Tunashukuru vile umekuja na kujibu maswali kwa wakati.Ahsante kwa ushuhuda wako
Tafadhali tusaidieni taarifa kamili tupo kuwahudumia
Tafadhali onyesha namba ya mita tuhakikiTunashukuru vile umekuja na kujibu maswali kwa wakati.
Unatakiwa kufanya nini ili kubadilishiwa tarrif? Mimi nimeunganishiwa umeme mwezi Januari 2020 nikapigwa tariff 1 nafikiri (ile ya elfu 10 unit 28), matumizi yangu kwa mwezi ni wastani wa unit 60, ninaona ninastahili kuwa katika tarrif ya matumizi madogo (tarrif 4 nafikiri - sina uhakika, kama nakosea nirekebishwe) nipo Kiluvya.
Pamoja na maelezo marefu.Katika juhudi za kuboresha uchumi, upatikanaji wa nishati ni muhimu sana.
Ila kama pia usambazaji wa nishati utalega tunaweza tusipate matokeo tarajiwa.
Mimi ni mkazi wa Ukonga, Imepita miezi 6 tangu nimalize mchakato wote wa kupata umeme, yaani kufanya e/wiring kwangu, maombi, survey, wakatoa ripoti, inahitajika nguzo moja, wakanipa control number, nikalipia. Almost 600,000TSH. Tangia mwaka jana August nimekuwa nikifuatilia Gongo la Mboto mpaka kuonana na Meneja ili nijue tatizo kwa nini hawajaja kuunganisha umeme bila mafanikio, danadana nyingi, uongo uongo mwingi, mwisho nenda tutashughulikia na hawashughulikii.
Je, kwa hali hii, mtu kuunganishiwa umeme uliopita 105m kutoka kwake TANESCO inachukua zaidi ya miezi sita, uchumi wa kati tutatoboa kweli, hili kwa kweli ni swali kwa Waziri wa nishati.
Mimi nafikiri kuna umuhimu wa kulivunja hili shirika ili kuongeza ufanisi wa huduma za nishati au kuhusisha mashirika binafsi kwa kiwango kikubwa katika shughuli wanazoweza kufanya. Mfano: kwa sasa hatupati shida kwenye suala la kuunganishiwa mawasiliano ya simu kwa sababu TTCL wana washindani, ila kipindi wakiwa wenyewe walikuwa na ukiritimba mwingi kama huu wa TANESCO
Kuna harufu kubwa ya rushwa hapa, hasa hapa branch la TANESCO Gongo la Mboto, watu wanacheleweshewa huduma kwa makusudi ili waingie mfukoni kutoa rushwa, Nashauri PCCB wamulike eneo hili.
TANESCO wafanye kazi zao, kwa nini nilipe laki sita kuunganishiwa umeme na nisubiri zaidi ya miezi 6, hiyo fedha ningekuwa nimeitumia kwa biashara ningekuwa na bakaa fulani ya kunitoa mwaka 2021, kuna umuhimu wa kuwa na mkataba kwa wateja, yaani ndani ya muda gani mteja atakuwa ameunganishiwa umeme, iwapo watavuka muda huo kuwe na hatua madhubuti za kumlinda mteja kwa uonevu huo.
Nimekwishatuma DMTafadhali onyesha namba ya mita tuhakiki
Mkuu hio alokupa ni taarifa kamili,unaweza kabisa fuatilia na kufanyia marekebisho.Au Hujaelewa ujumbe wake?Tuwekee taarifa kamili
Jina
Eneo
Wilaya
Simu
Tatizo
Toka lini
Na mimi naweza kutuma namba za mita? Shida yangu inafanana na ya member hapo juuTafadhali onyesha namba ya mita tuhakiki
Wanataka jina ili wakawaambie wenzao anaeleta chokochoko zote hizi ni pombe kalitunachokifanya hapa kinaitwa whistle blowing siyo ila mtoa taarifa anapenda kujulikana hapa tumeshawapa pa kuanzia ni swala la nyie wenyewe kujifanyia tathmini kila meneja aitishe mafaili yaliyokaa muda mrefu na ahakikishe yanafanyiwa kazi na siyo unihudumie mimi kwa sababu nimepaza sauti bali badilisheni mfumo wenu wa huduma….ushaambiwa bila kuwaona wale vishoka hupati huduma unataka jina la nini sasa
Taarifa kamili ndio huduma mpendwa mteja wetuWanataka jina ili wakawaambie wenzao anaeleta chokochoko zote hizi ni pombe kali
Vishoka tunaomaanisha ni wateja wanaojifanya wanafatilia kazi za wateja au kujifanya wafanyakazi ili wajipatia fedha isivyo kihalali
Vishoka tunaomaanisha ni wateja wanaojifanya wanafatilia kazi za wateja au kujifanya wafanyakazi ili wajipatia fedha isivyo kihalali
Tunashukuru sana mteja aliyelalamika hakutoa taarifa kamili tuone hicho alicholalamikia hivyo nie vema kuacha atoe ushirikiano tuone taarifa kwenye mfumo na kumuhudumiaNchi ina miaka 60 ya Uhuru lakini bado mnafanya kazi kizamaniiii. Yani hamuwahudumii watu mpaka walalamike, lipite zogo, vurugu za maongezi dah!, Mtu analipia huduma kumpa sasa haki yake ya kimsingi ya kile alicholipia mpaka lipite zogo.
Ni shirika lenye watu wavivu msio na mfano, miezi 6 toka mtu alipie mnazurura tu, Pesa yake mmekula kumpa huduma majanga.
Ningekuwa Jiwe au Waziri anaehusika na hii mamlaka yenu aisee ningeanza na wewe uliepo humu. Upo humu kila siku lakini malalamiko hayaishi, maana yake ni kwamba hata wewe ni mvivu. Uwepo wako humu ilitakiwa liwe ndio suluhisho la ucheleweshaji. Sasa kama upo humu kuwahudumia wale wanaolalamikia huduma yenu Vp wale ambao hawajajiunga humu huku wakicheleweshewa huduma, wao walalamike wapi ili kilio chao kisikike???
Tunasoma habari za shirika lenu mpaka tunasikia aibu. Mnatutia aibu kwa wageni. Kuna wageni wapo humu wanaojua Kiswahili, wanatusimanga wanaposoma malalamiko ya wateja wenu. Makazini humu na matusi kututukana huku wakitoa mifano ya shirika lenu kuwa lina mijitu mivivu.
Jirekebisheni bana.