kama ni hivyo mbona sheria inasema mtumishi wa umma akiwa na kesi ya jinai mahakamani, anapaswa asimame kazi hadi kesi itakapoamriwa? Je hawa wabunge wakiwa ni watumishi wa umma, sheria hii haiwabani? Au tusema sheria zina ubaguzi? Kama kwa sheria zenye maslahi kwao wao wanakuwa watumishi wa umma, na kwa sheria za kuwaadhibu wao wanaodoka katika fungu la watumishi wa umma, je sheria za namna hii hazivunji katiba? Maana ninavyokumbuka; katiba inazuia kutungwa kwa sheria za kibaguzi!
Wataalamu wa Katiba tusaidieni
 
Hapa inabidi nikubaliane kwa shingo upande kwa wabunge kukopeshwa mikopo kwa mtindo huu.

Wabunge kwa kweli wanakazi ya kuzunguka jimboni kote na mara nyingi magari haya wananchi wajimboni wanayaona kama wana haki nayo, kwa hiyo lifti, kubeba watu nk ni common mno, hivyo kwa upande mdogo magari haya yanasaidia jamii.

Hii ni the most cost effective way ya kuprovide usafiri kwa Hon Mps kuliko taratibu serikali inazotumia kwa mfano mawaziri, PS kuwa na magari ya serikali yanayolipiwa mafuta, dereva, utengenezaji, insurance blah blah.

Mimi ningependekeza mfuko huo uongezwe ufike hata 100 billion ili mawaziri, PS nao wapewe mikopo tuachane na kumaintain hayo MAVX ambayo nina uhakika cost baada ya miaka mitano ni zaidi mara kumi ya hiyo mikopo.
 
Hapa inabidi nikubaliane kwa shingo upande kwa wabunge kukopeshwa mikopo kwa mtindo huu.

Wabunge kwa kweli wanakazi ya kuzunguka jimboni kote na mara nyingi magari haya wananchi wajimboni wanayaona kama wana haki nayo, kwa hiyo lifti, kubeba watu nk ni common mno, hivyo kwa upande mdogo magari haya yanasaidia jamii.

Hii ni the most cost effective way ya kuprovide usafiri kwa Hon Mps kuliko taratibu serikali inazotumia kwa mfano mawaziri, PS kuwa na magari ya serikali yanayolipiwa mafuta, dereva, utengenezaji, insurance blah blah.

Mimi ningependekeza mfuko huo uongezwe ufike hata 100 billion ili mawaziri, PS nao wapewe mikopo tuachane na kumaintain hayo MAVX ambayo nina uhakika cost baada ya miaka mitano ni zaidi mara kumi ya hiyo mikopo.

Kwa hoja ulizotowa mimi naona ni bora wasipewe hiyo mikopo bali wakodishiwe magari kila miezi sita kabla ya Uchaguzi kwani uzoefu ni kuwa wakati huo ndio wabunge wanakuwa na kazi za kufanya majimboni. Kipindi cha miaka minne na miezi sitta inakuwa ni kipindi cha wabunge kufanya kazi za kutembelea Mawizara na Mashirika ya Umma kwa vuikundi kama Kamati.
 
Hapa inabidi nikubaliane kwa shingo upande kwa wabunge kukopeshwa mikopo kwa mtindo huu.

Wabunge kwa kweli wanakazi ya kuzunguka jimboni kote na mara nyingi magari haya wananchi wajimboni wanayaona kama wana haki nayo, kwa hiyo lifti, kubeba watu nk ni common mno, hivyo kwa upande mdogo magari haya yanasaidia jamii.

Hii ni the most cost effective way ya kuprovide usafiri kwa Hon Mps kuliko taratibu serikali inazotumia kwa mfano mawaziri, PS kuwa na magari ya serikali yanayolipiwa mafuta, dereva, utengenezaji, insurance blah blah.

Mimi ningependekeza mfuko huo uongezwe ufike hata 100 billion ili mawaziri, PS nao wapewe mikopo tuachane na kumaintain hayo MAVX ambayo nina uhakika cost baada ya miaka mitano ni zaidi mara kumi ya hiyo mikopo.

mimi sijamwona mbunge wangu akizunguka jimboni - anafanya kazi kwenye wizara - Dar es Salaam - anazunguka saa ngapi au una maana wakati wa kampeni????
 
Wanasiasa hapa Tanzania wanalipwa vizuri kuliko wafanyakazi ujuzi na wanaozalisha.
Kutokana na hilo jamii yetu lazima iwe maskini kwa kuwa watu wote wenye akili nzuri watatamani kuwa wanasisa ili wajipatie kipato kilaini, na matokeo yake ni upungufu wa ufanisi na tija katika fani mbalimbali.
Ufisadi umejijenga na unapata ulinzi katika siasa zaidi hasa hasa kwa wanasisa wakongwe na wenye nafasi za juu kwa kuwa wanajua siku zote wamekuwa wakivuna wasichostahili.
Viongozi wengi wakongwe wa siasa na siku hizi hata familia zao wanajua wazi kwamba mtandao wa wizi na ufisadi ndiyo salama yao na hivyo wataulinda na kurithishana kwa gharama yoyote ile.

Tunatakiwa kubadilisha jamii ya kitanzania ielewe na ione kwamba kipato kikubwa kinapatikana kwa juhudi na maarifa katika kazi za uzalishaji na siyo blahblah za wabunge na kwamba siasa ni ziada tu na mapato yake ni kidogo. Hapa watalamu watabaki kwenye fani zao na maendeleo yatakuwepo.

MABADILIKO YANAWEZEKANA, TIMIZA WAJIBU WAKO KWA SEHEMU YAKO!
 
Si wanalipa kodi kutoka kwenye hayo malipo kama walala hoi wengine?

Mapato ya wateule wabunge hayakatwi kodi...na ni hao hao waliopitisha sheria ya kuzuia mishahara na marupurupu yao yasiwe yanakatwa kodi...huku wapiga kura hao waliobahatika kuajiriwa wakikatwa kodi lukuki za kuwaongezea umaskini..na wala hawafikiri namna ya kupanua wigo wa kodi.
 
Back
Top Bottom