Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,162
Kwenye mfumo wa siasa wa vyama vingi, vyombo vyetu vya ulinzi na usalama havitakiwi kujihusisha na mambo ya siasa na vinatakiwa viwe neutral visivyofungamana na chama chochote cha siasa na vyombo hivyo vinatakiwa visionyeshe upendeleo kwa chama chochote na kuvionea vyama vingine.
Ingawa kinadharia vyombo hivyo vya ulinzi na isalsma huwa vinadai viko neutral na haviegemei upande wa chama chochote cha siasa, lakini sisi wananchi tunaofuatilia mwenendo wa vyombo vyetu hivyo vya ulinzi na usalama, hususani Jeshi letu la Polisi tumekuwa tukiliona Jeshi hilo likifanya upendeleo wa wazi kwa chama tawala cha CCM na kuwanyanyasa vyama vya upinzani hususani chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema.
Nitatoa mifano michache katika kuthibitisha kauli yangu.
Ingawa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 3(1) inaeleza kuwa nchi yetu itakuwa ya mfumo wa vyama vingi na katika utekelezaji wa shughuli zao vyama hivyo havipaswi kuingiliwa na chombo kingine chochote. Hata hivyo tumekuwa tukishuhudia Jeshi letu la Polisi likiingilia waziwazi shughuli za vyama vya siasa hususani katika uendeshaji wa mikutano ya kisiasa.
Tumekuwa tukishuhudia Jeshi letu la Polisi likivizuia Mara kwa Mara vyama vya siasa vya upinzani nchini. hususani chama kikuui cha upinzani cha Chadema kufanya mikutano yake huku Jeshi hilo hilo likiruhusu Chama cha CCM kufanya mikutano na shughuli zake bila kuzuiwa!
Nitatoa mfano mmojawapo kuonyesha namna gani Jeshi letu la Polisi linavyoonyesha upendeleo wa wazi kwa chama cha CCM.
Mbunge wa Chadema Esther Bulaya wa Jimbo la Bunda alienda kwenye Jimbo la mbunge mwenzake wa Chadema John Heche wa Jimbo la Tarime kwenda kushiriki harambee ya ujenzi wa shule ya Nyamongo na yeye mbunge Esther Bulaya akatoa mchango wake wa mifuko 100 ya cement.
Mbunge huyo baada ya kumalizika mkutano huo alikamatwa na Jeshi la Polisi na kwenda kulazwa kwenye selo za Polisi na wakati wowote kuanzia sass atafunguliwa mashitaka mahakamani ya uchochezi!
Hata hivyo mbunge Elibariki Kingu wa CCM wa jimbo la Singida Magharibi alifanya "the same thing" na kwenda Jimbo la Singida Mashariki la mbunge Tundu Lissu wa Chadema na akaendesha harambee ya ujenzi wa shule, hajakamatwa na Jeshi la Polisi!
Tumeshuhudia pia mbunge wa viti maalum wa CCM Tulia Ackson akienda Jimbo la Mbeya mjini la mbunge Sugu wa Chadema naye akishiriki harambee kuchangia ujenzi wa soko lliloungua la Sido, naye hajakamatwa na Polisi!
Tunachojiuliza sisi wananchi ni kwanini Jeshi letu la Polisi linakuwa na double standard na kutekeleza majukumu yao kwa ubaguzi kwa kukipendelea waziwazi chama tawala cha CCM na kuvinyanyasa na kuvionea vyama vya upinzani, hususani chama kikuu cha upinzani cha Chadema?
Iwapo Jeshi letu la Pokisi linataka kurejesha imani ya wananchi kuwa ni Jeshi linalowatumikia wananchi wote bila upendeleo ni lazima lijirekebisje na kuepuka kufanya ubaguzi katika utendaji wake wa kazi kwa kupokea maagizo toka kwa watawala wetu na kuyatekeleza.
Ingawa kinadharia vyombo hivyo vya ulinzi na isalsma huwa vinadai viko neutral na haviegemei upande wa chama chochote cha siasa, lakini sisi wananchi tunaofuatilia mwenendo wa vyombo vyetu hivyo vya ulinzi na usalama, hususani Jeshi letu la Polisi tumekuwa tukiliona Jeshi hilo likifanya upendeleo wa wazi kwa chama tawala cha CCM na kuwanyanyasa vyama vya upinzani hususani chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema.
Nitatoa mifano michache katika kuthibitisha kauli yangu.
Ingawa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 3(1) inaeleza kuwa nchi yetu itakuwa ya mfumo wa vyama vingi na katika utekelezaji wa shughuli zao vyama hivyo havipaswi kuingiliwa na chombo kingine chochote. Hata hivyo tumekuwa tukishuhudia Jeshi letu la Polisi likiingilia waziwazi shughuli za vyama vya siasa hususani katika uendeshaji wa mikutano ya kisiasa.
Tumekuwa tukishuhudia Jeshi letu la Polisi likivizuia Mara kwa Mara vyama vya siasa vya upinzani nchini. hususani chama kikuui cha upinzani cha Chadema kufanya mikutano yake huku Jeshi hilo hilo likiruhusu Chama cha CCM kufanya mikutano na shughuli zake bila kuzuiwa!
Nitatoa mfano mmojawapo kuonyesha namna gani Jeshi letu la Polisi linavyoonyesha upendeleo wa wazi kwa chama cha CCM.
Mbunge wa Chadema Esther Bulaya wa Jimbo la Bunda alienda kwenye Jimbo la mbunge mwenzake wa Chadema John Heche wa Jimbo la Tarime kwenda kushiriki harambee ya ujenzi wa shule ya Nyamongo na yeye mbunge Esther Bulaya akatoa mchango wake wa mifuko 100 ya cement.
Mbunge huyo baada ya kumalizika mkutano huo alikamatwa na Jeshi la Polisi na kwenda kulazwa kwenye selo za Polisi na wakati wowote kuanzia sass atafunguliwa mashitaka mahakamani ya uchochezi!
Hata hivyo mbunge Elibariki Kingu wa CCM wa jimbo la Singida Magharibi alifanya "the same thing" na kwenda Jimbo la Singida Mashariki la mbunge Tundu Lissu wa Chadema na akaendesha harambee ya ujenzi wa shule, hajakamatwa na Jeshi la Polisi!
Tumeshuhudia pia mbunge wa viti maalum wa CCM Tulia Ackson akienda Jimbo la Mbeya mjini la mbunge Sugu wa Chadema naye akishiriki harambee kuchangia ujenzi wa soko lliloungua la Sido, naye hajakamatwa na Polisi!
Tunachojiuliza sisi wananchi ni kwanini Jeshi letu la Polisi linakuwa na double standard na kutekeleza majukumu yao kwa ubaguzi kwa kukipendelea waziwazi chama tawala cha CCM na kuvinyanyasa na kuvionea vyama vya upinzani, hususani chama kikuu cha upinzani cha Chadema?
Iwapo Jeshi letu la Pokisi linataka kurejesha imani ya wananchi kuwa ni Jeshi linalowatumikia wananchi wote bila upendeleo ni lazima lijirekebisje na kuepuka kufanya ubaguzi katika utendaji wake wa kazi kwa kupokea maagizo toka kwa watawala wetu na kuyatekeleza.